Mkataba wa Uchimbaji wa Almasi kati ya Botswana na Muwekezaji vs wa Tanzania na wawekezaji

Ta Muganyizi

R I P
Oct 19, 2010
5,361
2,732
Katika kutafakari sababu za umaskini wa nchi yangu Tanzania, nikajikuta nashangaa hasa baada ya kuangalia raslimali zilizoko nchini hasa madini. Nikajiuliza wenzetu wa Botswana madini yao yanawafaidisha kuliko sisi hapa Tanzania tatizo ni nini? Nikaweza kupata mkataba mmojawapo wa uchimbaji madini kati ya Serikali ya Botswana na Muwekezaji (De Beers)

Kilichonifurahisha makubalinao ya uchimbaji na faida itokanayo na uuzaji wa almasi hiyo yalitangazwa ka Press Release kwa wananhci wote ili wajue kinachoendelea. Mkataba huo ninauweka hapa kama attachment View attachment Botswana_De_Beers_Sales_Agreement_Press_Release_-_.pdf ili kila mwenyekutaka kuusoma ausome pia nitaweka link.

http://www.debeersgroup.com/ImageVa...De_Beers_Sales_Agreement_Press_Release_-_.PDF

Baadhi ya maneno kwenye mkataba huo ni haya

1. Debswana is a 50/50 mining joint venture between Botswana and De Beers
2. Diamond Trading Company is the wholly-owned distribution arm of De Beers
3. Diamond Trading Company Botswana is a 50/50 sales joint venture between Botswana and De Beers

Nilifarijika kuona walau nchi inakomaa 50/50 na muwekezaji na kugundua kumbe inawezekana. Sasa naomba msaada mmoja kwa GT walioko hapa JF, mnitumie walau Press Release moja inayoonesha makubaliano kati ya muwekezaji mmojawapo nchini na inayoonesha asilimia ipatayo nchi kutokana na mauzo ya madini mojawapo kati ya yote tuliyonayo nchini. Asanteni
 
Kama mikataba ya kwetu na wawekezaji husainiwa notelini tena nje ya nchi kutangaziwa sijui kama inawezekana na ukute ni nyaraka za siri na zitakuwa zimegongwa ile seal ya CONFIDENTIAL
 
Kama hili lingewezekana tungekuwa mbali ....hasa kama tungefanya hivi kule Mwadui na Geita....tangu enzi hizo
 
Tutasubiri sana

Sisi tunauza pembe za ndovu yani viongozi wa chama cha mapinduzi na serikali wanafanya biashara haramu tena kwa kuua tembo wetu na kutorosha wanyama hai, sizani kama wananchi watapewa nafasi ya kujua deal za ndani za wakubwa wasio hata na tone la huruma.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Botswana waache Mungu amewajalia kuwa na viongozi waadilifu na mali za Serikali. Katiaka safari zangu huko Botswana nchi ni jangwa lakini hakuna siku maji yanakatika. Sasa hivi wana mpango wa kuchukua maji mto Chobe ambao unatenganisha mpaka kati ya Zambia na Botswana na kuyapeleka Gaborone ambapo ni umbali wa km 1000. Bomba lenyewe litakuwa na diameter ya mita mbili. Hii ni tahadhari kama dams zitakauka kwa ajili ya ukame
 
Sisi tunauza pembe za ndovu yani viongozi wa chama cha mapinduzi na serikali wanafanya biashara haramu tena kwa kuua tembo wetu na kutorosha wanyama hai, sizani kama wananchi watapewa nafasi ya kujua deal za ndani za wakubwa wasio hata na tone la huruma.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Pembe 569 ni sawa na Tembo 284, kwanin Kinana hata kama sio zake hizo pembe asikamatwe akaeleza mteja wake ni nani??

Hivi Leo nikikutwa na madawa ya kulevya Airport nikasema kua mi nimetumwa tu nibebe, lakini sio yangu nitaachiwa??

Are we real serious?
 
Hivi ni nani alituroga jamani????????Amini nakwambia,50/50??hiyo ni ndoto mkuu, hutaiona katika mikataba yetu,hata kama sijawah kuiona.Sana sana utakuta sijui 3% haaaaa!!!
 
Kwetu Tanzania ni ngumu kutokea tugawane 50/50 viongozi wetu wanatanguliziwa 10% U Swiss unafikiria hapo kutatokea nini ?
 
Botswana diamond inatembea kwa vingola na wanajeshi wakiwa na magari si chini ya matano. Najua wengi hawataamini lakini nilishawahi kusimama kwenye mataa yapo Gaborone na Rais Mstaafu Festus Mghae wakati Diamond inapita kuelekea Airport. Wanaheshimu Diamond kuliko.
 
Muganyizi, unadhani hawa wahalifu na majingili wa uchumi na rasilimali zetu hawajui kuwa inawezekana kuwa na 50/50?

Tatizo la msingi ni mfumo wetu (system) na sheria zetu. Kuna templates kibao za mikataba kwenye mitandao lakini si unaona nini kilichoandikwa (mkataba wa) Buzwagi, Richmond na Kiwira (kuzitaja chache ndogo).

Mwisho ujue hivi, Watanzania na hasa viongozi wetu hawajifunzagi mema. Wanajifunzaga mabaya tu, ila mema ni kama vile imetokea bahati mbaya!
 
Bila kuing'oa CCM madarakani tutaendelea kuteseka tu. Madini tunayo ya kutosha lakini ukimuuliza hata rais kwa nini sisi ni maskini atakwambia hata yeye hajui. Tanzania hatuna viongozi bali tuna bora viongozi. 2015 jitokezeni kwa wingi jamani tupige kura kukikataa CCM maana tumechoka kupora raslimali zetu na mafisadi wa CCM
Katika kutafakari sababu za umaskini wa nchi yangu Tanzania, nikajikuta nashangaa hasa baada ya kuangalia raslimali zilizoko nchini hasa madini. Nikajiuliza wenzetu wa Botswana madini yao yanawafaidisha kuliko sisi hapa Tanzania tatizo ni nini? Nikaweza kupata mkataba mmojawapo wa uchimbaji madini kati ya Serikali ya Botswana na Muwekezaji (De Beers)

Kilichonifurahisha makubalinao ya uchimbaji na faida itokanayo na uuzaji wa almasi hiyo yalitangazwa ka Press Release kwa wananhci wote ili wajue kinachoendelea. Mkataba huo ninauweka hapa kama attachment View attachment 71535 ili kila mwenyekutaka kuusoma ausome pia nitaweka link.

http://www.debeersgroup.com/ImageVa...De_Beers_Sales_Agreement_Press_Release_-_.PDF

Baadhi ya maneno kwenye mkataba huo ni haya

1. Debswana is a 50/50 mining joint venture between Botswana and De Beers
2. Diamond Trading Company is the wholly-owned distribution arm of De Beers
3. Diamond Trading Company Botswana is a 50/50 sales joint venture between Botswana and De Beers

Nilifarijika kuona walau nchi inakomaa 50/50 na muwekezaji na kugundua kumbe inawezekana. Sasa naomba msaada mmoja kwa GT walioko hapa JF, mnitumie walau Press Release moja inayoonesha makubaliano kati ya muwekezaji mmojawapo nchini na inayoonesha asilimia ipatayo nchi kutokana na mauzo ya madini mojawapo kati ya yote tuliyonayo nchini. Asanteni
 
Huwezi kuzipata taarifa za tanzania kuhusu madini, utapata hasard za bunge na umbea mwingine mwiiingi usiokuwa na maana. Tusubiri jinamizi CCM lizeeke lenyewe ndo tuanze kupanga upya. Kwa sasa naona kama limeshindakana!! Linatumia gharama kuubwa kubakia madarakani!
 
Huwezi kuzipata taarifa za tanzania kuhusu madini, utapata hasard za bunge na umbea mwingine mwiiingi usiokuwa na maana. Tusubiri jinamizi CCM lizeeke lenyewe ndo tuanze kupanga upya. Kwa sasa naona kama limeshindakana!! Linatumia gharama kuubwa kubakia madarakani!

Mbona wenzetu wameweka wazi
 
Tanzania Tanzania nchi yenye mali nyingi, watu wengi wa ulaya wanakulilia sana. Sasa hivi sio wa ulaya tu hata weusi wa hapahapa tanzania wanaikamua
 
Katika kutafakari sababu za umaskini wa nchi yangu Tanzania, nikajikuta nashangaa hasa baada ya kuangalia raslimali zilizoko nchini hasa madini. Nikajiuliza wenzetu wa Botswana madini yao yanawafaidisha kuliko sisi hapa Tanzania tatizo ni nini? Nikaweza kupata mkataba mmojawapo wa uchimbaji madini kati ya Serikali ya Botswana na Muwekezaji (De Beers)

Kilichonifurahisha makubalinao ya uchimbaji na faida itokanayo na uuzaji wa almasi hiyo yalitangazwa ka Press Release kwa wananhci wote ili wajue kinachoendelea. Mkataba huo ninauweka hapa kama attachment View attachment 71535 ili kila mwenyekutaka kuusoma ausome pia nitaweka link.

http://www.debeersgroup.com/ImageVa...De_Beers_Sales_Agreement_Press_Release_-_.PDF

Baadhi ya maneno kwenye mkataba huo ni haya

1. Debswana is a 50/50 mining joint venture between Botswana and De Beers
2. Diamond Trading Company is the wholly-owned distribution arm of De Beers
3. Diamond Trading Company Botswana is a 50/50 sales joint venture between Botswana and De Beers

Nilifarijika kuona walau nchi inakomaa 50/50 na muwekezaji na kugundua kumbe inawezekana. Sasa naomba msaada mmoja kwa GT walioko hapa JF, mnitumie walau Press Release moja inayoonesha makubaliano kati ya muwekezaji mmojawapo nchini na inayoonesha asilimia ipatayo nchi kutokana na mauzo ya madini mojawapo kati ya yote tuliyonayo nchini. Asanteni
At least you are a bad example
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom