Mkasa Wa Kweli Ulionipata Kwa Kutega Kitendawili Cha Wakubwa Nikiwa Mwanafunzi wa Darasa la Tano Shule ya Msingi Mgulani Jijini Dar es salaam

Daaaah nimesoma hapoo
Mwalimu wangu mkuu mwalimu Mwanahawa M Mwailafu
LY 1997 hapooo
Nilmkuta tandika primary school miaka ya 2000s , Kisha katika ya miaka hiyo hyo akahamishiwa unubini primary School iliyopo chango'mbe , nahisi Kesha staafu miaka kadhaa nyuma, alikuwa pombe mtu Yule Bibi
 
ndomana ulinyoosha mkono akawa hakupointi
Huna tofauti na jamaa aliitwa Kama shahidi Ila nimtoto nae akajibu mama mwongo baba hua anakula ugali kila akirudi usiku,akati shitaka mezani au madai yamama kwamba mumewe halagi msosi home
 
Nilmkuta tandika primary school miaka ya 2000s , Kisha katika ya miaka hiyo hyo akahamishiwa unubini primary School iliyopo chango'mbe , nahisi Kesha staafu miaka kadhaa nyuma, alikuwa pombe mtu Yule Bibi
Hahahahahha alikua chapombe haswaaa
 
Hahahahahha alikua chapombe haswaaa
Ha ha ha ha , Mimi nilikua bwana mdogo miaka hyo na nilimjua tu Kama ni chapombe maana Kila siku hasa asubuhi sura ime mvimba Ile mbaya na macho mekundu sna alafu kichwani kaweka curly nywele zake
 
Wadau wa JF

Nikiwa darasa la tano Shule ya Msingi Mgulani iliyopo jirani na DUCE Jijini Dar es salaam

Nakumbuka siku ya mkasa huo aliingia Mwalimu wetu wa lugha ya Kiswahili akijulikana kwa jina la Mwalimu Kanji ambaye alitoa somo la siku hiyo na kisha kutoa fursa kwetu kutoa vitendawili/ misemo/ methali

Utaratibu ulikuwa mwanafunzi mmoja anasimama na kutega kitendawili na kisha anayeweza kukitegua alinyoosha mkono wake na kusimama kutoa jibu kwa ruhusa ya Mwalimu

Tulifurahia sana zoezi hilo hadi ilipofika zamu yangu ndiyo hali ya hewa ikachafuka!

Nakumbuka nilinyoosha mkono wangu kwa muda mrefu na niliporuhusiwa nilisimama na nilianza kwa kuwaomba Wanafunzi wenzangu wakae kimya na wanisikilize kwa umakini

Kilichotokea hawakuamini na hata Mwalimu naye alipata mshtuko mkubwa kama sio mshangao kwani nilitamka "Mficha Uchi".....????

Ilikuwa mshikemahike darasani Wanafunzi wakishangilia huku wakicheka kwa nguvu!

Nakumbuka darasa hilo la vitendawili liliishia hapo hapo na Mwalimu alitaka kuniadhibu japo nilimsihi Sana asifanye hivyo kwani sikuwa na nia mbaya!

Namshukuru sana Mwalimu wangu alikuwa muelewa hakunichapa ila alinikanya nisirudie tena kutoa Vitendawili vya "Wakubwa"

Karibuni tujadili na kubadilishana uzoefu
Ulimaliza Mgulani mwaka gani? Mimi pia ni alumnus wa hapo
 
Back
Top Bottom