Mke kamkimbia jamaa yangu

kibenten

JF-Expert Member
Mar 12, 2018
499
507
Nina rafiki yangu dam dam kaoa mwaka huu mwezi wa pili,ndoa ya mkeka ya kiislam,kabla ya kuoana walikuwa kwenye mahusiano kwa miaka miwili.

Sasa jana umetokea ugomvi mdogo kisa mke alitaka jioni wale nyama na jamaa hakuagiza boda kupeleka iyo nyama ili ipikwe jioni.maisha yetu ni haya ya uswahilini katika hili jiji la Amos.

Sasa jamaa angu kabla ya haya mambo kutokea asubuh alikuwa amemwachia elf tano kwa ajili ya mboga tu maana kila kitu kipo ndani.sasa jamaa alimwambia kuwa nyama nimegairi tumia hiyo efu tano nilokwachia asubuh ununue mboga yoyote tule jioni mke hakumjibu chochote akakata simu.kufika usiku jamaa alirudi sa nne ana njaa ya atar kakuta mke kalala hajapika chochote jamaa akamaindi akamchapa kofi tatu tu.

Asubuh mapema jamaa huwa tunaenda nae kigamboni kufata mizigo ko alimwacha wife kalala,sa nne kakuta sms mke anasema KWAHERI NITUNZIE NGUO ZANGU UKIONA ZINAKUUDHI ZICHOME MOTO.

Kumpgia hapokei simu hata mi nkampigia hapokei simu yangu.

Ndo jamaa akawa anasema hii inshu ya kukuta mke hajapika imetokea mala mbili hii ni mala ya tatu sasa,na hizo siku zingine alikuwa anamuonya kwa maneno mke hasikii,,,
Tumepiga simu ukweni mama mkwe anasema hajamuona wala ndugu zake kwingine haonekani huko.

Leo mida ya sa nane kanitumia mimi sms anasema yupo kwa shoga yake ametoka kukata tiketi ili kesho aende singida kwa bibi ake eti hataki maisha hayo.

Jamaa hakawahi kumpgia jana ndo ilikuwa mala ya kwanza na anampenda kinoma uyu shemu.
shem ni under 24 jamaa ni 30s.

JAMAA ANAOMBA USHAURI AFANYAJE JUU YA HILI KEJELI SITAKI KAMA HUNA USHAURI TULIA.

(Samahanini kwa uandishi mbovu,mi nilivokuwa shule nilikuwa science pure so masuala ya imla,insha,nomino sijui vishaz tegemeo sivijui)
 
Kwa hiyo age miaka hii wanakuwa hawana akili ya maisha bado wadogo kiakili ingawa kimwili wameshakomaa.

Ni vema kijana atumie busara ya kumuelekeza taratibu kwa mahaba ataelewa haraka zaidi. Kwa umri wake yeye anatakiwa kuwa na experience ya akili za mabinti zina operate vipi ili aende nae kwa timing (ndio kuishi nao kwa akili kwenyewe).

Mambo madogo madogo kama hayo wala asiyape kipaumbele kwenye kichwa,mtu umerudi hajapika why ugombane nae,muamshe mwambie twenzetu tukatafute chakula my love ntazimia kwa hii njaa,fanya utani kabisa ila ndani ya nafsi yako unamuamsha na kumsumbua ili kesho ajue asipopika basi utamuamsha usiku mkatafute chakula.

Haina haja ya kugombana ataenda kuna umri atafika utaona automatically anaanza kuwa serious na mahusino yenu.

Hawa wa siku hizi hawapitishwi mafunzo ya unyago kuwaandaa kwaajiri ya ndoa tunaoa mabinti wamevurugwa akili hawapo serious na maisha wanamizaha mingi.
 
Eti nini! Hapana kwakweli acha akafuzwe na ulimwengu tu
Kwa hiyo age miaka hii wanakuwa hawana akili ya maisha bado wadogo kiakili ingawa kimwili wameshakomaa.

Ni vema kijana atumie busara ya kumuelekeza taratibu kwa mahaba ataelewa haraka zaidi. Kwa umri wake yeye anatakiwa kuwa na experience ya akili za mabinti zina operate vipi ili aende nae kwa timing (ndio kuishi nao kwa akili kwenyewe).

Mambo madogo madogo kama hayo wala asiyape kipaumbele kwenye kichwa,mtu umerudi hajapika why ugombane nae,muamshe mwambie twenzetu tukatafute chakula my love ntazimia kwa hii njaa,fanya utani kabisa ila ndani ya nafsi yako unamuamsha na kumsumbua ili kesho ajue asipopika basi utamuamsha usiku mkatafute chakula.

Haina haja ya kugombana ataenda kuna umri atafika utaona automatically anaanza kuwa serious na mahusino yenu.

Hawa wa siku hizi hawapitishwi mafunzo ya unyago kuwaandaa kwaajiri ya ndoa tunaoa mabinti wamevurugwa akili hawapo serious na maisha wanamizaha mingi.
 
Under 25 demu anakua na option kibao hata awe pisi mbovu.

Kwa stage hiyo jamaa ajifunze kuishi bila huyo mkewe, la sivyo tutarajie makubwa zaidi ya kuondoka nyumbani.

Na pia hawa mamanzi wadogo wadogo ukiwaoa hebu jaribu kuwazoesha life unalolimudu kwanza, hizi za kuacha kodi ya meza kubwa ndo inavunja ndoa za watu, hawa mabinti wakikupenda huwa wanakubali kila kitu em muweke kwenye angle ya kutokufilisi.
Kujimwambafy kunawaua wengi.

Enewei ai wishi yu gudi laki.

Kuepuka stress za hivo basi ndgu yetu Liverpool VPN ana ushauri mzuri tu USIOE.
 
Kwa hiyo age miaka hii wanakuwa hawana akili ya maisha bado wadogo kiakili ingawa kimwili wameshakomaa.

Ni vema kijana atumie busara ya kumuelekeza taratibu kwa mahaba ataelewa haraka zaidi. Kwa umri wake yeye anatakiwa kuwa na experience ya akili za mabinti zina operate vipi ili aende nae kwa timing (ndio kuishi nao kwa akili kwenyewe).

Mambo madogo madogo kama hayo wala asiyape kipaumbele kwenye kichwa,mtu umerudi hajapika why ugombane nae,muamshe mwambie twenzetu tukatafute chakula my love ntazimia kwa hii njaa,fanya utani kabisa ila ndani ya nafsi yako unamuamsha na kumsumbua ili kesho ajue asipopika basi utamuamsha usiku mkatafute chakula.

Haina haja ya kugombana ataenda kuna umri atafika utaona automatically anaanza kuwa serious na mahusino yenu.

Hawa wa siku hizi hawapitishwi mafunzo ya unyago kuwaandaa kwaajiri ya ndoa tunaoa mabinti wamevurugwa akili hawapo serious na maisha wanamizaha mingi.
sa nne usiku akatafute chakulamitaa tunayoishi nmekwambia uswahilini huku keko panya road kibao,,na ukumbuke bro hii si mala ya kwanza.

but asante kwa ushauri kuna vitu nimejifunza apo ntamfikishia.
 
Under 25 demu anakua na option kibao hata awe pisi mbovu.

Kwa stage hiyo jamaa ajifunze kuishi bila huyo mkewe, la sivyo tutarajie makubwa zaidi ya kuondoka nyumbani.

Na pia hawa mamanzi wadogo wadogo ukiwaoa hebu jaribu kuwazoesha life unalolimudu kwanza, hizi za kuacha kodi ya meza kubwa ndo inavunja ndoa za watu, hawa mabinti wakikupenda huwa wanakubali kila kitu em muweke kwenye angle ya kutokufilisi.
Kujimwambafy kunawaua wengi.

Enewei ai wishi yu gudi laki.

Kuepuka stress za hivo basi ndgu yetu Liverpool VPN ana ushauri mzuri tu USIOE.
shukurani broo
 
😅 sasa mwanaume mzima miaka 30+ unamlilia mwanamke arudi tena mwanamke mwenyew hana akili na ndoa yenyew ya mkeka... Wanaume sikuhiz mmekua wapumbavu sana, mnalilia mapenz kama wanawake.
The moment mwanamke anakuambia naondoka, the same time unaingiza mwanamke mwingine ndani...
 
23 Reactions
Reply
Back
Top Bottom