Mkasa wa kweli: Barua Ya Kifo Toka Kuzimu

Mar 17, 2020
46
63
MWANZO
Hebu jaribu kuwaza, upo ofisini kwako. Unapata taarifa kuwa mke wako kipenzi amepata ajali ya gari. Walioshuhudia wanakwambia watu watatu wamekufa hapo hapo na mke wako amepakiwa katika gari la hospitali akiwa mahututi huku nguo zake zimetapakaa damu.
Unaiacha ofisi na kutoka mbio ukiwa umerukwa na akili. Unapofika hospitali, mke wako ndio anakata roho kwenye wodi ya majeruhi.
Mwezi mmoja baada ya msiba wa mke wako unagutushwa usingizini saa tisa usiku na mtu aliyegonga mlango wa nyumba yako. Unapofungua mlango unamkuta mke wako aliyekufa mwezi mmoja uliopita akiwa amesimama mbele ya mlango akiwa na barua mkononi.
Ukimtazama hana tofauti na siku ile aliyokufa. Amevaa nguo zake zile zile zilizochanikachanika kutokana na ajali na mwili wake umetapakaa damu nyeusi iliyoganda!. Anakupa barua iliyokuwa mkononi mwake.
Unapoikunjua na kuisoma, imeandikwa.
“Bado wiki moja na wewe utakufa!”
Bila shaka utanishituka sana….
Sasa endelea.
Naitwa Hashim Mustafa. Kazi yangu ni ualimu. Umri wangu sasa unakaribia miaka arobaini na mitano. Nimeshafanya kazi ya ualimu katika shule mbalimbali za msingi za mkoa wa Tanga hadi kuteuliwa kuwa mwalimu mkuu.
Sikuteuliwa ualimu mkuu kwa rushwa, ukabila wala kujuana kama inavyotokea kwa baadhi ya walimu, bali niliteuliwa kutokana na uwezo wangu, elimu yangu na uzoevu wangu katika kazi za ualimu.
Baada ya kuwa mwalimu mkuu, shule nilizopewa zilikuwa zikifanya vizuri mwaka hadi mwaka na kunisababishia kupata sifa nyingi.
Binafsi nilipenda sana kufundisha shule za vijijini kwa sababu walimu wengi walikuwa hawazipendi kutokana na mazigira ya vijiji vyetu kutoridhisha kwa walimu.
Lakini mimi nilikuwa na sababu zangu za kupenda shule hizo. Kwanza ni kuwapa haki watoto wa vijijini na wao kupata elimu bora na si bora elimu. Pili mimi mwenyewe nilipenda sana kilimo na ufugaji. Nilikuwa mkulima mzuri na pia mfugaji. Nilipenda kufuga ng’ombe, mbuzi na kuku wa kienyeji.
Shughuli hizo za kilimo na ufugaji zilinipatia faida kubwa kutokana na kuuza mazao ninayopata kwenye kilimo na mifugo yangu.
Kabla ya kuwa mwalimu mkuu, tayari nilikuwa nimeshaoa mke ambaye nilizaa naye watoto watatu, wakike watupu. Wa kwanza nilimuita Wema, wa pili aliitwa Pili na wa tatu nilimuita Tatu.
Watoto hao walipokuwa wakubwa walikuwa wakinisaidia sana kazi za shambani kwangu baada ya muda wao wa masomo.
Wilaya nilizofanyia kazi ni Muheza, Korogwe na Handeni. Wakati nikiwa Handeni katika shule ya Msingi ya Chanika, binti yangu wa kwanza alipata mchumba. Alikuwa amemaliza kidato cha nne na kushindwa kufaulu kwenda kidato cha tano. Lakini mimi nilikataa kumuozesha mume. Nilitaka aendelee na masomo.
“Mwanangu soma kwanza halafu utakujaolewa” nilimwambia Wema ambaye alikuwa amekata tamaa baada ya kutofaulu kuendelea kidato cha tano.
Tulikubaliana na mwangu kuwa nitafute pesa ili nimpeleke chuo cha VETA kilichopo Tanga ili akasome masomo yoyote atakayopenda mwenyewe.
Miezi sita baadaye ndipo lilipotokea tukio ambalo sitalisahau hadi siku ya kufa kwangu. Mke wangu alikuwa anakwenda Korogwe kuwasalimia wazazi wake. Tulikubaliana kuwa angelala siku moja na siku ya pili yake angerudi.
Aliondoka saa moja asubuhi kwenda stendi, muda ambao na mimi niliondoka kwenda shule.
Nilifika shule dakika chache kabla ya saa moja na nusu. Kengele ya mstarini ikapigwa. Wanafunzi wakajipanga mistari chini ya mwembe. Tulifanya sala na paredi kidogo kisha niliwapa hutuba fupi wanafunzi kabla ya kuwaruhusu waingie madarasani.
Wakati nimeketi ofisini mwangu nikipanga kazi zangu nikapokea simu kutoka kwa mtu nisiyemfahamu ambaye aliniambia basi alilopanda mke wangu lilikuwa limepata ajali.
Ilikuwa taarifa iliyonishitusha lakini sikuwa na sababu yoyote ya kuitilia shaka kwani licha ya kutokumfahamu mtu aliyenipigia simu hiyo, mimi mwenyewe nilikuwa maarufu. Nilikuwa nikifahamika na watu ambao mimi mwenyewe nilikuwa siwajui kutokana na kazi yangu ya ualimu.
“Ni basi gani lililopata ajali?” nikamuuliza mtu aliyenipigia.
“Ni basi la Mamujeez, lililokuwa linaenda Korogwe’
N kweli kuwa mke wangu aliniambia kuwa angepanda basi hilo linaloondoka saa moja na nusu asubuhi kwenda Korogwe.
“Limepata ajali sehemu gani?’
“Ni mwendo wa kilometa tatu tu kutoka hapa Handeni. Watu watatu wamekufa hapo hapo na wengine wengi wamejeruhiwa”
Nikashituka na kumuuliza “Waliokufa ni akina nani?’
“Sikuwatambua lakini nimemuona mke wako amejeruhiwa vibaya na amepakiwa kwenye gari la hospitali pamoja na majeruhi wengine”
Hapo hapo mkono wangu ulioshika simu ulianza kutetemeka kwa taharuki.
“Unasema amepelekwa hospitali?” nikamuuliza mtu wa upande wa pili kwa sauti iliyoonesha wazi kufadhaika.
“Basi acha niende nikamuone. Asante sana kwa kunijulisha”
Nikaitia simu mfukoni na kunyanyuka kwenye kiti. Nilimuita msaidizi wangu na kumjulisha kuwa nilikuwa ninatoka kwenda hospitali ya wilaya.
“Kuna nini mwalimu?”
“Kuna mtu amenipigia simu ameniambia kuwa basi la Mamujeez limepata ajali na mke wangu alikuwa amepanda hilo basi kwenda Korogwe”
“Kuna abiria waliojeruhiwa?”
“Nilivyoelezwa ni kwamba mke wangu ni miongoni mwa abiria waliojeruhiwa na kupelekwa hospitali. Nataka kwenda kumuona”
Baada ya kuondoka pale shule niliona kwenda mwendo wa kawaida ningechelewa kufika huko hospitali, ikanibidi nipige mbio. Watu walioniona walishangaa.
Nilikimbia hadi hospitali ya wilaya. Ulikuwa mwendo wa karibu kilometa mbili. Nilipofika nilikuwa ninahema na shati lote lilikuwa limeloa jasho.
Niliwauliza wauguzi kama kulikuwa na majeruhi wa basi la Mamujeez lililokuwa limepata ajali.
Muuguzi mmoja niliyekuwa ninamfahamu aliniuliza majeruhi niliyekuwa namuhitaji.
“Ni mke wangu. Nimeambiwa amejeruhiwa vibaya” nikamwambia.
“Anaitwa nani?’
“Mariam Mohamed”
“Nasikitika kukwambia kuwa Mariam amefariki dunia sasa hivi”
Nikashituka na kumkazia macho muuguzi huyo.
“Mke wangu amefariki dunia?”
Muuguzi huyo aliponiona nimetaharuki aliniambia. “Hebu twende ukathibitishe wewe mwenyewe, nisije nikakutajia mtu ambaye siye”
“Hebu twende”
Nikaenda na yule muuguzi hadi Mochwari. Tulipofika alinitolea mwili wa mwanamke aliyekuwa na mavazi yaliyoloa damu.
Nilipomtazama tu niligundua kuwa alikuwa mke wangu. Ingawa nilishaona maiti nyingi katika umri wangu lakini mshituko nilioupata kwa kuiona maiti ya mke wangu ulifanya nionekane sikuwa na uzoevu wa kuona maiti.
“Loh masikini mke wangu…umeiaga dunia…kumbe ile asubuhi ndio ulikuwa unaniaga….!” Maneno yalianza kunitoka kama niliyepagawa.
“Umemuona ndiye yeye?” muuguzi akaniuliza.
“Ndiye yeye jamani!. Hivi mmehakikisha kama amekufa kweli? Isijekuwa amezirai tu!” nikamwambia muuguzi.
“Hapana. Amekufa na amethibitishwa na daktari. Kama angekuwa amezirai tusingemuweka humu”
“Alhamdulilahi!” nikabaki kushukuru.
Tulitoka na yule muuguzi katika kile chumba. Nilikuwa nimetoa kitambaa cha mkononi nikajifuta jasho na machozi usoni mwangu.
“Mke wangu ndio umekufa kweli?” nikawa najisemea peke yangu.
“Mbele yake, nyuma yetu. Sote sisi ni njia hiyo hiyo” Muuguzi akaniambia lakini uso wake haukuonesha hata chembe ya huruma.
“Ni kweli lakini ametangulia ghafla bila kutazamia. Asubuhi tulikuwa pamoja….” Nilishindwa kuendelea kumueleza. Nikajifuta tena machozi yaliyokuwa yakinitiririka.
Zile kumbukumbu za kuagana na mke wangu asubuhi zilikuwa zikijirudia akilini mwangu kama sinema inayorudia tukio lililopita.
“Sasa uende ukawaarifu ndugu na jamaa, muje muuchukue mwili wa marehemu. Cheti cha kifo chake kitakuwa kimeshatayarishwa na daktari” muuguzi akaniambia.
Nikaondoka hapo hospitali na kurudi nyumbani. Niliwaarifu wanangu ambao walipopata taarifa ya kifo cha mama yao waliangua kilio. Nikawapigia simu ndugu, jamaaa, marafiki na watu mbalimbali wakiwemo walimu wenzangu.
ITAENDELEA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 02
Mwili wa marehemu mke wangu ulichukuliwa hospitali siku ile ile na kuzikwa siku ya pili yake saa kumi jioni. Ulizikwa hapo hapo Chanika, Handeni..
Msiba wa mke wangu ulinitia majonzi makubwa kwani ulitokea wakati ambao sikuutarajia. Ulikuwa ni wakati ambapo nilihitaji sana ushauri wa mke wangu na ushirikiano wake katika kuendeleza maisha yetu.
Kuondoka kwake kuliniachia pengo ambalo nilihisi halitazibika wala kusahaulika maishani mwangu.
Marehemu mke wangu alikuwa amechangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo yangu hadi kuwa mwalimu mkuu niliyekuwa nikiheshimika katika wilaya zote nilizofanya kazi.
Siku ile ya kwanza ya msiba wetu ilikuwa ngumu sana kwangu na kwa wanangu ambao walilia sana. Lakini ndugu, jamaa na marafiki walitufariji sana. Kazini nilipata ruhusa ya siku tatu. Siku ya nne nikaanza kazi. Nilianza kazi nikiwa nimekosa uchangamfu wa kawaida. Karibu kazi zangu nyingi alikuwa akizifanya msaidizi wangu.
Mara nyingi nilipokuwa ofisini nilikuwa naduwaa tu nikimkumbuka mke wangu. Mara nyingine machozi yalikuwa yakinitoka bila kujitambua.
Baada ya siku saba niliwaita wanangu wote Wema, Pili na Tatu. Ilikuwa siku ya jumapili ambayo sikwenda kazini.
“Wanangu nimewaita ili tuelezane mawili matatu. Tangu mama yenu alipotutoka sijakaa na nyinyi tukazungumza” nikawambia.
“Mama yenu ametangulia mbele ya haki, na sisi tutafuata kila mmoja kwa wakati wake. Kwanza nataka niwambie kwamba msiwe na majonzi sana kwani kifo ni kawaida kwa binaadamu. Kila mtu kitamtokea. Ni kweli mtu akifiwa anahuzunika lakini mwisho wake anashukuru na kusahau”
“Ni kweli baba” Wema akanikubalia maneno yangu.
“Kwanza nilitaka mlijue hilo ili msikae mkahuzunika sana. Msione kuondoka kwa mama yenu ndio mwisho wa maisha. Hapana. Yeye ameondoka lakini sisi tupo. La pili nililotaka kuwambia ni kuwa nyinyi ndio mtakaoshika nafasi ya mama yenu hasa wewe Wema ambaye ndiye mkubwa. Umenielewa Wema?”
“Ndio baba, nimekuelewa”
“Utunzaji wa nyumba sasa ninawategemea nyinyi. Kazi za shamba, kuangalia mifugo yetu, sasa ni jukumu lenu nyinyi na mimi. Msingoje mpaka niwahimize au niwakumbushe. Nataka muwajibike nyinyi wenyewe, muone kuwa mna wajibu. Sawa jamani?”
“Sawa baba tumekuelewa” Safari hii alinikubalia Pili.
“Kama mmenielewa asanteni sana. Sasa mnaweza kwenda kuendelea na shughuli zenu”
Jumatatu yake nikaenda zangu kazini. Wakati niko ofisini mwangu, wanafunzi wakifanya usafi katika eneo la shule niliona mwanafunzi mmoja wa kiume amebebwa na wenzake akiletwa ofisini. Kulikuwa na walimu wawili wakiwafuata nyuma.
“Kuna nini?” nikawauliza.
“Amegongwa na nyoka?” Mwanafunzi mmoja aliniambia akinionesha yule mwenzao waliyembeba ambaye alikuwa akitokwa na damu mguuni.
Nikashituka na kuwauliza. “Amegongwa wapi?”
“Amegongwa pale, tulikuwa tunalima”
Niliondoka haraka kwenye kiti.
“Hebu tafuteni kamba au mpira tumfunge haraka, sumu isipande” nikawambia huku nimesimama.
Wanafunzi hao walimuacha mwenzao pale chini wakatoka mbio. Nikainama na kumbana kwa mikono yule mwanafunzi juu ya ile sehemu iliyokuwa inatoka damu.
Baada ya muda kidogo wale wanafunzi walirudi kila mmoja akiwa ameshika kipande cha kamba. Mmoja alikuwa ameshika kipande ch mpira wa ndani wa tairi uliokuwa umekatwa upapi.
“Lete huo mpira” nikamwambia yule aliyeshika mpira.
Aliponipa niliufunga juu ya pale mahali palipogongwa na nyoka, nikapakaza.
Wale walimu wawili walinishauri tumpeleke kwa mganga mmoja aliyeitwa Sumuyanyoka ambaye alikuwa maarufu kwa tiba za nyoka. Hakuwa akiishi mbali na eneo la shule.
“Kwanini tusimpeleke hospitali moja kwa moja?” nikawauliza.
“Tumpeleke kote kote. Tuanze na kwa yule mganga kisha tumpeleke hospitali” Mwalimu mmoja akaniambia.
“Haitakiwi upite muda mrefu kabla ya kupata tiba ya hospitali. Huyo mganga atamtibu kwa muda gani?” nikamuuliza mwalimu huyo.
“Ni dakika moja tu. Anamchanja na kumpa dawa yake”
“Basi tuharakisheni mara moja”
Tulikuwa na machela yetu pale shule. Tukamlaza yule mwanafunzi kwenye machela kisha wanafunzi wenzake wakamuinua na kwenda naye. Mimi na mwalimu mmoja tukawafuata nyuma.
Tulikwenda hadi alikokuwa akiishi mganga wa kienyeji aliyeitwa Sumuyanyoka ambaye alikuwa akisifika kwa tiba za nyoka.
Tulimkuta ameketi barazani akinusanusa tumbaku.
“Ana nini?” akatuuliza.
“Amegongwa na nyoka” Wanafunzi wakamjibu.
“Amegongwa wapi?”
“Hapa mguuni”
Mzee akamuangalia kisha akanyanyuka.
“Subirini”
Aliingia ndani. Baada ya muda kidogo alitoka akiwa ameshika bilauli ya maji na mfuko mdogo. Alichutama akampa yule mwanafunzi bilauli ya maji kisha akampa mavumba aliyoyatoa kweye ule mfuko.
“Tia mdomoni unywe na maji” akamwambia.
Mwanafunzi huyo aliyatia mdomoni yale mavumba akayagugumia na maji.
Mganga huyo akachukua kisu na kuyachomoa meno ya nyoka mguuni kwa yule mwanafunzi kisha akamchanja chale katika lile eneo la mguu. Akampaka dawa.
“Sasa tuite Bajaji aende hospitali” nikamwambia mwalimu mwenzangu.
“Sawa. Tutaenda naye mara moja”
Nikatoa simu yangu ya mkononi na kumpigia mwenye Bajaji niliyekuwa namfahamu.
Yule mzee aliposikia naita Bajaji aliniambia. “Hakuna haja tena ya kumpeleka hospitali, atapona tu kwa dawa zangu”
“Inabidi tumpeleke hospitali kwa sababu za kiserikali. Amegongwa na joka akiwa shuleni, hata kama tumemtibu kwa dawa za kienyeji bado tunalazimika kumpeleka hospitali. Vinginevyo tutakuwa tunafanya kosa” nikamwambia mzee huyo ambaye alikubali lakini alionesha kutoridhika.
Baada ya dakika chache bajaji iliwasili. Tukampakia yule mwanafunzi. Mwalimu mwenzangu akaenda naye hospitali. Mimi na wanafunzi wengine tukarudi shule.
Baada ya masaa mawili yule mwalimu alirudi.
“Imekuwaje?” nikamuuliza.
:Juma amepata huduma” akaniambia “Amepewa kitanda”
“Sasa ni vizuri tuwajulishe wazazi wake”
“Amenielekeza kwao, wakati narudi nimepitia nyumbani kwao. Nimeshawambia wazazi wake”
“Umefanya vizuri sana. Watakuwa wanakwenda kumuangalia”
“Ile dawa ya Sumuyanyoka imemsaidia sana. Amechangamka sana, sema mguu wake ulivimba kidogo kwa sababu tuliufunga kuzuia sumu isipande”
“Namuombea apone haraka ili wazazi wake wasiendelee kuwa na wasiwasi”
Nilipotoka shule saa tisa mchana nilikwenda moja kwa moja hospitalini kumtazama mwanafunzi huyo. Nikamkuta amewekwa dripu.
“Unajionaje Juma?”
“Sijambo sasa” Juma akaniambia. Sauti yake ilionesha kuwa hajambo kweli. Hali yake ilikuwa tofauti na ilivyokuwa wakati wa asubuhi.
“Wazazi wako wamekuja kukutazama?’
“Wamekuja na watakuja tena jioni”
“Basi ugua pole. Nitakuja kukuona tena kesho kama bado utakuwa upo hospitali”
“Asante mwalimu”
Nikatoka hapo hospitali na kurudi nyumbani kwangu.
Kama kawaida yangu nilipofika nyumbani nilianza kazi ya kuhudumia mifugo yangu iliyonichukua hadi saa kumi na mbili nilipooga na kupumzika.
Saa mbili usiku tulikula chakula cha usiku. Baada ya hapo niliendelea kukaa sebuleni nikiandaa kazi zangu za kesho yake. Wanangu Wema, Pili na Tatu walikuwa wameketi uani wakizungumza.
Ilipofika saa nne usiku nilimwambia Wema na wenzake waende kulala na mimi nikaingia chumbani kwangu.
Usiku ule kulinyesha mvua iliyonipa faraja. Si faraja ya kupata usingizi mnono tu bali pia faraja yakustawi mazao yangu shambani.
Nikajikuta nawaza mengi. Mawazo yangu yalikwenda mbali, nikakumbuka siku niliyokutana na marehemu mama watoto wangu. Ilikuwa ni usiku na kulinyesha mvua kama ile.
Tulikutana Korogwe. Sote tulikuwa tunasubiri gari twende Muheza. Wakati ule nilikuwa nafundisha shule ya msingi ya Muheza na nilikuwa nimekwenda Korogwe kufuatia msiba wa rafiki yangu.
Ilikuwa siku ya jumapili ambapo jumatatu yake nilitakiwa kazini. Maziko yalikuwa yamefanyika jioni. Mpaka tunamaliza kuzika, mabasi yote yanayokwenda Tanga na Muheza yalikuwa yameshaondoka. Sasa ilinibidi nisubiri mabasi yanayokwenda Tanga yakitokea Arusha.
Hapo ndipo nilipokutana na Mariam ambaye bila kujua ndiye aliyekuja kuwa mke wangu. Wakati tunasubiri basi kutoka Arusha tulinyeshewa na mvua lakini hatukukata tamaa. Tulisubiri hadi basi lililotoka Arusha likatuchukua.
Mimi na Mariam tulikaa katika siti zinazofuatana na kuanza kuzungumza na kufahamiana. Yeye alikuwa mwenyeji wa Handeni lakini alikuwa akifanya kazi Muheza.
Tulipofika Muheza tulipeana namba za simu. Ndio ukawa mwanzo wa mawasiliano yaliyozaa mapenzi na hatimaye uchumba na kuoana.
Sikujua niliwaza kwa muda gani kwani usingizi ulinipitia bila kujijua, nikalala.
Nikiwa katika usingizi mzito nilishitushwa na kishindo. Nikaamka na kufumbua macho. Niliwasha taa na kutega masikio huku nikijiuliza nimesikia nini.
Baadaye kidigo nilisikia mlango wa nje unabishwa. Ile mvua ilianza kunyesha tena kwa nguvu.
Nikashituka kitandani na kutoka ukumbini. Nikawasha taa. Mlango wa mbele uliendelea kubishwa. Sikuweza kujua alikuwa nani aliyekuwa akibisha mlango usiku ule.
Nikasogea kando ya mlango na kuuliza “Wewe nani?’
Nilisikia sauti kama ya mwanamke ikijibu lakini kutokana na mvumo wa mvua sikuweza kusikia ilijibu nini.
Nikashawishika kufungua mlango nikidhani pengine ni jirani amepatwa na matatizo, anaomba msaada.
Nilipofungua mlango nilipigwa na bumbuazi. Kama nisingekuwa jasiri, bila shaka ningeanguka na kuzirai kwa mshituko.
Unadhani alikuwa nani?
Alikuwa ni marehemu mke wangu, Mariam. Alikuwa amesimamama mbele ya mlango akinitazama. Alionekana kama alivyokuwa mochwari siku ile alipopata ajali na kufariki dunia. Nywele zake zilikuwa zimetimka na uso wake ulitepeta. Nguo aliyokuwa amevaa ilikuwa ni ile ile na ilikuwa imechanika vile vile na kutapakaa damu.
Mariam mwenyewe alikuwa mweusi na alichafuka kwa udongo wa kaburini.
Alikuwa ametota na mvua chapa!
Mkononi alikwa ameshika bahasha ya barua. Akaninyooshea mkono na kunipa ile bahasha. Nikaipokea haraka na kukimbilia kuifungua. Nilitoa barua iliyokuwa ndani yake na kuikunjua. Ilikuwa na mstari mmoja tu ulioandikwa.
“BADO SIKU SABA, MWANAO WEMA ATAKUFA!”
Je nini kitatokea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
MWANZO
Hebu jaribu kuwaza, upo ofisini kwako. Unapata taarifa kuwa mke wako kipenzi amepata ajali ya gari. Walioshuhudia wanakwambia watu watatu wamekufa hapo hapo na mke wako amepakiwa katika gari la hospitali akiwa mahututi huku nguo zake zimetapakaa damu.
Unaiacha ofisi na kutoka mbio ukiwa umerukwa na akili. Unapofika hospitali, mke wako ndio anakata roho kwenye wodi ya majeruhi.
Mwezi mmoja baada ya msiba wa mke wako unagutushwa usingizini saa tisa usiku na mtu aliyegonga mlango wa nyumba yako. Unapofungua mlango unamkuta mke wako aliyekufa mwezi mmoja uliopita akiwa amesimama mbele ya mlango akiwa na barua mkononi.
Ukimtazama hana tofauti na siku ile aliyokufa. Amevaa nguo zake zile zile zilizochanikachanika kutokana na ajali na mwili wake umetapakaa damu nyeusi iliyoganda!. Anakupa barua iliyokuwa mkononi mwake.
Unapoikunjua na kuisoma, imeandikwa.
“Bado wiki moja na wewe utakufa!”
Bila shaka utanishituka sana….
Sasa endelea.
Naitwa Hashim Mustafa. Kazi yangu ni ualimu. Umri wangu sasa unakaribia miaka arobaini na mitano. Nimeshafanya kazi ya ualimu katika shule mbalimbali za msingi za mkoa wa Tanga hadi kuteuliwa kuwa mwalimu mkuu.
Sikuteuliwa ualimu mkuu kwa rushwa, ukabila wala kujuana kama inavyotokea kwa baadhi ya walimu, bali niliteuliwa kutokana na uwezo wangu, elimu yangu na uzoevu wangu katika kazi za ualimu.
Baada ya kuwa mwalimu mkuu, shule nilizopewa zilikuwa zikifanya vizuri mwaka hadi mwaka na kunisababishia kupata sifa nyingi.
Binafsi nilipenda sana kufundisha shule za vijijini kwa sababu walimu wengi walikuwa hawazipendi kutokana na mazigira ya vijiji vyetu kutoridhisha kwa walimu.
Lakini mimi nilikuwa na sababu zangu za kupenda shule hizo. Kwanza ni kuwapa haki watoto wa vijijini na wao kupata elimu bora na si bora elimu. Pili mimi mwenyewe nilipenda sana kilimo na ufugaji. Nilikuwa mkulima mzuri na pia mfugaji. Nilipenda kufuga ng’ombe, mbuzi na kuku wa kienyeji.
Shughuli hizo za kilimo na ufugaji zilinipatia faida kubwa kutokana na kuuza mazao ninayopata kwenye kilimo na mifugo yangu.
Kabla ya kuwa mwalimu mkuu, tayari nilikuwa nimeshaoa mke ambaye nilizaa naye watoto watatu, wakike watupu. Wa kwanza nilimuita Wema, wa pili aliitwa Pili na wa tatu nilimuita Tatu.
Watoto hao walipokuwa wakubwa walikuwa wakinisaidia sana kazi za shambani kwangu baada ya muda wao wa masomo.
Wilaya nilizofanyia kazi ni Muheza, Korogwe na Handeni. Wakati nikiwa Handeni katika shule ya Msingi ya Chanika, binti yangu wa kwanza alipata mchumba. Alikuwa amemaliza kidato cha nne na kushindwa kufaulu kwenda kidato cha tano. Lakini mimi nilikataa kumuozesha mume. Nilitaka aendelee na masomo.
“Mwanangu soma kwanza halafu utakujaolewa” nilimwambia Wema ambaye alikuwa amekata tamaa baada ya kutofaulu kuendelea kidato cha tano.
