Mkasa wa kweli: Kazi za ndani nchini Oman zilivyonikutanisha na kifo

SEHEMU YA 02


Kwakweli nilifurahi kukutana na mwanamke yule anayezungumza Kiswahili kwenye taifa hilo la Kiarabu.
Lakini hata hivyo, kwa muda mchache sana niliotumia kutambuna na yule mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Mariamu Rashidi, kuna mambo niliyoyagundua kutoka kwakwe. Mambo ambayo yalinitisha vibaya mno.


Pamoja na kuwa na wasiwasi dhidi ya yule mtu, sikutaka kabisa kuonesha hali ya hofu waziwazi, wakati wote nilitengeneza uso wenye tabasamu bandia mbele ya macho ya mwanamke huyo.
Tulitoka nje ya uwanja ule na kuchukua tax kisha tukaanza safari ya kuelekea mahali nisikokujua.
Tulitumia nusu saa kufika sehemu iliyokuwa na nyumba nyingi, ambazo siyo tu hazikujengwa kiramani lakini pia zilikuwa ni nyumba zilizochoka. Nachelea kusema, ilikuwa ni ‘Uswahilini’ ya Oman.
“Hapa panaitwa Deira,” Mariamu alisema, tukiwa mbele ya nyumba moja iliyoonekana kuchakaa kwa kukosa ukarabati wa muda mrefu.
“Ndipo ninapoishi, lakini kwa sasa tutaishi wote kwa siku mbili. Nitatumia muda huo kukueleza sheria na taratibu za nchii hii kabla ya kwenda kuanza kufanya kazi za ndani.”
“Watu wanasema sheria za Uarabuni ni ngumu na kali sana?” nilimuliza.
“Hapana. Siyo ngumu. Inategemeana na wewe utakavyozipokea. Ukizipoea sheria za hapa katika mtazamo wa ugumu, kwa kweli utashindwa, lakini ukizichukulia kwa wepesi na ukazitekeleza, huwezi kupata tabu.”
Pamoja na maelezo ya Mariamu, bado hayakunifanya kutoogopa, matukio ya mabinti wa kitanzania kubakwa, kuunguzwa kwa maji ya moto wakati mwingine hata kusukumwa juu ya majengo marefu.
Sambamba na hayo yote, kila nilivyofikiria familia yangu. Familia iliyozingirwa na umasikini wa kupindukia. Nilijikuta napata nguvu hata kutoogopa lolote.
Taratibu za kisheria juu ya wasichana wa Kitanzania wanaokwenda kufanya kazi za ndani nchini Oman, tasisi ya ubalozi ilikuwa haiusishwi kabisa. Mambo mengi yalifanyika kinyamela.


