#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

KILICHOTOKEA SIKU HIYO KABLA YA SERVICE YA INJINI KUANZA

Baada ya oil iliyokuwemo kwenye injini kuwa imemwagwa; MTU HUYO alishauri kwamba kabla ya kufanyiwa service ya injini; mhusika inabidi airudishe gari kwa fundi mekanika kwanza, kwa sababu ilikuwa inaonyesha kuna leakage ya oil inatokea kwenye injini. Kwa maana hiyo MTU HUYO alikuwa anai-refer gari irudi kwa FME kwanza kabla ya kufanyiwa service ya injini siku hiyo

  • Mhusika alimjibu MTU HUYO kwamba hayo mambo mengine ayaache; amwachie mhusika. Yeye alichotakiwa siku hiyo ni kufanya kazi aliyokuwa anatakiwa kufanya
  • Mbali na hivyo, MTU HUYO hakuwa hasa aliyekuwa anahusika na service ya gari la mhusika, isipokuwa alikuwa amejipachika tu mamlaka hayo siku hiyo, akiwa kama mojawapo wa staff wa office hiyo tu
  • Mara zote gari la mhusika limekuwa likifanyiwa service na mtu mwingine ambaye ndiye aliyekuwa anaonekana kusaidiwa tu na MTU HUYO siku hiyo
Kwa kifupi tu ni kwamba alichokuja kukibaini baadaye kwa uhakika kabisa ni kwamba MTU HUYO na FME walikuwa wameshakuwa coordinated miezi kadhaa nyuma kabla ya service ya gari hiyo kuwadia.

Fundi umeme mgeni aliyekuwa ameletwa na MTU HUYO siku hiyo alikuwa ameshaandaliwa kabla, maalum kabisa kwa ajili ya kuja kuharibu kabisa mfumo wa umeme wa gari; na fundi mwenyeji wa siku zote wa gari angeweza kuja kuthibitisha hilo pasipo shaka yoyote

Yaliyotokea siku hiyo ni mengi ila kwa kifupi tu mwandishi wenu anaomba aishie hapa kwa tukio hili

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: SUNDAY 24TH APRIL 2022

MHUSIKA ANAOMBA KUTOA CHALLENGE (CHANGAMOTO) KWA MAMLAKA ZILIZO JUU YA KANISA A (MAMLAKA AMBAZO KANISA A LIKO CHINI YAKE)


Mhusika anaomba kama kuna uwezekano, mamlaka hizo zifanye uchunguzi wa kina na kujiridhisha kama yale YOTE ambayo huwa yanafanyika Kanisa A wakati wa Ibada HUWA YANAFANYIKA KATIKA NAMNA YA KAWAIDA (normal conduct in Praise and Worship of the Lord) na kwamba mambo hayo huwa yanafanyika KWA NAMNA HIYO HIYO PIA KATIKA NYUMBA NYINGINE NYINGI ZA IBADA zilizopo hapa nchini kwetu; ZINAZOJULIKANA NA MAMLAKA HIZO

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: MONDAY 02 MAY 2022

MHUSIKA ATUMIWA TENA MTU MGENI NDANI YA JENGO LEO ASUBUHI KABLA YA SAA 2:00 ASUBUHI AKIWA PEKE YAKE NDANI YA JENGO


  • Mtu mwingine pekee aliyekuwepo ndani ya jengo muda huo ni mfanyakazi mmoja tu wa Kampuni ya usafi
  • Mfanyakazi huyu ni mgeni ambaye hajamaliza hata wiki mbili tangu ahamie aletwe kwenye jengo hilo
  • Geti kuu lilikuwa wazi lakini mfanyakazi mgeni hakuweza kumtambua ni nani aliyefungua geti, japo mfanyakazi huyu mgeni anadai kuwa alimuona mtu huyo wakati anafungua geti
  • Wafanyakazi wenzake wengine wote ( wa kampuni ya usafi) walikuwa hawajafika, japo kawaida huwa wanakuwepo kuanzia saa 12:00 kamili asubuhi
  • Mhusika alikuwa na kipindi kilichokuwa kinaanza saa 1:00 kamili asubuhi
Waliohusika na kumtuma mtu huyo imebaininka kuwa ni MKUU WA IDARA MSTAAFU wa miaka ya 2006-2012 pamoja na ndugu yake mwingine (tribe mate) ambaye ofisi yake iko kwenye sakafu moja na ile ya mhusika

Taarifa za kina zaidi kuhusiana na tukio hili zitawajia muda siyo mrefu hapo baadaye

…………………inaendelea

MUBARIKIWE NA BWNA
 
UPDATE: TUESDAY 03RD MAY 2022

…….kabla hajaendelea na stori iliyopo hapo juu kuhusiana na ugeni aliotumiwa J3 asubuhi ya wiki

MHUSIKA AMENUSURIKA KUPOTEZA HELA YAKE YOTE ILIYOKUWA AMEWEKA KWENYE FIXED DEPOSIT ACCOUNT (FDR)


Mhusika amenusurika na tukio hili baada ya kubaini kuwa SOFT COPY RECEIPT ya FDR aliyokuwa nayo haipo kila mahali alipokuwa ameitunza

Wakati anagundua hilo ilikuwa tayari ni February 2022

Ikumbukwe kuwa HARD COPY RECEIPT ya FDR hiyo alikuwa tayari ameshaiteketeza kipindi kirefu huko nyuma, baada ya receipt hiyo kuonekana kumsumbua usiku anapokuwa amelala; na taarifa za uteketezaji huo aliwahi kuzileta humu jukwaani, receipt hiyo akiwa tayari alishaiteketeza

KIPINDI AMBACHO SOFT COPY HIYO ILIIIBIWA


Baada ya kuwa ameikosa, kumbukumbu zake zilimwonyesha kuwa SOFT COPY RECEIPT hiyo iliibiwa mwaka jana mwezi wa 9 wakati ambapo LAPTOP yake iliwahi kupata hitilafu na kuharibika kwa takribani mwezi mzima

Dhana aliyonayo ni kuwa baada ya LAPTOP kuharibika, RECEIPT hiyo ndiyo iliibiwa ikiwa kwenye LAPTOP na kufutwa kabisa, ikiwa ni pamoja na kwenye storage media zote ambazo ni za SOFT COPY yaani removable disks; alizokuwa nazo ofisini na nyumbani pia

Ilipofika February mwaka huu, miezi miwili tu kabla ya maturity date ya FDR, ndiyo aligundua kuwa RECEIPT hiyo haipo kila mahali kwenye storage media zote

  • Haikuwepo kwenye storage media zote za nyumbani na hata za ofisini pia
  • Baada ya hapo, alichofanya ni kui-retrieve kutoka mahali pengine mtandaoni kwenye storage media ambayo ni public
  • Aidha, receipt hiyo haikuwepo pia hata kwenye e-mails ambazo aliwahi kujitumia mwenyewe kama attachment kwenye official email yake
ALICHOKIONA KWENYE TUKIO LA KUIBIWA RECEIPT HIYO

Baadhi ya watu ambao evidence za kimazingira zinawaelekea kwa sana katika tukio hili la kupotea kwa soft copy receipt hiyo ya FDR ni SENIOR MSTAAFU WA KIKE (SMKE).

Mbali na hayo, huyu mtu ndiye pia ambaye kipindi cha nyuma kabisa mwaka 2012, aliwahi kupishana maeneo ya benki na mhusika; mhusika akiwa anatoka benki kuepeleka salary slip ambayo benki walikuwa wameng’ang’nania awapelekee, na SMKE naye akiwa hai hai kuwahi benki muda huo

Siku hiyo mhusika na SMKE walipopishana, ilikuwa ni mara yao ya kwanza na pia ya mwisho kwa mhusika na SMKE kukutana kwenye maeneo ya benki hiyo. Hapo awali hawakuwa wamewahi kukutana maeneo hayo, na baada ya pale hawakuwahi kukutana tena hata siku moja

Maelezo haya ya tukio hili la mhusika kukutana ghafla na SMKE; mhusika alishawahi kuyaleta humu kipindi cha nyuma na kwa kina sana

Ashukuriwe Mungu kwamba maturity date ya FDR ilikuwa ni tarehe 30 April na hadi muda huu, mhusika ameshaipata hela yake yote pasipo kupungua hata senti moja

MUBARIKIWE TENA NA BWANA

UP NEXT: Ugeni wa J3 saa moja asubuhi wiki hii
 
UGENI WA J3 ASUBUHI OFISINI KWA MHUSIKA, MHUSIKA AKIWA YUPO PEKE YAKE OFISINI NA PIA KWENYE JENGO ZIMA

……………………inaendelea


Mhusika alikuwa peke yake kwenye jengo isipokuwa mfanyakazi mwingine wa kampuni ya usafi; ambao wafanyakazi wa aina hii wakati mwingine wao huwa wana kawaida ya kufanya kazi kwa kuhama kutoka jengo moja kwenda jingine. Baada ya mhusika kukutana na mfanyakazi huyu kwenye korido na yeye (mhusika) kuelekea ofisini kwake, mhusika hana uhakika sana kama mfanyakazi huyu aliendelea kuwepo ndani ya jengo hilo au alitoka nje na au/ hata kuwa alihamia jengo jingine

Actually kuhusiana na ugeni alioupata mhusika J3 hiyo, ndani ya siku chache sana zilizokuwa zimepita, ugeni huo haukuwa wa kwanza bali wa pili. Kwa hiyo mgeni aliyefika ofisini kwa mhusika J3 alikuwa ni wa pili ndani ya siku chache zilizokuwa zimepita

MAELEZO MAFUPI KUHUSIANA NA GENI (VISTS) HIZI

UGENI WA KWANZA ulifanyika Ijumaa (SIKU YA MWISHO ya kazi) iliyopita ya tarehe 29 APRIL 2022, na kwenye muda ambao ulikuwa ni baada ya saa 10 kamili jioni (BAADA ya muda wa masaa ya kazi)

UGENI WA PILI
ndiyo ukafanyiak J3 (SIKU YA KWANZA ya kazi) ya tarehe 02 MAY 2022 ila KABLA ya muda wa masaa ya kazi

Vitu common kwenye geni (vists) zote hizi mbili ni kwamba WAGENI WOTE HAWA WAWILI


walifika ofisini kwa mhusika baada ya kuwa wamewakosa wenyeji wao maofisni kwao kwa sababu aidha muda wa kazi ulikuwa umeshapita (Ijumaa) au ulikuwa haujawadia (Jumatatu)

Wenyeji wao walikuwa ni wale wale, yaani wenyeji wa mgeni yule wa kwanza ndiyo wale wale walkuwa ni wenyeji wa mgeni yule wa pili

Hawakuwa mikono mitupu. Wa Ijumaa alikuwa na mkoba na yule wa Jumatatu asubuhi alikuwa muda wote ametupia mtandio mabegani; mikono yake yote miwili ikiwa imefichwa na mtandio huo aliokuwa amevaa; kitu ambacho kiliashiria kuwa possibly na yeye alikuwa na mkoba pia amebeba mkononi mwake au kitu kingine kilichofanana na hicho

Kabla ya kuendelea zaidi na wageni hawa wawili, turudi nyuma kidogo kwenye asubuhi moja ya Ijumaa ya tarehe 22 April 2022 na ndiyo tuanzie pale sasa kuja hadi hapa tulipo muda huu

…………………..inaendelea
 
KUHUSIANA NA IJUMAA YA TAREHE 22 APRIL 2022

Siku hiyo mhusika alifika ofisini kwa Mkuu wa Idara (MWI) ili kuazima ufunguo wa chumba cha darasa maalumu; alikuwa na kipindi kuanzia saa 3:00 kamili asubuhi

Mhusika angeweza pia kuazima DIGITAL PROJECTOR (DP) siku hiyo lakini mazingira aliyoyakuta ofisi kwa MWI hayakuwa conducive sana kumuwezesha aazime vyote viwili

Ni kwamba Katibu Muhtasi wa MWI (KMMWI), hakuwepo; alikuwa ametoka kidogo na badala yake alikuwepo kijana mwingine mgeni ambaye ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mhusika kumuona kijana huyo na pia ndani ya ofisi hiyo

Hata hivyo, baadaye baada ya muda wa takribani wiki moja na ushee kuwa umepita, mhusika alikuja kupata taarifa kuwa kijana huyu waliyekutana ofisini kwa MWI ijumaa hiyo tajwa, naye pia ni staff mgeni na ni msaidizi wa KMMWI. Kijana mwenyewe ndiye aliyejitambulisha hivyo baada ya mhusika kumkuta tena ofisini hapo kwa mara nyingine ya pili na hivyo mhusika kumuomba kijana huyo wafahamiane zaidi

SIKU YA KWANZA MHUSIKA ALIPOMKUTA KIJANA HUYU MGENI OFISINI KWA MWI NA PASIPO KUFAHAMU KUWA KIJANA HUYO NAYE ALIKUWA NI STAFF

Ikumbukwe kuwa KMMWI; hakuwepo ofisini siku hiyo, alikuwa ametoka kidogo

Wakati mhusika anaingia ofisni kwa MWI, wakati huo huo pia kuna mtu mwingine SENIOR MSTAAFU (SEM) naye pia aliingia ofisini hapo

SEM yeye alikuwa anarudisha DIGITAL PROJECTOR (DP), baada ya kuwa amemaliza kipindi cha asubuhi siku hiyo. SEM huyu ndiyo yule swahiba wa karibu sana na yule senior mwingine almaarufu kama SENIOR MSTAAFU WA KIUME

Ijumaa hiyo, kama mhusika naye angeamua kuazima DP pia, basi uwezekano mkubwa ni kwamba angechukua hii ambayo iilirudishwa na SEM wakati huo

Ikumbukwe kuwa iwapo mhusika angeamua kufanya hivyo, basi angeazima katika mazingira ambayo:

  • KMMWI asingekuwepo isipokuwa kijana mgeni tu aliyekuwepo ofisini hapo muda huo
  • DP hiyo ingepitiliza kutoka kwenye mikono ya SEM na kuingia moja kwa moja kwenye mikono ya mhusika, kitu ambacho ni kawaida kabisa kwa sababu incidences za namna hii huwa zinatokea maranyingi na mara kwa mara sana.
Still, ambacho hakikuwa cha kawaida sana (kinaweza kuwa ni cha kawaida) kwenye tukio hili ni kwamba

  • Kwa nini KMMWI hakuwepo ofisini muda huo; japo inaweza kuwa ilikuwa ni coincidental?
  • Je, kwa nini kulikuwa na mtu mgeni ambaye kama mhusika na SEM wangepeana DP hiyo, mshuhudiaji wa tukio hilo angekuwa ni mgeni ambaye mhusika hata alikuwa hamfahamu kama ni staff?
  • Kwa nini staff mgeni hakuamua kujitambulisha siku hiyo ya Ijumaa walipoonana kwa mara ya kwanza na mhusika, na hakujitambulisha kabisa hadi siku kadhaa mbele baadaye; mhusika mwenyewe alipoamua kumudadisi?
Kitu kingine ambacho kinaonekana kama coincidental ni kile kitendo cha KMMWI kuonekana ghafla ofisini hapo baada ya kujulikana kuwa mhusika hakuwa na mpango wa kuazima DP bali funguo peke yake

Wakati mhusika anaamua kuchukua funguo peke yake na si DP, KMMWI naye alikuwa tayari amesharudi ofisini na ndiye aliyefanya kazi ya kumkabidhi mhusika funguo

Mhusika kama angechukaua DP Ijumaa hiyo, uwezekano ni kwamba angeweza kukaa nayo na kuitunza ofisini kwake over the weekend, na J3 asubuhi ya wiki iliyokuwa inafuata, angehitaji kuitumia pia kwa sababu alikuwa na darasa jingine la J3 kuanzia saa moja kamili asubuhi

Mhusika alichukua funguo tu siku hiyo na kuondoka ofisini akiwa hajui kama kijana aliyekuwepo pale ofisini naye pia ni staff mwenzake

MUBARKIWE TENA NA BWANA

……………………itaendelea
 
UPDATE: WEDNESDAY 04 MAY 2022

MAELEZO MENGINE YA NYONGEZA KUHUSIANA NA GENI (VISTS) ZILIZOFANYIKA OFISINI KWA MHUSIKA KWA SIKU MBILI ZA IJUMAA YA TAREHE 29/04/2022 NA JUMATATU YA TAREHE 02/05/2022

UGENI WA J3 YA TAREHE 02/05/2022 SAA MOJA ASUBUHI


Ukiunganisha na maelezo ambayo mhusika tayari ameshayatoa hapo juu, ni kwamba ugeni ule wa J3 iliyotajwa hapo juu, kwa namna moja ama nyingine unamhusisha kwa kiasi pia, staff mgeni (tumwite STMG) ambaye maelezo yake yametolewa hapo juu, na possibly pengine hata KMMWI naye alihusika pia ila mhusika hana ushahidi concrete kuhusiana na uhusika wa huyu mwingine kwa tukio la J3 hiyo

Ni kwamba ilionekana kuwa J3 hiyo KMMWI na STMG walifika kwa muda mmoja au uliopishana kidogo tu; ambapo baadaye mhusika aliwaona STMG na mgeni wakiwa pembeni wakiteta jambo fulani na baada ya hapo, mgeni alielekea na kwenda kukaa kwenye chumba cha chai. Muda huo sasa ilikuwa ni saa 2 kasoro dakika chache sana; na ikiwa ni takribani dakika 40 tangu mgeni huyo aonekane na mhusika kwa mara ya kwanza akiwa ndani ya jengo hilo

  • Wakati STMG anateta na mgeni; tayari mgeni huyo alikuwa ameshatoka ofisini kwa mhusika
  • Baada ya kuachana na kupelekea mhusika kudhani kuwa mgeni huyo aliondoka; mgeni hakuwa ameondoka na badala yake kumbe alishuka chini ground floor na kwenda kusimama nje ya geti la lango kuu
Actually mgeni huyu hakufanikiwa kuingia ofisini kwa mhusika kwa sababu ofisi ya mhusika ilikuwa mlango wazi kuelekea kwenye korido na mhusika alimuuliza mgeni shida yake akiwa bado yuko umbali kiasi, kabla hajaingia ofisini kwake

Wakati huo ofisi ya mhusika ilikuwa wazi kwa sababu mpaka muda huu, bado hajafanikiwa kuwekewa AC nyingine inayofanya kazi, kwa hiyo inabidi muda wote aendelee kufungua madirisha na mlango wa ofisi ili angalau na yeye aweze kupata upepo wa kutoka nje; pale unapokuwa upo

MAELEZO KAMILI KUHUSIANA NA MGENI HUYU WA JUMATATU

  • Alikuwa ni wa jinsia ya kike; umri kati ya miaka 35-40
  • Alikuwa muda wote amevaa mtandio mabegani; na alifika ofisini kwenye mida ya kama saa 1:20, muda mfupi tu baada ya mhusika kuwa amewasili ofisini
  • Kwa mara ya kwanza, mhusika alimuona mtu huyu akiwa kwenye korido huku akiwa anatembea kuja uelekeo wa kule iliko ofisi ya mhusika
  • Baada ya kukaribia ofisi zilizo jirani na ile ya mhusika, na pasipo kumsemesha chochote mhusika, aliamua kugeuza na kuanza kutembea kurudi uelekeo wa kule alikokuwa ametokea na hatimaye kutoweka kabisa kwenye korido
  • Baada ya kuwa zimepita takribani dakika 5, mgeni huyu alirudi tena na safari hii alimsemesha mhusika huku akiwa bado yuko kwenye korido, umbali mrefu kidogo kutoka ofisini kwa mhusika
  • Mgeni aliomba kama anaweza kusogea na kuingia ofisini kwa mhusika ili waongee na mhusika alimjibu kuwa hapo alpokuwa amesimama palikuwa panatosha angeweza kuongea na mhusika pasipo shida yoyote
  • Baada ya hapo, mgeni alimuomba mhusika asogee pale mgeni yule alipokuwa amesimama; alimuomba kama mhusika anaweza kunyanyuka pale alipokuwa amekaa na kusogea pale alipokuwa amesimama mgeni huyu
Baada ya kusikia hivyo, mhusika, alimusihi mgeni huyu aondoke ili mhusika aweze kuendelea na kazi nyingine aliyokuwa anafanya asubuhi hiyo

Mgeni huyu aliitikia wito na aliondoka. na hapo ndipo mhusika alipodhani kuwa pengine mgeni huyo alikuwa ameondoka kabisa mazingira ya ofisini; kumbe hapana. Mgeni huyu hakuwa ameondoka bali alichofanya ni kushuka ground floor na kwenda kusimama mahali ambapo aliweza kuwaona watu wanaoingia na kutoka chumba cha MEN’S ROOM kilichopo floor hiyo.

Mhusika alikuja kulibaini hili baada ya kuwa ameshuka kwenye floor hiyo na kumkuta mgeni huyu akiwa amesimama eneo hilo. Hadi muda huo, zilikuwa zimepita takribani dakika 20 tangu mgeni huyu aondoke mazingira ya korido ilipo ofisi ya mhusika.

  • Baada ya hapo, mgeni huyu alipandisha tena juu, floor ya pili na hapo ndipo mhusika alipomkuta mgeni huyu akiteta na STMG
  • Wakati mhusika anashuka grond floor; alikuwa na mpango wa kuingia MEN’S ROOM ila aliahirisha baada ya kuona mgeni huyu akiwa bado yupo.
  • Baada ya kumuona mgeni, mhusika alivunga kama anarudi tena ofisini kwake na alikaa kwa dakika kadhaa na hatimaye tena akaamua kwenda MEN’S ROOM zilizoko sakafu ya juu kabisa.
  • Baada ya kupandisha juu, ndipo alpowakuta sasa STMG na mgeni wakiwa wamesimama wakiteta kuhusu jambo fulani.
  • Mhusika aliingia MEN’S ROOM pasipo kuwasemesha na alipotoka nje, hakuwaona tena STMG na mgeni; hawakuwepo tena nje.
  • Mhusika alielekea chumba cha chai na alipokaribia mlangoni, alimuona mgeni akiwa amekaa kwenye sofa zilizo karibu kabisa na mlango
Mhusika hakuingia ndani ya chumba na wala hakumsemesha mgeni, alirudi ofisini kwake na kuendelea na akaenda kuendelea darasa lake ambalo lilikuwa limesogezwa mbele kwa saa moja; na lilianza saa 2:00 kamili asubuhi na kumalizika saa 4:00 kamili. Kawaida lilitakiwa kuanza saa 1:00 kamili asubuhi na kumalizika saa 4:00

………………….inaendelea
 
…………….inaendelea

UGENI WA J3 YA TAREHE 02/05/2022 SAA MOJA ASUBUHI

HITIMISHO


Baada ya mhusika kupandisha floor ya juu na kuwakuta STMG na mgeni wakiteta jambo ndipo baadaye siku hiyo mhusika alipopata nafasi ya kuongea na STMG na kumuuliza kuhusu mgeni waliyekuwa wanaongea naye; kutaka kujua kwamba mgeni huyo alikuwa anamtafuta nani. STMG alimjulisha mhusika majina ya wenyeji wa mgeni huyu; ambao ni MKUU WA IDARA MSTAAFU WA MIAKA YA 200-2012 pamoja na ndugu yake mwingine (tribe mate) ambaye ofisi yake iko floor moja na ile ya mhusika

Wakati mhusika na STMG wanateta kuhusiana na mgeni huyu wa J3 asubuhi saa moja, walikuwa ndani ya ofisi ya MWI

Haya yalikuwa ni maelezo ya ugeni huu wa pili, baada ya ugeni wa ule wa kwanza ambao ulifanyika Ijumaa ya tarehe 29/04/2022.

Maelezo ya ugeni huu wa kwanza yanafuata hapa chini

MUBARKIKIWE TENA NA BWANA

………..UP NEXT: UGENI WA KWANZA WA IJUMAA YA TAREHE 29/04/2022 BAADA YA SAA KUMI JIONI
 
UGENI WA KWANZA WA IJUMAA YA TAREHE 29/04/2022; BAADA YA SAA KUMI JIONI

Ugeni huu ulifanywa na bibi ambaye mara kwa mara huwa anafika ofisini kwa wahusika wa ugeni ule wa pili uliofanyika J3 ya tarehe 02/05/2022

Bibi huyu alifika ofisni kwa mhusika akiwa amebeba mkoba, akauweka juu mezani kwa mhusika na kumuomba mhusika anunue vitabu

Ilikuwa ni baada ya kuwakuta wateja wake wa siku zote wakiwa tayari wameshaondoka ofisini kwa sababu ilikuwa tayari dakika nyingi zimepita baada ya saa 10 jioni

Ni kweli kuwa mara moja au mbili; mhusika alishawahi kununua vitabu kutoka kwa huyu bibi, na mara ya mwisho ilikuwa possibly mwaka 2014

Baada ya hapo, mhusika alimjulisha bibi huyu kuwa ameshasitisha tena kununua vitabu kwa sababu alivyonavyo vinamtosha na bado hajaweza kuvisoma vyote

Baada ya mhusika kumueleza bibi maneno haya walielewana.

Hata hivyo, yapata kama wiki tatu au nne zilizopita, bibi huyu alifika tena ofisini kwa mhusika akimsihi anunue vitabu, lakini hoja ya mhusika ilikuwa ni ile ile ya siku zote na mhusika aliendelea kumsisitizia bibi huyu kuwa hawezi tena kununua vitabu

Mhusika na bibi walielewana tena kwa mara nyingine siku hiyo lakini cha kushangaza, bibi huyu alirudi tena Ijumaa ya tarehe 29/04/2022 akiwa amebeba mkoba wake, akimsihi mhusika anunue vitabu. Mhusika hakununua tena vitabu siku hiyo

Baada ya huyu mgeni wa Ijumaa, ndiyo akafuatia tena huyu mgeni mwingine wa J3 asubuhi saa moja kamili

………..Na wageni hawa wote wawili; wenyeji wao wakiwa ni wale wale

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: FRIDAY 06 MAY 2022

RARE COINCIDENCE OR NORMAL COINCIDENCE?????!!!!!!!


KUNA MZEE ANA GARI KUBWA OFISINI NA KILA AKIPAKI JIRANI NA. GARI LA MHUSIKA, LAZIMA GARI LA MHUSIKA LIPATE HITILAFU

LEO NI MARA YA PILI SASA KITU HIKI KINATOKEA, NA MARA YA KWANZA KILITOKEAI ALHAMISI YA TAREHE 14/04/2022; YAANI ANAPAKI JIRANI KWENYE SIKU ZILE ZINAZOKARIBIANA NA WEEKEND TU

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UP NEXT: DHANA (HYPOTHESISI) ALIYONAYO MHUSIKA HADI MUDA HUU KUHUSIANA NA MTU ANAYEMWITA KAMA "SPECIALIST"

"SPECIALIST" huyu ndiye anaweza kuwa alikuwa mshiriki mkuu kwenye kuratibu tukio lile la kudondoka kutoka juu ghorofa ya kwanza na kuumia kiwiko; kwa aliyekuwa Mkuu wa Idara aliyewahi kupatwa na tukio la namna hiyo, na ambalo maelezo yake tayari yalishawajia kwa kina siku zilizopita kupitia uzi huu

Kwa kumbukumbu tu ni kwamba "SPECIALIST" ndiye mtu ambaye mnamo February 2016, mhusika alielekezwa kwake (SPECIALIST) na mamlaka za ofisini kwake (mhusika). Mamlaka hizo zimemwelekeza mhusika kwenda kumpa "SPECIALIST" taarifa zote alizokuwa nazo tokea huko nyuma ya safari yake hadi kufikia kipindi hicho, ambazo kwa sasa, baadhi yake ndiyo hizi zinazoendelea kuandikwa kupitia uzi huu

Tatizo kubwa kabisa lililompata mhusika tangia kipindi hicho alipowasilisha taarifa hizo hadi sasa ni baadhi ya taarifa hizo kuonekana kuwa zilianza kufanyiwa kazi katika namna ambayo ililenga kuhatarisha zaidi maisha yake badala ya kumsaidia kama ambavyo yeye mwenyewe alikuwa ametarajia
 
UPDATE: THURSDAY 12 MAY 2022

TAARIFA MUHIMU KWA WASOMAJI WOTE WA UZI HUU

KWA MWEZI HUU, SPENDING YA MHUSIKA KIFEDHA IMEBADILIKA SANA ILA SIYO KWAMBA AMEPATA FEDHA YA NYONGEZA AU KULIPWA MADAI YAKE ANAYODAI SIKU NYINGI HAPANA

SPENDING YAKE IMEBADILIKA BAADA YA KUTAARIFIWA DHARURA AMBAYO IMETOKEA NYUMBANI KWAO
VILE VILE KUNA INVESTMENT AMBAYO AMEIAHIRISHA KUIFANYA, NA HIVYO KUPELEKEA FEDHA YAKE KUI-CHANNELKWENYE ALTERNATIVE INVESTMENT

KWA HALI HIYO BASI, MALIPO ANAYODAI HAJAWAHI KULIPWA HADI MUDA HUU

MHUSIKA AMEONA ALISEME HILI KWA SABABU TAYARI MR X AMESHAANZA PILIKA PILIKA NA KWA WAKATI HUO HUO, MKUU WA IDARA (MWI) PAMOJA NA KATIBU MUHTASI WAKE (KMMWI) HAWAPO NA HAWAONEKANI IDARANI AND WITHOUT ANY OFFICIAL NOTICE.

MHUSIKA ANGEWEZA KUWA PIA NA SAFARI MUHIMU YA KUELEKEA AIRPORT LAKINI AMEIAHIRISHA

KUNA MAZINGIRA YA KUTISHA KIDOGO OFISINI KWAKE AMBAYO YAMEKUSUDIWA KUWA YAKITIKI BASI IONEKANE KWAMBA NA MALIPO YAKE NAYO TAYARI YALIKUWA YAMESHAFANYIKA

WAHUSIKA WAKUU WA JAMBO HILI NI WAFUATAO
SENIIOR MSTAAFU WA KIKE
MWI
KMMWI
MR
X
MKUU WA MAJOR UNIT
AMBAYE NDIYE ALIKUWA MWI WAKATI SWALA HILI LA MALIPO YA MHUSIKA LILIPOKUWA LINAANZA

SPENDING YA MHUSIKA IMEBADILIKA KWA SABABU AMEAMUA KUFANYA ALTERNATIVE INVESTMENT NA KWAMBA KULE NYUMBANI KWAO KUNA EMERGENCE AMBAYO ASINGEPENDA SANA KUIONGELEA HUMU. HATA HIVYO YEYE ANAVYOONA NI KWAMBA KUNA JITIHADA AMBAZO ZINAZIDI KUFANYWA NA KUNDI HILI ILI HAPO BAADAYE IJE IONEKANE KUWA HELA YA MATUMIZI HAYO ANAYOFANYA INATOKANA NA MALIPO YA ILE AMBAYO AMEKUWA AKIIDAI OFISINI KWAKE KWA KIPINDI KIREFU SASA

IKUMBUKWE PIA KUWA MATURITY YA FDR YAKE ILIKUWA TAREHE 50 APRIL, FEDHA AMBAYO BAADA YA KUICHUKUA NDIYO ILE AMBAYO AMEAMUA KUIFANYIA ALTERNATIVE INVESTMENT

HII POST ANGEWEZA KUWA AMEPOST J3 WIKI HII LAKINI YEYE PEKE YAKE HANA MTANDAO JENGO ZIMA

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
IT'S VERY FORTUNATE; ANGALAU LEO AMEKUTA MTANDAO UPO; UMESHARUDI
 
BREAKING NEWS;

MHUSIKA ANAOMBA MSAADA WA KIPEKEE SANA KWENYE FAMILIA YAKE HUKO NYUMBANI KWAO MWANZA.


KWA KUANZIA ANAOMBA WATU WAFUATAO WAWEKWE KWENYE UANGALIZII MAALUM, NI KATI YA WATU AMBAO MIENENDO YAO IMESHAMTIA SHAKA SANA, NA.KWA KIPINDI KIREFU SASA CHA TKRIBANI MWAKA NA USHEE. POSSIBLY HAWA NDIYO WANAOWEZA KUWA NA TAARIFA MUHIMU SANA YA YALE AMBAYO YAMEKUWA YAKIENDELEA HUKO NDANI YA KIPINDI HIKI TAJWA

WA KWANZA
HUYU NI MTU YULE AMBAYE NI MREFU KARIBIA KUPITA WATU WOTE NA AMBAYE NI MREFU KULIKO WATU WOTE KWENYE UKOO. HUYU AMEKUWA PIA MASTERMIND WA MATUKIO MENGI KWENYE UKOO TANGIA MWAKA 1990, NA KWA MARA YA KWANZA MHUSIKA ALIKUJA KULIBAINI HLI HIVI KARIBUNI TU KWEYE MIAKA YA KARIBIA NA 2020

WA PILI
SHEMEJI YAKE NA MHUSIKA, MIME WA DADA WALIYEKUWA WAMEFUATANA NA MHUSIKA, NA AMBAYE MKE WAKE HUYO ALITANGULIA MBELE YA HAKI MNAMO JULY 2021, YAANI MWAKA JANA

HUYU WA PLI NDIYO PIA BABA WA MTOTO ALIYEWAHI KUPOTEZA MAISHA MWAKA 2006; MTOTO AMBAYE PAMOJA NA KUPTIWA TIBA YA MADAKTARI BINGWA, MHUSIKA ALILI-RECOMMEND PIA AKAOMBEWE KWA ASKOFU MKUU KAKOBE, LAKINI MAMLAKA ZILIZOKUWA ZIMEMZUNGUKA ZIKA-RECOMMEND AKAOMBEWE KWENYE KANISA A, AMBAPO MHUSIKA NDIPO HUWA ANAABUDU MPAKA MUDA HUU. KIPINDI HICHO ALIKUWA BADO HAJAWA MUUMINI NA HAIKUWA BADO ANAABUDU MAHALI POPOTE. MTOTO HUYO ALIKUJA HATIMAYE AKAPOTEZA MAISHA.

HAWA WAWILI KWA SASA NDIYO WANAOONEKANA KU-COORDINATE KILA KITU HUKO NYUMBANI, NA POSSIBLY KUAMUA NANI AENDELEE KUWA HAI NA NANI ASIENDELEE

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NYONGEZA MUHIMU

Kuna mwingine WA TATU ambaye anaonekana ku-coincide na tukio moja kubwa na ambalo limesababisha uwepo wa details fupi zilizopo hapo juu. Details zake huyu zitawajia hivi punde. Huyu ni mmojawapo wa wale wawili waliowahi kumpatia mhusika cheti cha kifo mwaka 2006 ambacho baadaye alikuja kugundua kuwa kilikuwa forged!
..................inaendelea
 
HUYU MTU WA TATU ALIKUWA AMETOWEKA TU NYUMBANI KWA MIEZI KADHAA, NA POSSIBLY HATA MWAKA. ALIONDOKA NYUMBANI BILA KUMUAGA MTU YEYOTE NA BAADA YA KUWA AMERUDI TU, AME-COINCIDE NA TUKIO MOJA AMBALO MPAKA MUDA HUU, MHUSIKA BADO LINAMTIA MASHAKA SANA KAMA NI LA KAWIDA. ANAWEZA AKAWA NA BAHATI MBAYA TU KWAMBA KURUDI KWAKE NYUMBANI KUME-COINCIDE NA TUKIO HILO ILA KWA UPANDE MWINGINE, KURUDI KWAKE KUNATIA MASHAKA PIA KWA SABABU WAKATI ANAONDOKA NYUMBANI HAKUWAHI KUMUAGA NDUGU YEYOTE, NA POSSIBLY HATA NYUMBANI KWAKE HAWAKUWAHI KUJUA KULE ALIKOKUWA AMEENDA. TETESI ZILIKUWA ZINADAI KUWA ALIKUWA AIDHA DAR ES SALAAM AU ZANZIBAR, AU SEHEMU ZOTE MBILI. SASA HIVI AMESHARUDI NA NDIYO ANAKARIBIA KUMALIZA WIKI TATU AU MWEZI
 
KAMA MASHAKA YA MHUSIKA KUHUSIANA NA TUKIO LA HIVI KARIBUNI AMBALO DETAILS ZAKE KWA SASA ANAZI-WITHHOLD TANAWEZA KUWA YAKO GENUINE:

Uwezekano mkubwa ni kwamba staff-mates wafuatao (au MR X peke yake) walishakuwa na link ya mawasiliano na baadhi ya ndugu wa mhusika walioko nyumbani kwao Mwanza

SENIIOR MSTAAFU WA KIKE
MR X
MKUU WA MAJOR UNIT


Hawa ni miongoni mwa baadhi ya wale aliowataja kwenye post hii hapa #992

Mhusika anayo dhana hii kwa sasa kwa sababu hawa ndiyo wale walioanza “kumtishia nyau” J4 ya wiki hii ili kesho yake J5 asifanye safari yake ya kwenda Airport

  • Ili kuwapoteza lengo lao, mhusika aliamua kuigiza kama amekubali kutishiwa nyau huko na hivyo kutoa taarifa humu jukwaani kuwa safari hiyo ya kwenda airport hataifanya
  • Badala ya kutoifanya safari hiyo, jana J5 alikuwepo Airport asubuhi na mapema
BAADA YA MHUSIKA KWENDA AIRPORT JANA

Alichokutana nacho huko Airport ndiyo kile ambacho tukio lake limemtia mashaka sana na hadi muda huu yuko njia panda akiliwaza kama lilikuwa ni la kweli au lilitanguliwa na maigizo kwanza halafu hatimaye maagizo hayo ndiyo yakasababisha tukio hilo likaja kuonekana kuwa ni la kweli, possibly baada ya siku kadhaa kuwa zimepita igizo hilo likiwa linaendelea kufanyika.

Kwa kifupi tu ni kwamba tukio hilo linamkumbusha tukio jingine la Mkuu wa Idara wa zamani ambaye yeye aliwahi kudondoka kutoka juu ghorofa ya kwanza ofisini na kuumia kiwiko peke yake huku bega likiwa salama; na hivyo kupelekea kufungwa p.o.p kwenye kiwiko peke yake

MSAADA UNAHITAJIKA KATIKA HILI

Kwa tukio hili; iwapo kama litathibitika kuwa ni la kupikwa, anaomba sasa kama kuna uwezekano, msaada wa kipekee ufanyike kwake hasa kwa mtu ambaye ana m-refer humu kama MR X. Mhusika anaomba msaada huu kwa sababu huyu mtu yupo kila mahali mhusika alipo kuanzia ofisini, kanisani na hata nyumbani pia. Uhakika alionao mhusika mpaka muda huu ni kwamba MR X anaye mtu ambaye huwa anamtumia kama link ya kufanya mawasiliano na baadhi ya ndugu zake mhusika walioko Mwanza. Hiki kitu cha MR X kuonekana kuwa na link ya namna hii, kwa mara ya kwanza alikibaini mwezi Mei 2011, na tangu wakati huo amekuwa akikifanyia kazi na kujiridhisha pasipo shaka kabisa kuwa MR X aidha huwa ana mawasiliano hayo ya direct na baadhi ya ndugu zake na mhusika walioko kule Mwanza, au ana mtu ambaye ni link muhimu sana na hivyo huwa anamtumia huyo

MR X anaonekana ni mmojawapo wa watu waliojua kuwa mhusika angefanya safari ya kwenda Airport J5 na hivyo kuanza pilika pilika za kumtishia nyau ili asiende

Maelezo zaidi yatafuata siku za baadaye
 
UPDATE: SATURDAY 14TH MAY 2022

KUHUSIANA NA “SPECIALIST”………

TUKIO LA KWANZA KABISA LA MSIBA AMBALO MHUSIKA ALIWAHI KUHUDHURIA MAENEO JIRANI NA OFISINI KWAKE, NA PIA JIRANI NA MAHALI PALE ANAPOISHI YEYE NA KUKUTANA NA WATU WATATU TU ALIOWAFAHAMU; KWENYE MSIBA HUO


Ukiondoa tukio la msiba wa idarani kwake na mhusika ambalo aliwahi kuleta taarifa zake humu na lililotokea mwaka 2020; na ambalo mhusika alijulishwa taarifa zake na Kaimu Mkuu wa Idara (ambaye kwa sasa ndiye Mkuu wa Idara), kuna tukio jingine la aina hiyo ambalo tayari mhusika alikuwa ameshalishuhudia hapo kabla (nadhani mwishoni mwa mwaka 2016 au mwanzoni mwa mwaka 2017)

Kwa hiyo tukio hili la idarani kwake na mhusika LILIKUWA NI LA PILI, na lilishahibiana kwa kiasi na lile la kwanza la lililotokea nyumbani kwake na “SPECIALIST”; ila kwa wakati huo mhusika hakutaka kuuongelea mfanano wa matukio haya; ISIPOKUWA ALILLAZIMKA TU KULIONGELEA LILE LA IDARANI KWAKE (LA PILI) na kuliacha lile la “SPECIALIST” (LA KWANZA) baada ya kuwa ameona kwa mara nyingine tena kuwa hata lile la idarani nalo pia lilikuwa na namna ya mbinu fulani (tricks) hivi ambazo zilikuwa zimekusudiwa maalumu kwa ajili yake mhusika na zilizoshahibiana kwa namna fulani na za tukio lile la kwanza

NAMNA MHUSIKA ALIVYOTOKEA KUPATA TAARIFA ZA KILA MSIBA KWA MISIBA HII

Taarifa za tukio la msiba wa idarani kwake mhusika alizipata SIKU YA IJUMAA akiwa kwenye korido baada ya saa 6 mchana; maeneo ya ofisini. Ilikuwa ni baada ya kuwa amemaliza darasa alilokuwa nalo siku hiyo. Mhusika alijulishwa kuwa msiba wenyewe ulikuwa maeneo ya karibu kabisa na ofisini, nyumbani kwa mfiwa na ambapo pia ni jirani kabisa na mahali pale anapoishi mhusika.

TUKIO LA KWANZA LINALOFANANA NA HILO AMBALO MHUSIKA ALIKUWA TAYARI AMESHAKUMBANA NALO HAPO KABLA

Tukio la kwanza kabisa la namna hiyo mhusika aliwahi tayari ameshakumbana nalo kwa mara ya kwanza, nyumbani kwa “SPECIALIST”; hili la idarani kwake, lilikuwa la pili

Kwenye tukio la kwanza, mhusika hakupata taarifa kutoka kwa “SPECIALIST’ mwenyewe bali kwa binti msaidizi wake wa ofisini ambaye kwa bahati tu walikutana nje ya Ofisi ya Mkuu wa Idara ofisini kwa mhusika

  • Binti huyu alikuwa amefika ofisini pale kwa shida za kiofisi na wakati wanabahatika kukutana na mhusika, binti alikuwa tayari yuko njia moja anarudi ofisini kwake
  • Baada ya kusalimiana na mhusika, mhusika alimpa pia binti salaam za swahiba wake “SPECIALIST” ili amfikishie
  • Pale ndiyo binti alipomjulisha mhusika kuwa “SPECIALIST” hakuwepo ofisini kwake siku hiyo bali nyumbani kwa sababu alikuwa amepata msiba mkubwa. Siku hiyo ilikuwa ni SIKU YA IJUMAA wakiwa kwenye veranda iliyo mbele ya ofisi ya Mkuu wa Idara
Ilipofika kesho yake Jumamosi, mhusika aliamua kwenda kuhani msiba nyumbani kwake na “SPECIALIST”

Pamoja na kuwa ilikuwa ni Jumamosi, mhusika alikaa pale nyumbani kwa takribani masaa mawili, na katika muda wote wote huo watu pekee aliowaona na kuwafahamu msibani pale walikuwa ni watatu tu

  • “SPECIALIST” mwenyewe
  • Injinia mmoja kutoka miliki za nyumba ambaye alikuwa anasimamia ukarabati wa nyumba anayoishi “SPECIALIST”
  • Bwana Afya wa taasisi anayofanyia kazi mhusika
Hapakuwa na office-mate yeyote wa “SPECIALIST” kwenye msiba huo; yaani wale ambao anafanya nao kazi idara moja, hawakuwepo hata mmoja

Hawa office-mates wa “SPECIALIST” majority yake mhusika anawafahamu kutokana na interactions nao za kipindi kirefu kiasi cha takribani miezi mitatu; ambazo mhusika aliwahi kuwa nazo na wafanyakazi hao mwaka 2008.

Kwa hiyo walio wengi wa wafanyakazi wa idara hiyo mhusika anafahamiana nao na baadhi yake wamekuwa pia ni majirani zake kwenye mazingira ya makazi ya taasisi ambamo mhusika bado anaishi mpaka leo

Mfanano unaotokea hapa ni kwamba, kwenye matukio haya mawili; ni kwamba katika kila tukio

  • Mhusika alikuwa anapata taarifa za uwepo wa kila msiba, SIKU ZA IJUMAA aidha akiwa kwenye korido au kwenye veranda
  • Matukio yote mawaili yalitokea maeneo jirani kabisa na ofisini kwa mhusika na pia jirani na sehemu ya makazi yake
  • Taarifa zilizokuwa zinafikishwa kwa mhusika zilikuwa ni “second hand” kwa maana kuwa waliokuwa wanamjulisha mhusika kuhusiana na uwepo wa msiba walikuwa ni watu wengine na si wahusika wa msiba wenyewe pamoja na kwamba mawasiliano yake ya simu walikuwa wanayo
  • Bila kujali ukubwa wa msiba uliokuwa umetokea, kwenye msiba wa kwanza (2016/2017) alikutana na watu watatu aliowafahamu na ambao amewataja hapo juu
  • Vile vile, bila kujali ukubwa wa msiba uliokuwa umetokea, kwenye msiba wa PILI (2020) napo alikutana pia na watu watatu tu aliowafahamu. Hawa walikuwa ni jirani yake na mhusika pamoja na mke wake, pamoja na mama mwenye nyumba ambaye mume wake ndiyo alikuwa mfiwa
Staff-mates wengine wote kutoka idarani kwa mhusika hawakuwepo msibani, na mhusika aliondoka ofisini hai hai siku hiyo akiacha ofisi karibia zote zikiwa zimefungwa; huku akidhani kuwa wenzake wote watakuwa walikuwa wametangulia kwenye msiba kwa sababu yeye alikuwa amecchelewa kupata taarifa; alizipata siku hiyo hiyo

Siku hiyo, alipokuwa yupo nje kwenye parking za gari akiwa anajiandaa kuelekea msibani, pale ndiyo alibahatika kumuona SENIOR MSTAAFU WA KIUME (SMME), na akiwa anajiandaa kuwasha gari aondoke, na ndiye mtu pekee aliyekuwa amebaki ndani ya jengo muda huo, ukiondoa mhusika mwenyewe

  • Baada ya kumuona SMME, mhusika alidhani kuwa SMME naye alikuwa yuko njia moja kuelekea msibani kwa sababu ndiyo mtu pekee ambaye alikuwa ameabakia idarani siku hiyo
  • Baada ya kufika msibani, mhusika hakumkuta SMME
Aidha mhusika hakumkuta mtu mwingine yeyote yule kutoka idarani kwake, na wakati huo huo watu wote ofisini hawakuwepo wakati anaondoka idarani. Ofisi zote zilikuwa zimefungwa

Kabla hajaondoka ofisini siku hiyo, mhusika alikagua kwanza floor zote na alijiridhisha kuwa watu wote hawakuwepo idarani na alipotoka nje ndiyo alimuona SMME tu na hapo ndipo alipogundua kuwa huyo ndiyo alikuwa mtu pekee ambaye naye alikuwa amebakia ndani ya jengo muda huo

HITIMISHO

Tukirudi kwenye tukio hili la “SPECIALIST”, office mates wote kutoka idarani kwa “SPECIALIST”, hawakuwepo kwenye msiba huo, isipokuwa staff-mates hao wawili tu mhusika aliowataja hapo juu ikiwa ni pamoja na “SPECIALIST” mwenyewe ambaye ndiye aliyekuwa mfiwa

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
POST MAALUMU YA BAADHI TU YA MAMBO AMBAYO YAMEKUWA YAKIENDELEA MKOANI NYUMBANI KWAO NA MHUSIKA NA AMBAYO YANAWEZA KUANDIKWA HUMU JUKWAANI

MAELEZO YA UTANGULIZI: KILICHOPELEKEA MHUSIKA KUANDIKA POST HII HAPA #994 YENYE KICHWA “BREAKING NEWS” WIKI HII


J3 ya tarehe 17 April 2022, mhusika alipewa taarifa kuwa mmojawapo wa watoto huko nyumbani kwao Mwanza ana tatizo na alipelekwa hospitali kwa ajili ya vipimo. Mtoto huyu waliamua kumpeleka hospitali baada ya kuwa ameonyesha dalili za kuwa anatembea kwa mtindo wa zig-zag fulani ambayo ilikuwa inapelekea wakati mwingine kuanguka chini, kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kwake

Baada ya kuwa amepelekwa hospitali, kilifanyika kipimo cha MRI na baada ya hapo, mama wa mtoto aliombwa asubiri majibu ambayo yalikuwa yanatoka baada ya siku tatu tangu siku hiyo.

Siku mama wa mtoto alipompelekea mtoto hospitali kwa ajili ya kipimo cha MRI, ndiyo siku ile ambayo mhusika lipata taarifa za ugonjwa wa mtoto huyu kwa mara ya kwanza

  • Haya yote ni maelezo kwa mujibu wa mama wa mtoto; kwa mhusika
  • Mama wa mtoto huyu ni mdogo wake na mhusika, wanafuatana kwa kuzaliwa
  • Mama wa mtoto pia ni mmojawapo wa watu muhimu sana ambao walimsomesha mhusika tangu akiwa Sekondari kuanzia kidato cha kwanza na kuendelea
  • Wakati mhusika anaanza kidato cha kwanza, mama huyu alikuwa na umri wa miaka 13 kamili (Child Labour) na alikuwa anashinda shambani siku za weekend, akilima pamba kwa ajili ya kumsomesha mhusika pamoja na mwingine dada yake ambaye kwa sasa ameshatangulia mbele za haki
  • Wakati huo vile vile, mama huyu alikuwa bado anasoma shule ya msingi darasa la sita
  • Mama huyu yeye hakufanikiwa kuendelea na masomo, lakini pamoja na hayo, maisha yake yote aliamua kukaa na mama yake mzazi akimtunza na hadi leo yuko naye akiwa anamtunza
Kutokana na mhusika kuuona moyo wa mama huyu, baada ya mhusika kubahatika kupata kazi, aliamua kuwasomesha watoto wote wa huyu mama ambao kwa sasa, mmoja maeshajitegemea na mwingine kwa sasa yuko Chuo Kikuu mwaka wa kwanza

Wengine wawili bado wako shule ya msingi, na wa mwisho kabisa ndiyo yuko darasa la tatu sasa, ni mvulana mwenye miaka takribani tisa sasa

Huyu wa mwisho ndiyo aliyepelekea mhusika akaandika post hiyo hapo juu yenye kichwa “Breaking News” na ndiye ambaye taarifa zake zitaendelea kuwajieni mpaka pale mhusika atakapowajulisha vinginevyo

…………………..inaendelea
 
……………..inaendelea

BAADHI TU YA MAMBO AMBAYO YAMEKUWA YAKIENDELEA MKOANI NYUMBANI KWAO NA MHUSIKA

CHRONOLOGY OF EVENTS KUHUSIANA NA VIPIMO VYA MTOTO HUYU


J3 ya tarehe 17 April 2022 kipimo cha MRI kilichukuliwa na majibu yake yalitoka Alhamis ya tarehe 21 April 2022

Majibu yalionyesha mtoto ana tatizo kubwa kwenye ubongo na anatakiwa kupewa referral ya kwenda hospitali nyingine kubwa kwa sababu vifaa vinavyohitajika kwa ajili ya tiba yake, havikuwepo kwenye hospitali hiyo ya rufaa

Hata hivyo rufaa hiyo haikuweza kuandikwa siku hiyo baada ya CD/DVD iliyorekodi tatizo hilo kupotea ghafla ofisini kwa aliyekuwa anahusika kuandika rufaa hiyo

Mhusika hakumbuki vizuri maelezo ya namna DVD hiyo ilivyokuja kupatikanaje baadaye ila anachokumbuka tu ni kwamba rufaa hiyo ilichelewa kuandikwa kutokana na sababu zisizoweza kuzuilika na hatimaye ilikuja kuandikwa na kutolewa wiki hii J5 ya tarehe 12 May 2022

Kwa hiyo Alhamis ya tarehe 13 mtoto alliingia uwanja wa ndege akiwa anaendeshwa kwenye wheel chair ya Swissport, akiwa hawezi tena kutembea

Taarifa alizopewa mhusika ni kuwa hadi kufikia wiki jana, mtoto huyo alikuwa anaweza kutembea kutoka nyumbani hadi sokoni, umbali wa takribani km moja

Mtoto huyo pia anaongea vizuri na anakula vizuri hadi muda huu

Kuanzia wiki hii ambayo ndiyo amefanikiwa kupata rufaa, hali ndiyo ilizidi kuwa mbaya hadi ikapelekea akashindwa kutembea. Tangu anatoka ndani ya Airport alikuwa anasukumwa kwa msaada wa wheel chair ya Swissport

Mhusika alikuwa pia mara kwa mara akiongea na mtoto kwa simu na kila alipokuwa akimuuliza kuwa unaendeleaje, alikuwa anajibu “sijambo” na alikuwa anasema kuwa alikuwa anatembea pia. Sasa sijui kama huu ulikuwa ni utoto au nini, mhusika ameshindwa kuelewa

………………..inaendelea
 
Back
Top Bottom