Mke mbishi

Utingo

JF-Expert Member
Dec 15, 2009
10,270
8,031
Wapendwa

ndoa ya rafiki na jirani yangu iko hati hati ya kuvunjika, kisa jamaa katafuta mke mdogo (ofcourse anasema dini yake inamruhusu). Niliwahi kumwonya mke hakunisikia...kisa jamaa amechoshwa na tabia ya ubishi aliyo nayo mkewe. Nimeishiwa ushauri wa kutoa maana hata mimi tabia ya mke kuwa mbishi kupita kiasi kwa mume siipendi though I feel pity to those little girls (watoto wao). Naomba kujazwa maneno kwa ajili ya kujaribu kumshauri jamaa na mke pia.

NB: Jamaa hajaoa bado, amepose idea na hiyo ni baada ya kuitisha vikao vingi vya wazazi wao ili kumwonya mke na mke ndiyo ubishi umezidi na ujeuri umeongezeka
 
Huyo mke mdogo akiwa mbishi zaidi au mdokozi ataongeza mke mwingine(kwa kuwa dini inamruhusu)?mimi nilidhani unaongeza mke kwa upendo siyo kumwadhibu mke aliyetangualia,lol....binadamu bwana, hamna aliyekamilika na ndoa ni kufunzana/kuwasiliana siyo kukomoana. kama ni mbishi kupita kiasi ina maana alimfahamu tangia wako wapenzi, kwanini alimuoa?
 
ngoja na mie niache ubishi manake dah! basi nampongeza sana rafiki yako kwa kupata small house.mungu aliyemruhusu kuoa mke mwingine amjaalie apate tabia mpya kwa mke mdogo,walau ya umalaya ili asiteseke na ubishi mara mbili kama anavyohofia BJ. ila awanusuru wote na magonjwa ya kileo kwa hisani ya bi mkubwa.
 
Huyo mke mdogo akiwa mbishi zaidi au mdokozi ataongeza mke mwingine(kwa kuwa dini inamruhusu)?mimi nilidhani unaongeza mke kwa upendo siyo kumwadhibu mke aliyetangualia,lol....binadamu bwana, hamna aliyekamilika na ndoa ni kufunzana/kuwasiliana siyo kukomoana. kama ni mbishi kupita kiasi ina maana alimfahamu tangia wako wapenzi, kwanini alimuoa?

kwa maelezo yake na kwa kuwa nimeishi nao kwa ukaribu kwa zaidi ya miaka nane sasa, mwanamke hakuwa hivyo huko nyuma.
 
Wapendwa

ndoa ya rafiki na jirani yangu iko hati hati ya kuvunjika, kisa jamaa katafuta mke mdogo (ofcourse anasema dini yake inamruhusu). Niliwahi kumwonya mke hakunisikia...kisa jamaa amechoshwa na tabia ya ubishi aliyo nayo mkewe. Nimeishiwa ushauri wa kutoa maana hata mimi tabia ya mke kuwa mbishi kupita kiasi kwa mume siipendi though I feel pity to those little girls (watoto wao). Naomba kujazwa maneno kwa ajili ya kujaribu kumshauri jamaa na mke pia.
Nyumba ndogo inapoza machungu
 
Wapendwa

ndoa ya rafiki na jirani yangu iko hati hati ya kuvunjika, kisa jamaa katafuta mke mdogo (ofcourse anasema dini yake inamruhusu). Niliwahi kumwonya mke hakunisikia...kisa jamaa amechoshwa na tabia ya ubishi aliyo nayo mkewe. Nimeishiwa ushauri wa kutoa maana hata mimi tabia ya mke kuwa mbishi kupita kiasi kwa mume siipendi though I feel pity to those little girls (watoto wao). Naomba kujazwa maneno kwa ajili ya kujaribu kumshauri jamaa na mke pia.





Ameoa kwa sababu dini inamruhusu au kwa sababu mke mbishi?

UMALAYA TU UNAMSUMBUA JAMAA.
NO JUSTFCATION ON IT...mwenzako akiwa na mapungufu nd anakupa tiket ya kudigi nje?BADALA YA KUREKEBISHANA?
 
je yeye hajabadilika miaka yote waliyoishi na mke hakuwa na sababu ya kumtafutia nyumba ndogo ........au leo anamtafutia sababu,kwasababu amemchoka au labda anaendelea kutafuta kilichokamilika ambacho hakipo vile vile ilihali yeye akiwa si mtimilifu.


kwa maelezo yake na kwa kuwa nimeishi nao kwa ukaribu kwa zaidi ya miaka nane sasa, mwanamke hakuwa hivyo huko nyuma.
 
je yeye hajabadilika miaka yote waliyoishi na mke hakuwa na sababu ya kumtafutia nyumba ndogo ........au leo anamtafutia sababu,kwasababu amemchoka au labda anaendelea kutafuta kilichokamilika ambacho hakipo vile vile ilihali yeye akiwa si mtimilifu.

hajaoa bado, amepose idea na hiyo ni baada ya kuitisha vikao vingi vya wazazi wao ili kumwonya mke na mke ndiyo ubishi umezidi na ujeuri umeongezeka
 
Kesi za aina hii huwa nakumbana nazo sana, mara nyingi ushauri wangu, kwa kifupi namshauri mume kutafuta sababu ya mkewe kuwa mbishi, kwa jinsi ninavyofahamu, mabadiliko ya kitabia kwa wanandoa hajaji hivihivi, ni lazima kuna mahali inaanzia, na akishajua sababu, itakuwa ni rahisi kwake kupata tiba ya tatizo hilo. kuoa mke wa pili au kuwa na nyumba ndogo hakusaidii kutibu tatizo, na badala yake kulikuza na wakati mwingine kujitafutia balaa, lisilo na mwisho.
Zipo sababu nyingi kutegemeana na mazingira yaliyowazunguka wanandoa, ambazo zinaweza kuchochea mke au mume kuwa mbishi........ ninachoweza kuwashauri ni kujikagua upya, hasa mume atafute sababu ya mkewe kuwa mbishi akiijua hiyo.... then itamsaidia kupata suluhu.
 
Kama hakuwa hivyo mwanzo then obvious kuna sababu zimemfanya abadilike,na zinaweza kuwa ni huyo huyo mume. Na hata kama sio hivyo,kwa nini mume akimbilie tu kusema ataoa mke mwingine kabla ya kutafuta mbinu ya kumbadilisha mkewe? Pengine hata ni huo umalaya wake na hao mabibi wadogo ndo umemfanya mama abadilike. Mume ajipeleleze ndani yake kwanza.
 
Back
Top Bottom