Mkataba ushirikiano wasainiwa DIT na Taasisi ya Ufundi (CQVIE) ya China

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,807
11,969
WANAFUNZI TANZANIA NA CHINA KUBADILISHANA UZOEFU

Na WyEST
DSM

# Mkataba ushirikiano wasainiwa DIT na Taasisi ya Ufundi (CQVIE) ya China

# Prof. Mkenda ashuhudia utiaji saini makubaliano

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda ameshuhudia utiaji saini wa makubaliano ya ushirikiano kati ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT) na Taasisi ya Ufundi ya Chonqing (CQVIE) kutoka nchini China.

Waziri Mkenda amesema ushirikiano huo umekuja wakati muafaka Tanzania ikiwa katika mchakato wa MAGEUZI makubwa katika elimu.

Miongoni mwa makubaliano ya ushirikiano baina ya Taasisi hizo ni kubadilishana Wanafunzi na Walimu (exchange program ) ili kubadilishana uzoefu katika ujuzi wanaopata katika mafunzo.

Pia wanafunzi wanufaika wa programu hiyo watakuwa na sifa za kufanya kazi katika makampuni mbalimbali nchini China.

Prof. Mkenda amesema Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia itahakikisha ushirikiano huo unadumu na unakuwa endelevu kwa maslahi ya nchi hizo mbili.
IMG-20221201-WA0014(1).jpg
IMG-20221201-WA0018(1).jpg
IMG-20221201-WA0021(1).jpg
IMG-20221201-WA0017(1).jpg
IMG-20221201-WA0022(1).jpg
IMG-20221201-WA0023(1).jpg
IMG-20221201-WA0020.jpg
IMG-20221201-WA0024.jpg
 
Back
Top Bottom