#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

UPDATE: FRIDAY 17 SEPTEMBER 2021

J2 YA TAREHE 05 SEPTEMBER 2021 HAPAKUWA NA TANGAZO LOLOTE “KANISA A” LA KUWA JULISHA WAUMINI KUWA KUTAKUWA NA UJIO WA WATUMISHI (WAHUDUMU) WAGENI J2 ILIYOKUWA INAFUATA YA TAREHE 12 SEPTEMBER 2021

COINCIDENCE (YA KAWAIDA TU) ILIYOTOKEA BAADA YA WATUMISHI WOTE WENYEJI WA KANISA A KUTOKUSIMAMA MADHABAHUNI J2 HIYO YA TAREHE 12 SEPTEMBER 2021


Ni kwamba somewhere kuna msiba mzito umetokea, wiki hii

Kwa kawaida yake, mara zote mhusika amekuwa akifuatilia sana swala la nani alisimama madhabahuni J2 iliyopita, kufuatia wiki ya tukio lolote la msiba linalokuwa limempata

Safari hii imekuwa tofauti kidogo kwamba amepata tukio la msiba kwenye wiki ambayo J2 iliyopita hapakuwa na mhudumu mwenyeji aliyesimama kwenye madhafbahu ya Kanisa A kwa ajili ya huduma ya Ibada ya J2
  • Badala yake kulikuwa na wahudumu wageni ambao tangazo la ujio wao halikuwa limetolewa J2 ya nyuma yake
  • Ujio wa wahudumu hao wageni ulikuwa wa ghafla na kwa waumini walio wengi, na ulijulikana siku hiyo hiyo ya J2 ambayo watumishi hao wageni waliletwa kuja kutoa huduma
Inaonyesha kama watumishi wenyeji walijua kuwa kutakuwa na tukio baada ya J2 hiyo na hivyo wao wenyewe kuamua kukwepa kupanda madhabahuni kwa ajili ya kutoa huduma

Mhusika ameamua kuileta kwenu coincidence hii kwa sababu hata huko nyuma alishawahi kutanhibisha kuwa kuna baadhi ya J2 ambazo watumishi wa Kanisa A huwa wanakakwepa kupanda madhabahuni wao wenyewe hasa pale wanapokuwa wamejua kuwa wiki inayofuata kutakuwa na tukio lisilo zuri.

Huwa wanafanya hivyo katika kujaribu kupunguza maswali kwamba ‘NANI ALISIMAMA MADHABAHUNI J2 HIYO”?

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
Audio clip nyingine yenye makofi ya "NAOMBA WALIOKAA TUSIMAME" hii hapa



Hata hivyo, kwenye post hii #592 mhusika aliwahi kumpongeza sana KM-A kwa fundisho lake alilowahi kulitoa kwenye Ibada ya J2 ya tarehe 22.03.2021
 
UPDATE: MONDAY 20 SEPTEMBER 2021

MHUSIKA ANAJUTIA SANA KOSA ALILOFANYA KWA KUWAHI KUTOA POST HII HAPA #784


Post hiyo hapa tajwa alitakiwa assitoe kabla ya J2 iliyopita ya tarehe 19 Septemba 2021. Post hii amewahi kuitoa na hivyo kupelekea kuharibu utafiti wake ambao angeweza kuuthibitisha J2 iliyopita, iwapo tu asingekuwa ameitoa post hiyo kabla ya J2 tajwa

Utafiti huu unahusiana na ratiba ya Kiongozi Mkuu Kanisa A (KM-A) kuwa na ratiba ya kuhudumu madhabahuni siku za J2, kila unapokuwa umetokea msiba ndani ya siku za wiki hiyo

Kuhusiana na ratiba ya kiongozi huyu, mhusika alikuwa tayari ameshakusanya data za myakati tofauti tofauti kuanzia mwanzoni mwa March 2020 (mwaka jana) hadi April 2021 (mwaka huu), kila mhusika anapokuwa amepata mhusika

TUKIO LA KWANZA

Ni kwamba mwanzoni mwa march 2020, KM-A alisimama kuhudumu Ibada kuu madhabahuni
  • Siku ya J2 ambayo ndani ya wiki hiyo kulikuwa kumetokea msiba mkubwa
  • J2 iliyokuwa imepita nyuma yake, yaani kabla ya hiyo aliyosimama kuhudumu, kulikuwa na MHUDUMU MGENI Kanisani, hakuna mwenyeji aliyehudumu madhabauni J2 hiyo
MATUKIO MENGINE YALIYOFUATA
Vile vile, mwishoni mwa Julai 2020, KM-A alisimama kuhudumu Ibada kuu madhabahuni
  • Siku ya J2 ambayo ndani ya wiki hiyo mhusika mwenyewe binafsi alipata msiba mkubwa.
  • J2 iliyokuwa imepita nyuma yake, yaani kabla ya hiyo aliyosimama kuhudumu, kulikuwa na MHUDUMU MGENI Kanisani, hakuna mwenyeji aliyehudumu madhabauni J2 hiyo
Kama hiyo haitoshi, mwishoni April 2021, KM-A alisimama tena kuhudumu Ibada kuu madhabahuni
  • Siku ya J2 ambayo ndani ya wiki hiyo mhusika mwenyewe binafsi alipata msiba mkubwa
  • J2 iliyokuwa imepita nyuma yake, safari hii kulikuwa na MHUDUMU MWENYEJI KANISANI, isipokuwa alikuwa ni mmojawapo ya hawa vijana ambao wameanza kazi ya uchungaji hivi karibuni. WAZOEFU WOTE hawakuwa kwenye ratiba ya huduma madhabahuni siku hiyo
HITIMISHO
Ndani ya wiki iliyopita yenye kuishia tarehe 19 Septemba 2021, kwa mara nyingine tena mhusika amepata msiba mwingine mkubwa na katika mazingira mengine ambayo
  • Wahudumu wa J2 ya wiki iliyokuwa imepita nyuma yake, yaani ile ya tarehe 12 Septemba 2021 walikuwa ni WAGENI,hakuna mwenyeji aliyehudmu J2 hiyo
  • Kama mhusika alivyowahi kusema hapo awali kwenye post yake hapo juu , ujio wa wageni hao ulikuwa ni wa ghafla na tangazo la ujio wao halikuwa limetolewa J2 ile ya 05 Septemba 2021
Kwa hiyo J2 iliyopita ya tarehe 19 Septemba 2021, mhusika alitarajia pia kuwa KM-A angesimama tena kuhudumu madhabahuni kwa sababu ni wiki ambayo ndani yake kulikuwa kumetokea msiba, ila kwa bahati mbaya mhusika alijisahau akawa ametoa post hii hapa #784 mapema kabla ya wakati. Post hiyo alitakiwa aitoe kuanzia leo na kuendelea mbele
Kuna uwezekano kuwa post hiyo imefanyika msaada kwa KM-A kumu-alert na looming danger iliyokuwa mbele yake, yaku-expose pattern ambayo tayari ilikuwa imeshaanza kupata ushahidi thabiti na wenye nguvu, just in case angeasimama madhabahuni J2 hiyo

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: WEDNESDAY 22 SEPTEMBER 2021

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA NDUGU WA MHUSIKA ALIOWAHI KUWAONGELEA KWENYE POST HII HAPA #660

WAPO NDUGU WENGINE WATATU ZAIDI WANAOWEZA KUWA NA TAARIFA ZA MSINGI SANA KUHUSIANA NA HAYA YANAYOENDELEA HUKO KIJIJINI


Mhusika atawaongelea wawili kati ya watau hawa kwa leo. Mmoja wao anaishi Ushirombo, Kahama na mwingine kwa sasa mhusika hana taarifa sahihi sana za wapi anapoishi, ila mpaka mwaka 2009 alikuwa anaishi Masanza Kona, barabara ya kuelekea Musoma
  • Yule wa ushirombo tayari kuna baadhi ya taarifa zake za awali humu ambazo mhusika aliwahi kuzileta kupita kwenye post hii hapa #175
  • Huyu ndiye ndugu ambaye hapo awali, alikuwa yuko karibu sana na mhusika na ndiye aliwahi kuwa mgeni wa kwanza kabisa nyumbani kwa wa mhusika hapa Dar es salaam, aliyekuwa ametokea kijijini kwao na mhusika
  • Ugeni wake aliufanya mwanzoni mwaka 2005 na alikaa kwa muda usipungua mwezi mmoja
  • Kuhusiana na yule mwingine aliyekuwa akiishi Masanza Kona, yeye naye aliwahi pia kufanya ugeni nyumbani kwa mhusika kati ya Septemba na Desemba 2009, na alikaa kwa muda usiopungua miezi mitatu
Wawili hawa ndiyo atakaowaongelea kwa kifupi, halafu yule mwingine wa tatu taarifa zake bado anaziandaa vizuri.

Mhusika anaamini kuwa watu hawa wan taarifa za muhimu sana ambazo watu wanatakiwa wazifahamu

…………………..inaendelea
 
NDUGU WENGINE WATATU ZAIDI WANAOWEZA KUWA NA TAARIFA ZA MSINGI

…………………..inaendelea

MAELEZO MUHIMU KUHUSIANA NA KILA MMOJAWAPO WA NDUGU HAWA:

MTU WA KWANZA: YULE ANAYEISHI USHIROMBO KWA SASA (TUMWITE USHIROMBO-X)

  • Huyu USHIROMBO-X ni motto wa kuzaliwa wa Baba Mkubwa (RIP) wa mhusika, marehemu aliyefariki mwaka 2006, baba wa mhusika na baba wa USHIROMBO-X wakiwa wamezaliwa baba mmoja mama mmoja
  • Ni mwenzao na wale wawili waliokuwa wakimuuguza marehemu hospitalini, na ambao waliwahi kukabidhi cheti cha kifo cha mzee huyo kwa mhusika
  • Ni mmojawapo ya watu wachache sana kati ya ndugu zake mhusika ambao alikuwa anawaamini mno na kuwa nao kwa ukaribu zaidi kuliko karibia ndugu zake wengine wote, na possibly hii ndiyo ilipelekea akawa mtu wa kwanza kabisa kufanya ziara ya ugeni nyumbani kwa mhusika
Ikumbukwe pia kuwa huyu mzee marehemu alifariki baada ya kuugua ghafla akiwa yuko huko Ushirombo ambako alikuwa amepitia tu na safari yake hasa alikuwa yuko safarini kuja Dar es Saalam
  • Alikuwa hajawahi kufika nyumbani kwa mhusika hata mara moja tangu mhusika aanze kazi mwka 2000
  • Angefanikiwa kufika, basi ingekuwa ni mara yake ya kwanza
Akiwa yuko huko Ushirombo, aliugua ghafla ikabidi arudi mwanza, akaenda akauguzwa hosppitalini Sumve na hatimaye kufariki dunia baada ya siku chache

PINDI MHUSIKA ALIPOKUWA AMEENDA KUHANI MSIBA WA MZEE HUYU MWAKA 2006

TABIA ZA AJABU ALIZOKUWA AKIZIIONYESHA USHIROMBO-X

USHIROMBO-X alikuwa anaonyesha hali fulani ya kuwa na “excitement” isiyokuwa ya kawaida na ambayo ilikuwa haiendani kabisa na mazingira ya tukio lililokuwa limetukia, yaani msiba
  • Alikuwa yuko “excited” katika namna ambayo alikuwa anashindwa kuficha furaha fulani aliyokuwa nayo ndani rohoni mwake, possibly pasipo yeye mwenyewe kujua hilo, ila wengine akiwemo mhusika mwenyewe, walikuwa wanamuona hivyo
  • Zaidi alikuwa anawaeleza watu wote kuwa ana mpango wa kununua Lori Semi-Trela; wakati kwa wakaati huo, hakuwa na project yoyote ya maana ambayo ingemuwezesha kununua hata pikipiki tu
Hili swala la ununuzi wa Lori alikuwa anafikia hadi hatua ya kutangaza kwenye makundi ya watu, katika namna ambayo ilionrekana kuwa ikitokea siku wakimuona ana Lori wasishangae, na alikuwa anajitahidi sana kuhakikisha kuwa watu wengi wanazipata taarifa mpango wa ununuzi wa Lori hilo.

USHIROMBO-X alifikia hadi hatua ya kutangaza juu ya ununuzi wa Lori hilo, ndani ya basi la abiria alfajiri moja siku mhusika alipokuwa anapanda basi kutoka kijijini kuelekea Mwanza tayari kwa safari yake ya kurudi Dar es salaam, mara baada ya kuwa amemaliza kuhani msiba wa Baba Mkubwa

Hata hivyo, USHIROMBO-X hajawahi ufanikiwa kununa Lori hilo, na mpaka leo hii halipo
  • Mhusika hajawahi kujua hadi leo ununuzi wa Lori hilo ulikwama wapi
  • Zaidi ni kuwa USHIROMBO-X alishakwepa kufika tena huko kijijini kipindi kirefu sasa, possibly kukwepa kuulizwa maswali na ndugu na jamaa aliokuwa anwapa taarifa za ununuzi wa Lori hilo. Hata misiba yote inayotokea huko sasa, hajawahi kufika hata siku moja
  • Hata hivyo, aadaye sana USHIROMBO-X alikuja akafanikiwa kununua pikipiki
Umbali kutoka Ushirombo kwenda nyumbani kijijini kwa pikipiki kwa ajili ya kuhani misiba, si zaidi ya masaa manne kwa mwendo wa kawaida kabisa wa wale ambao huwa hawatumii mmea ule wa kijani

Hsya ni maelezo kwa kifupi sana kuhusiana na huyu mtu anayeitwa USHIROMBO-X

MTU WA PILI: YULE ALIYEKUWA ANAISHI MASANZA KONA (TUMWITE MASANZA -X)

Huyu alihamia huko Masanza akiwa anatokea Ushirombo. Kwa hiyo hapo kabla, MASANZA –X naye pia alikuwa anaishi Ushirombo. Actually, MASANZA –X alitangulia kuhamia huko halafu USHIROMBO-X ndiyo naye akafuata baadaye. Baadaye kulikuja kutokea mkanganyiko fulani usiokuwa mzuri hapo Ushirombo; MASANZA –X akapata kesi na kwenda jela akiwa ameambtana na mdogo wake, kwa kesi ambayo hawakusingiziwa, ilikuwa ni ya kweli. Ukimwondoa USHIROMBO-X, mtu wa pili aliyekuwa anafuata kwa kuaminika na kuwa karibu sana na mhusika ni MASANZA –X

  • MASANZA –X na USHIROMBO-X ni mtu na binamu yake, wa shangazi wa mjomba, mjomba na shangazi wakiwa wamezaliwa baba mmoja mama mmoja
  • Baba yake mzazi na mhusika ni mdogo wa wazazi wa hawa wa akina MASANZA –X na USHIROMBO-X, baba mmoja mama mmoja vile vile
  • MASANZA –X ni mdogo pia wa yule mtu mrefu kuzidi karibia watu wote, ambaye yupo kwenye kundi la ndugu wale wa mwanzo ambao mhusika tayari alishawahi kuwaongelea kwenye post hii hapa #175
  • MASANZA –X na mtu mrefu kuzidi karibia watu wote wamezaliwa baba mmoja mama mmoja
KILICHOSABABISHA MASANZA –X KUHAMA KUTOKA USHIROMO KWENDA MASANZA KONA

Stori kamili inakuja na ni kwa mujibu wa maelezo ya MASANZA –X pamoja na mdogo wake ambaye walihukumiwa wote kwenda jela, kama walivyowahi kumweleza mhusika mwenyewe kwa midomo yao wenyewe baada ya kuwa wametoka jela.

Walihukumiwa kwenda jela baada ya kuingia ndani nyumbani kwa mtu usiku wakaiba na kuvunja; na kwa mtu ambaye alikuwa ni rafiki wa karibu sana na “mdogo wake na MASANZA –X”

……………..inaendelea
 
KILICHOSABABISHA MASANZA –X KUHAMA KUTOKA USHIROMBO KWENDA MASANZA KONA

………………inaendelea


Ni baada ya kushiriki kwenye tukio la wizi wa kuingia ndani usiku nyumbani mwa mtu. wenyeji wakiwa hawapo na kuiba fedha pamoja na radio. Aliyeingia ndani na kuchukua mali hizo hakuwa MASANZA –X bali mdogo wake (tumwite MDOGO-X)

NAMNA MCHORO ULIVYOFANYIKA


MDOGO-X alikuwa rafiki yake wa karibu sana na bwana mmoja mfanyabiashara hapo Ushirombo aliyekuwa anaitwa Vicent (hili ni jina halisi la mtu mwenyewe, si la bandia). Tukio lilifanyika mwishoni mwa mwaka 1997

Bwana Vicent akawa siku moja amerudi kutoka kwenye migodi hii ya wachimbaji wadogo wadogo. Alikuwa amefanikiwa kupata hela kiasi kama laki 7 hivi (kwa kipindi hiki, hela hizi zinaweza kulingana hata na million 10). Bw. Vicent akiwa amefurahi, akaamua jioni moja kuwachukua MDOGO-, rafiki yake pamoja na MASANZA –X; kwenda kupata nyama choma kwenye sehemu pekee iliyokuwa maarufua pale Ushirombo Center, ilikuwa inaitwa Bazizane Bar. Kwa bahati mbaya, siku bwana huyu anaamua kuwakirimu hivyo watu hawa, hapakuwa na watu nyumbani kwake kwa sababu alikuwa ni kijana ambaye ameoa hivi karibuni na mke wake alikuwa amesafiri

Wakati huo huo pasipo Vicent kuwa anajua, MDOGO-X na MASANZA –X walikuwa wame-set kutekeleza mpango wao siku hiyo kwa kujua kuwa nyumbani kwa Vicent hapatakuwa na mtu jioni hiyo

Hivyo siku hiyo, watatu hao wakiwa wapo Bazizane Bar
  • MDOGO-X alitoka kidogo kama anakwenda kujisaidia haja ndogo, akiwaacha MASANZA –X na Vicent wakiwa wanaendelea na vinywaji
  • Nyumbani kwa Vicent hapakuwa mbali sana na pale walipokuwa
  • MDOGO-X alinyoosha moja kwa moja hadi nyumbani kwa Vicent akaenda akaingia ndani kwa kupitia dirishani, aka-search ndani akiwa anaitafuta ile laki 7 lakini hakuiona
  • Hatimaye aliambulia kupata TZS 90/000/= akachukua hizo pamoja na redio
Redio hiyo kwa wakati huo ikaenda ikafichwa kwa muda nyumbani kwa MASANZA –X

Baada ya kama wiki mbili hivi kuwa zimepita, redio hiyo ikaja kuchukuliwa na rafiki yake na MASANZA –X aliyekuwa anaishi kijiji kingine jirani. Wakati makabidhiano ya redio hiyo yanafanyika na kwa usiri fulani ambao haukuwa wa kawaida, Msamaria mwema mwingine ndugu yao na akina MDOGO-X na MASANZA –X ambaye alikuwa amesikia taarifa za wizi ila hakuwa amejua ni akina nani walihusika, akabahatika kuiona redio hiyo
  • Huyu msamaria mwema akawa ameitambua redio hiyo kuwa ni ya Vicent na ambayo taarifa za kuibiwa kwake zilikuwa zimevuma ila alikuwa hajafanikiwa kujua ni akina nani walihusika
  • Baada ya hapo msamaria mwema alifanya utaratibu wa kwenda kumjulisha Vicent, na pia watu waliokuja kuichukua redio hiyo ambao nao pia alikuwa anawafahamu ikiwa ni pamoja na kule walikokuwa wametokea
Baada ya hapo dola ilichukua mkondo wake na hivyo kupelekea MDOGO-X na MASANZA –X kuhukumiwa kwenda jela ambako walikaa kwa miezi kadhaa na hatimaye kubahatika kutoka kabla ya kipindi cha hukumu yao kuwa kimefikia mwisho

Kwa hiyo, kwa kifupi sana, huyu ndiyo MASANZA –X, mdogo wake na mtu ambaye ni mrefu kuzidi karibia watu wote, anayeishi pale Igoma, jijini Mwanza

HITIMISHO

Maisha ya shule ya mhusika yalikuwa yameshatenganisha kwa kiasi kikubwa na ndugu zake hawa kiasi kwamba waliweza ku-develop tabia zingine za ziada na mbaya sana, ambazo mhusika hakuwa na hata lile wazo lakwamba wangeweza ku-develp tabia za namna hiyo

Kwa pcha aliyonayo mhusika kichwani kwake kwa sasa ni kwamba MASANZA –X na USHIROMBO-X, wanao uwezo wa kufanya chochote kile ili mradi tu kuna hela itapatikana baada ya kuwa wamefanya kitu hcho
  • Walipokuwa wamemtembelea nyumbani kwake mhusika kila mmoja kwa wakti wake, walikuwa wamekuja pia kutengeneza link ya mtandao unaofanya kazi huku aliko mhusika na kule waliko wao, yaani nyumbani kijijini kwao na mhusika
  • USHIROMBO-X alikuja Dare s Salaam mwanzoni mwa 2005 na mzee wake alifariki mwaka uliofuata wa 2006, ugonjwa ulimkamata akiwa yuko huko ushirombo na alikuwa yuko njiani kuelekeaDar es Salaam
  • MASANZA –X na USHIROMBO-X dhahiri walishabadilika na kuwa watu wenye tabia zingine ambazo hawakuwahi kuwa nazo hapo kabla
Swala linapokuwa linahusisha hela MASANZA –X na USHIROMBO-X, wanaweza kufanya chochote. Hawana tofauti sana na Kiongozi Mkuu wa Kanisa A

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: THURSDAY 23 SEPTEMBER 2021

MASTERMIND ANAYEENDELEA KUSABABISHA MATUKIO YA AJABU AJABU KUTOKEA KIJIJNI NYUMBANI KWAO NA MHUSIKA


Mtu huyu ndiye yule ambaye mhusika amekuwa akimtaja kama mtu mrefu kuzidi karibia watu wote (tumwite MREFU-X)

Huyu mtu MREFU-X
  • Ni kaka yao na MASANZA-X na MDOGO-X, wamezaliwa baba mmoja mama mmoja
  • MDOGO-X ana taarifa zingine ambazo si rahis sana kwa mhusika kuzitaja humu jukwaani, ila inaonyesha yeye ndiye aliwahi kutumwa kutokea huko kijijini kuja huku Dar es salaam kwa misheni maalum
  • Alitumwa kutoka huko chini ya maelekezo maalumu ya MREFU-X na kwa mara ya kwanza aliwasili hapa Dar es salaam mnamo Septemba 2001 akiwa anatokea Ushirombo, yaani miaka 20 iliyopita
Mengi zaidi yatafuata kuhusiana na mtu huyu MDOGO-X

………………….inaendelea
 
UPDATE: FRIDAY 24 SEPTEMBER 2021

MREFU-X:


MASTERMIND ANAYEENDELEA KUSABABISHA MATUKIO YA AJABU AJABU KUTOKEA KIJIJNI NYUMBANI KWAO NA MHUSIKA

……………inaendelea


Kwa namna anavyojaribu kukadria mhusika, yeye anhisi kuwa itakuwa ilikuwa ni kati ya miaka ya 1997-2000 ambapo MREFU-X aidha aliwa-train wadogo zake hawa wawili yaani MASANZA-X na MDOGO-X au aliwaunganisha na mtandao usiokuwa mzuri, na hivyo kupelekea kuwa wahalifu tema wa kiwango kile cha juu kidogo
  • Mpaka kufikia katikati ya mwaka 1997, MDOGO-X alikuwa anaishi kijijini Kwimba, Mkoani Mwanza
  • MASANZA-X yeye alikuwa tayari yuko Ushirombo kwa wakti huo
  • Mwaka huo huo wa 1997, MDOGO-X naye alihamia Ushirombo, na kuanzia pale sasa wakawa wako pamoja na MASANZA-X
Baada ya hapo sasa ndiyo wakaja wakapata ile kesi ambayo ilipelekea wakafungwa jela na baadaye wakatoka tena

Baada ya hapo MDOGO-X akawa sasa anajishughulisha na shughuli za ulinzi kwenye jeshi la akiba, ila kwa wakati ule wa mchana tu, usiku hapana. Hasa hasa alikuwa ameaminiwa kukagua bidhaa za magendo zilizokuwa zinadhaniwa kuwa zinaweza kuwa zilikuwa zinasafirishwa na watu wasiokuwa wema, kwenye bararabara kuu ya Ushirombi-Kahama

MAELEZO YA MDOGO-X KUHUSIANA NA NAMNA ALIVYOKUWA AKIIFANYA KAZI HIYO YA UASKARI KAMA ALIYOWAHI KUYATOA YEYE MWENYEWE KWA MHUSIKA

Maaelezo haya aliyatoa kwa mhusika huku akiwa anadai kuwa alishaacha kazi hiyo na hivyo alikuwa anajuta kuwa kwenye kipindi fulani katika maisha yake, amewahi kufanya mambo hayo yasiyokuwa mazuri

Akiwa anafanya kazi hiyo ya ukaguzi wa bidhaa za magendo kwenye barabara kuu
  • MDOGO-X aliamua kutafuta kipande cha Ngozi ya Simba ambacho alikuwa anatembea nacho akiwa amekiweka mfukoni muda wote pindi anapokuwa yupo kazini barabarani
  • Kipande hicho alikuwa anakitumia kukichomeka kwenye mizigo ya watu ambao alikuwa anawashuku kuwa mizigo yao haikuwa sawasawa
  • Trick aliyokuwa anatumia ni kumsimamisha mtu na hatimaye MDOGO-X mwenyewe kuanza kuukagua mzigo husika kwa muda mfupi tu
  • Baada ya hapo, alikuwa anabadilisha mawazo na kumuamuru mwenye mzigo aanze kupekua vilivyomo kwenye mzigo wake mwenyewe, huku yeye akiwa anasimamia kwa makini upekuzi huo
  • Mwenye mzigo akishaanza kupekua, ghafla alikuwa anahamaki kuona kuna kipande cha ngozi ya mnyama amabcho yeye mwenyewe alikuwa hakitambui
Hapo hapo mtu huyo alikuwa anakamatwa na kutishiwa kuchukuliwa hatua kali. Wazee maskini wa Kisukuma walikuwa wanafikia hadi hatua ya kulazimika kuuza hadi ng’ombe kadhaa ili kumpa rushwa

Wenye mamlaka waliokuwa wamemkabidhi kazi hiyo wenyewe walikuwa hawana taarifa kabisa ya kilichokuwa kinaendelea huko barabarani; walikuwa wanajua MDOGO-X alikuwa anafanya kazi yake sawasawa na walikuwa wanamheshimu mno

KAZI NYINGINE ALIZOKUWA MDOGO-X ANAFANYA WAKATI WAUSIKU

MOJA:
KUVAMIA USIKU MAJUMBANI KWA WATU AKIWA NA SILAHA KAMA VILE MAPANGA

Kazi za usiku alizokuwa anafanya MDOGO-X wakati wa usiku ni zile zile kama zilizowahi kumpeleka jela mwaka 1997. Ikumbukwe kuwa wakati anafanya kazi hizi tayari alikuwa amesharudi kutoka jela
  • Hizi za usiku sasa hata MASANZA-X naye pia alikuwa ni mshiriki, kulingana na maelezo yake MDOGO-X
  • Details za namna MASANZA-X alivyokuwa anashiriki hakuweza kuzitoa kwa uwazi sana lakini alichohakikisha ni kuwa alikuwa anashiriki
  • Hizi sasa zilikuwa ni zile za kwenda kuvamia usiku kwenye makazi ya mtu na yeye mwenyewe (mvamiwa) akiwepo ambaye MDOGO-X alikuwa tayari ameshajiridhisha kabisa kuwa (mtu huyo) ana pesa
  • Uvamizi huu ulitumia silaha kama vile mapanga
MBILI: KUTEKA MAGARI YA ABIRIA/ MABASI USIKU AKIWA NA SILAHA KAMA VILE MAPANGA
  • Hii ilikuwa ni kwa ajili ya kupora mali za abiria
  • Abiria wote walikuwa wanashushwa kwenye basi, wanaamrishwa kulala chini kifudifudi
  • Alikuwa anavaa mask usoni, iliyotobolewa sehemu ya macho
Haya ni kwa kifupi sana kuhusiana na MDOGO-X ambaye ni mdogo wake na MREFU-X, na ambaye coaching ya aina hii, aidha kwa ushauri au kwa matendo, mhusika ana uhakika kabisa kuwa atakuwa aliipta kutoka kwa kaka yake huyo MREFU-X

UP NEXT

KILICHOMLETA MDOGO-X DAR ES SALAAM MWAKA 2001

Safari yake MDOGO-X ya kuja Dar es Salaam ina sababu zilizogawanyika katika makundi mawili
  • Sababu kama alivyozitaja yeye MDOGO-X kwa mhusika
  • Na sababu kama mhusika alivyomsoma MDOGO-X kutokana na matendo yake baada ya kuwa amekutana naye mwaka 2001
…………………..inaendelea
 
KILICHOMLETA MDOGO-X DAR ES SALAAM MWAKA 2001

…………………..inaendelea

SABABU KAMA ALIVYOZITAJA YEYE MDOGO-X KWA MHUSIKA


Yeye alidai kuwa amekuja kufanya kazi ya Kilimo Kigamboni sehemu zinazoitwa Mwongozo na Kimbiji. Na kweli alikuwa anapotea kwa muda na ilikuwa anaporudi kuja kumtembelea mhusika, alikuwa anakuja na hela ili amtunzie

Ilipofika mwaka 2003, mhusika aliamua kufanya ziara ya kumtembelea kwenda kupaona mahali alipokuwa anakaa huko Kigamboni. Mhusika alifuata maelezkezo yote kama walivyokuwa wameelekezana, lakini hakufanikiwa kumpata. Watu wote kwenye eneo hilo walishindwa kumfahamu. Mbaya zaidi ni kuwa simu yake ilikuwa haipatikani

SABABU KAMA MHUSIKA ALIVYOMSOMA MDOGO-X KUTOKANA NA MATENDO YAKE BAADA YA KUWA AMEKUTANA NAYE MWAKA 2001

Kadri siku zilivyokuwa zinaenda, hatimaye mhusika alikuja kubaini kuwa MDOGO-X alikuwa na mambo mengi sana ya kisirisiri na kwamba hata iliwezekana hakuwa na nia njema na mhusika. Vile vile mambo mengi sana aliyokuwa anaongea kuhusiana na mipango yake iliyokuwa imemleta huku, yalikuwa yanakinzana

Mbali na hayo, kwa usiri wake huo huo MDOGO-X, hatimaye mhusika alikuja kugundua pia kuwa alikuwa ameshafanikiwa kutengeneza uhusiano wa mazoea ya ukaribu fulani usiokuwa wa kawaida, uhusiano wa kificho fulani hivi na baadhi ya majirani zake mhusika, pasipo mhusika yeye mwenyewe kujua hilo wala pasipo mhusika kuwa amemtambulisha kwa majirani hao
  • Ilikuwa mhusika anapokuwa yupo, majirani na mgeni huyu wanavunga kuwa hawafahamiani, na wala walikuwa hawaongei
  • Katika mazingira yale ambayo mhusika alikuwa anakuwa hayupo maeneo ya nyumbani, uhusiano na majirani hao ulikuwa unakuwa “paka akiondoka panya hutawala”
Zaidi ni kuwa mhusika alikuja pia kubaini uhusiano wa mawasiliano ya aina ile ile kati ya MDOGO-X na rafiki wa kike wa mhusika wa wakati huo ambaye yeye (rafiki wa kike) alikuwa anakuja pale nyumbani kwa nadra sana.

Kwa kifupi tu ni kwamba hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2006, mhusika alimfukuza MDOGO-X nyumbani kwake na kumpiga marufuku kufika pale hadi leo. Tangia pale mhusika hajawahi kuonana tena na MDOGO-X hadi leo.

Kingine cha kushangaza zaidi ni kuwa karibia mara zote MDOGO-X alikuwa anakuja nyumbani kwa mhusika nyakati za usiku, hasa baada ya saa 2 za usiku

PICHA ALIYONAYO KWA SASA MHUSIKA KUHUSIANA NA HUYU MTU MDOGO-X

………………inaendelea
 
UPDATE 19 MAY 2020

Mwendelezo kuhusiana na kazi ambayo mhusika aliletewa na Mr. T


Zaidi ni kuwa safari hiyo ilikuwa na ughafla wa aina fulani uliokuwa unaashiria KAMA mhusika alitakiwa aondoke pasipo watu wengi kujua. Akakumbuka pia mwaka 1999 aliwahi kukumbana na hali ya namna hiyo wakati akiwa anasaka ajira ya kudumu.

Kumbuka kuwa maelezo haya ameyaleta kwa ajili ya kugusia kidogo tu uhusiano uliopo mpaka sasa, kati yake na Mr. T, ambaye alimthibitisha kuwa tayari yeye ameshapokea malipo zaidi ya million 50 kama malimbikizo.

Msomaji inabidi akumbuke pia kuwa hapa mhusika yeye alikuwa tayari ameshasimama kudai maslahi yake miezi kadhaa nyuma, baada ya kuona kuwa mchakato huo unakuwa wa hatari kwake.

Hata hivyo, pamoja na taarifa hizi za Mr. T, mhusika:

  • Yeye bado hajalipwa malimbikizo hayo mpaka leo
  • Kwa hiyo inaonyesha KAMA wote Mr T pamoja na Mkuu wa Idara walikuwa na nia ya kum-trigger aanze tena kufuatilia maslahi hayo, na ndiyo maana hajaweza kulipwa mpaka leo
  • Na kama ni kweli kwamba walikuwa na nia ya kumuanzisha ili aanzishe tena mchakato wa kudai masslahi hayo, basi obviously kulikuwa na set-up ya mitego mingine mipya kwenye mchakato wa kudai maslahi hayo
Hata hivyo, mhusika pamoja na kupata taarifa hizo nzuri kutoka kwa Mr T, bado hakuweza kuwa tempted kubadilisha msimamo wake, aliendelea na msimamo wa kuendelea kuusitisha kwa muda mchakato huo



KIKAO (CHA PILI) CHA DHARURA NA AMBACHO KILICHOITISHWA NA MR X

  • Tofauti na kile cha mwanzo ambacho kilimhusisha Mr T, hiki cha pili kilikuwa ni rasmi
  • Kilikuwa ni cha dharura, na kilifanyika mwezi wa pili mwishoni au wa tatau mwanzoni
  • MR X alimfuata mhusika ofisini kwake na kumkaribisha mhusika kwenye kikao hicho kikiwa na agenda ya moja tu ya kumthibitishia kuwa atarekebishiwa maslahi na mshahara wake March 2020 na hatimaye malimbikizo ya mshahara huo mwezi unaofuata; maslahi ambayo amekuwa akiyadai kwa takribani miaka mitano (5) sasa
  • Kikao hicho kilihudhuriwa na watu takribani 6 wenyeji pale ofisini, na mtu mwingine mmoja mgeni kutoka nje ya ofisi, na ambaye ni mstaafu wa pale, ila alikuwa akifanyia idara nyingine
  • Kwa hiyo, Mr X alimfuata mhusika ofisini kwake siku hiyo na kumuomba ahudhurie kikao hicho cha dharura akimweleza kuwa yeye ndiye alikuwa ni mdau mkubwa wa kikao hicho
  • Mhusika alikubali na alihudhuria kikao hicho na ambacho kiliweka wazi kuwa mwezi huo huo, ambao ulikuwa ni March 2020, angelipwa mshahara uliorekebishwa na kwamba malimbikizo ya mshahara huo uliorekebishwa, yangefuata mwezi unaofuata, yaani baada ya ule wa malipo ya mshahara mpya
  • Mkuu wa Idara hakuwepo kwenye mkutano huo ila ilionyesha wazi kabisa kuwa waliokuwa waki-coordinate mkutano huo walikuwa na mandate yake, yaani alikuwa amewa-authorise kuendesha kikao hicho
  • Hata hivyo hadi leo, hali haijatokea sawasawa na minutes za kikao hicho
Pamoja na kwamba hali haijatokea hivyo mpaka leo (May 2020) kwa maana kuwa hakuna malipo yoyote ambayo yameshafanywa kwa mhusika kulingana na minutes za kikao hicho, bado mhusika hana sababu yoyote ya kutilia shaka kilichojadiliwa kwenye kikao hicho

HATA HIVYO: Mhusika anaona KAMA Mr X alimpeleka mhusika kwenye kikao ambacho pengine

  • HAKIKUWA SHAHIHI na wala taarifa zake hazikuwa sahihi, nia ikiwa ni kum-trigger mhusika aanze kupita pita tena kwenye ofisi ambazo huko mwanzo alikuwa ameamua kuacha kupitapita kwa sababu alikuwa tayari ameshaona hatari katika mchakato huo
  • KILIKUWA SAHIHI isipokuwa taarifa zake kwamba malipo yake yangeweza kufanyika mwezi huo hazikuwa sahihi, nia yake ikiwa ni ile ile ya kum-trigger mhusika aanze kupita pita tena kwenye ofisi ambazo huko mwanzo alikuwa ameamua kuacha kwa sababu alikuwa tayari ameshaona kuna hatari katika pita pita hizo
  • Alifanya hivyo baada ya trigger ya Mr. T (aliyedai kulipwa zaidi ya million 50) kuwa imeshindwa kufanya kazi
Hii inatkna na ukweli kwamba vikao vyote viwili vinaonekana kuwa na taarifa ambazo haziko sahihi sana, na hivyo kumfanya mhusika kuwa na notion kwamba wote Mr X na Mr T walikuwa na nia ya kum-trigger ili aanze tena kupita pita kwenye maofisi ya watu ambao tayari ameshayaogopa.

Zaidi ni kuwa mahusiano yaliyopo kati ya mhusika na watoa taarifa hizi njema, na kama alivyoyaainisha kwa kifupi sana hapo juu, hayako sawia sana kiasi cha kumfanya mhusika asiwe katika hali ya kiwango ambacho angeweza kuendelea kuwaamini tena, kama ambavyo anaweza kuwaamini binadamu wengine wa kawaida. Ni kwa sababu muda wote wako tricky na kwa ndani siyo watu ambao anaweza akasema kuwa ni marafiki kwake

Kwa hali hiyo basi, assuming sasa mhusika angepata shauku ya kutaka kujua ni nini kinaendelea kuhusiana na maslahi yake, halafu akaamua kuyafuatilia kwenye ofisi husika, na kwa bahati mbaya katika kupita pita kwenye maofisi ya watu, kukatokea chochote kile ambacho ni cha madhara kwake, picha ya haraka haraka ambayo ingejitokeza ni kuwa mhusika angekuwa responsible kwa madhara yale ambayo yangempata, kwa sababu lazima watu wangehoji, kama huyu mtu alikuwa ameamua kusitissha mchakato wa kufuatilia maslahi hayo, na akatangaza hivyo hadharani , je kilichomfanya auanzishe tena ni nini? Wengine wangeweza hata kufikia conclusion kuwa kwa vile alikuwa anadai maslahi, possibly ameshafrustrate na hivyo alikuwa katika mchakato wa kuwadhuru wengine, isipokuwa kwa bahati mbaya madhara yakamrudia yeye mwenyewe



MWANDISHI WENU ATARUDI KWA MATUKIO ZAIDI YASIYO YA KAWAIDA, YANAYOMHUSISHA MR X NA WASHIRIKA WAKE
Sahihisho muhimu
Huyu MR T aliyetajwa hapa ni mtu yule yule ambaye amekuwa akitajwa kama MR Y
 
PICHA ALIYONAYO KWA SASA MHUSIKA KUHUSIANA NA HUYU MTU MDOGO-X

MAELEZO YA UTANGULIZI


MDOGO-X alifika hapa Dar es Salaam mwezi Septemba 2001. Wakati huo mhusika alikuwa anaishi mtaani nyumbani kwenye familia ya jamaa zake

Ndani ya mwezi huo huo wa Septemba, mhusika alikuwa ameshapata nyumba maeneo ya ofisini na akawa anajiandaa kuhama kutoka kwenye familia hiyo kuja kuishi peke yake kwenye nyumba hiyo aliyokuwa amepata maeneo ya ofisini.

Akiwa yuko kwenye pilika pilika hizo za kuhamia kwenye nyumba ya ofisini
  • MDOGO-X aliwasili Dar es Salaam muda huo huo
  • Baada ya kama wiki nyingine moja mbele, kaka mwingine mkubwa wa MDOGO-X (tumwite KAKA-X), baba mmoja mama mmoja, naye aliwasili pia Dar es Salaam
  • Huyu KAKA-X alikuja kama DEPENDANT wa mhusika kutoka na umri aliokuwa nao kuwa mkubwa sawa na wa baba yake mzazi na mhusika
  • KAKA-X alikuwa agemate na baba yake mzazi wa mhusika na wakati mwingine wakati wa utoto wao walipokuwa wananyonya, watoto hawa walikuwa wanalazimika kunyonya ziwa moja la shangazi yake mhusika. Kipindi shangazi yake mhusika alipokuwa anamnyonyesha mtoto wake wa kwanza yaani KAKA-X, alikuwa wakati mwingine anamnyonyesha pia mdogo wake ambaye ni baba yake mzazi na mhusika, especially ilipokuwa imetokea dharura ya bibi wa mhusika kumnyonyesha mtoto wake mwenyewe
Kwa hiyo Septemba 2001 mhusika alihamia kwenye nyumba nyingine maeneo ya ofisini, akiwa ameambatana na DEPENDANT wake wa kwanza katika maisha yake. Hadi kufikia Desemba 2002, mhusika na KAKA-X walikuwa wote

Hata hivyo, by January 2002, KAKA-X aliamua kuhamia kwa jamaa yake mwingine maeneo hayo hayo ya ofisini, staff-mate wa mhusika ambaye yeye alikuwa na nyumba kubwa zaidi
  • Huyu hakuwa ndugu wa KAKA-X au mhusika isispokuwa ni mtu tu ambaye walifahamiana wakiwa wanaishi wote Shinyanga mjini
  • By 2008 staff-mate huyu alistaafu na kuhamia Iringa. KAKA-X naye alihamia kwenye nyumba ya mfanyakazi huyu iliyopo pale Mwananyamala Hospitalini
Baada ya staff-mate kustaafu na kuhamia Iringa, MDOGO-X ambaye mhusika alimpiga marufuku kufika nyumbani kwake tangu mwaka 2006, naye pia alihamia huko Iringa

Mpaka muda huu, staff-mate na MDOGO-X wako wote huko Iringa

MLOLONGO WA BAADHI TU YA MATUKIO MUHIMU KUANZIA MWAKA 2006
  • Mwaka 2006 MDOGO-X apigwa marufuku kufika nyumbani kwa mhusika
  • August 2008 MR Y (staff-mate) ambaye taarifa zake mhusika aliwahi kuzitoa humu (post #119) kuwa aliwahi kumuunganisha mhusika na watu kwenda kufanya kazi kusini (kuna baadhi ya sehemu zingine amem-refer kama MR T. Kwa hiyo ieleweke kuwa MR Y na MR T ni mtu yule yule)
  • Novemba/ Desemba 2008 mhusika alipewa taarifa za ndugu yake mwingine ambaye kwa kipindi kirefu alikuwa ametengana na mume wake, kuwa amehamia Dar es Saalam maeneo ya Tabata wakiwa wamerudiana na mume wake
Hadi kufikia mwaka huo wa 2008, wanandoa hawa walikuwa wametengana kwa kipindi kisichopungua miaka 15
  • Mume alikuwa anafanya biashara na alikuwa anaishi Zambia
  • Mke alikuwa mkulima na kabla ya hapo alikuwa anaishi kijijini Kwimba Mwanza
MDOGO-X sasa akawa amepata tena nafasi ya kufanya ziara za ugeni wake mahali pengine baada ya kuwa amepigwa marufuku kufika nyumbani kwa mhusika

Hii nsasa ikawa tena ndiyo sehemu pekee ambayo ingeweaa kuwakutanisha mhusika na MDOGO-X, japo hawakubahatika kukutana tena hata nyumbani kwa wanandoa hawa wapya

Mpaka muda huu, wanandoa hawa walishatengana tena na mume alisharudi tena Zambia na mke yuko Mwanza mjini

Maelezo zaidi ya wanandoa hawa yatafuata muda mfupi ujao

Novemba/ Desemba 2010
mhusika akiwa kwenye safari zake binafsi wakati wa likizo kusini mwa Tanzania, alibaini uwepo wa watu wasiokuwa wazuri wakimfuatilia na kuamua kwenda kuripoti kituo cha Polisi ambapo alikaa kituoni pale muda wa siku tatu akihojiwa

Safari hii aliifanya baada ya kuwa amepewa ushauri na mmojawapo wa wanfamilia wa kule alikokuwa akiishi kabla hajahamia kwenye nyumba iliyopo maeneo ya ofisini

UP NEXT

Maelezo zaidi ya wanandoa waliowahi kurudiana mwaka 2008 baada ya kuwa wametengana kwa kipindi kirefu sana lakini kwa sasa walishatengana tena kwa mara nyingine
 
..........................inaendelea
Binti huyu aliyerudiana na mume wake kwa muda tu na hatimaye kuachana naye tena, ni yule ambaye mhusika aliwahi kutoa taarifa zake kwenye post hii hapa #655

Ni yule ambaye mdogo wake wa kiume aliuawa na kundi la watu hivi karibuni mwanzoni mwa mwezi wa sita mwaka huu

Siku binti huyu anampigia simu mhusika, kumjulisha juu ya msiba huu, alikuwa pia anamuomba nauli kwa ajili ya kuwahi kwenye mazishi kesho yake saa 11 asubuhi

Taarifa za msiba huu zililetwa kwa mhusika siku hiyo zikiwa zimecheleweshwa kwa makusudi

MUBARIKIWE TENA NA BWANA

 
UPDATE: SATURDAY 25 SEPTEMBER 2021

HITIMISHO
MREFU-X

Kama ambavyo mhusika aligusia hapo mwanzo, MREFU-X ndiye mastermind hasa ambaye huwa anapanga matukio yote ya ajabu ajabu huko kijijini, nyumbani kwao na mhusika; akishirikiana na baadhi ya waliotajwa humu wakiwemo wawili wale waliowahi kufanya forgery ya cheti cha kifo cha baba yao mzazi na kukikabidhi kwa mhusika mwaka 2006
Zaidi mhusika anashauri MDOGO-X afuatiliwe huko aliko kwa sasa ili ajulikane kwa muda huu anafanya kazi gani. Mbali na hayo, kutokana na hali kama ambavyo mhusika ameshaeleza kwenye maelezo yake kuhusiana na watu hawa, mhusika yuko pessimistic kwamba kuna uwezekano mkubwa MREFU-X anazo details sahihi zaidi za vifo vinavyoendelea kutokea huko kijijini, vikiwemo vilivyowahi kutokea zamani kama vile kile cha baba yake mzazi na mhusika (Augusr 1990) na pia cha baba yake mkubwa na mhusika (August 2006)

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
MREFU-X
DOKEZO MUHIMU

Just in case kwamba kweli ni yeye MREFU_X yuko kwenye operation, mhusika anaomba sana mtu huyu adhibitiwe, atamaliza watu
Huwa ana sura mbili kamili, ya ndani na ya nje; na kwa mara ya kwanza mhusika alilijua hilo ilikuwa ni mwaka 2004 baada ya mhusika kutapeliwa na MREFU-X; 1/3 ya sehemu ya kiwanja alichokuwa amepanga kununua na hivyo kuuziwa 2/3 ya kiwanja hicho hicho ila kwa bei ile ile ya kiwanja kizima. MREFU_X alikuwa anamzunguka mhusika kwa kumtumia mtu mwingine, mdogo wake MASANZA-X
 
UPDATE: FRIDAY 08 OCTOBER 2021

ANAVYOONEKANA MR-X KWA SASA ANAPOKUWA YUKO KWENYE MAZINGIRA YA OFISINI


Mhusika alirudi ofisini kutoka likizo, J3 ya tarehe 26 Septemba 2021. Tangu amerudi ameshaona mengi isipokuwa kwa sasa anaomba adonoe kidogo tu

Kuna hali ambayo inaonekana kama alarming kutoka kwa MR X, something might be wrong somewhere, bado mhusika hajajua ni kitu gani hasa

Anavyoonekana MR X kwa sasa ni kwamba yuko kwenye set-up ya kitu, na yuko very calculative. Nyuma yake wapo watu kadhaa na, kama kawaida Senior Mstaafu wa Kiume na wa Kike pia

Kama kawaida ilivyo siku zote set-up za MR X huwa ni za matukio yale ambayo siyo ya kawaida kama ambavyo mhusika ameshawahi kuyaeleza humu hapo awali

Details zaidi zitawajieni kadri muda unavyopita

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: WEDNESDAY 13 OCTOBER 2021

KWA WALE WAUMINI WA KANISA “A” AMBAO HUWA WAKO MAKINI NA KILA KINACHOTOENDELEA HAPO KANISA “A”

MLISIKIA MANENO ALIYOTAMKA HUYO “KENGE” a.k.a “KIONGOZI MKUU WA KANISA A” WAKATI ANATOA SALA YA KUWAOMBEA WAONGOFU WAPYA WALIOTOKANA NA MIKUTANO YA CFaN, AKIWA MAESIMAMA PALE JUU MADHABAHUNI J2 YA TAREHE 10 OKTOBA 2021 WAKATI WA IBADA YA PILI?


Aliwaombea akiwa anatamka maneno kwa haraka haraka sana isivyo kawaida yake, huku akiwa na jiccho la uangaalifu sana utadhani si la binadamu bali la Cobra. Ni kawaida yake huwa anakuwa hivyo pindi anapokuwa ameandaa makakati wake kwa ajili ya kuhujumu MADHABAHU YA BWANA

Kwenye sala hiyo akiwa anawaombea waongofu hao wapya, alitamka maneno kuwa YESU ALIFANYIKA DHAMBI kwa ajili yao, badala ya kuwaambia kuwa YESU ALIFANYIKA DHABIHU kwa ajili yao

Kawaida maneno haya huwa anapenda sana kuyatamka mhubiri chipukizi alyesimama madhabahuni kuhudumu J2 hiyo wakati wa Ibada ya Pili, lakini inaonekana kwa kwa bahati mbaya chipukizi huyu ambaye anaandaliwa na anachipuka kwa kasi sana kwenye swala hili la ubabaishaji kupitia MADHABAHU YA BWANA, alisahau kuyatamka maneno hayo J2 hiyo. Huyu chipukizi ndiye ambaye ana kawaida ya kuwa kila akipata nafasi ya kusimama MADHABAHUNI PA BWANA, mara nyingi huwa anatamka maneno hayo

Kwa sababu chipukizi hakufanikiwa kuyatamka siku hiyo, ilibidi sasa KM-A asimame na kuyatamka yeye mwenyewe

Hiyo MADHABAHU YA BWANA itawachinja na kuwamaliza kabisa wapumbavu wote wanaoendelea kusimama kwenye madhabahu hiyo kwa hila, UNLESS WANATUBU NA KUACHA KABISA KUFANYA UPUMBAVU HUO

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: THURSDAY 14 OCTOBER 2021

UJUMBE MUHIMU SANA
KWA KIONGOZI MKUU WA KANISA A (KM-A); VIONGOZI WENZAKE WOTE PAMOJA NA KIKUNDI CHAKE CHA WAUMINI WACHACHE AMBAO HUWA ANASHIRIKIANA NAO KUFANYA MAMBO YA KIPUMBAVU KWENYE MADHABAHU YA BWANA:

ONYO LA MWISHO AU “LAST TRUMPET”


  • Mlango wa rehema wa kuendelea kufanya upumbavu kwenye madhabahu ya BWANA, umefungwa RASMI kuanzia J2 iliyopita ya tarehe 10 OKTOBA 2021
  • Kwa hiyo huo mlango haupo tena na hakuna tena muumini yeyote yule atakayesimama KWENYE MADHABABU au MBELE YA MADHABAHU YA BWANA akiwa na nia ya ndani ambayo iko kinyume na dhumunu la kusimama mbele au kwenye MADHABAHU hiyo
Hii mana yake ni kwamba haupo mguu wa hila utakaonyanyuka kutoka mahali popote pale kuelekea kwenye MADHABAHU YA BWANA, kwa maana kuwa

  • Mguu huo kama utajitokeza baada ya ujumbe huu, basi BWANA ataukata, na shingo ya mwenye mguu huo ataichinja
  • ILI MANENO YA UJUMBE HUU YAWEZE KUTHIBITIKA, ITAPENDEZA MIGUU HIYO YENYE HILA IWEPO ANGALAU KWA MUDA, ILI WAUMINI WOTE (WENYE NIA NJEMA NA WASIO NA NIA NJEMA), WAWEZE KUYATHIBITISHA MANENO HAYA
HITIMISHO

Mlango wa rehema wa kuendelea kufanya upumbavu kwenye MADHABAHU YA BWANA umeshafungwa rasmi kuanzia J2 YA TAREHE 10 OKTOBA 2021, na wale wote ambao hapo KABLA wamekuwa wakifanya yasiyompendeza BWANA kupitia MADHABAHU hiyo, MARA MOJA wanatakiwa wafanye toba na kuomba rehema, na baada ya hapo waache kabisa MILELE

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: MONDAY 18 OCTOBER 2021

TAARIFA AMBAZO MHUSIKA ALIKUWA AMEZI-WITHOLD KWA MUDA MREFU

STAFF-MATES WOTE ALIOWAHI KUWATAJA KWEMYE MAZUNGUMZO YAKE NA “SPECIALIST” FEBRUARY 2016, WOTE WALISHAHAMISHWA KWENYE TAASISI ISIPOKUWA MMOJA


Ni kwamba mhusika amerudi ofisini hivi karibuni na kukuta mambo yako “hot” kidogo tofauti na alivyokuwa akitarajia, na hivyo anaona ni busara aka-disclose kila aina ya taarifa alizonazo

Ni kwamba kuna baadhi ya “staff-mates” wenzake aliowahi kuwataja kwamba kwa namna moja ama nyingine, waliwahi kuhusika na baadhi ya mambo ambayo yaliwahi kumpata mhusika katika vipindi tofauti tofauti

Wafuatao ni staff-mates ambao walihamishwa baada ya mhusika kuwa amewasilisha taarifa zake kwa “SEPCIALSIT”

  • WA KWANZA: Huyu ni yule ambaye aliwahi kuwa Afisa Mkuu Tawala kwenye taasisi anayofanyia kazi mhusika hadi kufikia Desemba 2014. Huyu ndiye alihusika na tukio la kukatwa kwa mshahara wa mhusika kwa jumla ya TZS 700,000/= mnamo Februari 2014, na ndiye pia aliyehusika na lile tukio la kumwandikia barua ya tuhuma mhusika mnamo May 2014, huku akimtishia kumfukza kazi. By Februri 2016, huyu yeye alikuwa tayari ameshahamishiwa TCU, na baada ya Februari 2016 alifukuzwa TCU na kwa sasa hivi yuko NIMR
  • WA PILI: Kuna yule ambaye alikuwa Afisa Rasilimali watu ambaye yeye ndiye aliisaini barua ya kukatwa kwa mshahara wa mhusika; na hatimaye tena Septemba 2014 Ofisa huyo huyo kuchukua jukumu la kumwandikia barua mhusika barua nyingine ya pili akimwita kwenye kiako cha nidhamu kilichohusiana na barua ya tuhuma za May 2014. Huyu yeye alihamishiwa DIT na mpaka muda huu yuko huko
  • WA TATU: Kuna yule ambaye alikuwa Mkuu wa Idara kipindi mshahara wa mhusika unakatwa jumla ya TZS 700,000/= mnamo Februari 2014, na hatimaye tena mnamo May 2014, na Septemba 2014, Mkuu huyo huyo huyo wa Idara kupokea barua mbili za tuhuma kwa mhusika. Huyu yeye alihamishiwa Tume ya Madini, na kwa sasa hivi yuko Wizara ya Madini
  • WA NNE: Kuna yule aliyewahi kuwa Mkuu wa Idara baada ya huyu aliyetajwa hapo juu kuwa amehamishwa, na ambaye aliwahi kuanguka kutoka juu ghorofa ya kwanza. Huyu yeye alipata transfer ya ndani kwa ndani, alihamishwa idarani tu lakini yupo kwenye kitengo kingine ndani ya taasisi hadi leo hii. Huyu pekee ndiye ambaye hakuwahi kuhamishwa kwenda nje ta Taasisi
  • WA TANO: Kuna mmoja wa wale staff-mates ambao mhusika aliwahi kukutana nao akiwa amesafiri nje ya nchi kwenye safari ambayo aliambatana na Boss X. Kuna staff-mates watatu alikutana nao siku hiyo akiwa yuko Airport; ilikuwa ni jioni wakati wa safari ya kurudi Tanzania. Wawili kati yao walikshastaafu siku nyingi na mmoja wao alihamishiwaVETA na yuko huko mpaka muda huu
  • WA SITA: Kuna mmoja ambaye mhusika hajawahi kumwongelea sana humu kwa sababu details zake zimefichika fichika sana na huwa anafanya matukio yake kwa kuvizia vizia sana kama chui, ila ni mtaalamu na anaendelea mpaka leo. Huyu sometimes huwa anashirikiana na MR X Staff-mate huyu waliwahi kukutana na mhusika kwenye kituo cha kupigia kura, siku ya kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015. Ilikuwa ni kwenye queu au foleni ya wapiga kura. Siku hiyo kulikuwa na tukio ambalo mhusika alilikwepa na mmojawapo wa wahusika wa tukio hilo alikuwa ni huyo staff-mate. Huyu yeye alihamishiwa Wizara ya Maji, na kwa sasa hivi yuko Viwanda na Biasahara
Hili tukio la siku ya kupiga kura baada ya kugonga mwamba, mhusika tayari alikuwa ameshakutana na “SPECIALIST” kwa mara ya kwanza, ila hawakufanikiwa kufanya mazungumzo. Mara ya kwanza mhusika alikutana na “SPECIALIST” ilikuwa ni Agost/ Septemba 2015 wanafunzi wakiwa wako likizo. Mazungumzo na “SPECIALIST” walikuja kuyafanya baadaye kuanzia Februari 2016

HITIMISHO

Ukiondoa yule wa kwanza kabisa aliyetajwa hapa, hamisho hizi za hawa wengine wote waliobaki zilitokea mara tu baada ya mhusika kuwa amefanya mazungumzo yake na “SPECIALIST”. Kipindi mhusika anafanya mazungumzo yake na “SPECIALIST”, huyo wa kwanza alikuwa tayari yuko TCU, ila baada ya hapo kwa bahati mbaya mwanzoni mwa 2016 ndiyo alifukuzwa huko TCU na hatimaye kubahatika tena kuteuliwa NIMR ambako ndiko aliko mpaka muda huu

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
QN: In an "air of mystery situation" where coincidences become very dominant; how many coincidences should happen before someone looks for some other explanations?
 
Back
Top Bottom