Tanzania Sweetheart
Member
- Mar 17, 2020
- 46
- 63
MTUNZI: KULWA MWAIBALE
MWANZO
Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 25 ambaye ni yatima niliyezaliwa peke yangu kwa wazazi wangu ambao sikubahatika kuwaona, kwa sasa naishi jijini Dar es Salaam.
Kutokana na mikasa niliyopitia maishani mwangu, sitapenda kuliweka wazi jina langu halisi ila nitambue kwa jina la Dorcas.
Kwa mujibu wa mama niliyejikuta nipo mikononi mwake kimalezi, mama yangu yangu alikuwa mtu wa Rukwa na baba yangu alikuwa raia wa Zambia aliyekuwa akifanya biashara za bidhaa tofauti pamoja na samaki kutoka Ziwa Tanganyika eneo la Nkasi na kuwapeleka kwao Zambia.
Nilielezwa kwamba, mama na baba walikutana Kilando Namanyele, Rukwa wakaanzisha uhusiano wa kimapenzi ambao ulisababisha kupata ujauzito ambao mama aliubaini baada ya baba kurudi kwao.
Nilielezwa na mama huyo ambaye alifahamiana na mama mjini Sumbawanga katika biashara zao kwamba, mama alipobaini alikuwa mjamzito alitarajia baba akifika Kilando angemfahamisha kuhusu hali yake.
Jambo la kusikitisha ni kwamba baba hakurudi tena Tanzania ambapo mpaka leo haijulikani kama alikufa au alikumbwa na masaibu gani.
Kwa mujibu wa mama huyo ambaye naye hivi sasa ni marehemu, mama aliyekuwa amepanga chumba eneo la Chanji Sumbawanga aliendelea kuilea ile mimba peke yake.
Mama mlezi aliniambia kwamba, mama alipokaribia kujifungua alikwenda kwao Mpanda ili Mungu atakapomsaidia kujifungua salama awe chini ya uangalizi wa wazazi na ndugu zake.
Rafiki huyo wa mama aliniambia alimfanyia maandalizi ya safari ambapo mama alikwenda Mpanda akajifungua salama na kurejea Sumbawanga mjini kuendelea na maisha.
Aliongeza kunieleza kwamba, waliendelea kushirikiana na mama waliyeitana mtu na mdogo wake kiasi cha watu ambao hawakuwafahamu vizuri kudhani walikuwa ndugu wa damu.
Maisha yaliendelea lakini kutokana na mama kuwa na mtoto mdogo yaani mimi, hakuweza kusafiri kwenda mbali zaidi ya kuwa bize kunilea na kufanya biashara ndogondogo.
Nilielezwa kuwa nilipofikisha miezi sita, mama aliondoka na mimi kwenda mkoani Mbeya kwa rafiki yake waliyesoma pamoja aliyemuomba aende huko wakashirikiane kufanya biashara.
Kufuatia ombi hilo la rafiki yake, mama alikwenda Mbeya na kufikia Isanga ambapo rafiki yake huyo ambaye ni Mnyakyusa wa Masukulu wilayani Rungwe alikuwa amepanga chumba.
Mama huyo alinieleza, mama na rafiki yake huyo walikuwa wakifanya biashara ya kununua marahage, mchele na mahindi na kwenda kuyauza.
Wakati mwingine, siku ya Jumanne na Ijumaa ambayo inakuwa na mdana sehemu inayoitwa Kiwira, walikuwa wakienda kufanya biashara huko.
Aliongeza kunieleza kuwa, kwa vile hawakuwa na mtaji mkubwa walikuwa wanapata fedha kiasi walizoendeshea maisha yao huku mama akinilea.
Baada ya mama kukaa Mbeya kama miezi sita alikutana na mama mmoja wa Sumbawanga ambaye alikuwa akifahamu uhusiano wake na baba akamwambia aliwahi kumuona baba akifanya biashara zake Nkasi.
Kufuatia habari hiyo ambayo kwa mama ilikuwa njema sana, aliamua kurudi Sumbawanga kwa lengo la kwenda Nkasi akiwa na imani kabisa angeweza kukutana na baba.
Lengo lake lilikuwa ni kumuonesha mwanaye (mimi) na kama angekuwa tayari waanze kuishi maisha ya mume na mke.
Yule mama alinieleza, alipomshirikisha rafiki yake wa Mbeya alifurahi sana. Baada ya maandalizi tuliondoka na mama kwenda Sumbawanga na kufikia kwa rafiki wa mama aliyekuwa anaitwa mama James.
Sumbawanga tulikaa wiki moja tukaenda Kirando lengo likiwa ni kumtafuta baba..
MWANZO
Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 25 ambaye ni yatima niliyezaliwa peke yangu kwa wazazi wangu ambao sikubahatika kuwaona, kwa sasa naishi jijini Dar es Salaam.
Kutokana na mikasa niliyopitia maishani mwangu, sitapenda kuliweka wazi jina langu halisi ila nitambue kwa jina la Dorcas.
Kwa mujibu wa mama niliyejikuta nipo mikononi mwake kimalezi, mama yangu yangu alikuwa mtu wa Rukwa na baba yangu alikuwa raia wa Zambia aliyekuwa akifanya biashara za bidhaa tofauti pamoja na samaki kutoka Ziwa Tanganyika eneo la Nkasi na kuwapeleka kwao Zambia.
Nilielezwa kwamba, mama na baba walikutana Kilando Namanyele, Rukwa wakaanzisha uhusiano wa kimapenzi ambao ulisababisha kupata ujauzito ambao mama aliubaini baada ya baba kurudi kwao.
Nilielezwa na mama huyo ambaye alifahamiana na mama mjini Sumbawanga katika biashara zao kwamba, mama alipobaini alikuwa mjamzito alitarajia baba akifika Kilando angemfahamisha kuhusu hali yake.
Jambo la kusikitisha ni kwamba baba hakurudi tena Tanzania ambapo mpaka leo haijulikani kama alikufa au alikumbwa na masaibu gani.
Kwa mujibu wa mama huyo ambaye naye hivi sasa ni marehemu, mama aliyekuwa amepanga chumba eneo la Chanji Sumbawanga aliendelea kuilea ile mimba peke yake.
Mama mlezi aliniambia kwamba, mama alipokaribia kujifungua alikwenda kwao Mpanda ili Mungu atakapomsaidia kujifungua salama awe chini ya uangalizi wa wazazi na ndugu zake.
Rafiki huyo wa mama aliniambia alimfanyia maandalizi ya safari ambapo mama alikwenda Mpanda akajifungua salama na kurejea Sumbawanga mjini kuendelea na maisha.
Aliongeza kunieleza kwamba, waliendelea kushirikiana na mama waliyeitana mtu na mdogo wake kiasi cha watu ambao hawakuwafahamu vizuri kudhani walikuwa ndugu wa damu.
Maisha yaliendelea lakini kutokana na mama kuwa na mtoto mdogo yaani mimi, hakuweza kusafiri kwenda mbali zaidi ya kuwa bize kunilea na kufanya biashara ndogondogo.
Nilielezwa kuwa nilipofikisha miezi sita, mama aliondoka na mimi kwenda mkoani Mbeya kwa rafiki yake waliyesoma pamoja aliyemuomba aende huko wakashirikiane kufanya biashara.
Kufuatia ombi hilo la rafiki yake, mama alikwenda Mbeya na kufikia Isanga ambapo rafiki yake huyo ambaye ni Mnyakyusa wa Masukulu wilayani Rungwe alikuwa amepanga chumba.
Mama huyo alinieleza, mama na rafiki yake huyo walikuwa wakifanya biashara ya kununua marahage, mchele na mahindi na kwenda kuyauza.
Wakati mwingine, siku ya Jumanne na Ijumaa ambayo inakuwa na mdana sehemu inayoitwa Kiwira, walikuwa wakienda kufanya biashara huko.
Aliongeza kunieleza kuwa, kwa vile hawakuwa na mtaji mkubwa walikuwa wanapata fedha kiasi walizoendeshea maisha yao huku mama akinilea.
Baada ya mama kukaa Mbeya kama miezi sita alikutana na mama mmoja wa Sumbawanga ambaye alikuwa akifahamu uhusiano wake na baba akamwambia aliwahi kumuona baba akifanya biashara zake Nkasi.
Kufuatia habari hiyo ambayo kwa mama ilikuwa njema sana, aliamua kurudi Sumbawanga kwa lengo la kwenda Nkasi akiwa na imani kabisa angeweza kukutana na baba.
Lengo lake lilikuwa ni kumuonesha mwanaye (mimi) na kama angekuwa tayari waanze kuishi maisha ya mume na mke.
Yule mama alinieleza, alipomshirikisha rafiki yake wa Mbeya alifurahi sana. Baada ya maandalizi tuliondoka na mama kwenda Sumbawanga na kufikia kwa rafiki wa mama aliyekuwa anaitwa mama James.
Sumbawanga tulikaa wiki moja tukaenda Kirando lengo likiwa ni kumtafuta baba..