Inasikitisha kuona hapa tz mwanafunzi ananyimwa mkopo wakati serikali hiyohiyo inamgharamia mwanafunzi mmoja TSh 20,525,000/= kwa mwaka hapo nchini msumbiji. Kwa habari za kuaminika nilizozipata zinasema kuwa wanafunzi hao wa kitanzania ni 29 waliopelekwa chini ya mpango wakubadilishana wanafunzi yaani Tanzania-Mozambique students Exchange Program (TAMOSE). Inasemekana makubaliano kt ya tz na msumbiji yalikuwa wanafunzi 50 kwa 50 ila tz ikapeleka 29 wakati wao waliletwa 50. Kitu ambacho kinatia wasiwasi ni kwamba fedha hizo ambazo wanalipiwa ni mkopo! Tena kwa mwaka wa lugha tuu, Je? Wakianza masomo rasmi baada ya lugha itagharimu kiasi gani? Inavyoonekana hapo kuna ufisadi au mkataba wa kizembe na wakitapeli kwani haiwezekani serikali ikubali kuendelea kumlipia mwanafunzi mmoja zaidi ya milioni 20 kwa mwaka wakati ingetosha kuwalipia wanafunzi kadhaa hapa tz. WADAU wanaofahamu mikataba naomba wafuatilie ijulikane kama kuna nini hapo sababu kwa mtaji huu tz tunanyonywa.