Masaa arobaini na nane badaye, mimi na Marimu tulikuwa kwenye tax tukielekea sehemu moja iitwayo Suwaiq kilometa 50 kutoka mjini Muscut. Huko ndipo mahali nilipotakiwa kwenda kufanya kazi ni huko ambapo kulikuwa na familia ya tajiri aliyeitwa Abdallah Mustapha ambaye ndiye niliyetakiwa kwenda kuanza kazi nyumbani kwakwe.
“Karatasi za majibu yako ya vipimo vya hosptali unazo?” Mariamu aliniuliza wakati gari likikunja kushoto na kuiacha barabara kubwa ya lami na kuingia kwenye barabara iliyokuwa na changarawe nyingi.
“Karatasi zipo kwenye begi, kwani majibu ya vipimo, bado yanahitajika hadi huku?”
“Ndiyo” alinijibu kwa ufupi. Nilijiuliza moyoni inaamna huko niendako, wao waajiri hawajui kuwa siwezi kuwa kwenye nchi hiyo pasina kupima, vipi tena wahitaji majibu ya vipimo.
Wakati nikiwa bado najiuliza, gari lilikata kona na kuiacha ile njia yenye changarawe na kuingia kwenye njia nyembamba iliyokuwa na marumaru, pembeni ya njia hiyo kukiwa na miti mingi iliyopandwa kwa mpangilio mzuri.
Gari lilikwenda kwa mwendo wa taratibu. Mita kama ishirini tukawa mbele ya nyumba kubwa iliyokuwa na sifa zote za kuitwa nyumba ya kifahari.
Baada ya dereva tax kulipwa ujira wake na kuondoka , tukasogea kwenye geti la jumba lile. Mariamu alibonyeza Swich ya kengele iliyokuwa pale getini na muda mfupi badaye, alikuja mvulana wa Kisomali kufungua.
Nilipogonganisha macho na yule mvulana kitu fulani kisichoelezeka lilipita kichwani mwangu. Macho yangu yalinata kwa yule mvulana kwa nukta kadhaa.
Alizungumza na Mariamu kama watu wenye kufahamiana kwa muda mrefu kilichonishangaza zaidi aliongea kwa Kiswahili. Alikuwa ni mtu mcheshi na makalimu. Kiswahili chake kilikuwa na lafudhi ya Kimombasa, kwa kweli alionekana ni mtu mwenye kufurahia maisha wakati wote.
Baada ya maongezi ya hapa na pale, alitufungulia geti na kuingia ndani.
Ndani ya lile jumba lile kifahari kulikuwa na eneo kubwa la wazi ambalo lilipandwa bustani ya maua na nyasi fupi za kijani kibichi, upande wa kaskazini kukikuwa na bwawa dogo la kuogelea sanjari na viti vichache vya kukalia vilivyokuwa chini ya miavuli midogo mahususi kwa kimvuli, mbele ya nyumba hiyo kulikuwa na magari ya bei mbaya yaliyopaki kwenye ‘parking’ maalumu iliyojengwa kiustadi.
“Hapa ndipo utakapo fanya kazi” hatimaye Mariamu aliniambia.
“Pazuri sana”
“Ndiyo ni pazuri, hata mshahara utakaolipwa utakuwa mnono, mradi uwe tayari kukabiliana na changamoto zitakazo kukabili” aliposema hayo taswira ya kubakwa ikanijia.
Kabla sijatia neno wakati huohuo, alitokea mwanamke mmoja wa kiarabu aliyekuwa na sifa zote za kuitwa mrembo. Pamoja na uzuri wake lakini midomo na macho yake yalinijulisha kuwa mtu yule alikuwa na majivuno na dharau.
“Asalam aleykum,” alitusalimia
“Waleykum salama.”
“Huyu ndiye yule mtu mweusi kutoka Tanzania?” alisema. kauli ile ilinifanya niendelee kuamini kuhusu fikra zangu juu ya tabia ya yule mwanamke wa Kiarabu.
“Ndiye” Mariamu alimjibu.
“Mmepima na mmeona hana Ukimwi”
“Hana?”
“Ebora na Tb je?”
“Hana pia”
“Piteni ndani” alisema yule mmwanamke.
“Huyu anaitwa Zakia Almajidi mke wa Abadallah Mustapha.” Mariamu alininong’oneza tukiwa tunaingia ndani, nilishusha pumzi ndefu na kwa mara ya kwanza nafsi yangu ikikiri kuwa nipo kwenye uwanja wa vita.

UKITAKA YOTE NJOO WHATSAP NA ELFU MBILI YAKO NAMBA NI 0687750295, VINGINEVYO SUBIRI HADI KESHO.
 
Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi @Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad @Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya Lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO @multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij @addenbwii ONTARIO Kobe The Vein mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya SITAKI ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo @shedede kamtu33 SteveMollel Ngushi DONALD stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 Ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha auxillius Goma Son Hubeb pes KING DUBU VILLAIN mwayena donbeny @Aleppo JipuKubwa shoo61 BOMBAY John mungo Nyakageni bato Dogo 1 sufra chamlungu painscott wegman Bravo Engliash MOSELBAY wa stendi FaizaFoxy bigmind cadabraa Internal Kelvin mwalukas mnonje Kelvin X Somoche Wgr30 Miiku Poise Jabman kalamuyamwalimu BOMBAY the say juxhb witnessj Gide MK Mmanyema mgogoone Mnongane Mandingo koncho77 afsa ngaboru Paradoxer Heavy Metal KIMBURU 06 Raaj kichekoh ngumba njeche kikale DullahTza Goodluck Mshana julius Darcy Denis Kasekenya mashonga kitalembwa Khaleed Shaban middle east SirChief jiwe jeusi Mkambarani mansakankanmusa gambada ynwa ney kush mossad 03 white wizard xtaper Mzigua90 Ollachuga Oc Gidbang Mateja M.G Yango jipu abaa4all DIBAJI Agenda1 Grahnman The MaskmaN Slim5 Xubzero agprogrammer JoJiPoJi @Architectus blance86 Mamtolo monde arabe Ngao Ya Imani stardust JK naiman64 Dharra seledunga ABB SHAMMA Richard Waziri wa Kaskazini Mwinjuma1 Kanungila Karim baracuda Mwamba028 besaro Pyepyepye Bilionea Asigwa ibn Kiti Chema Tugas Royal Warrior mederii mmangO manzi james LIKUD adrenaline Royal Son Mhadzabe salaniatz Natasha Ismail jiwe jeusi chibalangunamchezo
John Mloy conjuget Van Pauser great G Mtoto wa nzi Zeus1 hindustan Sci-Fi MAN OF PEACE kashata emnly danny baraka bb MTOTELA kbosho TEMLO DA VINCA
 
SEHEMU YA 03



PAMOJA na kukarahishwa na maswali yaliyokuwa katika dhana halisi ya kibaguzi, lakini nilivyoingia tu ndani ya lile jumba, akili yangu ikahamia kwenye mandhari ya mule ndani. Niwe mkweli, tangu nizaliwe hadi leo hii, sijawahi kuona sebule nzuri kama lile la jumba la kifahari la tajiri Abdallah Mustapha lililopo Suwaiq nje kidogo ya Jiji la Muscut nchini Oman.
Macho yangu yalikuwa hayatulii, niligeuza shingo huku na kule, nikivutiwa na fenicha ghali zilizokuwa mule ndani. Nilikuwa mtulivu wakati Marimu akifanya mazungumzo na yule msichana wa Kiarabu utaratibu wa mkataba wangu.
“Shika hii,” yule msichana wa Kiarabu alinipa karatasi.
“ Agripina Soma vizuri huo mkataba wako wa kazi mama, kisha tia saini hapo chini, ” Mariamu ambaye alikuwa kama wakala wangu alishadadia baada ya kuwa nimepokea karatasi ile.
Nilipitia ule mkataba ulioandikwa kwa Lugha ya Kingereza. Pamoja na kwamba sijui lolote kuhusu mambo ya sheria, hasa sheria za mikataba ya ajira. Nilihisi tu, mkataba ule ulikuwa na mapungufu fulani ambayo nashindwa kuyabainisha hapa moja kwa moja.
Nilipo gota kwenye nukta ya mwisho ya mkataba ule, sikuamini nilipoona nitalipwa kiasi cha Riyal 100 ambayo kwa pesa za kwetu ilikuwa ni karibu shilingi laki sita na ushee.
Yanii kufanya usafi, kuosha vyombo, kufua na kupika, hivyo tu. Nalipwa laki sita na ushee!!!
Niliona ni pesa nyingi nilizo takiwa kulipwa ukilinganisha na kazi nitakazokuwa nikifanya. Niliamini wakati wa kupunguza umasikini kwenye familia yangu ndiyo huo.
Sikutaka kuchelewa. Nilimwaga saini kwenye ile karatasi na nikawa nimeingia mkataba wa miaka miwili Kwa makubaliano ya kuongezewa mkataba endapo mwajiri wangu atakubaliana na utendaji wangu wa kazi.
Muda mfupi badaye, nilielekezwa mazingira ya jumba lile sanjari na kutambulishwa kwa wafanya kazi wenzangu wawili mmoja mwanamke aliyeitwa Fatuma emeke kutoka Liberia na yule mvulana wa Kisomali, ambaye nilitambulishwa kwa jina la Hussein Jabal, baada ya mambo hayo kukamilika Mariamu aliniaga:
“Mimi naondoka.”
“Sawa...Lakini kuna ajambo nilitaka kukuuliza Mariamu.”
“...kuhusu?”
“Kuhusu uvumi wa wasichana wa kazi kufanyiwa ushenzi wakiwa huku ikiwemo kubakwa.”
“Kubakwa!!!” Mariamu alishangaa.
“Ndio, kubakwa”
“Kubakwa ni sehemu ndogo sana ya changamoto zilizopo huku, kwanza ni jambo la kawaida tu, kikubwa unachotakiwa kufanya ni kuwa tayari kuipokea hali hiyo pale itakapokutokea.” Mariamu aliongea kauli hiyo kiwepesi sana.

“Niwe tayari kubakwa pale hali hiyo itakapo tokea?”niliuliza nikiwa nimemkazia jicho.
“Siyo uwe tayari kubakwa...”
“Bali?”
“Uwe tayari kufanya mapenzi kwa hiyari.”
“Sijaja huku kufanya mapenzi na mtu wa aina yeyote. Lakini pia, sikuja huku ili ninyanyasike kwa namna yeyote ile Mariamu, hukunieleza mambo hayo kabla ya kupanda ndege, kwa nini unanigeuka?” nilisema kwa sauti kavu lakini yenye viashiria vya hofu kubwa.

“Ngoja nikupe siri moja...” Mariamu alisema. Kabla hajamaliza mara Zakia alitokea na kunitaka nianze majukumu yangu.
Mariamu aliniaga, akanipa miadi ya kuonana wakati mwingine. Nikabakia nikiwa na mashaka na wasiwasi moyoni.
Mashaka yalikuwa makubwa sana. Sikuwa na imani tena na Mariamu. Kama nilivyosema awali, mwanamke huyo nilimwona ni mtu aliyejaa hila usoni mwake, tangu siku ya kwanza aliponipokea uwanja wa ndege wa Muscat.
Siku hiyo, nilianza kazi kwa nidhamu na umakini. Mwenyeji wangu akiwa ni Fatuma Emeke msichana mweusi na mzuri wa umbo kutoka nchini Liberia.
Siku kadhaa nikiwa ndani ya ile nyumba ya kihafahari, kama mfanya kazi wa ndani (house girl) nilibaini jambo jipya.

Yule mwanamke wa kiarabu. Zakia Al Majidi mke wa Abdallah Mustapha alikuwa ni mke wa pili wa tajiri huyo ambaye alikuwa na watoto wawili wa kiume kutoka kwa mke wake waliokuwa wakiishi na mama yao katika mji wa Al Jibrih mashariki mwa Jiji la Muscut nchini Oman.
Niliendelea kufanya kazi nikiwa ni mtu mwenye mori na ari. Sikuwahi kukutana na matukio kama yalivyokuwa yakivumishwa nikiwa Tanzania. Ama nilivyokuwa nikihisi. Hapakuwa na mtu aliyewahi kunisumbua kimapenzi aidha kuninyanyasa kwa namna yoyote ile ingawa majivuno na ubaguzi wa rangi wa Bi Zakia, sikuwa napendezwa nao.
Nilimaliza mwezi mmoja salama, nililipwa mshahara wa kwanza vizuri bila tatizo lolote. Siku napokea pesa kama malipo ya kazi zangu lilikuwa ni jambo la furaha mno kwenye maisha yangu. Niliamini huo ndiyo muda wa kukamilisha ndoto zangu za kupunguza hali ya maisha duni kwenye familia yangu.
Hapa kuna jambo moja nimesahau kulieleza: Nimesahau kueleza kwamba, moja ya sheria ambazo ziliwekwa na Bi Zakia pale nyumbani kwake, dhidi ya wafanyakazi wa ndani ilikuwa ni kutotumia simu za mkononi. Hadi leo sijui yule Mwarabu kwa nini alituwekea sheria ya kijinga vile.
Nakumbuka Kila mwisho wa wiki, nilikuwa nikifunga safari hadi Muscut. Huko nilipiga simu nyumbani, nikawasiliana na na familia yangu. Lakini pia, nilikuwa nikiwatumia pesa kwa njia kama ‘mape-xpress’ ‘western union’ ‘telegram’ na kadhalika.
Katika kipindi chote cha maisha yangu ndani ya nyumba ya tajiri Abdallah Mustafa, mtu wa karibu kwangu alikuwa ni yule mvulana Hussein Jabal, raia wa Somalia. Ukiachilia mbali Fatuma ambaye alikuwa ni mfanyakazi mwenzangu wa wa kike tuliyeshirikiana kwenye kazi zote za ndani. Ukaribu wangu na mvulana huyu ulitokana na uwezo wake wa kuzungumza Kiswahili.
Mbali na hilo, Hussein alikuwa ni mtu mcheshi na msikivu, Kila siku baada ya kazi, tulikaa kwenye bustani ya majani na kuzungumza mambo mengi, nilipata kuelewa mambo mengi kuhusu mtu yule. Hata yeye alijua mambo kadhaa kuhusu maisha yangu.
Ukaribu wangu na Hussein ulinifanya nimzoe. Kumzoea kukazaa hali ya kumuwaza kila wakati. Hali ile ya kumuwaza kila wakati, kukatengeneza hali nyingine ya kummisi hususani pale awapo mbali na mimi.
Taswira ya sura ya Hussein Jabal ilianza kuniganda kichwani mwangu. Sikutaka kujiongopea kabisa kwamba moyo wangu hauvutiwi na uso wenye pua ndefu, macho makubwa sanjari na meno yaliyojipanga vizuri mithili ya punje za muhindi.
Sikutaka kabisa kujifariji kuwa nafsi yangu haikuvutika na umbo kakamavu la yule mvulana.
Lakini hata hivyo, akili yangu haikuwa tayari kuukubali ukweli uliotoka moyoni mwangu, ukweli wenye viashiria vyote vya mapenzi kwa mvulana yule.
Nilijikumbusha na kujionya juu ya msukumo huo. Sauti moja kichwani iliniambia jiepushe na mapenzi, yatakuletea matatizo mapenzi, fuata kilichokuleta Agripina. Sauti hiyo ilikuwa ikigonga kichwa changu kama kengele, lakini pamoja na hilo, bado moyo wangu ulikumbwa na wazimu dhidi ya mvulana yule. Taa nyekundu ilikwisha waka moyoni.

UKITAKA YOTE NJOO WHATSAP NA ELFU MBILI YAKO TU NAMBA NI 0687750295,
 
SEHEMU YA 04


Nilijikumbusha na kujionya juu ya msukumo huo. Sauti moja kichwani iliniambia jiepushe na mapenzi, yatakuletea matatizo mapenzi, fuata kilichokuleta Agripina. Sauti hiyo ilikuwa ikigonga kichwa change kama kengele, lakini pamoja na hilo, bado moyo wangu ulikumbwa na wazimu dhidi ya mvulana yule. Taa nyekundu ilikwisha waka moyoni.
Bila kutarajia nikajikuta mimi na mvulana yule tunaanzisha mahusiano ya kimapenzi. Mapenzi ambayo yalikuja kuleta madhila makubwa mno kwenye maisha yangu hadi leo hii ninapo simulia mkasa huu.
mahusiano yetu yalianza kama mzaha. Awali nilichukulia kama nimepitiwa na jinamizi la mahaba na tamaa za mwili kwa bahati mbaya. Niliamini mwisho wa penzi lile ni kupotea kama lilivyokuja, akini kadri siku zilivyokuwa zikiyoyoma ndivyo mapenzi yangu na mtu yule yalivyozidi kustawi na kukua kwa kasi.
Hussein Jabal alikuwa ndiyo mvulana wa kwanza kuujua mwili wangu. Nakumbuka siku ya kwanza kugaragara nae kitandani, ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kuingia kwenye sayari ya mahaba kunako sita kwa sita. Huwa siwezi kuisahau siku hiyo.
“Asante Agripina,” Hussein alisema akiwa amelala chali. Kichwa changu kikiwa juu ya kifua chake. Tukiwa kama tulivyozaliwa.
“...kwa?”
“Kwa penzi tamu...na...Kwakuwa mwanaume wa kwanza kufungua bikira yako.”
“Usijali Hussein ila jambo moja....”nilisema huku nikigeuza shingo yangu na kumwangalia machoni. Tukawa tunatizamana.
“Usiniache tafadhali.”
“Siwezi kukuacha Agripina, nataka siku moja tukaishi Mogadishu, huko kwetu Somalia.”
“Kweli?”
“Kabisa.”
Huo ulikuwa ni mwanzo wa mimi kuingia kwenye mambo ya kiutu uzima. Uhusiano kati yangu na mvulana yule ulikuwa ni siri ya watu watatu. Kwa maana ya mimi mwenyewe, Hussein pamoja Fatuma Emeke, ambaye alikuwa ni mfanyakazi mwenzangu kutoka Liberia.
Usiri wa penzi langu na mvulana yule, raia wa Somalia ulitokana na jambo moja kuu. Tuliogopa Sheria kali ya nchi ya Oman iliyokuwa ikisimamia misingi ya ‘sharia’
Ilikuwa hairuhusu vijana ambao hawajaoana kuwa kwenye uhusiano wa kimapanzi. Adhabu yake ilikuwa ni kuchapwa viboko hadhalani au kufukuzwa nchini humo kwa wageni.
Tuliendelea kufanya kazi kwa bwana Abdallah Mustapha kwa nidhamu kubwa huku mahusiano yangu na Hussein yakiendelea kwa kasi lakini yakiwa kwa siri kubwa.
Kila siku usiku nilikuwa nikiondoka chumbani kwangu na kwenda chumbani kwa Hussein. Huko nilifanya nae mapenzi usiku kucha na alfajiri kabla ya adhana, nilirejea chumbani mwangu.
Hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu huko Suwaiq nchini Omani kabla ya siku moja kutokea tukio moja lililobadili dira ya maisha yangu!

****

“Ta, ta, ta...” sauti ndogo ya mshale wa saa ya ukutani ilisikika. Ilikuwa yapata saa sita na nusu usiku, nilikuwa nimelala chali huku macho yangu yakitizama kwenye dari.
Hakuna kilichosikika zaidi ya sauti ndogo ya saaa ya mshale sanjari na mkoromo mdogo uliokuwa ukitoka kwa Fatuma aliyekuwa kwenye usingizi wa pono.
Nilijinyanyua kitandani na kuketi kitako, macho yangu yalihamia kwenye kipimo cha kupima ujauzito, bado moyo wangu ulishindwa kukubaliana na ukweli kwamba nilikuwa mjamzito. Niliogopa. Muda wa kuwa na mtoto haukuwa sahihi.
Nilivuta pumzi kwa ndani na kuzitoa kwa mkupuo. Kwa mujibu wa saa ile ya ukutani ilikuwa yapata saa sita kasoro, usiku.
Nilavaa nguo, nikatoka nje. Nikatembea kwa kunyata kukifuata kibanda alichokuwa akilala Hussein, ndani ya nyumba ile ya tajiri Abdallah Mustapha.
Kulikuwa na ukimya eneo lote la nyumba ile ya kifahari. Nilisogea hadi mlangoni mwa chumba cha Hussein na kusukuma mlango.
Alaa!
Mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani.
Haikuwa kawaida kwa Hussein kufunga mlango hasa kwa kipindi ambacho tunakuwa tumekubaliana kuwa nitakwenda chumbani kwakwe.
Nikasukuma tena. Mlango haukufunguka.
Kuna nini? Nilijiuliza kimoyomoyo.
Nikayatembeza macho kulia na kushoto nikichukua tahadhali ya kubambwa.
Nikarudi tena mlango, sasa nikataka niugonge kidogo kumwamsha Hussein nilihisi huenda alipitiwa na usingizi na alijisahau akafunga mlango.
Lakini kabla sijatekeleza hilo, ghafla nikasikia sauti kutokea mule ndani.
Ilikuwa ni sauti ya kilio cha mwanamke, nikamakinika na hali hiyo. Nikatega sikio.
Toba!
Nikaendelea kugundua kuwa ilikuwa ni sauti ya kimahaba ya mwanamke aliyekuwa ndani ya chumba cha Hussein Jabal.
Ndani ya chumba kulikuwa na watu waliokuwa wakifanya mapenzi.
Hussein ananisaliti!....
Ndiyo wazo la kwanza kupita kichwani mwangu.
Mwili ukanitetemeka. Donge zito likanikaba kooni, nikahisi uchungu wa ndani kwa ndani. Wivu ukanivaa.
Nikaugonga mlango kwa nguvu. Sikujibiwa zaidi ya kuendelea kusikia sauti ya mwanamke aliyekuwa akilia. Kilio cha raha.
Kitendo hicho kikazidisha wahaka ndani ya nafsi yangu. Kichwa changu kikawa na maswali lukuki.
Ndani ya lile jumba la kifahari, tulikuwa wanawake watatu. Fatuma Emeke, Zakia ambaye ni mke wa Abdallah Mustapha pamoja na mimi.
Kivyovyote vile Hussein ndiye alikuwa akifanya mapenzi na mwanamke mule ndani. Swali kuu ni Je mwanamke huyo ni nani?
Ni Fatuma au ni Zakia? Fatuma nilimwacha chumbani akikoroma. maana yake ni kwamba siyo Fatuma. Ni nani? Zakia.
Nilipo muwaza tu mwanamke huyo, hapo hapo taswira ya tabia zake zikanijia akilini.
Mbali ya wivu dhidi ya mumewe, Alikuwa ni mwanamke mwenye dharau na majivuno, mtu mweusi kwakwe alikuwa ni kikatuni kisicho na maana yoyote.
Alikuwa ni mbaguzi asiye na mfano. Hakupenda kuchangia meza moja ya chakula na watumishi wake wa ndani. Siku zote alimini mtu mweusi yupo duniani kwa ajili ya kumtumikia mtu mweupe.
Kwa mantiki hiyo anawezaje kuwa ndiye mtu aliye ndani wakifanya mapenzi na Hussein Jabal mvulana asiye na mbele wala nyuma kutoka huko Mogadishu nchini Somalia.
Sasa kama ni hivyo mwanaume huyo anafanya mapenzi na nani?
Nilijihoji huku nikijawa na wivu mwingi kifuani kwangu, donge zito lilinikaba kooni kila nilivyozisikia kelele za kilio cha mahaba kutoka mule ndani.
“Yanii huyu bwana anipe mimba halafu kama haitoshi ananisaliti!! Nilifadhaika san.
kwa nguvu zangu zote niliusukuma mlango na kuingia ndani.
Sikuamini macho yangu....

UKITAKA YOTE NJOO WHATSAP NA ELFU MBILI YAKO TU NAMBA NI 0687750295
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom