Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Mke amkata ulimi mume wakibusiana
Wednesday, 08 December 2010 18:53 newsroom
LONDON, Uingereza
MWANAUME mwenye umri wa miaka 79 amengatwa hadi kukatwa ulimi na mkewe, wakati akimpa busu la kumtakia usiku mwema.
Habari zilisema mume huyo Willard Luenders, baada ya kukatwa ulimi aliweza kumunyamunya maneno na kuita gari la wagonjwa. Luenders anaishi Wauwatosa, Wisconsin. Taarifa zilisema baada ya Luenders kufikishwa hospitali, madaktari walihitaji kipande cha ulimi kilichokatwa kwa ajili ya kukirejesha mahali pake. Hata hivyo polisi walipofika nyumbani kwa Luenders, Karen (57), alikataa kuwaruhusu polisi hao kuingia ndani ya nyumba, ambapo alichukua kahawa ya moto na kuwamwagia.
Taarifa zilisema polisi hao walitumia nguvu kuingia ndani na walifanikiwa kukipata kipande cha ulimi kilichokatwa na Karen, walikichukua na kukipeleka hospitali kwa ajili ya kujaribu kukirejeshea kwa Luenders. Msemaji wa polisi Terry Meyer alisema wanandoa hao kabla ya kungatana ulimi walikuwa wakiimba nyimbo za krismas, huku wakiwa kwenye hatua za kwenda kulala. Alisema Luenders aliamua kumpa mkewe busu la kumtakia usiku mwema, lakini Karen alingata ulimi na kuukata kipande. Meyer alisema Karen amekamatwa na amefunguliwa mashitaka ya kufanya vurugu nyumbani, na pia imeamuliwa akapimwe akili. Luenders katika taarifa yake ya maandishi polisi, alielezea tukio lilianza wakati yeye alipokuwa akienda bafuni na mkewe alikuwa akienda chooni. Alisema alipojaribu kumbusu mkewe alishangaa kushikwa sehemu nyeti na kungatwa ulimi hadi kutatika kipande. Luenders alisema katika siku za karibuni mkewe amekuwa akifanya vitu vya ajabu, ikiwemo kuzungumza mambo ya mizimu.
Wednesday, 08 December 2010 18:53 newsroom
LONDON, Uingereza
MWANAUME mwenye umri wa miaka 79 amengatwa hadi kukatwa ulimi na mkewe, wakati akimpa busu la kumtakia usiku mwema.
Habari zilisema mume huyo Willard Luenders, baada ya kukatwa ulimi aliweza kumunyamunya maneno na kuita gari la wagonjwa. Luenders anaishi Wauwatosa, Wisconsin. Taarifa zilisema baada ya Luenders kufikishwa hospitali, madaktari walihitaji kipande cha ulimi kilichokatwa kwa ajili ya kukirejesha mahali pake. Hata hivyo polisi walipofika nyumbani kwa Luenders, Karen (57), alikataa kuwaruhusu polisi hao kuingia ndani ya nyumba, ambapo alichukua kahawa ya moto na kuwamwagia.
Taarifa zilisema polisi hao walitumia nguvu kuingia ndani na walifanikiwa kukipata kipande cha ulimi kilichokatwa na Karen, walikichukua na kukipeleka hospitali kwa ajili ya kujaribu kukirejeshea kwa Luenders. Msemaji wa polisi Terry Meyer alisema wanandoa hao kabla ya kungatana ulimi walikuwa wakiimba nyimbo za krismas, huku wakiwa kwenye hatua za kwenda kulala. Alisema Luenders aliamua kumpa mkewe busu la kumtakia usiku mwema, lakini Karen alingata ulimi na kuukata kipande. Meyer alisema Karen amekamatwa na amefunguliwa mashitaka ya kufanya vurugu nyumbani, na pia imeamuliwa akapimwe akili. Luenders katika taarifa yake ya maandishi polisi, alielezea tukio lilianza wakati yeye alipokuwa akienda bafuni na mkewe alikuwa akienda chooni. Alisema alipojaribu kumbusu mkewe alishangaa kushikwa sehemu nyeti na kungatwa ulimi hadi kutatika kipande. Luenders alisema katika siku za karibuni mkewe amekuwa akifanya vitu vya ajabu, ikiwemo kuzungumza mambo ya mizimu.