Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,918
- 31,160
Hakimu wa mahakama ya mwanzo Ukonga Ndevera Kihengu na wenzake Karani wa mahakama ya Ukonga Evelyne Mowo na karani wa mahesabu Victoria Mtasiwa wamefikishwa mahakama ya Hakimu Mkaazi Kisutu wakikabiliwa na mashitaka matatu likiwemo la kuomba rushwa ya Tsh 100,000.Bi Ndevera Kihengu ni mke wa aliyekuwa RPC mkoa wa Mwanza Kamanda Eliah Kihengu.
Bibi Ndevera Kihengu,Evelyne Mowo na Victoria Mtasiwa wote kwa pamoja walimshawishi Joyce Msaki awape rushwa ya Tsh 100,000/= iliwaweze kumpatia dhamana katika kesi inayomkabili mahakamani hapo [Ukonga].tayari hakimu Kihengu alishalamba kiasi cha tsh 40,000/= toka kwa Joyce Msaki.
Washitakiwa Hakimu kihengu na Victoria wako nje baada ya kukamilisha taratibu za dhamana,Karani Mowo yuko rumande baada ya kushindwa kukamilisha masharti ya dhamana.
Bibi Ndevera Kihengu,Evelyne Mowo na Victoria Mtasiwa wote kwa pamoja walimshawishi Joyce Msaki awape rushwa ya Tsh 100,000/= iliwaweze kumpatia dhamana katika kesi inayomkabili mahakamani hapo [Ukonga].tayari hakimu Kihengu alishalamba kiasi cha tsh 40,000/= toka kwa Joyce Msaki.
Washitakiwa Hakimu kihengu na Victoria wako nje baada ya kukamilisha taratibu za dhamana,Karani Mowo yuko rumande baada ya kushindwa kukamilisha masharti ya dhamana.