Mkate wa ufuta

Mrs Kharusy

JF-Expert Member
Sep 23, 2013
1,244
670
Wana jiko!! Ni mda sasa nimekua nikienjoy mapishi ya chef wetu farkhina. Naomba nami niwaekeeni kaujuzi hapa wa kutengeneza mkate simple wa ufuta!!

Mahitaji;
Unga vikombe 2
Maziwa kikombe 1na robo
Samli aseel vijiko vya kula 3
Mafuta vijiko vwa kula 4
Sukari vijiko 4-5
Hamira kijiko 1
Mayai 2
Iliki Kijiko 1
Ufuta kiasi

Jinsi ya kupika.
Changanya vyote kwenye bakuli safi
Kosha mikono uchanganye na uupigepige vizur hadi uwe laini.
Unatakiwa uwe mzito kiasi km ni mgumu weka maji kidogo ili ulainike
Chukua trey yako, weka baking paper
Mimina mchanganyiko na unyunyize ufuta juu
Wachaa uumuke, choma kwa dkk km 20
Utoe na uuwache upoe.
Mkate tayar kwa kuliwa

Pic zinagoma au mchina wangu haukubali kuattach!! Lol
 
Ukitaka kupika kwenye jiko la mkaa, hakikisha moto ni kidogo mno na mikono ni misafi wakati wote.

Tenga maji ya chumvi kiasi na uweke pembeni.

Nyunyizia haya maji juu ya kikaango n uache yakauke kisha chota mchanganyiko kwa mkono na uutandaze.

Nyunyizia ufute kwa juu na ufunike kwa mfiniko kama wa saucepan vile.

Hauhitaji kugeuza upande wa pili.
 
Dear huu sio km uliouongelea ww.
Huu ukishaupiga unauweka wote kwenye trey au sufuria. Unaacha unaumuka unabake kwenye kuka km cake
 
Ukitaka kupika kwenye jiko la mkaa, hakikisha moto ni kidogo mno na mikono ni misafi wakati wote.

Tenga maji ya chumvi kiasi na uweke pembeni.

Nyunyizia haya maji juu ya kikaango n uache yakauke kisha chota mchanganyiko kwa mkono na uutandaze.

Nyunyizia ufute kwa juu na ufunike kwa mfiniko kama wa saucepan vile.

Hauhitaji kugeuza upande wa pili.

Kwenye kuupiga shurti uuvalie suruali mi nna suruali special kwa kuupiga.
Hii njia mi naijua as sina oven
 
Picha ingekubali ungeona muonekano wake ungeelewa mara moja Karucee . Na ladha yake km cake nzuri sana try
 
Last edited by a moderator:

Attachments

  • 1400769641080.jpg
    1400769641080.jpg
    85.4 KB · Views: 224
Kwenye kuupiga shurti uuvalie suruali mi nna suruali special kwa kuupiga.
Hii njia mi naijua as sina oven

Hahahhahha amu huishi vituko leo umekuja na mpyaa mie huwa napiga goti tu naupiga kisawa sawa ila nkikanda unga ndo lazma nivae tight nsije picha picha watu
 
Last edited by a moderator:
Hahahhahha amu huishi vituko leo umekuja na mpyaa mie huwa napiga goti tu naupiga kisawa sawa ila nkikanda unga ndo lazma nivae tight nsije picha picha watu

Ahahhahaha. Huu hauna hata kutumia nguvu kiasi hicho.
Unaweza kutumia mashine ya cake.
 
Last edited by a moderator:
Hahahhahha amu huishi vituko leo umekuja na mpyaa mie huwa napiga goti tu naupiga kisawa sawa ila nkikanda unga ndo lazma nivae tight nsije picha picha watu

Ha ha nimegundua why chapati za jana zilinitosa as sikuvaa pajama langu
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom