#COVID19 Mkasa wa kipekee kuhusu pilikapilika za kujikinga na COVID-19

NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA SENIOR MSTAAFU WA KIKE NA NAMNA ANAVYOONEKANA AIDHA KUKWEPANA AU KUUMANA VIZURI ZAIDI NA BAADHI YA MATUKIO YALIYOTOKEA IJUMAA WIKI JANA YAKIMHUSISHA FUNDI WA AC

Kwa wiki yote nzima ya kazi iliyoishia Ijumaa ya tarehe 08/04/2022; huyu mama alihudhuria ofisini siku moja tu yaani hiyo ya Ijumaa na ambayo ndiyo siku maandalizi ya fundi wa AC yalikamilika na hatimaye fundi huyo kufanikiwa kufika ofisini kwa mhusika. Kwa siku zingine zote nne za mwanzo wa wiki kabla ya Ijumaa, mama huyu hakuwepo kabisa ofisini. Mhusika hakumbuki vizuri lakini possibly hata wiki iliyokuwa imepita nyuma yake, mama huyu hakuwepo pia ofisini kwa angalau siku moja au mbili zile za mwisho wa wiki ya kazi (possibly siku ya Alhamis au Ijumaa au zote mbili)
 
BY THE WAY: MUDA KAMA WA SAA MOJA NA USHEE ILIYOPITA: FUNDI WA AC AMERUDI TENA OFISINI KWA MHUSIKA AKIWA PEKE YAKE

Baada ya kufika, mhusika amemshauri asifanye kazi tena ofisini kwake; na wamekubaliana katika hilo
Baada ya hapo, fundi aliomba aangalie kuna kifaa chake alikisahau jana, akidai possibly alikisahau sehemu ambayo alisimama wakati wanapandisha AC juu. Mhusika alimjulisha kuwa hakuna kifaa ambacho amekiona ofisini humo kinachoendana na maelezo ya fundi huyo. Hata hivyo mhusika alinyanyuka kwenye kiti wakaambatana hatua kwa hatua na fundi hadi pale alipokuwa anadai alikisahau kifaa na hawakukiona. Baada ya zoezi hilo kufanyika, fundi aliondoka
 
UPDATE: THURSDAY 14TH APRIL 2022

TUKIO LA AC YA OFISINI KWA MHUSIKA KUTOKUFANYA KAZI KUANZIA J4 YA TAREHE 29 APRIL 2022; NA NAMNA LINAVYOHUSIANA NA MATUKIO MENGINE MENGI SANA YA AC YA GARI LA MHUSIKA KUTOKUFANYA KAZI MARA KWA MARA YALIYOWAHI KUTOKEA HUKO NYUMA; TANGU AANZE KUIMILIKI GARI HIYO MWAKA 2013


Kwa uzoefu wake alionao wa matukio haya ya AC, ni kwamba AC hii ya ofisini kwa mhusika itakuwa ilitolewa Gas na ndiyo maana ikawa haiwezi tena kupoza hewa.

  • Fundi aliyeletwa kuja kuifanyia marekebisho, hakuwa na mitungi ya gas na hivyo ilikuwa haiwezekani kwa yeye kuweza kuirekebisha
  • Kwa hiyo kilichokuwa kinaendelea kwenye swala hili ilikuwa ni mipango mingine tu ambayo mhusika haiwezi kuijua in details zaidi, ikiwa ni pamoja na ubabaishaji tu
Matatizo mengine ya aina hii yamewahi pia kutokea kwenye AC ya gari la mhusika mara kwa mara; gas ya AC ya gari lake ilikuwa inatoka mara kwa mara; wakati huo kwenye cooling system nzima ya air-conditioning ya gari hapakuwa na tatizo lolote na wala leakage ya aina yoyote ile

  • Kwa hiyo kila lilipokuwa tatizo hilo linatokea kwenye AC ya gari, alichokuwa anafanya mhusika ni kwenda kujaza gas nyingine kule mjini gerezani na baada ya hapo anaendelea na kazi zake kama kawaida
  • Kwa mwaka, alikuwa anajaza gas mara mbili au mara tatu na trend hii imekuwa ikiendelea hivyo tangu mwaka 2013 hadi mwaka jana 2021, alipoamua kupumzika kutumia AC ya gari kwa muda
  • Akiwa katika muda huo wa mapumziko, ndiyo sasa gari ikaibiwa Engine na hivyo kusababisha uwepo wa compressor nyingie ya AC ambayo yeye ilikuwa ni mbovu kabisa; ilikuwa completely haifanyi kazi
  • Ile Compressor ya AC ya gari yake iliyokuwa kwenye engine iliyoibiwa; yenyewe ilikuwa inafanya kazi vizuri tu isipokuwa wakati engine inaibiwa, compressor hiyo ilikuwa haitumiki tena kwa sababu mhusika alikuwa hajaenda kujaza gas baada ya gas kuwa imetolewa
  • Meneo ambayo gas ilikuwa inatolewa ni kwa mara nyingi sana KANISANI kwenye siku za J2 na kwa mara chache OFISINI,
  • Kwa matukio ya ofisini ilikuwa ni KARIBIA MARA ZOTE gari la MR X linapokuwa limepaki jirani na lile la mhusika
  • Kwa hiyo mitindo miwili ya kutowesha gas kwenye AC ya gari la mhusika ilikuwa inatumika; mtindo wa OFISINI na mtindo wa KANISANI
  • Mtindo uliokuwa unatumika OFISINI ni ule wa HUJUMA ZA KUTUMIA MAIGIZO yaliyokuwa yamedhamiriwa kumuonyesha mhusika kuwa kutoweka huko kwa gas lilikuwa shambulio la KIROHO na si HUJUMA
  • Mtindo uliokuwa unatumika KANISANI kidogo unafanana na ule wa ofisni; ilikuwa ni lazima kwanza gari la mhusika liwe limepaki kwenye sehemu ambayo linakuwa limepakana na magari makubwa au lilipokuwa limepaki kwenye parking za mwanzoni (ya pili au ya tatu) kutoka geti kuu la kuingilia kanisani
  • Zaidi ni kuwa mtindo wa Kanisani ulikuwa unatumia mbinu ya kutoa gas inabaki kidogo kiasi tu cha kuweza kumtosha mhusika kutumia AC kutoka Kanisani hadi nyumbani; na kesho yake J3 asubuhi gas hiyo inakuwa haipo tena hivyo kupelekea AC kutokufanya kazi tena tangu siku hiyo ya J3
Ruling yake kwa kipindi hicho kuhusiana na matukio haya ya kutolewa Gas, ilikuwa inampeleka nyumbani zaidi mahali anapoishi, lakini kwa sasa anaelewa matukio hayo yalikuwa yanakuwa coordinated kutokea Kanisani na uhakika huo anao kwa zaidi ya asilimia 100

Zaidi ni kwamba zaidi ya asilimia 95% ya matukio ya kutoweka kwa Gas ya AC ya gari la mhusika; yalikuwa yanabainika J3 asubuhi; na kwa mara nyingi sana kwenye tarehe za mwisho au mwanzoni mwa mwezi. Na hii ndiyo mojawapo ya sababu zilizowahi kupelekea mhusika akasitisha kwa muda kwanza kutoa sadaka Kanisani

Kwa hali basi hiyo zaidi ya asilimia 95% ya matukio ya kutolewa gas ya AC ya gari la mhusika, yamekuwa yakiwa coordinated kutokea Kanisani na yalikuwa ynabainika J3 asubuhi mhusika anapowasha gari asubuhi kuanza kuelekea ofisini

TUKIO LA MWISHO KABISA (LA OFISINI) LA KUTOLEWA GAS YA AC YA GARI LA MHUSIKA NA KABLA YA ENGINE KUIBIWA


Hili lilifanyikia ofisini; na mhusika wa tukio alikuwa ni MR X

  • Baada ya kufika ofisini asubuhi siku hiyo; mhusika alipaki gari lake likiwa kawaida kabisa na baada ya kupaki, MR X naye alikuja akapaki pembezoni mwa gari la mhusika, na katika namna ambayo aliliziba gari hilo kwa upande ule ambao lingeweza kuonekana na watu walio ndani ya jengo zilimo ofisi zao
  • Kawaida MR X huwa anawahi sana ofisini, possibly kabla ya saa 1:30 au hata kabla ya saa moja kamili anakuwa tayari ameshafika ofisini. Ni mmojawapo wa watu wanaowahi sana ofisini ikiwa ni pamoja na mahudhiurio mazuri sana ofisini
  • Kwa hiyo ikitokea katika muda wake huo wa kawaida kuwa hajabahtika kufika ofisini; ujue ana dharula au ana mission maalum; kuna kitu anakuwa amepanga kuja kufanya ofisini
  • Mali na MR X; mhusika naye pia ana tabia moja kwamba akiingia ofisini hatoki; kwa hiyo akishafika ofisini na kupaki gari lake sehemu; chances kubwa kabisa ni kwamba gari lake litakaa kwenye parking hiyo hadi muda wake wa kuondoka ofisini utakapofika
  • Vile vile mara nyingi sana, kama si mara zote, mhusika huwa hawezi kupaki jirani na pale lilipo gari la mhusika
Kwa hiyo mara nyingi sana; kama si mara zote ukikuta gari la mhusika limepakana kwa kupaki na lile la MR X, ujue kuwa aliyetangulia kupaki pale ni mhusika



HITIMISHO

Ni kwamba kilichokuwa kinaendela kwenye AC ya gari la mhusika, zilikuwa ni hujuma ambazo zilikuwa zinakuwa coordinated katika namna ambayo wahusika wke walitamani zionekane kuwa ni mashambulio ya kiroho na possibly MR X alikuwa ana coordinate hujuma hizi kwa upande wa Kanisani pia

Hadi mara ya mwisho AC ya gari la mhusika inatolewa, mhusika alikuwa ni MR X na hivyo hadi kufikia muda ule gari linaibiwa engine; AC ilikuwa haifanyi kazi japo COMPRESSOR ilikuwa ni nzima kabisa; haikuwa na tatizo lolote

Baada ya Engine kuibiwa, compressor iliyokuwepo kwenye engine kuukuu iliyowekwa kwenye gari la mhusika ndiyo iikaw ni mbovu.

Wakati huo huo, Fundi mekanika (FME) wa gari la mhusika ndiyo akaanza kumshauri aweke compressor nyingine. Wakati huo mhusika alikuwa bado hajagundua kama kuna swapping ya engine ilikuwa tayari imeshafanyika

………………….inaendelea
 
KUHUSIANA NA FUNDI MEKANIKA (FME) WA GARI LA MHUSIKA

MAELEZO YA UTANGULIZI


Kwa matukio ya hivi karibuni kuhusiana na FME, tunaweza kuanzia mwaka jana kwenye siku ambayo gari la mhusika lilipata hitilafu akiwa mtaani sehemu jirani na mahali pale anapoishi; siku ya Ijumaa jioni mara baada ya kuwa ametoka ofisini.

Kwa hiyo kwa sasa, tutatembea na matukio muhimu tu kuanzia kipindi hicho hadi leo, halafu baadaye tena ndiyo tutayarudia tena yale yaliyowahi kutokea kabla, focus yetu ikiwa ni kwa huyu FME tu

Tukirudi sasa kwenye mada yetu, hitilafu hiyo iliyowahi kutokea siku ya Ijumaa jioni baada ya mhusika kutoka ofisini, ilisababisha usukani wa gari kuwa mgumu na hivyo mhusika kushindwa kuendesha gari kawaida.

Na kwa sababu siku hiyo ilikuwa ni Ijumaa tena jioni, kama ageamua kulipeleka gari gereji, ingebidi liende likalale huko kitu ambacho alikuwa hataki kwa sababu matukio ya kabla ya siku hiyo tayari yalikuwa yameshampa indicator za wasiwasi kuhusiana na FME; kwamba fundi huyu hakuwa na nia njema na gari la mhusika. Kwa hiyo hadi kufikia siku hiyo, matukio ya nyuma yalikuwa tayari yameshamfanya mhusika kupoteza kabisa imani na FME; japo mhusika hakuwa ameidhihirisha hali hii kwa FME; na hajui kama labda FME mwenyewe alikuwa amegundua hilo ama la; pamoja na yeye (mhusika) kujitahidi kuificha hali hiyo

Hata hivyo hadi kufikia muda huo, na mhusika mwenyewe pasipo kuwa na ufahamu kuwa alichokuwa anajaribu kukikwepa kilikuwa kimeshatokea lakini ukweli ulikuwa ni kwamba tayari watu walikuwa wameshafanya kazi; na engine hiyo ilikuwa tayari imeshaibiwa tangu mwanzoni mwa mwezi wa tatu; na possibly hicho ndicho kilichopelekea tatizo hili la usukani kuwa mgumu. Uwezekano mkubwa ni kwamba kuharibika kwa kifaa hicho siku hiyo (kilichohusiana na usukani) kulisababishwa na engine nyingine iliyowekwa kwenye gari la mhusika kutokuwa imefungwa vizuri baada ya kutolewa ile iliyokwepo mwanzo

Baada ya kutokea tatizo la kifaa hiki ambcho yeye kwa lugha ya ki-layman alikiita “steering wheel belt roller” mhusika aliamua kwenda kulipaki gari nyumbani kwanza Ijumaa hiyo

  • Kesho yake Jumammosi mhusika hakulitumia gari hilo
  • J2 pia hakulitumia gari hilo na hivyo ilibidi aahirishe kwenda Kanisani
Siku ya J3 asubuhi ndiyo alilitumia gari hilo kwenda ofisini na baada ya muda asubuhi hiyo hiyo, ndiyo aliamua sasa kulipeleka gereji kwa FME. Gari lilirekebishwa na haikuchukua muda mrefu, na baadaye mhusika aliondoka baada ya dakika kadhaa kupita akarudi ofisini na kuendelea na kazi zake zingine

BAADA TENA YA SIKU KADHAA KUPITA…………

  • J3 asubuhi rectifire ya umeme ikaharibika, betri illikataa kupiga
  • Jana yake J2 baada ya mhusika kuwa ametoka Kanisani alipaki gari ikiwa salama kabisa, halafu ghafla kesho yake J3 asubuhi betri ikawa haiwezi kupiga
Kwa experience yake aliyonayo mhusika kwa sasa, uwezekano mkubwa ni kwamba uharibifu huu ulifanyikia kwenye parking za Kanisani J2 alipokuwa yupo kanisani

Baada ya kutokea hitilafu hiyo, mhusika aliipeleka tena gari gereji siku hiyo kwa ajili ya marekebisho ya ku-replace kifaa kilichokuwa kimeharibika, na ilikuwa ni lazima kufungua boneti la gari kwanza na hatimaye COMMPRESSOR ya AC halafu ndiyo kifaa hicho kiweze kufungwa.

BAADA YA BONETI KUWA LIMEFUNGULIWA KWA MUDA MREFU, NDIYO PALE MHUSIKA ALIBAINI KUWA ENGINE ILISHABADILISHWA

Swali lililomjia kichwani ni je, engine imebadilishwaje wakati gari haijawahi kulala gereji hata siku moja?

Baadaye mhusika alikuja kubaini window moja mwanzoni mwa mwezi wa tatu ambapo taa za kwenye parking kwa maghorofa mawili yaliyo jirani likiwemo lile analoishi yeye mhusika, zilizimwa kwa siku kadhaa kukawa na giza totoro. Mbali na hivyo, mita ya umeme wa taa za kwenye parking kwa ghorofa lile analoishi mhusika ilikuwa imeondolewa kabisa

Hata hivyo kitu hiki kuhusiana na engine hii nacho aliamua kukificha pia kwa kujua kuwa pengine hata FME naye atagundua pia tatizo hilo

  • Tofauti na matarajio yake mhusika, FME hakuweza kugundua wakati hata muonekano wa radiator tu ambayo alikuwa siku zote akicheza nayo akiisafisha au kubadilisha coolant; ulikuwa tofauti mno
  • Engine iliyokuwepo awali ilikuwa almost mpya, hadi rangi yake ilikuwa ni mpya na ilikuwa safi kabisa bila vumbi jingi na matope yaliyogandamana siku nyingi
  • Hii iliyokuwepo siku hiyo ilikuwa kuukuu hadi rangi; na ilikuwa ni chafu mno.
Mhusika anaweza kuwa ni mchafu kwenye vitu vingine, lakini haikuwa hivyo kwa gari lake ikiwa ni pamoja na engine ya gari hilo

Kwa hiyo, wakati utaratibu wa kutafuta kifaa kilichokuwa kimeharibika ili kiweze kufungwa kwenye gari ukiwa unaendelea siku hiyo; FME alimshauri mhusika afunge pia COMPRESSIOR nyingine ya AC na kwamba yeye anawajua watu wanaoweza kumletea COMPRESSIOR nyingine nzuri pale pale gereji walipokuwapo. Actually haikuwa mara ya kwanza kwa FME kutoa ushauri huu siku hiyo, bali hapo awali FME alikuwa amewahi pia kutoa ushauri wa aina hiyo siku ya kwanza mhusika alipokuwa amepeleka gari kwa ajili ya kurekebisha “steering wheel belt roller”; sema tu kitu unique alichokuwa anafanya FME wakati anamshauri mhusika ni kwamba alikuwa anahakikisha kuwa hakuna fundi mwingine yoyote yule pale gereji, anayesikia wanachoongea. Kwa hiyo ushauri wa mwanzo aliwahi kuutoa katika mazingira ambayo walikuwa pia wawili tu na katika muda ambao mhusika alikuwa tayari ameshawasha gari anajiandaa kuondoka na alikuwa ameshafika getini kabisa anatoka nje ya uzio wa gereji. Hapo ndipo FME alimsogelea mhusika na kuteta naye pale getini; gari ikiwa inaunguruma tayari

MHUSIKA AKUBALI USHAURI WA KUFUNGA COMPRESSOR NYINGINE

Baada ya FME kushauri mhusika afunge COMPRESSIOR nyingine ya AC; mhusika alikubaliana na uamuzi huo kwa sababu

  • Ili fundi aweze ku-replace kifaa kilichokuwa kinahitaji matengenezo siku hiyo, ilikuwa ni lazima pia COMPRESSIOR ya AC ifunguliwe
  • ilikuwa ni tayari mwisho wa mwezi; mhusika
Mpaka hapa mhusika akawa hana shaka kabisa kuwa engine iliyokuwa kwenye gari haikuwa ile ya kwake. Kazi sasa ikabaki kuwa anaweza kuthibitisha hilo kwa watu wengine na mafundi wengine waliopo hapo gereji? Atathibitishaje?

Akiwa anachekecha akili yake, hatimaye mhusika alifikia uamuzi wa jambo moja kubwa kwamba kama akikosa kabisa namna ya kuthibitisha kuwa engine iliyoko kwenye gari siyo ile yake, itabidi akae kimya, ………..kimya kimya kimya kabisa; unless anapata namna ya kuthibitisha hilo

Zaidi ni kuwa kipindi mhusika anabaini swapping ya engine hizo kufanyika; alikuwa hana hata idea ya kama engine hiyo iliyokuwa imewekwa inaweza kuwa haikufungwa vizuri kiasi cha kuwa loose; hakuwa na idea hiyo. Idea hiyo alikuja kuipata kutoka na kubabaika kwa FME mwenyewe; kwenye tukio jingine siku nyingine ambapo mhusika alikuwa sasa ameirudisha gari makusudi kwa FME na kijanja kwa ajili ya kumpima ili kupata taarifa zaidi kama aliyehusika na tukio ni yeye ama la. Test simple aliyoitumia siku hiyo ni kumuomba fundi abadilishe COOLANT na hapo ndipo alipopatia zaidi ya asilimia 200% halafu na ushahidi mwingine wa ziada wa kutosha na usio shaka yoyote (BEYOND REASONABLE DOUBT) ukapatikana

Taarifa zaidi za namna FME alivyopaniki na hivyo kupelekea mhusika apate ushahidi mwingine mkubwa wa ziada kuhusiana na engine hiyo, zitafuata baadaye

…………….inaendelea
 
UPDATE: SATURDAY 16TH APRIL 2022

KUHUSIANA NA FUNDI MEKANIKA (FME) WA GARI LA MHUSIKA

……………….inaendelea


MHUSIKA ARUDI TENA GARAGE KWA MARA YA PILI NDANI YA WIKI MOJA KWA AJILI YA KUBADILISHA COOLANT YA GARI

Ikumbukwe kuwa, baada ya kuwa engine meshabadilishwa, ndani ya kipindi ambacho siyo kirefu sana, mhusika alikuwa tayari amesharipoti garage mara mbili; na safari hii nyingine ya kwenda kubadilisha coolant ilikuwa ni ya tatu; na ya pili ndani ya kipindi cha mfululizo wa wiki moja

Baada ya engine kuwa imeshabadilishwa:

  • Safari ya kwanza ni le ambayo mhusika alifika kwa ajili ya kubadilisha “steering wheel belt roller”
  • Kifaa hicho FME alishauri wakakinunue kwenye kwenye duka moja la “used spare parts” maeneno ya Mwenge kwenye duka moja lililo karibu na Nakiete Pharmacy
  • Mhusika na FME walienda wote pamoja wakakinunua kifaa hicho, na hatimaye walirudi garage na kuja kukifunga
Baada ya muda kupita; ndiyo tena rectifier iliharibika na betri ikagoma kupiga

  • Mhusika alirudi tena garage J3 moja asubuhi kwa mara ya pili kwa ajili kurekebisha tatizo hilo.
  • Baada ya kufika garage, mafundi husika walienda wenyewe kununua kifaa kingine kizima “used” wakaja wakakifunga kwenye gari
  • Siku kifaa hiki kinafungwa, ndiyo siku ambayo mhusika alikubaliana na ushauri wa kufunga pia COMPRESSOR nyingine ya AC kwenye gari
Kwa hiyo, baada ya kifaa hicho kuwa kimefungwa kwenye gari, COMPRESSOR nyingine ya AC ilifungwa pia siku hiyo

  • Awali, FME alidai kuwa COMPRESSOR hiyo iliagizwa kutoka kwa watu anaofahamiana nao fundi wa umeme, ambaye ndiye alihusika na kufunga kifaa hiki cha umeme, yaani rectifier
  • Hata hivyo; kwenye siku za hivi karibuni imekuja kuthibitika kuwa COMPRESSOR hiyo haikuagizwa kutoka na fundi wa umeme bali FME ndiyo aliagiza COMPRESSOR hiyo kutoka kwa watu anaofahamiana nao yeye mwenyewe.
  • Kwa hiyo fundi wa umeme hakuhusika na uagizaji wa COMPRESSOR hiyo isispokuwa hapo awali FME alimdangaya mhusika kuwa ni fundi wa umeme aliyeagiza COMPRESSOR hiyo
Issue ya nani aliagiza COMPRESSOR hiyo ilikuja kubaninika hivi karibuni tu baada ya jioni moja Ijumaa, mhusika akiwa anatokea ofisini; alifika tena maeneo ya garage kwa swala jingine ambalo halikuwa linahitaji matengenezo ya gari

  • Mafundi karibia waote walikuwepo jioni hiyo na wengi waliikagua gari kutaka kuona iko na hali gani kwa sasa
  • FME na fundi wa umeme nao walikuwepo pia siku hiyo
  • Mhusika alimuuliza fundi wa umeme kama ndiyo yeye hasa aliagiza COMPRESSOR hiyo siku alipokuwa nafunga kifaa cha umeme; mbele ya umati wa mafundi wote waliokuwepo karibu siku hiyo
  • Mbele ya umati wa mafundi wote, fundi huyu wa umeme naye alijibu kwa kusema kuwa siyo yeye aliyeagiza COMPRESSOR hiyo bali ni FME
  • Na katika hali ya kuonyesha uaminifu; FME mwenyewe naye alidakia pia akisema kuwa “aliyeagiza COMPRESSOR ni mimi (yaani FME) na siyo fulani (fundi wa umeme); mafundi wengine wote waliokuwepo wakiwa wanasikia
Kwa hiyo wakati wawili hawa wanatoa maelezo hay mafundi karibia wote walikuwepo.

Ikumbukwe kuwa COMPRESSOR hiyo ilifungwa siku kifaa cha umeme kilipokuwa kinakuwa replaced

………………..inaendelea
 
……………….inaendelea

MHUSIKA ARUDI TENA GARAGE KWA MARA YA PILI NDANI YA WIKI MOJA KWA AJILI YA KUBADILISHA COOLANT YA GARI


Ikumbukwe kuwa kifaa cha uneme kilifungwa J3 asubuhi na mhusika alirudi tena Alhamis asubuhi ndani ya wiki hiyo kwa ajili ya kubadilisha COOLANT

Kwa hiyo J3 hiyo wakati kifaa cha umeme kinafungwa, COMPRESSOR nao pia iliagizwa na kuja kufungwa

BAADHI TU YA YALIYOJIRI SIKU YA KUFUNGA RECTIFIER YA UMEME: FUNDI WA AC ANAYEISHI MAENEO YA JIRANI NA GARAGE AITWA KWA AJILI YA KUJA KUFUNGA COMPRESSOR NA KUJAZA GAS PIA

Ikumbukwe kuwa siku hii ndiyo ile ambayo kwa mara ya kwanza mhusika alibaini kuwa ENGINE tayari ilishabadilishwa. Kwa hiyo wakati anakubali ushauri wa kuagiza na kufunga COMPRESSOR nyingine; tayari alikuwa ameshajua kuwa engine iliyokuwepo kwenye gari haikuwa ile ya kwake

Baada ya mafundi husika kumaliza kufunga kifaa cha umeme siku hiyo; FME alimleta sasa fundi wa AC ambaye hakai mbali sana na maeneo yale. Hata hivyo, hapo kabla, FME mwenyewe alikuwa amemtaarifu mhusika kuwa fundi huyo wa AC alikuwa ameletwa pale na fundi yule wa umeme; kitu ambacho kwa sasa mhusika hana uhakika nacho sana



FUNDI WA AC ATOA USHAURI NA BAADAYE KUTOWEKA GHAFLA BILA KUAGA: FUNDI HUYU ALIMSHAURI MHUSIKA KUBADILISHA KWANZA FENI LA KUPOZA RADIATOR HALAFU NDIYO AC ITAWEZA KUFANYA KAZI

Fundi huyu wa AC hakutumia muda mrefu sana pale garage na baada ya kumaliza kujaza gas, huku injini ya gari ikiwa inaunguruma; alisema kuwa AC haiwezi tena kufanya kazi kwa sababu lile panga (feni) ambalo huwa linazunguka ili kupoza radiator, lilikuwa ni bovu, halizunguki kwa kasi ya kutosha kuweza kupoza vyote radiator na condenser

  • Kwa hiyo fundi huyu wa AC alidai kuwa AC hiyo itafanya kazi iwapo tu panga hilo litabadilishwa
  • Zaidi ni kuwa fundi huyu alidai kuwa kwa mizunguko ya hapa mjini tu mhusika anaweza kutumia AC ila kwa safari za mbali; GARI LAZIMA ITACHEMSHA
  • Muda huo huo baada ya fundi huyu kumaliza kuongea maneno hayo, huku mhusika akiwa bado anafikiria nini cha kufanya, ghafla fundi huyu akawa tayari ameshaondoka; alitoweka ghafla; hakuaga
Mpaka hapa, lengo la mhusika kuhangaika na AC hiyo lilikuwa ni kwamba pamoja na kwamba engine siyo ile ya kwake, lakini bado alihitaji muno kutumia AC

BAADA YA FUNDI WA AC KUWA AMETOWEKA GHAFLA MAENEO YA GARAGE SIKU HIYO

Mhusika alimuomba FME wamfuate ofisini kwake ambayo haiko umbali mrefu kutoka pale walipokuwapo. Fundi huyu walimkuta ofisini na mhusika alipotaka kumdadisi ili ajue ni nini hasa kilichokuwa na shida kwenye panga hilo kwa sababu yeye (mhusika) alikuwa analiona linazunguka kwa speed inayotakiwa

Fundi AC huyu aliamua kulikagua tena panga hilo na baada ya kulikagua alibadilisha maneno na kusema kuwa mwanzoni panga hilo aliliangalia vibaya

  • Kuanzia hapo fundi huyo akadai tena kuwa panga hilo halina shida yoyote na hivyo halihitaji kubadilishwa
  • Zaidi akasema hakuna shida yoyote inayoweza kusababishwa na panga hilo hata kama mhusika ataamua kusafiri safari ya mbali kama vile Mwanza
Baada ya hapo mhusika na FME waliondoka ofisini kwa fundi wakiwa sasa njia moja kurudi barabarani kwa ajili ya ku-test compressor ya AC iliyokuwa imefungwa kwenye gari

  • Walikimbia mwend mrefu hadi Tegeta na AC ilikuwa haiwezi kupoza isipokuwa kula mafuta kwa kiasi kikubwa sana
  • FME akazidi kumshauri mhusika kuwa inabidi abadilishe lile panga, anuunue jingine yapo mjini yanauzwa “used”
Mhusika alimkubalia FME, wakaachna siku hiyo hadi aliporudi tena siku nyingie Alhmasi asubuhi kwa ajili ya kubadilisha COOLANT

Siku mbili baadaye mbele, ndani ya wiki hiyo yaani Alhamis asubuhi ya wiki hiyo hiyo; ndiyo sasa mhusika akampigia FME akiwa anamjulisha kuwa angependa kuleta gari gereji kwa ajili ya kubadilisha COOLANT na FME hakuwa na pinganizi juu ya hilo; na hapo ndiyo BREAKTHROUGH ya kila kitu kilichokuwa kimefanyika ilipokuja kujidhihirisha

……………………inaendelea
 
……………….inaendelea

MHUSIKA ARUDI TENA GARAGE KWA MARA YA PILI NDANI YA WIKI MOJA KWA AJILI YA KUBADILISHA COOLANT YA GARI

KABLA HAJAENDA GARAGE, ALIENDA KUNUNA COOLANT MPYA


Coolant iliyokuwemo kwenye injini ya awali ilikuwa Castro Radiocool nyekundu; aliinunua pale Victoria Service Station Kijitonyama. Safari hii aliamua kurudi tena pale pale na kununua Lita 10; ila barnd nyingine na ambayo ni ya kijani. Kawaida injini ile ya awali ilikuwa inachukua ujazo lita zisizozidi 8; ilikuwa inachuka kama lita 7 na nusu hivi

BAADA YA KURUDI NYUMBANI AKITOKEA KWENYE MAUNUNUZI YA COOLANT

  • Aliamua kumpigia FME kumjulisha kuwa anatamani kuleta gari kwa ajili ya kubadilisha COOLANT; kitu ambacho FME hakutoa objection yoyote
  • Baada ya hapo mhusika aliwasha gari kuelekea ofisini kwanza na baada ya muda si mrefu alielekea garage moja kwa moja
BAADA YA KUFIKISHA GARI GARAGE

Pale garage; kuna sehemu ya mwanzoni kabisa ambapo karibia mara zote anapokuwa ameipeleka gari huwa anaiweka pale halafu mafundi ndiyo huanza kuifanyia kazi ikiwa pale. Mara nyingi sehemu hiyo huwa iko wazi muda wa asubuhi, isipokuwa baadaye mchana huwa inakuwa occupied na magari mengine.

Ni sehemu ambayo mtu akiiweka gari yake pale, mafundi karibia wote pale garage huwa wanaweza kuona ni nini kinafanyika kwenye gari husika, ikiwa ni pamoja na hata wale ambao siyo mafundi pia kama vile wateja wanaoffika pale garage kwa ajili ya kurekebishiwa magari yao

  • Kwenye Alhamis hiyo, mhusika alifanikiwa kuiwahi tena nafasi hiyo lakini tofauti na ilivyo siku zote, alikuta pale chini pamemwagwa maji na kulikuwa na tope jingi
  • Hata hivyo bado hiyo haikumkatisha tamaa mhusika kuweka gari pale kwa sababu kazi iliyokuwa inahitajika kufanyika ilikuwa haimlazimu FME kuchungulia uvunguni mwa gari; ilikuwa ni kubadilisha COOLANT tu, kazi ambayo huwa anaifanya akiwa amesimama
Tofauti na ilivyokuwa hapo kabla siku hiyo FME alimshauri mhusika asiiweke gari kwenye nafasi hiyo bali aiweke mbele kabisa karibu na shimo la gereji. Hii ni sehemu ambayo watu walio wengi huwa hawafiki huko, na hata mafundi pia nao huwa si rahisi sana kusogea huko unless fundi husika ana shida maalumu

Mhusika aliitii maelekezo ya FME na kuiweka gari mahali kama FME mwenyewe alivyokuwa ameelekeza na hatimaye kazi ya kubadilisha COOLANT ilianza

  • COOLANT iliyokuwemo mwanzo ilibidi imwagwe yote, ilikuwa nyekundu na sasa alikuwa anataka kuweka ya kijani
  • Baada ya kumwaga COOLANT ya zamani, kazi ya kuweka COOLANT mpya ikaanza
Kazi hii ilivyoanza ndiyo nayo ikaweza kuibua tena mambo kadhaa ya msingi yaliyoweza kumthibitisha mhusika kuwa injini na radiator vilivyokuwa vinakunywa COOLANT hiyo havikuwa vile ilivyokuwepo kwenye gari siku zote kabla

  • Mfereji wa radiator wa kupitisha COOLANT ulionekana kuwa ulikuwa mwembamba kiasi cha kushindwa kpitisha COOLANT hiyo kwa kasi sawa na ile ya radiator iliyokuwepo awali kwenye gari
  • Kwa hiyo; COOLANT hiyo ilikuwa inapita kwa shida sana na ilichukua muda mrefu sana kujaa
  • Vile vile LITA 9 na ushee za COOLANT ziliingia kwa mpigo mmoja; wakati hapo awali COOLANT ilikuwa haizidi LITA 8
Baada ya kujaza COOLANT lita 9, FME aliamua kumpeleka mhusika maeneo ya Mwenge ili akaichomelee RADIATOR. Huu ni ushauri mwingine tena ambao FME alikuwa ameutoa tangu kipindi cha mwanzo kwenye siku ile ambayo mhusika alifika garage kwa ajili ya kurekebisha kile kifaa kinachoitwa “steering wheel belt roller”

Waivyofika Mwenge; ile wanafungua tu boneti ili Radiator iweze kuchomelewa, COOLANT ikawa inatokota kama maji ya yaliyoinjikwa kwenye jiko tayari kwa kupika ugali. Injini ilikuwa inataka kuchemsha kutokana na kutokuwemo COOLANT ya kutosha kwenye injini.

Baada ya muda mfupi kupita; ikathibitika kuwa kutokota huko ni kweli kulisababishwa na COOLANT kutokuwemo ya kutosha kwenye COOLING SYSTEM YA engine

Hapo hapo wakalazimika kununua COOLANT nyingine ya ziada LITA MBILI zaidi

Bada ya hapo; wakaongeza kwenye injini kiasi cha COOLANT ile iliyokuwa imebakia kwenye zile LITA 10 za awali; halafu wakaongeza tena nyingine kutoka kwenye mojawapo ya zile chupa mbili walizonunua siku hiyo hapo Mwenge

Baada ya kuongeza COOLANT nyingine; gari ndiyo ikatengemaa na kuwa shwari hadi leo haina tatizo lolote linalohusiana na COOLANT

Kwa hiyo mpaka hapo, COOLANT nayo pia ikawa imemsaidia mhusika ku-confirm theory yake kuwa engine ilikuwa tayari imeshabadilishwa

Baada ya kuachana na FME siku hiyo, mhusika akakumbuka tena kitu kingine muhimu. Kilichowahi kutokea J3 ya wiki hiyo wakati wanafanya test ya kutaka kujua kama AC aliyofuniwa siku hiyo ilikuwa inafanya kazi vizuri ama la; walifanya test hiyo kwa kuendesha gari kuelekea maeneo ya Tegeta wakati wa mchana

Wakiwa bado hawafika Tegeta siku hiyo, pale katikati kama unataka kupandisha kuelekea maeneo ya Kunduchi mtongani; FME alim-restrict speed mhusika kwa kudai kuwa huwa kuna Askari wa Usalama Barabarani; japo ule mwendo aliokuwa anaendesha haukuwa umevuka kasi inayoweza kupelekea mtu kukamatwa na Askari; FME alikuwa anamtahadharisha tu dereva

  • kwa kutii tahadhari hiyo, mhusika aliamua kutembea kwa mwendo mdogo zaidi sehemu hiyo
  • Ilipofika Alhamis ya wiki hiyo, mhusika alikuwa tayari ameshapata mawazo kuwa pengine J3 hiyo FME alihofia kuwa mhusika angeweza kukimbia na kufikia speed ya 80 au zaidi kwenye sehemu hiyo kwa sababu haikuwa na magari mengi bararbarani
Kwa hiyo, baada ya mhusika na FME kuwa wameachana siku hiyo ya ubadilishaji wa COOLANT, mhusika aliamua kwenda pale kwenye interchange ya Ubungo, akashuka akiwa anaendesha kuelekea Mwenge huku akikimbia speed ya 80; magari yalikuwa machache. Na hapo ndipo BREAKTHROUGH nyingine ilipojidhirisha

Kawaida, mara zote mhusika huwa anakimbia speed kati ya 40 na 60 tu kwa sababu muda wote huwa anazunguka hapa mjini tu

…………………itaendelea siku nyingine
 
UPDATE: SUNDAY 17TH APRIL 2022
KUHUSIANA NA MAIGIZO YALIYOWAHI KUFANYIKA KWENYE GARI LA MHUSIKA OFISINI WIKI JANA: MAIGIZO HAYO YAMEFANYIKA PIA KANISANI LEO


ILI MAIGIZO HAYO YAWEZE KUFANYIKA, LAZIMA KUWE KUNA GARI NYINGINE INAYOKUWA IMEPAKI KARIBU KABISA NA GARI LA MHUSIKA.

INAONYESHA KAMA GARI HIYO INAKUWA IMEBEBA KIFAA NDANI CHA KITAALAMU AMBACHO KINA UWEZO WA KU-AFFECT UMEME UNAOHITAJIKA KWA AJILI YA STARTUP CYCLE YA ENGINE ( LAYMAN'S ASSUMPTION)

GARI INAPOKUWA IMEPAKI NYUMBANI AMBAPO HUWA INAKUWA PEKE YAKE MUDA WOTE, TATIZO HILO LINAKUWA HALIPO.

TATIZO LINGEKUWA LA KIROHO, LINGEWEZA KUJITOKEZA MUDA WOWOTE BILA KUJALI GARI IMEPAKI PEKE YAKE AU IMEZUNGUKWA NA. GARI ZINGINE. LINGEWEZA KUJITOKEZA HATA PALE GARI INAPOKUWA IMEPAKI PEKE YAKE

PALE NYUMBANI ANAPOISHI, JANA USIKU ALISTUKIA KUNA GARI NGENI IMELETWA NA KUJA KUPAKI UBAVUNI KABISA MWA GARI LAKE, WAKATI PARKING IPO YA KUBWA MUNO NA YA KUTOSHA KIASI KABISA KWAMBA HAKUNA ULAZIMA WA GARI NGENI KUJA IPAKI UBAVUNI KABISA MWA LILE LA MHUSIKA.
GARI HIYO NI T.758 DPB SALOON. ANAITAJA GARI HII KWA SABABU NDANI YA MIAKA KADHAA ILIYOPITA, HAPAJAWAHI KUTOKEA GARI NGENI AMBAYO IMESHAWAHI KUPAKI UBAVU UBAVU KWA NAMNA HIYO KWA SABABU PARKING IPO KUBWA MNO NA YA KUTOSHA KIASI KWAMBA PALE AMBAPO HUWA INATOKEA GARI NGENI ZIMEKUJA KUPAKI MAHALI ANAPOISHI, HUWA ZINAPAKI SEHEMU NYINGINE TOFAUTI NA SI UBAVUNI MWA LILE LA MHUSIKA. HII ILIYOLETWA JANA USIKU YENYEWE IMEKUJA KUPAKI UBAVUNI KABISA MWA LILE LA MHUSIKA WAKATI PARKING IPO KUBWA TU NA YA KUTOSHA
 
UPDATE: MONDAY 18TH APRIL 2022

Baada ya mhusika kuvuka interchange ya Ubungo na kukimbia kwa kasi ya km 80 kwa saa huku akiwa ameweka gia namba 5, gari ilitikisika mbele ya Boneti, mtikisiko ambao haukuwa wa kawaida

  • Mhusika aliirudisha tena gari gereji kwa mara ya pili siku hiyo
  • Alipofika gereji, FME akashauri warudi tena barabani ili na yeye akauone mtikisiko huo
  • Mhusika na FME walirudi barabarani na GARI ILITIKISIKA TENA
Baada ya FME kuuona mtikisiko huo, pale pale alifanya ruling na kudai kuwa tatizo lilikuwa ni BUSH, zilikuwa zimeisha. Mhusika na FME walirudi tena garage, wakaagiza BUSH MPYA zikaja na hatimaye kufungwa kwenye gari

  • FME na mhusika wakarudi tena barabani kwa ajli ya kufanya test nyingine kwa mara ya pili (ya tatu sasa ukiunganisha na ile ya ambayo mhusika aligundua tatizo)
  • Safari hii FME alimchukua pia kijana mwingine msaidizi wake kutoka pale gereji wakaenda naye kwenye test
  • Kijana huyu ALIKAA KWENYE SITI ZA KATIKATI, NA KWENYE KITI KILE CHA KATIKATI KABISA KWENYE GARI AMBAYO NI “SUV 8 SEATER”
Walipofika barabarani na kuanza kufanya test kuona kama mtikisiko huo utatokea tena; huku kijana fundi msaidizi akiwa amekaa katikati ya mojawapo ya siti za katikati

  • Mhusika alifanikiwa tena kupata “window” ambayo haikuwa na foleni kubwa barabarani na hivyo kuendesha gari na kufikisha tena speed ya km 80 kwa saa; SAFARI HII GARI HAIKUTIKISIKA
  • Baada ya hapo, mhusika alimshauri FME walirudie tena zoezi hilo huku kijana aliyekuwa amekaa siti za katikati, akiwa hayupo kwenye gari
  • Kijana fundi msaidizi alishuka kwenye gari halafu FME na mhusika walirudi tena barabarani kwa ajili ya test nyingine
  • Mhusika alifanikiwa kupata tena “window” ambayo haikuwa na foleni, akaendesha gari na kufikisha tena speed ya 80km kwa saa, NA SAFARI GARI ILITKISIKA TENA
Baada ya hapo FME na mhusika, walimpandisha tena kijana kwenye gari na kuanza kurudi gereji

Walipofika gereji, FME alimuomba mhusika aipandishe gari juu kwenye shimo la gereji

  • Mhusika aliipandisha gari juu ya shimo
  • Baada ya hapo FME alishuka chini ya shimo na kuanza kufunga baadhi ya sehemu zilizokuwa zimelegea, akiwa chini ya shimo
Baada ya kutoka kwenye shimo, FME alimshauri mhusika waende sehemu anayoijua ili wakafanye wheel balance. Wakati huo giza lilikuwa limeshaanza kuingia na wakati FME anakaza baadhi ya sehemu akiwa chini kwenye shimo, alikuwa anafanya hivyo kwa kutumia tochi; giza tayari lilikuwa limeshaingia

Mhusika alistuka baada ya kuwa amenusa harufu ya kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kwenye ushauri huo; bearing in mind mood aliyokuwa nyo FME wakati huo. Ilikuwa ni mood ya panic ya hali ya juu na ambayo alikuwa ameamua kuificha ili isionekana na watu wengine nje, huku bila yeye mwenyewe kujua kuwa kwa kufanya hivyo; mood hiyo ndiyo alikuwa anai-expose zaidi

Mengine yaliyojiri siku hiyo mhusika aliwahi kuyapost jioni hiyo hiyo KUANZIA kwenye post hii hapa #729 NA KUENDELEA

Na kwa masahihsho zaidi ni kwamba siku hiyo ilikuwa Ijumaa ya tarehe 30 Julai 2021 na si Alhamis kama mhusika alivyosema hapo awali

……………….itaendelea
 
TAARIFA MUHIMU YA NYONGEZA

KUHUSIANA NA NYUMBA ILIYOPO KWENYE GHOROFA ANALOISHI MHUSIKA, AMBAYO HAINA WAKAZI KWA MUDA WA MIAKA MITATU SASA


Hii nyumba pengine inaweza kuwa na sababu za msingi sana kuendelea kukaa wazi; hilo mhusika halikatai. Still, anachokiona yeye ni kuwa pamoja na nyumba hiyo kuwa na sababu za msingi za kuendelea kuwa wazi; bado anaamini kuwa kuna uwezeakono mkubwa kwamba nyumba hiyo ndiyo inayohusika na baadhi ya matukio kadhaa ambayo huwa yanaendelea mahali pale wakati wa usiku

Mbali na hayo, mhusika mpaka muda huu bado anaamini kabisa kuwa nyumba hiyo ndiyo ilitumika hata wakati ile wa ku-swap engine ya gari la mhusika

Zaidi, mhusika anaamini pia kuwa gari ngeni ambazo huwa zinazofika mahali anapoishi na kulala pale, baadhi ya wamiliki wake wanaweza kuwa huwa wanakuwa hosted kwenye nyumba hiyo

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA SIKU AMBAYO MHUSIKA NA FME WALIENDA KUCHOMELEA RADIATOR YA GARI MWENGE

WALIPOFIKA KWENYE KARAKANA YA MAFUNDI WA KUCHOMELEA, FME ALMWELEKEZA MHUSIKA KUPAKI GARI PEMBENI MBALI KABISA NA SEHEMU WALIYOKUWEPO MAFUNDI WA WELDING

BAADAYE FME ALIENDA PALE WALIPOKUWEPO MAFUNDI NA ALIPORUDI ALIKUWA AMEAMBATANA NA FUNDI MMOJA ALIYEKUWA AMEBEBA KIBATARI CHA MOTO WA KUTUMIA GAS. FUNDI HUYU MWENYE KIBATARI NDIYO ALIKUJA AKAICHOMELEA RADIATOR KWA KUTUMIA MOTO WA KIBATARI CHA GAS. WALE MAFUNDI WENGINE WALIOKUWEPO PALE WALA HAWAKUWEZA KUJUA NI NINI KILICHOKUWA KINACHOMELEWA KWENYE GARI.

KWA UJUMLA TU NII KWAMBA KULIKUWA PIA NA MAZINGIRA YA USIRI FULANI ULIOTENGENEZWA NA FME KWENYE UCHOMELEAJI WA RADIATOR HIYO SIKU HIYO
 
UPDATE: 20TH APRIL 2022

SABABU MBILI KUBWA
ZIKIWA NI BAADHI TU YA SABABU KADHAA ZOLIZOSABABISHA MHUSIKA ASHINDWE KUUPOKEA USHAURI WA FME KWENDA KUPIMA WHEEL BALANCE USIKU HUO


Baada ya mhusika akiwa na mafundi wawili kuwa wametoka kwenye test ya pili iliyohusiana na mtikisiko uliokuwa unatokea kwenye boneti la gari; FME alimshauri mhusika waende wakapime wheel balance. Mhusika hakuweza kuuafiki ushauri kutokana na sababu kubwa mbili ambazo ni

Kwanza usiku ulikuwa tayari umeshaingia Ikumbukwe kuwa kabla ya siku hiyo, tayari kulikuwa kuna hujuma kadhaa zilikuwa tayari zimefanyika kwenye gari hilo na ambazo zilikuwa zimelenga mhusika kuipeleka gari hiyo gereji usiku; kitu ambacho alikuwa anasita kukifanya na badala yake alikuwa anasubiria muda wa asubuhi wa siku zilizofuata na hivyo kuipeleka gari gereji kwenye muda huo

Pili: Test ya barabarani ilikuwa imeshadhihirisha kuwa tatizo la mtikisiko wa injini lilitokana na injini kutokuwa imefungwa vizuri na siyo wheel balance, kwa sababu wheel balance huwa haisababishi gari kutikisika mbele ya bonet

Still, pasingekuwa na tatizo lolote kupima pia wheel balance iwapo tu FME angeshauri lifanyike kama zoezi jingine tu linalojitegemea na si kama test kwa ajili ya ku-ascertain kile kilichokuwa kinasababisha mtikisiko kwenye boneti.

Sababu hizi mbili zilimfanya mhusika ahitimishe siku hiyo kwa kuwasha gari lake na kurudi nyumbani. TUKIO LA SIKU HIYO LIKAWA LIMEPITA
 
TUKIO JINGINE LA HIVI KARIBUNI: MHUSIKA ALIFIKA TENA GEREJI ILI KUWAONYESHA MAFUNDI WENGINE BAADHI YA VIFAA AMBAVYO VIMESHAANZA KUBADILISHWA REJA REJA BAADA YA INJINI KUBADILISHWA

Mhusika aliwahi kufika tena gereji takribani mwezi mmoja ulipita

  • Safari hii hakuwa ameipeleka gari kwa ajili ya matengenezo bali kwa ajili ya ukaguzi (physical inspection) ili waone baadhi ya vifaa vya ndani ambavyo navyo vimeshabadilishwa pia
  • Vifaa hivi vimebadilishwa baada ya injini kuwa imebadilishwa, na zoezi hilo limekuwa likifanyikia nyumbani usiku mahali ambapo gari huwa inapaki
  • Baadhi tu ya vifaa hivyo ni kama DRIVING MIRROR, POWER WINDOW, SUNROOF SHIELD, DOOR HANDLES, na STEERING WHEEL
  • Ukiondoa STEERING WHEEL ambayo yenyewe ilibadilishwa na FME huku mhusika akiwepo gereji, vingine vyote vimebadilishwa usiku gari ikiwa kwenye parking nyumbani
  • Siku FME anabadilisha usukani, alikuwa akifanya kazi pamoja na yule kijana ambaye aliwahi kumkalisha kwenye siti za katikati ya gari siku ya test ya mtikisiko uliokuwa unatokea kwenye bonnet
Kwa hiyo siku hiyo mhusika alifika tena gereji ili mafundi wengine nao washuhudie baadhi ya vifaa vilivyokuwepo kwenye gari hiyo na ambavyo vilikuwa vinaonyesha dhahiri kabisa kuwa havikuwa vya gari hilo

Mhusika alifanikiwa kuwakuta mafundi wengi wakiwa wapo gereji siku hiyo na FME naye pia alikuwepo. Hii ndiyo siku ambayo mhusika alifanikiwa pia kujua kuwa aliyeagiza COMPRESSOR ya AC hakuwa fundi wa umeme bali FME. Hapo kabla, FME alikuwa anadai kuwa COMPRESSOR ya AC iliagizwa na fundi wa umeme

  • Mhusika aliwaonyesha vifaa hivyo na mafundi kadhaa walivikagua
  • Wakati mafundi wanafanya ukaguzi huo, gari ilikuwa imepaki mahali ambapo mara nyingi (kama siyo mara zote) huwa inapaki
  • Sehemu ilipokuwa imepaki siku hiyo ni ile ambayo siku ile ambayo mhusika alienda kubadilisha COOLANT, alimkuta FME amemwaga maji pale na hivyo kumshauri mhusika asipaki gari hapo siku hiyo
Kwa hiyo; gari ilipaki hapo siku hiyo wakati mafundi wanaikagua

Baada ya ukaguzi huo, mhusika alikumbuka tatizo dogo kwenye SUNROOF, akamuomba FME ampe mmojawapo wa mafundi Bodi pale ili alishughulikie kwa dakika kadhaa

Tatizo hilo huwa ni dogo sana na huwa halihitaji muda kulishughulikia

  • Huwa linatatuliwa kwa kuchokonoa tu na kijiti sehemu ya mferejii ule wa kupitisha maji ya mvua kutoka juu kwenye SUNROOF kwenda chini ardhini, wakati mvua ikiwa inanyesha
  • Ni tatizo ambalo hata MR X analijua na possibly ukimpa hata yeye pamoja na kwamba siyo fundi, anaweza akalitatua ndani ya muda wa dakika kadhaa tu (ukitaka kuyasema yote ya MR X, huwezi ukapata muda wa kufanya kazi zingine; MR X huwa yupo kila mahali utafikiri ni hewa; asomaye na afahamu)
  • Actually, tatizo hilo ni hujuma ambazo zimekuwa zikifanyika tangu gari iwasili kutoka Japan mwaka 2013
  • Kila msimu wa mvua unapoanza, kwa kila mwaka; mhusika lazima huwa analazimika kwenda kuzibua mfereji wa kupitishia maji hayo yanayotoka kwenye SUNROOF, mara moja au mara mbili (kwa kila msimu wa mvua)
Mfereji huu una unene wa kiasi cha kidole cha mtu mzima, lakini eti huwa unaziba kutokana na tope linalotengenezwa linalotokana na vumbi ambalo huwa linachanganyikana na maji ya mvua wakati mvua inanyesha

Baada ya mhusika kumweleza FME tatizo hilo, gari ikiwa imepaki pale pale ilipokuwa, FME alimshauri mhusika aisogeze mbele kabisa kwenye sehemu karibu na pale alipopaki siku walipokuwa wanabadilisha COOLANT

Wakati mhusika anaambiwa hivyo, hakujua sababu ni nini; yeye alidhani labda pengine kuna gari nyingine ilikuwa inaingia alitakiwa aipishe kidogo kumbe hapana
  • Hapakuwa na gari nyingine iliyokuwa inaingia gereji muda huo, na ilikuwa Ijumaa jioni kwenye mida ya saa 12 jioni
  • Baada ya dakika kadhaa kupita pasipo mhusika kuona kitu chochote kinaendelea, alijaribu kumhoji FME nini kilikuwa kinaendelea
FME alijibu kwa kusema kuwa kazi hiyo ilihitaji bisibisi na hivyo kulikuwa na mtu aliyekuwa yuko busy kutafuta bisi bisi kwanza ili aje afungue sehemu kuona tatizo ni nini

Baada ya mhusika kuona FME anaanza tena kufanya ubabaishaji na ambao ungepelekea gari kukaa pale hadi giza linaingia, wakati kazi hiyo huwa inafanyika ndani ya muda wa dakika 5 tu miaka yote tangu mwaka 2013, mhusika aliamua kuwasha gari na kuondoka gereji.

Wakati anaondoka ndiyo akakumbuka pia kumuuliza fundi umeme kama ni yeye aliyewahi kuagiza COMPRESSOR YA AC, na fundi umeme alijibu kuwa hakuwa yeye bali aliyeagiza alikuwa ni FME. FME mwenyewe naye pia alikiri hivyo mbele ya kundi la mafundi kadhaa waliokuwepo mahali pale siku hiyo
HAYA NDIYO BAADHI TU YA YALE YALIYOJIRI BAADA YA INJINI YA GARI KUWA IMEBADILISHWA

MUBARIKIWE TENA NA BWANA

UP NEXT: YALIYOWAHI KUJIRI HUKO NYUMA YANAYOHUSIANA NA FME, KABLA INJINI YA GARI LA MHUSIKA HAIJABADILISHWA
 
TAARIFA MUHIMU KWA WAUMINI WA KANISA: KUNA UTOTO MWINGINE TENA ULIKUWA UNAENDELEA KWA MHUSIKA SIKU YA J2 YA PASAKA

Kuna utoto mwingine ulikuwa umepangwa kufanywa kwa mhusika siku ya J2 ya Pasaka ila haukufanikiwa

Anavyoona yeye, utoto huo ungefanikiwa tu kuchota fikra za baadhi ya observers waliokuwepo kanisani hapo J2 hiyo, kama mhusika angepita njia ile nyingine ambayo mara zote huwa hapiti, au possibly kama angeenda akapitia sehemu mtaani jirani na maeneo ya kanisani au hata mbali

Itafikia wakati atakuwa anatoka Kanisani halafu ananyoosha moja kwa moja nyumbani bila kupita sehemu nyingine

Kwa sasa inabidi akae kimya kuhusiana na utoto huo; ila siku akija kubahatika kupata concrerete evidence zinazo-pin vizuri na mhusika wa utoto huo, atakuja na makala ndefu nzito, tena possibly ya kuanzia nyuma kabisa kwenye miaka ya 2018 au 2019 hadi leo

Kwa ushauri tu ni kwamba kama KM-A madhabahu hiyo imemshinda, awapishe wengine. Kanisa lina maelfu ya watumishi wanaoweza kufanya kazi ya Mungu. Awaachie wengine halafu yeye akatumike kule ambako analazimisha kutumika kwa kutumia sehemu ambayo siyo sahihi

Kuna utoto mwingine ulikuwa unaendelea siku hiyo unaoelekea kufanana na ule aliuopigia kelele kwenye J2 moja iliyopita hivi karibuni

Mbinu za utoto huo hakuzigundua J2 hiyo alipokuwa yupo Kanisani; ila amekuja kuzibaini baadaye baada ya kuwa ame-connect dots za matukio.

Halafu hizi hela zake anazodai kazini kwake; nadhani inabidi sasa wafikie mahali wamlipe, short of which mwishowe zitamsababisha aonekane kama kuna aina ya kundi la watu anaowachukia kumbe siyo. Hana kundi la watu analolichukia, ukiachilia mbali mtu binafsi anayemchukia

TATIZO KUBWA LA KM-A YEYE PRIORITY YAKE NI MASLAHI YAKE BINAFSI TU NA SI MADHABAHU YA BWANA. KWA HIYO MHUSIKA ANAOMBA SANA KM-A AACHE KUENDELEA KUKAA ANATENGENEZA MBINU ZA KUMCHONGANISHA NA AINA FULANI YA KUNDI LA WATU

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
NYONGEZA MUHIMU KUHUSIANA NA PANGA LILILOSEMEKANA KUWA INABIDI LIBADILISHWE HALAPU BAADA YA HAPO NDIYO AC YA GARI IWEZE KUFANYA KAZI

IWAPO KAMA MHUSIKA ANG.EKUBALIANA NA USHAURI HUO, CHANCES NI KWAMBA HATA HII INJINI MBOVU ALIYOWEKEWA KWENYE GARI LAKE; NAYO PIA ASINGEKUWA NAYO MUDA HUU, ISINGEKUWEPO INGEKUWA IMESHAHARIBIKA.

ACTUALLY KILICHOFANYIKA NI KWAMBA COMPRESSOR ALIYOUZIWA NDIYO MBOVU, INAKATA MOTO KABLA YA KUPOZA HEWA. AIDHA KAMA NI NZIMA BASI KUNA UWEZEKANO KUWA INAWEZA KUWA KWA NAMNA FULANI IMECHEZEWA KWENYE THERMOSTAT KIASI CHA KUPELEKEA KUWA INAKATA MOTO KABLA HEWA HAIJAFIKIA KWENYE JOTO LA UBARIDI UNAOTAKIWA.

KWA HIYO, HIYO NDIYO COMPRESSOR ALIYOAGIZIWA MHUSIKA NA FME NA HATIMAYE COMPRESSOR HIYO KUPELEKEA KITU KINGINE TENA KUONEKANA KUWA NI KIBOVU KWENYE GARI

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
 
UPDATE: THURSDAY 21ST APRIL 2020

HUJUMA KWENYE GARI LA MHUSIKA ILIYOWAHI KUFANYIKA MWISHONI MWA MWEZI NOVEMBA AU MWANZONI MWA DESEMBA 2019: ZAIDI YA LITA MOJA YA INJINI OIL ILITOLEWA KWENYE INIJI YA GARI LA MHUSIKA


J3 moja mhusika akiwa anaelekea ofisini alibaini taa ya injini oil kuwaka

  • Jana yake J2 alikuwa Kanisani na hakuwa amelibaini tatizo hilo
  • Hata hivyo ruling yake kwa sasa inaonyesha kuwa hujuma zote ambazo zimekuwa zikibainika J3 asubuhi kufuatia jana yake J2 ambayo mhusika alikuwa Kanisani; hujuma hizo zimekuwa zikifanywa kijanja kanisani kwa mlengo kuwa zitakapoainika, zitajulikana kuwa zilifanyikia nyumbani usiku wa J2 kuamkia J3
Kwa hiyo tukio hili la kumwagwa injini oil litakuwa lilifanyikia Kanisani, na taa haikuweza kuwaka papo kwa papo; on the spot, kwa sababu ya umbali mfupi mno uliopo kati ya kanisa lilipo na mahali pale mhusika anapoishi

Baada ya kugundua tatizo hilo, mhusika alichukua oil ya akiba na kuipeleka gari gereji ili ikaongezwe

Kawaida service ya gari alikuwa anafanya kila baada ya km 10,000 na wakati huo zilikuwa zimebaki takribani km 400 kufikia service nyingine

  • Baada ya kufika gereji, FME aliongeza oil na kumshauri mhusika abadilishe baadhi ya vitu kadhaa kwenye injini ikiwa ni pamoja na gaskets
  • Huu ushauri wa gaskets FME alianza kuusisitiza siku nyingi kabla; muda mfupi tu baada ya gari kuwa imewasili kutoka Japan
  • Madai yake yalikuwa ni kwamba kuna sehemu oil huwa inavuja; wakati ukweli ni kuwa zilikuwa ni hujuma nyingine tu zilizokuwa zinafanywa kijanja kijanja
  • Hakuna injini oil iliyokuwa inavuja; mhusika alikuwa tayari ameshajiridhisha kwa uhakika kabisa kuhusu hilo; na kilichokuwa kimebaki alikuwa ansubiria tu nini kitatokea huko mbele ya safari kwa yeye kuttekeleza ushauri huo
  • Ujanja huo ulikuwa unafanyika kwa kumwaga/ kunyunyiza oil pembezoni mwa cover la engine ili ionekane kama inijini oil huwa inavuja kidogodogo
Baada ya FME kuongeza oil, alimshauri mhusika amalizie pia km kadhaa zilizokuwa zimebakia halafu ndiyo akafanye service ambayo ilikuwa imekaribia. Sehemu aliyokuwa anafanyia service ya engine ni nyingine tofauti na kwenye gereji anapofanyia FME

Mhusika alizingatia maelekezo hayo ya FME, na muda ulipofika, tarehe 01 march 2020 majira ya asubuhi akiwa anatokea Kanisani, aliripoti tena mahali hapo ambapo huwa anafanyia service ya gari kwa ajili ya zoezi hilo

Baada ya kufika kumaliza service ya gari; hatimaye matukio kadhaa yalijitokeza siku hiyo, ikiwa ni pamoja tukio la betri ya gari kugoma kupiga; kitendo ambacho kilipelekea hatimaye mhusika kubaini mambo kadhaa yafuatayo

  • Injini oili iliyomwagwa mwishoni mwa mwaka 2019; ilimwagwa makusudi ili kum-prompt mhusika akafanye service ukizingatia kuwa ni km chache sana zilizokuwa zimebakia kufikia service nyingine
  • Wakati oil hiyo inamwagwa, kulikuwa na mtu mwingine tena aliyekuwa ameandaliwa huko ambako huwa anafanyia service ya gari
  • Mtu huyo aliyekuwa ameandaliwa, naye pia mara zote alikuwa anamsisitiza mhusika abadilishe vitu kadhaa kwenye injini sawia kabisa na vile ambavyo FME alikuwa anashauri vibadilishwe; kila mhusika alipokuwa anapeleka gari kwa ajili ya service
  • Baada ya service ya gari kumalizika, wakati gari ikiwa bado inaoshwa injini; alichokuja kukibaini mhusika baadaye ni kwamba mtu huyu alizunguka kijanja kinja na kwenda kufanya kitu cha ktaalamu kati ya terminal za battery na waya ambazo huwa zinashika kwenye terminal za betri
  • Mtu huyu hakulegeza nyaya hizo isipokuwa alifanya kitu ambacho hata ukizikaza nyaya pamoja na terminal za betri, bado betri ilikuwa haiwezi kupiga wakati ni nzima
Kwa hiyo baada ya service kuisha, na injini kuwa imeoshwa, mhusika aliwasha gari ikawaka vizuri tu na akasogea kwenye pump ya mafuta ili ajaze mafuta. Baada ya hapo gari haikuwaka tena, betri ilikuwa haiwezi tena kupiga kuanzia pale

Baadaye mtu mhusika wa tukio hilo la betri kutokupiga, alisema kwamba tatizo litakuwa ni umeme wa gari na wakati huo akawa tayari ameleta fundi wake wa umeme ili amsaidie mhusika, na baada ya hapo yeye akaamewa toweka kabisa eneo la tukio

Baada ya kuona mtu huyo amepotea kwenye eneo la pale gari ilipokuwepo, mhusika alimfuata mtu huyo na kumjulisha kuwa yeye ndiye aliyemleta fundi wa umeme na ndiye anayetakiwa kumsimamia. Hata hivyo mtu huyo “alichomoa” (vijana wa mjini huwa wanasema) kumsimamia fundi umeme.

Baadaye mhusika alimpiga FME na baada ya muda wa takribani masaa mawaili hivi walikuja wakiwa wameambatana na fundi umeme
…………………….inaendelea
 
KILICHOTOKEA SIKU HIYO KABLA YA SERVICE YA INJINI KUANZA

Baada ya oil iliyokuwemo kwenye injini kuwa imemwagwa; MTU HUYO alishauri kwamba kabla ya kufanyiwa service ya injini; mhusika inabidi airudishe gari kwa fundi mekanika kwanza, kwa sababu ilikuwa inaonyesha kuna leakage ya oil inatokea kwenye injini. Kwa maana hiyo MTU HUYO alikuwa anai-refer gari irudi kwa FME kwanza kabla ya kufanyiwa service ya injini siku hiyo

  • Mhusika alimjibu MTU HUYO kwamba hayo mambo mengine ayaache; amwachie mhusika. Yeye alichotakiwa siku hiyo ni kufanya kazi aliyokuwa anatakiwa kufanya
  • Mbali na hivyo, MTU HUYO hakuwa hasa aliyekuwa anahusika na service ya gari la mhusika, isipokuwa alikuwa amejipachika tu mamlaka hayo siku hiyo, akiwa kama mojawapo wa staff wa office hiyo tu
  • Mara zote gari la mhusika limekuwa likifanyiwa service na mtu mwingine ambaye ndiye aliyekuwa anaonekana kusaidiwa tu na MTU HUYO siku hiyo
Kwa kifupi tu ni kwamba alichokuja kukibaini baadaye kwa uhakika kabisa ni kwamba MTU HUYO na FME walikuwa wameshakuwa coordinated miezi kadhaa nyuma kabla ya service ya gari hiyo kuwadia.

Fundi umeme mgeni aliyekuwa ameletwa na MTU HUYO siku hiyo alikuwa ameshaandaliwa kabla, maalum kabisa kwa ajili ya kuja kuharibu kabisa mfumo wa umeme wa gari; na fundi mwenyeji wa siku zote wa gari angeweza kuja kuthibitisha hilo pasipo shaka yoyote

Yaliyotokea siku hiyo ni mengi ila kwa kifupi tu mwandishi wenu anaomba aishie hapa kwa tukio hili

MUBARIKIWE TENA NA BWANA
Mkuu hii ni dairy ya gari yako au??
 
Back
Top Bottom