Mkasa Wa Kweli Ulionipata Kwa Kutega Kitendawili Cha Wakubwa Nikiwa Mwanafunzi wa Darasa la Tano Shule ya Msingi Mgulani Jijini Dar es salaam

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Mar 8, 2020
2,204
4,692
Wadau wa JF

Nikiwa darasa la tano Shule ya Msingi Mgulani iliyopo jirani na DUCE Jijini Dar es salaam

Nakumbuka siku ya mkasa huo aliingia Mwalimu wetu wa lugha ya Kiswahili akijulikana kwa jina la Mwalimu Kanji ambaye alitoa somo la siku hiyo na kisha kutoa fursa kwetu kutoa vitendawili/ misemo/ methali

Utaratibu ulikuwa mwanafunzi mmoja anasimama na kutega kitendawili na kisha anayeweza kukitegua alinyoosha mkono wake na kusimama kutoa jibu kwa ruhusa ya Mwalimu

Tulifurahia sana zoezi hilo hadi ilipofika zamu yangu ndiyo hali ya hewa ikachafuka!

Nakumbuka nilinyoosha mkono wangu kwa muda mrefu na niliporuhusiwa nilisimama na nilianza kwa kuwaomba Wanafunzi wenzangu wakae kimya na wanisikilize kwa umakini

Kilichotokea hawakuamini na hata Mwalimu naye alipata mshtuko mkubwa kama sio mshangao kwani nilitamka "Mficha Uchi".....????

Ilikuwa mshikemahike darasani Wanafunzi wakishangilia huku wakicheka kwa nguvu!

Nakumbuka darasa hilo la vitendawili liliishia hapo hapo na Mwalimu alitaka kuniadhibu japo nilimsihi Sana asifanye hivyo kwani sikuwa na nia mbaya!

Namshukuru sana Mwalimu wangu alikuwa muelewa hakunichapa ila alinikanya nisirudie tena kutoa Vitendawili vya "Wakubwa"

Karibuni tujadili na kubadilishana uzoefu
 
Tofauti ya kitendawili na methali ni ipi

KITENDAWILI
ni semi zilizofumbwa ambazo hutolewa kwa hadhira ili zifumbuliwe. ... anayeuliza na anayeulizwa, ama maneno yalivyo na maana yake ya fumbo. Kw mfano Kuku wangu amelalia kwenye miba jibu nanasi

Methali
Ni mpangilio wa maneno unaoeleza mafunzo juu ya jambo fulani. Kwa mfani asiefunzwa na mame hufunzwa na ulimwengu
 
Tofauti ya kitendawili na methali ni ipi
Kitendawili ni maneno ya kufikirisha na kuchangamsha akili Kwa kuyafananisha na kitu. Mfano, pamparapa mlango wa chuma ukiufungua hauna huruma...bunduki
Methali ni sentensi zenye maana, mafunzo. Mfano asiyesikia la mkuu ...huvunjika mguu.
 
Daaaah nimesoma hapoo
Mwalimu wangu mkuu mwalimu Mwanahawa M Mwailafu
LY 1997 hapooo
 
Sisi watoto na mama yetu tulikuwa tunapigia vitendawili au hadithi usiku enzi zileee mambo ya tv BADO hayajaenea
Basi dogo langu moja likaanza
Kitendawiliiii......tukajibu tegaaa....

Dogo,"nivue nguo nikupe utamu"
Wote tulibaki tumebaki tumeduwaa aisee ...hapo mi nawaza"hapa jibu LAZIMA litakuwa tusi tu"
Basi bwana, maza alimaindi akashika stiki akamwambia dogo "haya tupe jibu sisi hatujui
Dogo(kwa upoole huku macho yote kwenye stiki) "jibu Ni NDIZI mama

Itaendelea
 
KITENDAWILI
ni semi zilizofumbwa ambazo hutolewa kwa hadhira ili zifumbuliwe. ... anayeuliza na anayeulizwa, ama maneno yalivyo na maana yake ya fumbo. Kw mfano Kuku wangu amelalia kwenye miba jibu nanasi

Methali
Ni mpangilio wa maneno unaoeleza mafunzo juu ya jambo fulani. Kwa mfani asiefunzwa na mame hufunzwa na ulimwengu
Yap; kitendawili kwa kawaida ni furahisha genge muda usogee. Methali brings deep thinking, kioo cha maisha, hufundisha, huadabisha, na hata hutoa maonyo kwa wenye kuelewa.
 
Back
Top Bottom