Mkasa wa Dr. Ulimboka: Inawezekana Kabisa Sio 'Inside Job'!, bali ni 'Smear Campaign'?!

Dr Ulimboka ni raia kama raia mwingine na watu wengi washakumbwa na makubwa zaidi yake. Tanzania ina watu milioni 45 sasa itawezekana vipi mtu mmoja awashughulishe watu wa JAMII FORUMS namna hii? Kuna watu wamekufa na wameteseka zaidi ya huyu mtu mmoja, sasa sielewi kwa nini baadhi ya watu wanataka kuilaumu serikali kwa yaliyotokeaSerikali iko bize kushughulikia hii migomo na jeshi la polisi haliwezi kupeleka resources zake zote kushughulia kesi ya mtu mmoja wakati wengine wanapata taabu zaidi yake.Hoja za msingi hapa ni 2.1. Serikali haiwezi kulaumiwa kuwa ilimteka na kumpiga. Tanzania sio banana republic na ni nchi inayoendeshwa na sheria na kama hakuna mwenye ushahidi wa kutosha kuwa serikali ilimteka ulimboka then fikirieni conspiracy theories zingine lakini sio kumteka na kumpiga huyu jamaa. Kuna watu ambao wanaiendesha mbio serikali kama akina Issa Ponda wapo na hakuna aliyewateka wala nini.2. Jeshi la Polisi hawawezi kulaumiwa kwa lolote. Na sikuona sababu ya mkuu wa polisi kuitisha press conference juu ya Dr Ulimboka. wao wangesema kuwa jalada limefunguliwa na wataishughulikia kesi yake kama mtu mwingine.Just thinking outside the box

1. Kama Tanzania ina watu milioni 45 ina maana kwanza umetambua umuhimu wa mtu mmoja na ukimwondoa hutasema tena watu milioni 45.

2. Ili ionekane ni tukio muhimu, wewe ungetaka wapigwe watu wangapi kaa Dr Ulimboka? Kwa maneno mengine, inatakiwa ifike idadi gani ya watu ili tukio liwe muhimu?

3. Huwezi katika hatua hii useme: "serikali haihusiki na jeshi la polisi halihusiki". Nani anayehusika? Ili ionekane serikali haihusiki na jeshi la polisi halihusiki ndio maana wapenda haki wanashauri iundwe tume huru ili kufanya uchunguzi usio wa upendeleo.

4. Tukio la Dr Ulimboka ni muhimu kwa sababu kama halitafutiwi ufumbuzi basi hata hao Watanzania milioni 45 unaodai huenda nao wakawa wanatendewa kama Dr Ulimboka na hata wengine wakawa wanapotea au uliwa katika mazingira kama hayo na kwa kutumia 'reasoning' yako, kama atakuwa anauliwa mtu mmoja mmoja tu kwako haitakuwa issue hadi watu milioni 45 watakapotoweka maana hiyo ndiyo namba kubwa zaidi kwa hapa Tanzania.
 
Hans maneno haya hujafikiria umeyakariri kutoka kauli za Pinda na Bosi wake.Kisichoeleweka ni udhaifu wa wahusika na watuhumiwa kujieleza hadi wakutumie wewe!
 
Yaani hata mseme nini au mfanye chochote kile ukweli utabaki kwamba serikali imehusika moja kwa moja, siyo rahisi serikali ikakwepa lawama ya unyama huu uliokithiri, na kwa vile polisi wamekuwa wakiua na hawaadabishwi, moja kwa moja tunaamini ni serikali imehusika kwa kutumia polisi na mlijua mmemuua Dr. Ulimboka lakini amefufuka na sasa mnahaha hamkuwa na plan B na ndo kinachowasumbua, na wala msihangaike sana kutushawishi na maneno kama haya kwani ukweli uko wazi sana, kwani serikali ndo wahusika
 
Dr Ulimboka ni raia kama raia mwingine na watu wengi washakumbwa na makubwa zaidi yake. Tanzania ina watu milioni 45 sasa itawezekana vipi mtu mmoja awashughulishe watu wa JAMII FORUMS namna hii? Kuna watu wamekufa na wameteseka zaidi ya huyu mtu mmoja, sasa sielewi kwa nini baadhi ya watu wanataka kuilaumu serikali kwa yaliyotokea

Serikali iko bize kushughulikia hii migomo na jeshi la polisi haliwezi kupeleka resources zake zote kushughulia kesi ya mtu mmoja wakati wengine wanapata taabu zaidi yake.

Hoja za msingi hapa ni 2.

1. Serikali haiwezi kulaumiwa kuwa ilimteka na kumpiga. Tanzania sio banana republic na ni nchi inayoendeshwa na sheria na kama hakuna mwenye ushahidi wa kutosha kuwa serikali ilimteka ulimboka then fikirieni conspiracy theories zingine lakini sio kumteka na kumpiga huyu jamaa. Kuna watu ambao wanaiendesha mbio serikali kama akina Issa Ponda wapo na hakuna aliyewateka wala nini.

2. Jeshi la Polisi hawawezi kulaumiwa kwa lolote. Na sikuona sababu ya mkuu wa polisi kuitisha press conference juu ya Dr Ulimboka. wao wangesema kuwa jalada limefunguliwa na wataishughulikia kesi yake kama mtu mwingine.


Just thinking outside the box


One man can lead to the FUTURE we need, huu ni ukombozi zaidi ya ule wa SOWETO makaburu dhidi ya Africans. Hii ni Afri-Tourist dhidi ya Tanzanian , In Dr. Ulimboka lies the truth you and the CCM doesnt want to hear.......
Woke up!
 
Wakati tukiendelea kugumia kilichomkuta Dr. Ulimboka, kama kawaida lazima "conspiracy theories' ziwepo ili kujifariji kuwa kuwa aliyefanya hivyo ni nani na kwa malengo gani?. 'Conspiracy theory' Number 1: " It is "inside job"!. theory hii ambayo ndiyo ya walio wanaamini kabisa ile ni kazi ya serikali, kwa msingi kuwa yeye ndio chanzo cha mgomo toka mwanzo, kwa hiyo, akishughulikiwa, mgomo ndio utamalizika rasmi, hivyo serikali ikawatumia vijana wake waitwao "the oparatives" wamshughulikie vile wataona inafaa, na kweli vijana wakaingia kazini na kilichotokea ni motokeo ya kazi "nzuri" ya vijana wale ambao wameitekeleza vibaya (incomplete), hivyo sasa kui embarass serikali!. Wanabodi, hakuna ubishi, "the oparatives wapo", na hizo ndizo kazi zao, lakini naomba kutofautiana na simple thinkers wanaoamini its an 'inside job', kwa sababu ili "oparatives" waingie kwenye any 'covert' oparation, lazima kwanza waweke malengo, "what do they want to achieve", ili kujaustify "the motive behind", na kabla ya utekelezaji, lazima wapime, "impact" na "consequences" ndipo huamua "the best way" ya utekelezaji, na kwa vile "they are proffessionals", siku zote hutekeleza with very high degree za 'precise' na leaving no trace behind!. Kilichomtokea Dr. Ulimboka ni kazi ya "amateures" kwa kuacha loop holes kibao ambapo ukiwa "deep thinker", uta doubt kama ile ni kazi ya "professionals", hivyo inawezekana kabisa sio "inside job", unless kilichofanyika kiwe ni tactics za vijana wa "inside job" to carry out kihovyo hovyo ili ionekana ni amateures na huko kumuacha aishi pia ndio lengo na sio aliachwa kuishi kwa bahati mbaya!. Normal comon sense inanishawishi nijiulize, kama Dr. Ulimboka ndie adui wa serikali, kama serikali hiyo hiyo imeamua kumshughulikia kwa njia hiyo ili iachieve nini?. Ule msemo wa mchawi, mpe mwanao akulelee kwa imani kuwa hawezi kumdhuru!, hivi inawezekana kweli serikali yetu ndio iliyomshughulikia Dr. Ulimboka na kwa nanma ile?!. Kama ni kweli, hii ni kazi ya "inside job", then for sure, "hii itakuwa ni serikali ya vichaa!". Conspiracy Theory No. 2. Could it be just a "Smear Caipaign"?!. Adui wa adui yako ni rafiki yako, kwa vile Dr. Ulimboka ndiye kiongozi wa hii migomo, na hii migomo imeishaipasua sana kichwa serikali, hadi rais Jakaya Kikwete, akautangazia umma kuwa mgomo ule ni wa mwisho, na kwa vile sasa mgomo umeibuka tena na kuwafanya wote waliojifanya kuuepusha tangu mwanzo kuonekana wajinga, akiwemo rais JK, its obvious Dr. Ulimboka ndie alishaonekana ni adui wa serikali na kila mtu anajua, hivyo jambo lolote litakalomtokea Dr. Ulimboka, automatically, fingers zitakuwa pointed kwa serikali kuwa sio mshukiwa bali ni mhusika mkuu!. Kwa msingi kuwa, Dr. Ulimboka ni adui wa serikali, automatically atakuwa ni rafiki wa maadui wa serikali, hivyo sasa amegeuka target nzuri kwa maadui wa serikali waliomo within, ambao hawaitakii mema serikali yao, wakaamua kumshughulikia Dr. Ulimboka ili kuiembarass serikali kunyooshewa vidole vya lawama kwa utaratibu unaojulikana kama "smear Campagn"!. Could it be?. Pole Dr. Ulimboka. Get well soon!. Pasco.

Conspiracy theories zimekuwepo for years.Ila hapa ulipofananisha na amateur artwork hujakosea.Kwani siku hizi intelligence yetu ipo chini sana kwa sababu ya undugunizations na kuzeeka kwa taasisi na fikra za akina mtoto wa mkulima.wao kuprove kama wapo ni kwa raia ila zaidi ya hapo ni vilaza tuu.

Haata kama ni maadui wa utawala uliopo ,bado watakuwa ni watu katika system na wametumia vifaa vya system.ambavyo navyo kuweza risk kwa kiasi hicho na kupatiwa ulinzi watakuwa wame involve powerful entities.So its means resources na nia waliyokuwa nayo vilitosha fanya yote hayo in an efficient way. Its more plausible kuwa conspiracy theories zingebase katika survicability ya huyu jamaa na si who was the mastermind.

Inawezekana haya:
1. Mungu tuu lisaidia.
2. Ulimboka aliwatrick kuwa amekufa au anaelekea kufa.Na hawa jamaa hawakuwa Wakristu wzuri au si wakristu kabisa ndio maana hawakukumbuka kuwa skari wa Kirumi walipokuwa akimuua Yesu alimalizia kwa mkuki ili kuondoa chance ya kusurvive.

3.Inaelekea kati ya hawa jamaa kuna waliokuwa na mashaka na kusitasita katika roho yake na hivyo kuamua wapa moyo wenzie kuwa jamaa hatopona,ili jamaa ajitete baadaye,huku akiamini kuwa jamaa hata akipona ni ngumu kuwatambua watu.Inawezekana pia kuna watu hawakuridhia haya mamabo ila iliwapasa kufanya.

4.Hawa jaa inawezekana hawakuwa professionala kabisa,ingawa wapo katika vikosi maalumu kwa kazi hiyo,pengine waliwekwa kwa minajili ya dini, ukanda, kabila etc ili wawe loyal kwa mabosi wao.na hiyo wakawa si watu wenye kuweza determine kiwango cha kusababisha kifo straight away.

5. inwezekana walipewa multiple confusing commands kiasi cha wao kuamua ishia hapo.

6. Inawezekana walikutana na watu wengine katika pilikapilika na hivyo kuondoka ktk eneo la tukio ili kujinusu au hata kuepeusha kuwa marked.Na pengine walihitaji hata kuwaua hao watu wengine waliona kisha wakaondoka haraka, huku wakiwa wamepoteza attention kwa huyu jamaa.

7.Inawezekana pia hilo kundi pinzani ulilojaribu lielezea lilituma kikosi kingine kwenda tibua na hilo ndilo pengine linasaidia anika mambo hadharani. Yapo mengi ya kuhisi, ila lillilo wazi ni kuwa serikali haiwezi jitoa, kwani kama tendo halikuwa professional ,serikali legelege hii kila mahala hawajawa professional.

Hapa theories zingekuwa nyingi ni vipi kasurvive?
 
kiukweli tanzania kuna watu wanajua kupiga na ukapigika kweli kweli....hali yake inaendelea kuwa mbaya japo kwa msaada wa madaktari na mashine ya kupumulia...
 
dr ulimboka anawakilisha kikundi cha watu wenye maoni ya pamoja ,wasomi ,kikundi chenye umuhimu kwa maisha ya kila siku ya mwanadamu hastahili kupuuzwa hata kidogo .asikilizwe na hoja zao zijibiwe kwa hoja.
 
Hans nafikiri huelewi kwanini Dr Uli ni muhimu 1 huyu alikuwa kiunganishi kati ya madaktari na meza ya mazungumzo iliyosemekana ipo 2. Kiongozi wa jumuia ya madaktari 3. Daktari
Anatofauti na hao unaosema watu, pia umejisajili kwa jina lingine unaficha nn?
 
Na si haki pia kuilaumu serikali bila ya kuwa na ushahidi kuwa serikali ndio imefanya hivyo

si haki hata kidogo
Ohoo,we sasa unataka kuleta masikhara kwenye utani na maudhi kwenye kero! Dr Uli katamka wazi wazi kuwa watu wa serikali ndio waliokuwa katika zoezi zito la kumpunguza uzito kwa njia ya kumpunguza viungo na kujaribu kumbadilisha sura kwa kipigo!leo hii unataka kutuambia kuwa Dr Uli kauli yake ya kigonjwa na kwamba hajui asemalo? Ndugu usitutanie tafadhali!
 
wimbi la mbele pole sana mkuu naona umeparamiwa kweli kweli. Nakubaliana na wewe kwa upande mwengine na mwengine hapana.

Thinking out of the box kwa upande wangu umelenga more in the sub-groups za groups ambazo zipo ndani ya CCM. Na as much as kimsingi serkali na Chama ni tofauti, kiuhalisia katika taifa letu CCM ndio serkali yenyewe. Kwa mtazamo wangu ni kuwa wale ambao ni wabaya wa wa JK katika serkali hiyo hiyo ndio hasa walohusika na hilo tukio.


  1. I refuse to think nor believe kuwa JK na watu wake wangekuwa wajinga kiasi hicho. Kumtafuta Ulimboka within days hadi pale ambapo angekuja in his own convienience.
  2. I refuse to think nor believe eti yule mtu alikuwa ni wa usalama kweli, ana niya ya kumuua na anajuwa kabisa; ajitambulishe hivo tena three days before tukio kwa kuacha mwanya wa Ulimboka tutaarifu wa karibu wake kuna wa usalama wanamtafuta.
  3. I refuse to think nor believe kuwa katika watu watatu wote ambao walikumshughulikia mboka wote wawe ni amatures wakiondoke wakidhani kuwa ameua. Na hilo ndio kubwa kuliko. Wakamuacha makusudi hadi alipopoteza fahamu kwa malengo kuwa;
-Alikuwa intended kwa kuuwawa hivo ni bahati tu.
-Kuwe na maelezo dhahiri toka kwake of what happened ili kusiwe na assumptions zozote. Iwe clear kuwa alipaniwa kuteswa na kuuwawa thus creating fuse ambayo ni nzito.
 
Ni vile tu nimeambiwa ule mtambo wa Mtoto wa mwenzetu unaweza kutrace hata unapochapisha ningekutukana walah tena
 
Na si haki pia kuilaumu serikali bila ya kuwa na ushahidi kuwa serikali ndio imefanya hivyosi haki hata kidogo
kwa kuwa sisi wananchi tumeidhamini serikali itumie rasilimali, ikusanye kodi na pia itumie majeshi na TISS ili itupe huduma na kutulinda basi ina kazi ya kutimiza hayo. lakini cha ajabu huduma mbovu zaidi watu wanaumizwa na inaleta maelezo yenye utata unategemea nini? kama haijahusika basi imlete mhusika halisi au ikubali iunndwe tume huru.bulshit.... napoteza muda wangu kukueleza wewe wakati najua una low I.Q....THREAD YAKO inaonesha hivyo...sorry!
 
Ili kuweza kukandamiza watu, lazima Polisi, mahakama, majasusi na usalama wa taifa watumike ili kufanikisha ukandamizaji... HII ni kama mafia system...

Kwanza wanajeruhi watu, kisha kesi yapelekwa mahakamani ambapo kila hakimu pale katulizwa chini. Kesi ya nyani huwezi kumpelekea tumbili, ni wale wale. Hata ukiwa na evidence kubwa aina gani??? kesi yawezwa kufanywa behind closed doors....

Tumefikia total mafia controll of the governmental operations. Mafisadi wanaogopa, mambo yanafichuliwa, watu wanaelewa, na watu wamechoka na mizaha. Wakati huo huo mafisadi yanajikinga...
Miaka mi3 hii ijayo itakuwa ya balaa, watu watakufa, watu wataiba, na watu wataumia...
Lakini kumbuka wahenga walisemaje...

Asiyefunzwa na mamaye ( wahenga) atafunzwa na dunia ( majambazi makoloni mambo leo).
 
endela kufikiria hivyohivyo nje ya box na usirudi ndani ya box ..chowderhead
 
Back
Top Bottom