Tulikubaliana na mwangu kuwa nitafute pesa ili nimpeleke chuo cha VETA kilichopo Tanga ili akasome masomo yoyote atakayopenda mwenyewe.
Miezi sita baadaye ndipo lilipotokea tukio ambalo sitalisahau hadi siku ya kufa kwangu. Mke wangu alikuwa anakwenda Korogwe kuwasalimia wazazi wake. Tulikubaliana kuwa angelala siku moja na siku ya pili yake angerudi.
Aliondoka saa moja asubuhi kwenda stendi, muda ambao na mimi niliondoka kwenda shule.
Nilifika shule dakika chache kabla ya saa moja na nusu. Kengele ya mstarini ikapigwa. Wanafunzi wakajipanga mistari chini ya mwembe. Tulifanya sala na paredi kidogo kisha niliwapa hutuba fupi wanafunzi kabla ya kuwaruhusu waingie madarasani.
Wakati nimeketi ofisini mwangu nikipanga kazi zangu nikapokea simu kutoka kwa mtu nisiyemfahamu ambaye aliniambia basi alilopanda mke wangu lilikuwa limepata ajali.
Ilikuwa taarifa iliyonishitusha lakini sikuwa na sababu yoyote ya kuitilia shaka kwani licha ya kutokumfahamu mtu aliyenipigia simu hiyo, mimi mwenyewe nilikuwa maarufu. Nilikuwa nikifahamika na watu ambao mimi mwenyewe nilikuwa siwajui kutokana na kazi yangu ya ualimu.
“Ni basi gani lililopata ajali?” nikamuuliza mtu aliyenipigia.
“Ni basi la Mamujeez, lililokuwa linaenda Korogwe’
N kweli kuwa mke wangu aliniambia kuwa angepanda basi hilo linaloondoka saa moja na nusu asubuhi kwenda Korogwe.
“Limepata ajali sehemu gani?’
“Ni mwendo wa kilometa tatu tu kutoka hapa Handeni. Watu watatu wamekufa hapo hapo na wengine wengi wamejeruhiwa”
Nikashituka na kumuuliza “Waliokufa ni akina nani?’
“Sikuwatambua lakini nimemuona mke wako amejeruhiwa vibaya na amepakiwa kwenye gari la hospitali pamoja na majeruhi wengine”
Hapo hapo mkono wangu ulioshika simu ulianza kutetemeka kwa taharuki.
“Unasema amepelekwa hospitali?” nikamuuliza mtu wa upande wa pili kwa sauti iliyoonesha wazi kufadhaika.
“Basi acha niende nikamuone. Asante sana kwa kunijulisha”
Nikaitia simu mfukoni na kunyanyuka kwenye kiti. Nilimuita msaidizi wangu na kumjulisha kuwa nilikuwa ninatoka kwenda hospitali ya wilaya.
“Kuna nini mwalimu?”
“Kuna mtu amenipigia simu ameniambia kuwa basi la Mamujeez limepata ajali na mke wangu alikuwa amepanda hilo basi kwenda Korogwe”
“Kuna abiria waliojeruhiwa?”
“Nilivyoelezwa ni kwamba mke wangu ni miongoni mwa abiria waliojeruhiwa na kupelekwa hospitali. Nataka kwenda kumuona”
Baada ya kuondoka pale shule niliona kwenda mwendo wa kawaida ningechelewa kufika huko hospitali, ikanibidi nipige mbio. Watu walioniona walishangaa.
Nilikimbia hadi hospitali ya wilaya. Ulikuwa mwendo wa karibu kilometa mbili. Nilipofika nilikuwa ninahema na shati lote lilikuwa limeloa jasho.
Niliwauliza wauguzi kama kulikuwa na majeruhi wa basi la Mamujeez lililokuwa limepata ajali.
Muuguzi mmoja niliyekuwa ninamfahamu aliniuliza majeruhi niliyekuwa namuhitaji.
“Ni mke wangu. Nimeambiwa amejeruhiwa vibaya” nikamwambia.
“Anaitwa nani?’
“Mariam Mohamed”
“Nasikitika kukwambia kuwa Mariam amefariki dunia sasa hivi”
Nikashituka na kumkazia macho muuguzi huyo.
“Mke wangu amefariki dunia?”
Muuguzi huyo aliponiona nimetaharuki aliniambia. “Hebu twende ukathibitishe wewe mwenyewe, nisije nikakutajia mtu ambaye siye”
“Hebu twende”
Nikaenda na yule muuguzi hadi Mochwari. Tulipofika alinitolea mwili wa mwanamke aliyekuwa na mavazi yaliyoloa damu.
Nilipomtazama tu niligundua kuwa alikuwa mke wangu. Ingawa nilishaona maiti nyingi katika umri wangu lakini mshituko nilioupata kwa kuiona maiti ya mke wangu ulifanya nionekane sikuwa na uzoevu wa kuona maiti.
“Loh masikini mke wangu…umeiaga dunia…kumbe ile asubuhi ndio ulikuwa unaniaga….!” Maneno yalianza kunitoka kama niliyepagawa.
“Umemuona ndiye yeye?” muuguzi akaniuliza.
“Ndiye yeye jamani!. Hivi mmehakikisha kama amekufa kweli? Isijekuwa amezirai tu!” nikamwambia muuguzi.
“Hapana. Amekufa na amethibitishwa na daktari. Kama angekuwa amezirai tusingemuweka humu”
“Alhamdulilahi!” nikabaki kushukuru.
Tulitoka na yule muuguzi katika kile chumba. Nilikuwa nimetoa kitambaa cha mkononi nikajifuta jasho na machozi usoni mwangu.
“Mke wangu ndio umekufa kweli?” nikawa najisemea peke yangu.
“Mbele yake, nyuma yetu. Sote sisi ni njia hiyo hiyo” Muuguzi akaniambia lakini uso wake haukuonesha hata chembe ya huruma.
“Ni kweli lakini ametangulia ghafla bila kutazamia. Asubuhi tulikuwa pamoja….” Nilishindwa kuendelea kumueleza. Nikajifuta tena machozi yaliyokuwa yakinitiririka.
Zile kumbukumbu za kuagana na mke wangu asubuhi zilikuwa zikijirudia akilini mwangu kama sinema inayorudia tukio lililopita.
“Sasa uende ukawaarifu ndugu na jamaa, muje muuchukue mwili wa marehemu. Cheti cha kifo chake kitakuwa kimeshatayarishwa na daktari” muuguzi akaniambia.
Nikaondoka hapo hospitali na kurudi nyumbani. Niliwaarifu wanangu ambao walipopata taarifa ya kifo cha mama yao waliangua kilio. Nikawapigia simu ndugu, jamaaa, marafiki na watu mbalimbali wakiwemo walimu wenzangu.
ITAENDELEA

Sent using Jamii Forums mobile app
Nzuri Sana Tunaomba mwemdelezo ndugu mrembo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA 03
Niliposoma maneno yale nilishituka sana. Nikainua uso wangu kumuangalia yule mwanamke. Lakini sikumuona tena. Alikuwa kama aliyetoroka baada ya kunipa ile barua.
Nikatoka nje kabisa na kuangalia kila upande nikidhani labda aliondoka wakati nasoma ile barua. Lakini huko nje pia sikumuona na mvua ilikuwa inanyesha.
Baada ya kushangaa shangaa kidogo nilirudi ndani nikafunga mlango. Moyo wangu ulikuwa ukienda mbio na ni wazi kuwa nilipata mshituko mkubwa. Niliwasha taa pale sebuleni nikakaa na kuisoma tena ile barua.
Baada ya kuisoma nilijiuliza, marehemu mke wangu alifufukaje kaburini na kuja kunipa hii barua?
Na ni tangu lini wafu hufufuka na kurudi tena duniani?
Na hii barua nani aliiandika?
Nilipotazama mwandiko ni wa mke wangu kabisa.
Tuseme yeye ndiye aliyeandika kunijuisha juu ya kifo cha Wema?
Alipata wapi kalamu na karatasi?
Au alipewa huko huko kuzimu. Au ni malaika waliomwambia aandike na ndio waliomleta hapa na kisha kuondoka naye?
Niliwaza kila jambo na kila nilichowaza nilikiona hakiwezekani.
Haiwezekani mke wangu kufufuka!
Na haiwezekani aniandikie mimi barua ya kunijulisha juu ya kifo cha Wema ambaye ni mwanangu na yeye pia ni mwanawe.
Haiwezekani kabisa!
Sijapata kusikia wala kuona jambo kama hili kwani haliingii akilini kabisa.
Lakini ndio limetokea. Nimemshuhudia Mariam kwa macho yangu na barua aliyonipa ipo mikononi mwangu hadi sasa.
Nikahisi labda nilikuwa kwenye ndoto. Kutokana na uzoevu wangu nilikuwa najua kuwa mtu anaweza kuota ndoto huku akitenda kweli vitendo anavyoota. Nikashuku kwamba huenda nilikuwa naota.
Kama naota, nilijiambia, nitagundua asubuhi. Acha nirudi chumbani.
Nikanyanyuka na kurudi chumbani. Ile barua niliiweka juu ya meza. Nikaweka simu yangu juu yake. Nikapanda kitandani.
Nilijaribu kufumba macho ili nilale lakini usingizi haukuja kabisa. Akili yangu yote ilikuwa kwa mke wangu aliyekufa pamoja na ile barua aliyoniletea.
Kama itakuwa si ndoto, je ni kweli mwanangu Wema atakufa kumfuata mama yake? Na kwanini afe? nikajiuliza.
Nilihisi hofu na majonzi kwa pamoja. Kama mwanagu atakufa kweli litakuwa ni pigo jingine kwa upande wangu, nilijiambia.
Nakuhurumia mwanangu Wema unakabiliwa na tishio la kifo! nikajisemea kimoyomoyo.
Nilikaa macho na kuwaza hadi asubuhi. Kulipokucha nilishuka kitandani, nikaitazama ile barua kuona kama bado ilikuwepo. Kama isingekuwepo ningegundua kuwa lile tukio lilikuwa ndoto. Lakini barua niliikuta vilevile juu ya meza kama nilivyoiweka usiku.
Sasa hapo niliamini kuwa lile tukio lilikuwa la kweli. Mke wangu alifufuka kweli kaburini na kuniletea ile barua. Sasa hofu yangu iliongezeka mara mbili. Kwanza ilikuwa hofu ya kutokewa na tukio la ajabu kama lile. Na pili hofu ya kufa mwanangu Wema!
Hofu hizo mbili zilinichanganya akili yangu. Niliishika tena ile bahasha nikaifungua na kuisoma barua iliyokuwemo ndani. Haikuwa imebadilika. Ujumbe ulikuwa ni ule ule.
BADO SIKU SABA MWANAO WEMA ATAKUFA!
Moyo ulinishituka tena kama vile ndio naanza kuisoma sasa. Kulihitajika moyo kukivumilia kitisho kama kile! Na ni ukweli kwamba kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angeweza kulipuuza tukio lile hata angekuwa mpuuzaji kiasi gani. Nilitumia ujasiri wangu wote kuhakikisha kuwa ninaimudu hofu yangu.
Nikafikiria niwaite wanangu niwaeleze kuhusu lile tukio pamoja na kuwaonesha ile barua lakini akili yangu ilikataa.
Ilikataa kwa sababu niliona wanangu walikuwa bado wadogo na wanaweza kupata mshituko mkubwa ambao ungeweza kuwasababishia madhara.
Kwa upande wa Wema ambaye ndiye aliyeelezwa kuwa atakufa isingekuwa vyema kwake kulijua jambo hilo.
Nikaamua nisiwaite wala nisiwaeleze chochote.
Nilitoka mle chumbani nikaenda kuoga. Wakati narudi kutoka bafuni Wema na wenzake walikuwa wameshaamka na walikuwa wakifanya usafi wa nyumba.
Baada ya kuvaa nilichukua ile bahasha nikamuita Wema na kumuachia pesa za matumizi na kisha nikatoka kwenda kazini.
Huko shule pia sikuweza kufanya kazi yoyote. Nikamuachia ofisi msaidizi wangu nikaenda kwa ndugu yangu mmoja aliyeitwa Kassim. Kassim alikuwa anafanya kazi katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Handeni.
Niliingia ofisini kwake na kusalimiana naye.
“Karibu mwalimu” alinikaribisha kiti.
Nikaketi.
“Nimekuja kukueleza tukio lililonitokea jana usiku” nikamwambia Kassim
“Tukio gani?’
“Jana usiku wakati nimelala alikuja mtu akabisha mlabgo wa mbele wa nyumba yangu. Nikaamka na kutoka ukumbini. Nilipomuuliza wewe nani akanijibu lakini sikuweza kumsikia vizuri kwa sababu mvua ilikuwa inanyesha ila sauti yake ilikuwa ya kike. Basi nikadhani alikuwa jirani amepata tatizo, nikaenda kufungua mlango”
“Kumbe walikuwa wezi? Mustafa akadakia kuuliza.
“Hapana, hawakuwa wezi. Ni afadhali wangekuwa wezi. Wizi ni jambo la kawaida tu”
“Kumbe alikuwa nani?”
“Alikuwa matrehemu mke wangu!”
“Shemeji ndiye aliyekuwa anakubishia mlango?” Kassim alishituka.
“Ndiye yeye!”
“Haiwezekani!”
“Kassim hilo tukio ni la ajabu. Mpaka muda huu moyo wangu haujakaa sawa!” nilimwambia Kassim kwa mkazo.
“Sasa ulivyoona ni yeye ikawaje?”
“Subiri nitakueleza. Kwanza vile alivyokuwa ni kama siku ile nilivyomuona mochwari. Alikuwa amevaa nguo zilezile na zilikuwa zimechafuka na kujaa damu. Yeye mwenyewe alikuwa amechafuka kwa udongo”
“Sasa alikwambia nini?”
“Hakuniambia kitu. Nilipofungua mlango alinipa barua, nikaipokea na kuisoma. Iliandikwa “Bado siku saba mwanao Wema atakufa”
“Mwalimu si kwamba ulikuwa unaota?” Kassim akaniuliza akiwa amekunja uso.
“Si ndoto, ni tukio la kweli. Barua yenyewe hii hapa, nimekuletea uisome”
Nikaitoa ile barua na kumpa.
Kassim akaikunjua na kuisoma.
“Huo mwandiko ni wa mke wangu” nikamwambia Kassim wakati akisoma ile barua.
Kassim akatikisa kichwa kwa mshangao.
“Sasa mlipozunguma alikwambia anatoka wapi?’
“Hatukuzungumza. Wakati nasoma hii barua alitoweka pale pale. Nilipomaliza kuisoma sikumuona tena”
“Hilo tukio ni la ajabu sana. Marehemu kutoka kaburini na kukuletea barua….!”
“Hebu nisaidie ndugu yangu kunipa mawazo. Sijamueleza mtu yeyote. Nimekuja kukueleza wewe ndugu yangu”
“Kwa kweli mimi sijapata kusikia wala kuona tukio kama hilo. Ninashangaa sana”
“Tuseme ndio ameagizwa huko kuzimu aje aniletee barua hii ya kunijulisha kuwa mwanangu atakufa?’
Kassim akatikisa kichwa.
“Hapo sina jibu ndugu yangu”
“Na kwa upande wa huyu mwanangu unalichukuliaje suala hili? Ni kweli kuwa atakufa baada ya siku saba?”
“Hapo inabidi tujiulize tena, kama atakufa ni kwanini afe?”
“Sioni kama tutakuwa na jibu”
“Sasa sikiliza mwalimu, hebu twende kwa sheikh tumueleze kuhusu hilo tukio. Tusikie atatueleza nini?”
“Sawa twende. Mimi hata ukinishauri twende wapi tutakwenda”
Dakika chache baadaye mimi na Kassim tukawa njiani kuelekea nyumbani kwa sheikh mmoja, imamu wa msikiti mkuu wa Chanika.
“Unaonaje twende nyumbani kwake moja kwa moja au tupitie msikitini kwake?” Kassim akaniuliza.
“Sidhani kama atakuwa msikitini muda huu kwa sababu saa ya swala bado”
“Lakini acha tupite tu pale msikitini. Kama atakuwa hayupo tutaenda nyumbani kwake”
“Sawa”
Tulipitia katika msikitini ambao sheikh huyo alikuwa anaswalisha, tukaambiwa kuwa sheikh huyo alikuwa hajafika. Tukaenda nyumbani kwake ambako hakukuwa mbali na msikiti huo.
ITAENDELEA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom