Mke wa Dk Slaa apata dhamana

Prodigal Son

JF-Expert Member
Dec 9, 2009
1,067
696
Mussa Juma, Arusha

MKE wa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa, Rose Kamili, ambaye Diwani wa CCM wa Kata ya Bassotu, wilayani Hanang, amelituhumu jeshi la polisi wilayani Hanang kutumika kisiasa kutokana na kutekeleza maagizo ya kigogo mmoja kutaka yeye akamatwe pamoja na viongozi wa wafugaji.

Diwani huyo, ambaye ametangaza kugombea ubunge jimbo hilo la Hanang katika uchaguzi mkuu ujao kupitia CCM, alisema kukamatwa kwake juzi pamoja na wananchi wengine 13 ni shinikizo la kigogo huyo.

"Polisi wamenikata na kunipa dhamana mimi na Ally Kaoga jana na wamegoma kutoa dhamana kwa wananchi wengine 12 hili ni shinikizo la kigogo huyo tumepata taarifa amewaahidi baadhi ya wakulima kuwapa mashamba na wanataka kuzuwia dhamana ili walazimishe ugawaji wa mashamba," alisema Rose Kamili.

Kamili ambaye ni Diwani wa CCM tangu mwaka 1994 na amewahi kushika nyadhifa mbali mbali ndani ya CCM ikiwepo ujumbe wa mkutano mkuu wa CCM Taifa, alisema mgogoro wa mashamba ya Hanang hivi sasa umefanywa wa kisiasa ili kuficha ukweli.

"Mimi nasema ugawaji wa mashamba Hanang uwe wa haki na wafugaji wapewe haki yao kwani kihistoria wao ndio walipokonywa na serikali maeneo yao na kuwafanya watawanyike karibu nchi nzima ili kuanzisha shirika la chakula la NAFCO," alisema Kamili.

Diwani huyo alisema kitendo cha kigogo huyo, kutembelea eneo la mgogoro kufanya mkutano wa hadhara juzi na kuahidi kuwashughulikia watu aliowaita wachochezi ni ishara kuwa suala hilo limekuwa la kisiasa.

"Mimi wanasema ni mchochezi nawachochea wafugaji wasikubali mgawanyo wa shamba eti nafanya mikutano usiku....huu ni uongo kwani wafugaji kama watanzania wengine lazima haki yao ijulikane na ndicho nimekuwa nikitetea,"alisema Kamili.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi mkoani Permena Sumari alikanusha tuhuma kuwa polisi inatumika kisiasa katika kutatua mgogoro wa ugawaji wa mashamba ya Hanang.

"Sisi hatufuati siasa tunaowakamata tutawafikisha mahakamani kwa tuhuma za kufanya uvamizi kwa viongozi wasigawe ardhi na kuwashambulia wananchi wengine kwa silaha,"alisema Sumari.

Kamanda huyo alifafanua kuwa,operesheni ya kuwakamata wananchi wote waliohusika na vurugu itaendelea hadi wote wawe wamekamatwa na kufikishwa mahakamani.

"Ambao tumewakamata tumewanyima dhamana kwa sababu za kiusalama na sio kisiasa kwani hakuna shaka kuwa vurugu zilitokea na watu kujeruhiwa,"alisema Sumari.

Februari 11 mwaka huu, viongozi wa serikali ya kijiji cha Mulbadaw pamoja na wananchi wengine walishambuliwa na kundi la wafugaji ambao walikuwa wanapinga eneo lao kugawanywa kwa wakulima.

Katika vurugu hizo watu zaidi ya 10 walijeruhiwa vibaya kwa silaha za jadi na hadi jana watu wanne walikuwa bado wamelazwa katika hospitali ya kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) ya Haydom.

Chanzo: Mwananchi
 
serekali hii kila kukicha inawaonea wafugaji, na kwa sasa wamekuwa kama wakimbizi katika nchi yao, kati ya viongozi ambao walikuwa mstari wa mbele kuwatetea wafugaji alikuwa Sokoine peke yake
 
2010-02-15

17384.jpg

Opposition parliamentarian Willibrod Slaa with his wife, CCM councillor Rose Kamili, who was arrested on Saturday for allegedly inciting violence.

The wife of opposition leader Willibrod Slaa yesterday accused powerful forces of being behind her arrest and overnight detention in a police cell in Hanang District.

Ms Rose Kamili told journalists after her release that police were being used to undermine her politically, adding that she was arrested on Saturday on the orders of a "big shot".

But the Hanang District police boss, Mr Permena Sumari, swiftly denied the claims, saying the police were only performing their duties as custodians of the law.

Ms Kamili said police had become partisan, adding that this was unacceptable. "The police are being used to undermine me 'they are being used to further the political interests of a big shot' they were ordered by the big shot to arrest me."

Ms Kamili, who is the Councillor for Bassotu Ward in Hanang District, has declared her intention to vie for the Hanang parliamentary seat currently held by Dr Mary Nagu, who is also the Industry, Trade and Marketing minister.

She was arrested along with 13 other people on suspicion of incitement, but said yesterday that only two of them were released on police bond.
 
2010-02-15
...........................[Snip]
Ms Kamili, who is the Councillor for Bassotu Ward in Hanang District, has declared her intention to vie for the Hanang parliamentary seat currently held by Dr Mary Nagu, who is also the Industry, Trade and Marketing minister.

Imeshaelezwa baadhi ya wanasiasa hawana kazi kama wataanguka ktk siasa. wanaweza hata kuua kabisa!
 
2010-02-15

17384.jpg

Opposition parliamentarian Willibrod Slaa with his wife, CCM councillor Rose Kamili, who was arrested on Saturday for allegedly inciting violence.

kwamba wife wa mh. slaa ni ccm?! sasa kama ameshindwa kum-influence wife wake kwa sera za chama chake watz wengine inakuwaje? au sioni vizuri miye?
 
kwamba wife wa mh. slaa ni ccm?! sasa kama ameshindwa kum-influence wife wake kwa sera za chama chake watz wengine inakuwaje? au sioni vizuri miye?

Mkuu kwani ukiwa na mke hamruhusiwi kutofautiana kimawazo na kimsimamo? Rose Kamili anaweza kuwa mke wa Dr. Slaa. LAKINI anabaki yeye kama yeye na uhuru wa kujiamlia what she thinks is good for her and her country. Ni wanasiasa wengi sana ulimwenguni wana spouses ambao wanatofautiana kimtizamo. Mfano Gavana wa Carlifornia ni Republican damu na mke wake ni Democrat damu. Anyway, kwa hili la Slaa nadhani ni jambo jema kuona couple yote iko active kwenye politics. Inaonyesha kwenye hiyo familia kuna "democracy". Maana mume hajamlazimisha mke akubaliane naye kimawazo.

Big up Dr. Slaa, big up mama Kamili.
 
kwamba wife wa mh. slaa ni ccm?! sasa kama ameshindwa kum-influence wife wake kwa sera za chama chake watz wengine inakuwaje? au sioni vizuri miye?

Kaazi kweli kweli kwa Great Thinkers,kumbe ni makosa kwa mke na mume kutofautiana kisiasa?Sikujua kama hilo ni kosa hadi mwenzetu Great Thinker Outlier alipotueleza hivyo!

Na labda sijakuelewa vyema Outliner,sasa kama mme akawa unamueleza sera za chama chako mkewe lkn mke hajavutiwa nazo na kukataa kujiunga na chama cha mme, ungekuwa wewe unamuacha kwa kumpa talaka huyo mkeo au?

Soma habari hii mkuu Outlier;Kule CALIFORNIA-USA; wakati Anorld Sch ni Gavana wa jimbo hilo kupitia chama cha Republican lkn mke wake ni mwanachama maarufu wa Democratic na hata alimsadia waziwazi Obama kwa fedha kwenye uchaguzi wa mwaka 2008!Kwa maana hiyo Gavana amuache mkewe au?

Si kweli kuwa mkiwa Mke/mme basi ni lzm muwe mnafuatana kwa sera na eti hamna kupingana,kumbuka no matter what kila mtu ana haki ya kuamini akiaminicho!
 
There is only one part in the bedroom( CALLED FAMILY), how was in when anorld showzneger ;s wife and girl was with obama while the dad is with McCain?? Only Kenyan women where able to boycott their man on their conjugal rights
 
Ms Rose , kumbuka wewe kiongozi wa serikali ya mtaa(local government).Wewe umevunja sheria kwa sababu serikali kuu ilikuwa ikiwagawia ardhi wananchi. Uliwezaje kukiuka maamudhi ya serikali kuu wakati wewe ni diwani.Ulitakiwa kujiuzulu kabla ya kuwatetea hao unaosema kwamba wanaonewa.Ulitakiwa kutetea serikali kuu kwa sababu it's ur boss.Uwemwangalifu sana. Usije ukaishia pabaya.

I know you and I love u
 
James Carvel is Democrat and Mary is Republican,Mary is Jame's wife.It's democracy.Zip ur mouth dude
 
kwamba wife wa mh. slaa ni ccm?! sasa kama ameshindwa kum-influence wife wake kwa sera za chama chake watz wengine inakuwaje? au sioni vizuri miye?

wewe vipi? wengine wakigombea kwa tiketi ya ccm wanaaandamwa wanakuwa gumzo na wanaonekana kioja.

Lakini mke wa kigogo wa chadema kugombea ccm, utasikia wakisema mwacheni atumie uhuru wake, eti hapo ndo inaonekana jinsi gani Slaa kakomaa kisiasa.

kwa kweli falsafa hii binafsi siilewi wana i-apply vipi?
 
Mimi nadhani hakuna ubaya wowote kwa mke wa Katibu wa CHADEMA kuwa Diwani wa CCM na hata kuwa Mbunge wa CCM.

Marehemu Chacha Wangwe alipokasirishwa na CHADEMA walipomwambia anatoa siri za chama chao, akawauliza kati ya yeye na Slaa nani anatoa siri. kwani yeye makamu Mwenyekiti akimpigia simu Katibu Mkuu, anapokea mwana CCM anasema Mzee anaoga..... Chacha alikuwa na vituko kweli.

Kwa demokrasia kukomaa nadhani masuala ya watu binafsi yawe binafsi tu la muhimu ni kutekeleza wajibu tu wa kila mmoja.

Wasiwasi mkubwa ni huyu mwanamke kutumiwa kama alipotumiwa wakati ule wa Sumaye kwa kutengeneza fumanizi bandia pale Dodoma dhidi ya Dokta Slaa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom