Mkataba wa TRL (TRC)

Mpita Njia

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
6,997
1,163
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ameushtukia mkataba baina ya Serikali ya Kampuni ya Rites ya India kuhusu ukodishwaji wa lililokuwa Shirika la Reli nchini (TRC).

Akizungumza na wafanyakazi wa Kampuni ya Reli (TRL), iliyoundwa baaya ya kukodishwa kwa TRC, Pinda alisema mkataba huo una mushkeli, kwani kuna mambo ambayo hayaelewi jinsi yanavyoendeshwa.

Akitoa mfano, alisema kuwa wakati TRC ikikaribia kumaliza shughuli zake, ilieleza kuwa ina injini zaidi ya 90, lakini mara baada ya TRL kuanza kazi, ilieleza kuwa kuna injini takriban 50 tu.

Pia, wafanyakazi wa TRL wamesema kuwa mwekezaji huyo hakujali kukarabati vifaa hivyo vilivyopo, badala yake alikwenda kukodi injini nyingine kwenye kampuni yake ya Rites na tayari zimeshaingia injini saba ambazo zinalipiwa ‘capacity charge’ ya sh 600,000 kila siku hata kama hazifanyi kazi.

Jambo hilo limemfanya Pinda auone mkataka huo kama ile ya umeme ambayop inalikamua Tanesco. Wafanyakazi wa TRL wameshamuomba Pinda kuwa mkataba huo nao upelekwe Bungeni ukachunguzwe.

 
India kwenyewe reli yao imewashinda,nenda huko huone abiria wao wanapanda mpaka kwenye mapaa?

Hili wazo la kuwapa wahindi lilitoka wapi?
 
Unauliza hilo wazo lilitoka wapi,jamani hiyo ni kale katen percent ndio kanako tuangamiza.Lakini jamani kauli ya Pinda ameamua nini juu ya sakata hili?Unajua kwa sisi watu wa TBR reli ndio njia muhimu kuliko usafiri wa aina yoyote ile.Pinda lishughulikie suala hili mapema.
 
Waanzishe kesi nyingine kutaka kuvunja mkataba itakayowagharimu mamia ya mamilioni ya shilingi huku wakisaini mikataba mingine mibovu, ambayo itakuja kugunduliwa baadaye na wakuu wengine watakaoanzisha kesi nyingine kutaka kuvunja mkataba itakayogharimu mamilioni ya dola, day in day out.

Kusaini, kuvunja, kusaini, kuvunja.

as long as some people get their 10% who cares if Tanzania loses billions of dollars.

That is where we are, plain and simple.
 
inauma sana na nakumbuka wakato wa mchakato wa kupata hii zabuni...walikuwepo south Africa Railways na Mozambique...SAL walikuwa wanaelekea ki win tender nikashangaa ghafla wamepigwa chini inasikitisha sana.....maana nahisi wenzetu SAL wako juu hata kwa technologia na wako serious kwenye uwekezaji....hawa nina mashaka naoo
 
Huu mkataba wa TRL was doomed from the beginning. By the time hawa wahindi wanaondoka shirika litakuwa taabani. Nasikia wamekuwa wakuchukua expensive parts na kupeleka India.
Ni wakati muafaka viongozi wetu wakafungua macho, wafanyakazi wameonyesha njia.
 
inauma sana na nakumbuka wakato wa mchakato wa kupata hii zabuni...walikuwepo south Africa Railways na Mozambique...SAL walikuwa wanaelekea ki win tender nikashangaa ghafla wamepigwa chini inasikitisha sana.....maana nahisi wenzetu SAR wako juu hata kwa technologia na wako serious kwenye uwekezaji....hawa nina mashaka naoo

Wawekezaji wa SA binafsi nina wasi wasi nao sana, angalia walivyotaka filisi ATC....kaburu balaa hacheki na nyani...
 
Nchi masikini zimevamia mambo ya kubinafsisha mashirika ya umma,hili ndio tatizo ambalo baadhi ya nchi masikini imepinga hatua hii,lakini Tanzania chini ya Mkapa alikuwa akifanya juu chini amalize kuyaondoa mashirika yote ndani ya mkono wa serikali,huku akipatiwa na kuweka hisa yake.Kumbuka Mkapa ni mfanya biashara wa ikulu.

Shirika la Umeme Shirika la Usafiri shirika la anga, bahari na Reli ni moja ya mihimili mikuu ya Nchi ,ni mambo ambayo shirika binafsi likihama au kufilisika basi ni tatizo kubwa kwa nchi nzima,ila mashirika haya kuwepo ndani ya Serikali basi ni vizuri japo kutatokea matatizo madogo madogo lakini linaweza kuboreshwa na kuwa na kiwango cha kimataifa ikiwa usimamizi utakuwa mzuri hata kama mameneja wanaweza kutoka nchi za nje maana hata waTanzania wengine wanafanya kazi nchi za nje kwenye nafasi nyeti hivyo si vibaya nafasi nyeti za hapa napo tukawapatia wenye kuwaona watatimiza wajibu wao hata kama ni wazungu mbona makocha tunawakodi kutoka nje ?.
 
india walitusamehe madeni kwa sharti la kupewa reli..wakati rais wao alipokuja hapa akiitwa RAMSUNA RAO...kimsingi hawana uwezo na hata reli yao huko india kila siku ni ajali na wanakufa wengi..hawana teknelojia ya maana...bora wangewapa wajerumani au wamarekani amabao waliomba wakajitoa.....

kinachoniuma zaidi hajakarabati chochote kwa kuwa kimsingi wahindi huwa hawangalii ubora wao kwao faida.....zaidi kibaya amefunga reli ya TANGA wakati huu muhimu ambako bandari ya salama imeelemewa...kwani kama reli ya tanga ingekuwa functional..mizigo iliyozidi dar ingeteremshiwa tanga hasa inayoenda kanda ya kaskazini na baadhi ya dar es salaam na ingeweza kupelekwa na reli toka tanga hadi arusha au dar...pia kuna reli ya taveta ambayo ingeweza kuchukua mizigo mingine toka MOMBASA...
 
Unajua ukiangalia hawa jamaa ni waendeshaji, manake sio wawekezaji au nimekosea kusoma kale kadondoo ka mkataba kao?? Inawezekana mimi ndio sikuelewa huu mkataba wao lakini umefananafanana na ule wa NetGroup pale Samora Avenue zamani (sasa Ubungo).

Ni kwamba sielewi elewi hii maneno Wakuu..............
 
Unajua ukiangalia hawa jamaa ni waendeshaji, manake sio wawekezaji au nimekosea kusoma kale kadondoo ka mkataba kao?? Inawezekana mimi ndio sikuelewa huu mkataba wao lakini umefananafanana na ule wa NetGroup pale Samora Avenue zamani (sasa Ubungo).

Ni kwamba sielewi elewi hii maneno Wakuu..............


...mkuu morani upo right...hawa jamaa wamepewa concession ya kuendesha shirika kwa miaka 25..kama wawekezaji...lakini morani upo right kwani pamoja na kuwa walitakiwa waingize karibu dola milioni 100 kwenye shirika..lakini KWA MUELEKEO WAO NI KAMA WA WAENDESHAJI...wanategemea income ya shirika ndio iliendeshe...

kimsingi kama wawekezaji hawakutakiwa kusema hawana pesa za kulipa mishahara kwa kuwa shirika halina pesa..wakati inajulikana wazi kuwa wao ndio walitakiwa kuongeza mtaji kwenye shirika ambao pamoja na mambo mengine ungeongeza mishahara....na ndio maana serikali kabla ya kuwapa shirika ilipunguza wafanyakazi ili wabaki wachache muwekezaji aweze kuwalipa vema!!!
 
inauma sana na nakumbuka wakato wa mchakato wa kupata hii zabuni...walikuwepo south Africa Railways na Mozambique...SAL walikuwa wanaelekea ki win tender nikashangaa ghafla wamepigwa chini inasikitisha sana.....maana nahisi wenzetu SAL wako juu hata kwa technologia na wako serious kwenye uwekezaji....hawa nina mashaka naoo

Kuhusu hui mkkataba, wafanyakazi wa TRL wamewataja viongozi ambao wameiingiza mkenge serikali.

hao ni:
Waziri wa Miundombuni, Andrew Chenge,
Abdallah Kigoda,
Profesa Mark Mwandosya,
Linford Mboma na
Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa
 
Mkuu Philemon, hapo ndipo penyewe.... Manake jamaa wanavyofanya kazi inaonekana kama vile wao ni waendeshaji na sio wawekezaji. Tukumbuke kuwa Serikali bado inafanya kazi kutafuta fedha za kuikarabati reli/treni (mfano ni recent grant/loan from WB).....

Bottom line ni kwamba hawa jamaa wa Rites wanajua kilichokuwa kwenye mkataba na mapungufu yake na ndicho wanachokitumia katika kuendelea kumnyonga mTanzania.... Kwa vile tupo kwenye dunia ya "Survival for the fittest" mimi lawama kubwa sio kwake Rites, mimi najilaumu mimi (yaani mTanzania) niliyetayarisha mkataba wa kuninyonga mimi (yap cat eat cat system hapo).... Mpita njia hapo juu amesema mchawi ni nani, sisemi nakubali lakini akili yangu inanituma kwamba kuna zaidi wanachojua wafanyakazi ambacho sisi wengine huenda hatuwezi hata kuki imagine.......

Yetu macho labda kuanzia 08 April kule Dodoma wabunge wetu watatupia japo jicho ya sunna huku mahali ambapo ni muhimu kwa Taifa letu.....
 
mara Ya Kwanza Rites ...walikuja Tanzania Miaka Kama 5 Iliyopita Kwa Mkataba Maalum Wa Kiufundi Uliofadhiliwa Na Bank Ya Dunia[100 Wagons Rehabilitation Project]...wakati Serikali Inatafuta Mbia Wa Kuendesha Na Kuwekeza Trc...nao Wakaamua Kuomba ...jambo Hili Lilifanya Makampuni Mengine Yajitoe Kwa Sababu Kimsingi Tayari Rites Walikuwa Na Mkataba Wa Kiufundi Na Serikali Trc..kwa Hiyo Ushiriki Wao Kwenye Tenda Uliwaogofya Washiriki Wengine Kuhisi Haki Haitatendeka Kwa Kuwa Rites Walikuwa Pia Washauri Wa Kiufundi Kwenye Kurugenzi Ya Trc Wakati Huo..ndio Maana Washiriki Wa Tenda Ile Woote Walijitoa Ikabakia Rites Peke Yao...

Kumbukeni Rites Kwa Kiasi Kikubwa Walisaidiwa Na Wahindi Wazawa ...andy Chande..na Subash Patel Kushinda Hii Tenda ..na Hadi Sasa Subash Patel Kupitia Kampuni Yake Ya Mm Grooup Ana Interest Kwenye Trl[through Rites]..chende Pia Ana Interest Lakini Sasa Sina Uhakika Sana Hasa Baada Ya Kampuni Yake Ya Gapco Ambayo Ilikuwa Pia Iwe Mbia Au Ni Mbia Wa Rites Kupata Matatizo Na Bank.........

Hao Wenyeji Wa Rites Subash ..mnajua Uhusiano Wake...na Chende Mnajua Uhusiano Wake Na Makampuni Ya Serikali Kama Njumbe Kwenye Bodi Nyingi...
 
Philemon, you are not serious Mkulu...... Ina maana walikuwa washauri wa TRC na kisha wakashiriki mchakato wa kutafuta muzimwaji (inaitwa kuwekeza ee) shirika hilo hilo.....

Halafu tunasema Madiwani wenye makampuni hawaruhusiwi ku tenda kwa kazi za halmashauri?? Duh, kaazi kweli kweli.....

Yaani jamaa walitayarisha mkataba/vigezo vya mwekezaji pale TRC, kisha wakaomba kazi na kisha wakaishauri TRC (technical advisor, usisahau hii cheo hapa) kujipa pasi........ Kweli hujafa hujaumbika....

On top of that wale bidders wengine wakaliona hili wakaamua kujitoa (walisema why?) and yet we proceeded with the whole process and gave the mighty TRC to Rites......

I rest my case, this is too much for my small head....

Mkuu Phillemon, asante sana kwa kunifungua macho........

Mungu Ibariki Tanzania na waTanzania............
 
MUHINDI ALIYEKUWA AKISIMAMIA HUO MRADI WA KUKARABATI MABEHEWA NA KUISHAURI MANAGEMENT KUPITIA HUO MKOPO WA BANK YA DUNIA KATI YA MWAKA 2002 HADI 2006 KUTOKA KAMPUNI YA RITES ..ANAITWA ENGNEER MUKESH..NA NDIE ALIYEHUSIKA KUANDAA SOME TECHNICALITIES...NA BAADAYE KWA KUSHIRIKIANA NA SUBASH PATEL NA CHANDE ..WAKAISHAURI RITES INUNUE TRC....

KWA SASA ENGENEER MUKESH AMERUDI TENA BAADA YA ZOEZI KUKAMILIKA AKIWA SASA NDIYE MKURUGENZI WA UFUNDI WA TRL...[CHIEF MECHANICAL ENGNEER...]WA TRL...

KWA KIASI KIKUBWA HUJUMA ZA KULIFANYA HILI SHIRIKA LA UMA KIYUMBE NA HATIMAYE KUWA MZIGO KWA SERIKALI HADI KUAMUA LIUZWE ZILIFANYWA NA HAWA WAHINDI WAKISHIRIKIANA NA SUBASH NA ANDY KAMA MWENYEKITI WA BODI NA HAWA KINA MBOMA KWA KUJUA AU KUTOJUA ..HASA PALE WALIPOKATIZA SAFARI ZA RELI ZIISHIE DODOMA ...MZIGO UKAWA MKUBWA KWA SHIRIKA KULIPIA WASAFIRI..NA MIZIGO MABASI HADI DODOMA...WASWAHILI WENZETU WAO WALIFAIDIKA KWA KUPEWA COMMISSION NA MAKAMPUNI YA USAFIRI AMBAYO YALIPATA KAZI KUPELEKA WASAFIRI NA MIZIGO DODOMA....NA HAPO SHIRIKA LIKAZIDI KUYUMBA KWA NAKISI YAO KUWA KUBWA...KUTOKANA NA KULIPA GHARAMA KUBWA HIZO NA ZILE ZA MAFUTA AMBAZO WALIKUWA WAKINUNUA KWA PESA TASLIM[BANKERS CHEQUE]..KUTOKA GAPCO AMBAYO NI KAMPINI YA MWENYEKITI WAO WA BODI ANDY CHANDE.....IKAWA HOOI KIPESA ...IKABIDI SERIKALI YA AWAMU YA NNE ILIPOINGIA IKAKUBALI MKATABA UANZE KAZI..UKISAINIWA NA CHENGE AMBAYE NDIYE PIA ALIYEDRAFT MKATABA UPANDE WA SERIKALI WAKATI AKIWA MWANASHERIA MKUU AWAMU YA TATU...

MKITAKA KUJUA RITES WALIFANYA HUJUMA MAKUSUDI WAKISHIRIKIANA NA MA ENGENEER WAZALENDO KUSHAURI NJIA YA RELI YA DODOMA TO DAR ILIKUWA MBOVU..SHANGAA KUWA NI HAO HAO TENA WIKI MBILI TU BAADA YA KUINGIA TENA BILA UKARABATI WA AINA YEYOTE ..WALIANZISHA SAFARI ZA RELI KUANZIA DAR [MABEHEWA NA ABIRIA].......

TENA MASIKINI RAIS WETU JK NA MAWAZIRI WAANDAMIZI BILA KUJUA AU WAKIJUA WAKAKARIRIWA WAKISIFIA WAHINDI WA RITES ETI ">>>wamefanikiwa kuanzisha safari za treni kutoka dar es salaam kwa abiria na mizigo ndani ya wiki mbili tu......bila hata kujiuliza ...."
 
mara Ya Kwanza Rites ...walikuja Tanzania Miaka Kama 5 Iliyopita Kwa Mkataba Maalum Wa Kiufundi Uliofadhiliwa Na Bank Ya Dunia[100 Wagons Rehabilitation Project]...wakati Serikali Inatafuta Mbia Wa Kuendesha Na Kuwekeza Trc...nao Wakaamua Kuomba ...jambo Hili Lilifanya Makampuni Mengine Yajitoe Kwa Sababu Kimsingi Tayari Rites Walikuwa Na Mkataba Wa Kiufundi Na Serikali Trc..kwa Hiyo Ushiriki Wao Kwenye Tenda Uliwaogofya Washiriki Wengine Kuhisi Haki Haitatendeka Kwa Kuwa Rites Walikuwa Pia Washauri Wa Kiufundi Kwenye Kurugenzi Ya Trc Wakati Huo..ndio Maana Washiriki Wa Tenda Ile Woote Walijitoa Ikabakia Rites Peke Yao...


Kumbukeni Rites Kwa Kiasi Kikubwa Walisaidiwa Na Wahindi Wazawa ...andy Chande..na Subash Patel Kushinda Hii Tenda ..na Hadi Sasa Subash Patel Kupitia Kampuni Yake Ya Mm Grooup Ana Interest Kwenye Trl[through Rites]..chende Pia Ana Interest Lakini Sasa Sina Uhakika Sana Hasa Baada Ya Kampuni Yake Ya Gapco Ambayo Ilikuwa Pia Iwe Mbia Au Ni Mbia Wa Rites Kupata Matatizo Na Bank.........

Hao Wenyeji Wa Rites Subash ..mnajua Uhusiano Wake...na Chende Mnajua Uhusiano Wake Na Makampuni Ya Serikali Kama Njumbe Kwenye Bodi Nyingi...
...true story...
 
Somebody shoot me please..............

Jamani, ni mimi au kuna baadhi ya watu wanatumia dhana ya kwamba "WaTanzania ndivyo walivyo we piga bao tuchukue chetu mapema"??
 
yap! ndivyo tulivyo!...
Mjarumani ambaye aliijenga reli yetu alitoa offer ya contracting wakamwona mchawi kwa sababu hakuahidi asilimia 10.. Leo nasikia vipuli kibao vyenye gharama kubwa (spare parts) zinachukuliwa na wahindi kupelekwa kwao.. No wonder tumepoteza tayari vichwa 40 na bado tunalipia gharama ya vichwa 7 taka kwao.. mahesabu mazito....ama kweli win win situation ya JK inafanya kazi..
 
Wengi mnaweza kataa nikayo yasema but the only true investor bongo ni SISI WENYEWE WALIPA KODI!! Hawa wengine ni hewa tuu..viongozi wetu na wafanya biashara fulani tanzania wanatuchezea akili wanatengeneza makampuni hewa nje na kujifanya ma investor wakifika na kupewa tenda wanatumia hela zetu hizo hizo kuendesha investment zao (KAMA KWELI TUNAUCHUNGU NA NCHI YETU TUFUATILIA KILA INVESTOR HISTORY YAKE HUKO ALIKOTOKEA KAMA HATUJAZIMIA!!..Pinda na Kikwete mpo?? Mnaboa sana CCM your time is almost up..Mugabe 30yrs in power soon atatoka kwa vita au kifo!! U R NEXT!!!HII SIO TANZANIA YA 1970'S n 1980'S madili yenu yapo wazi saizi...only a matter of time kabla hatujasikia mnaumwa kama balali...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom