''Mkasa'': Niliiba mtoto kwenye wodi ya wazazi ili nitunze ndoa yangu

ndusyepo

Senior Member
Jul 2, 2013
165
41
"MKASA"
NILIIBA MTOTO KWENYE WODI YA WAZAZI ILI NITUNZE NDOA YANGU


Nilikua nafanya biashara ya kuuza mwili wangu, kila aliyetaka kunitumia alipanda dau awezavyo! Kwa siku ilikua radhi nilale na wanaume zaidi ya watatu ilimradi nipate hela itakayonikimu, lakini sikuwahi ata siku moja kufikiria kwamba nitaolewa
Lakini siku moja alitokeza mwanaume mmoja na kuninunua nilipompa mapenzi ya maana mwishoni alitamka maneno ya kunioa. Haikuwa kawaida kwangu kwani tangu nianze biashara ya kujiuza sikuwahi kutamkiwa na mwanaume yeyote kutaka kunioa.
Sikutafuta ushauri wala sikutaka kusubiri, suala lile nililifikisha kwetu ambapo walikua wanajua nafanya kazi kiwanda kikubwa pale mbeya mjini.

Baada ya kuwaeleza kuhusu kuolewa kwangu hawakukataa na harusi yetu mimi pamoja na David ilifanikiwa bila kipingamzmizi nikawa mwanamke kweli niliwekwa ndani ya jumba ya kifahari nikasahau uchangudoa wa miaka ya nyuma.
Nikiwa katika ndoa na David tulianza jitihada za kutafuta mtoto lakini ziligonga mwamba kila alipojaribu sikubahatika kushik mimba. la hasha! nilijua tatizo langu kwani nilipokuwa najiuza kipindi cha nyuma niliwahi kutoa mimba zaidi ya tano huwenda ndio ikawa sababu ya Mimi kutoshika mimba.
Nilimrudia daktari aloyekua ananitoa mimba, nakumuuliza kuhusu swala la kushika mimba lakini majibu niliyopata sikuwa na uwezo wa kubeba mimba wala kuzaa taarifa iliyothibitishwa na vipimo. Kichwa kilipata moto ni mwaka mmoja tu tangu niolewe na kila nilipokumbuka maneno ya David kuhusu mtoto ndio nilichanganyikiwa "Nahitaji mtoto sijakuoa uje kunijazia choo, la sivyo utarudi nilipokuchukua" yalikua ni maneno kila kukicha ata ule upendo ukawa umepungua.
Nilianza kutafta ushauri kwa marafiki na mashoga zangu japo wengine walinicheka na kunikejeli ila siwezi msahau mmoja wa rafiki yangu alipo nishauri
"Shoga yangu acha kuigiza kama umekuja mjini leo, Huyo David amekukuta ushakuwa mjanja ndio maaana kakuoa, Yaaani hujapata utamu wa ndoa unataka kuachika kisa mtoto? " alinivuta sikio kisha akaninong'oneza
"We hujui kwa sasa kuna mimba bandia?" Nilishangaa kidogo kwan ujanja wangu wote sikuwahi sikia mimba bandia. Lakini yule rafiki yangu alinielezea mimba hiyo kwa kununua matumbo ya bandia kila baada ya kipind fulani cha mimba kisha nikikaribia kujifungua naingia leba kama mama mjamzito kisha niibe mtoto katika wodi ya wazazi.
Halikuwa wazo rahisi kuiba mtoto lakini shoga yangu aliniongezea kwa kusema anajua pa kupata hayo matumbo bandia na pia ana manurse katika hosptali kubwa hapa mjini mbeya ambao wanaweza kunisaidia kuiba mtoto

Nilikubali wazo lile na baada ya mwezi mmoja niliweka tumbo la mimba la bandia, Furaha ilirejea ndani ya nyumba kwa mume wangu sio kwake tu bali ata familia yake na yangu ilifurahia swala lile.
Tumbo la bandia likawa linabadilishwa kuendana na miezi huku nikiwa nazuia mume wangu David kushika tumbo kwa visingizio mbali mbali.
Miezi Tisa ilipofika nilienda katika hosptali kubwa hapa mbeya ambapo nilikua nishawalipa manurse watakohusika kuiba mtoto. Nililazwa wodi ya wazazi kama siku mbili na siku ya tatu wale manurse walikamilisha ule mpango wa kuniibia mtoto wa mama mmoja ambaye nilimjua mpaka sura kwani alikua analala kitanda cha pembeni yangh ndani ya wodi.
Kitendo cha kuiba mtoto niliruhusiwa siku hiyo hiyo kwenda nyumbani jambo lilowashangaza weng lakini tulizima midomo yao kwa ujanja ujanja.
Alikua ni mtoto wa kiume tukampa jina la Jackson huku Huduma za nyumbani kwa mama mzazi akinipa yule rafiki yangu ambaye alikua anajua siri hiyo.
Miaka ikasonga jackson akazidi kukua huku akipata matunzo zaidi kwani familia aliyoletwa ilikua ni ya kitajiri.
Lakini siri ni ya MTU mmoja wakizidi wawil basi sio siri tena. Yule rafiki yangu akanigeukia akanifanya Mimi ndio mtaji wake wakupata hela kila anapohitaji kwani alinambia nisipompa hela anaweza akavujisha siri ya kuwa Jackson sio mtoto wangu kwa David ama kwa mama mtoto aliyeibiwa kwan anamjua. Vitisho hivyo nilivichoka nikaona ipo siku nitakosa hela ataniharibia ndoa yangu hivyo nilichofanya nilituma majambazi wamuue na suala lile likafanikiwa sasa nikawa najua hakuna anayejua siri yangu zaidi ya wale manurse na pia hakuwa tena katika ile hosptali.
******
Sasa Jackson wangu yuko darasa la kwanza akiwa amepata malezi bora kutoka kwa baba na mama wa bandia.
Balaa limeanza wiki iliyopita siku moja nikiwa ndani ya nyumba, Mme wangu kazini na Jackson shuleni ndipo niliposikia zogo kwenye geti baina ya mlinzi na sauti ya mwanamke. Nilipotoka nje haraka haraka kwenda kutazama lakini moyo ulishtuka baada ya kukutana na sura ambayo miaka saba iloyopita tulikua tumelazwa wodi ya wazazi pamoja. Mlinzi akiwa anamzuia, yule mama alilalamika
"Nataka mtoto wangu, mlimuiba miaka mingi mkaniharibia maisha yangu, nipeni mtoto wangu" kweli aliyosema hayakuwa uwongo nguvu zilinishia lakini nilifanya kitendo cha haraka kuwaita polisi waje kumtoa kabla mume wangu hajarudi.
Alipotolewa nilimripoti kama chizi kisha niliwasiliana na lile kundi la kijambazi wamtafute na wamuue huku nikiwapa hela nono. lakini baada ya siku tatu kupita yule mwanamke alirudi kama awali kumbe wale majambazi hawakumuua na hela wametokomea nazo, nilipowaita polisi waje wamtoea waliniambia akirudi tena basi watachunguza kama yule mama ni chizi na pia watamsikiliza.

Naombeni ushauri ndugu zangu nifanyaje ili nisijulikane kwani mama halali wa Jackson anamtaka mtoto wake kila nikituma majambazi wamuue wanatokomea bila kumuua. Nifanyaje kwani napenda ndoa yangu sitaki kurudi maisha ya zamani?
 
"MKASA"
NILIIBA MTOTO KWENYE WODI YA WAZAZI ILI NITUNZE NDOA YANGU


Nilikua nafanya biashara ya kuuza mwili wangu, kila aliyetaka kunitumia alipanda dau awezavyo! Kwa siku ilikua radhi nilale na wanaume zaidi ya watatu ilimradi nipate hela itakayonikimu, lakini sikuwahi ata siku moja kufikiria kwamba nitaolewa
Lakini siku moja alitokeza mwanaume mmoja na kuninunua nilipompa mapenzi ya maana mwishoni alitamka maneno ya kunioa. Haikuwa kawaida kwangu kwani tangu nianze biashara ya kujiuza sikuwahi kutamkiwa na mwanaume yeyote kutaka kunioa.
Sikutafuta ushauri wala sikutaka kusubiri, suala lile nililifikisha kwetu ambapo walikua wanajua nafanya kazi kiwanda kikubwa pale mbeya mjini.

Baada ya kuwaeleza kuhusu kuolewa kwangu hawakukataa na harusi yetu mimi pamoja na David ilifanikiwa bila kipingamzmizi nikawa mwanamke kweli niliwekwa ndani ya jumba ya kifahari nikasahau uchangudoa wa miaka ya nyuma.
Nikiwa katika ndoa na David tulianza jitihada za kutafuta mtoto lakini ziligonga mwamba kila alipojaribu sikubahatika kushik mimba. la hasha! nilijua tatizo langu kwani nilipokuwa najiuza kipindi cha nyuma niliwahi kutoa mimba zaidi ya tano huwenda ndio ikawa sababu ya Mimi kutoshika mimba.
Nilimrudia daktari aloyekua ananitoa mimba, nakumuuliza kuhusu swala la kushika mimba lakini majibu niliyopata sikuwa na uwezo wa kubeba mimba wala kuzaa taarifa iliyothibitishwa na vipimo. Kichwa kilipata moto ni mwaka mmoja tu tangu niolewe na kila nilipokumbuka maneno ya David kuhusu mtoto ndio nilichanganyikiwa "Nahitaji mtoto sijakuoa uje kunijazia choo, la sivyo utarudi nilipokuchukua" yalikua ni maneno kila kukicha ata ule upendo ukawa umepungua.
Nilianza kutafta ushauri kwa marafiki na mashoga zangu japo wengine walinicheka na kunikejeli ila siwezi msahau mmoja wa rafiki yangu alipo nishauri
"Shoga yangu acha kuigiza kama umekuja mjini leo, Huyo David amekukuta ushakuwa mjanja ndio maaana kakuoa, Yaaani hujapata utamu wa ndoa unataka kuachika kisa mtoto? " alinivuta sikio kisha akaninong'oneza
"We hujui kwa sasa kuna mimba bandia?" Nilishangaa kidogo kwan ujanja wangu wote sikuwahi sikia mimba bandia. Lakini yule rafiki yangu alinielezea mimba hiyo kwa kununua matumbo ya bandia kila baada ya kipind fulani cha mimba kisha nikikaribia kujifungua naingia leba kama mama mjamzito kisha niibe mtoto katika wodi ya wazazi.
Halikuwa wazo rahisi kuiba mtoto lakini shoga yangu aliniongezea kwa kusema anajua pa kupata hayo matumbo bandia na pia ana manurse katika hosptali kubwa hapa mjini mbeya ambao wanaweza kunisaidia kuiba mtoto

Nilikubali wazo lile na baada ya mwezi mmoja niliweka tumbo la mimba la bandia, Furaha ilirejea ndani ya nyumba kwa mume wangu sio kwake tu bali ata familia yake na yangu ilifurahia swala lile.
Tumbo la bandia likawa linabadilishwa kuendana na miezi huku nikiwa nazuia mume wangu David kushika tumbo kwa visingizio mbali mbali.
Miezi Tisa ilipofika nilienda katika hosptali kubwa hapa mbeya ambapo nilikua nishawalipa manurse watakohusika kuiba mtoto. Nililazwa wodi ya wazazi kama siku mbili na siku ya tatu wale manurse walikamilisha ule mpango wa kuniibia mtoto wa mama mmoja ambaye nilimjua mpaka sura kwani alikua analala kitanda cha pembeni yangh ndani ya wodi.
Kitendo cha kuiba mtoto niliruhusiwa siku hiyo hiyo kwenda nyumbani jambo lilowashangaza weng lakini tulizima midomo yao kwa ujanja ujanja.
Alikua ni mtoto wa kiume tukampa jina la Jackson huku Huduma za nyumbani kwa mama mzazi akinipa yule rafiki yangu ambaye alikua anajua siri hiyo.
Miaka ikasonga jackson akazidi kukua huku akipata matunzo zaidi kwani familia aliyoletwa ilikua ni ya kitajiri.
Lakini siri ni ya MTU mmoja wakizidi wawil basi sio siri tena. Yule rafiki yangu akanigeukia akanifanya Mimi ndio mtaji wake wakupata hela kila anapohitaji kwani alinambia nisipompa hela anaweza akavujisha siri ya kuwa Jackson sio mtoto wangu kwa David ama kwa mama mtoto aliyeibiwa kwan anamjua. Vitisho hivyo nilivichoka nikaona ipo siku nitakosa hela ataniharibia ndoa yangu hivyo nilichofanya nilituma majambazi wamuue na suala lile likafanikiwa sasa nikawa najua hakuna anayejua siri yangu zaidi ya wale manurse na pia hakuwa tena katika ile hosptali.
******
Sasa Jackson wangu yuko darasa la kwanza akiwa amepata malezi bora kutoka kwa baba na mama wa bandia.
Balaa limeanza wiki iliyopita siku moja nikiwa ndani ya nyumba, Mme wangu kazini na Jackson shuleni ndipo niliposikia zogo kwenye geti baina ya mlinzi na sauti ya mwanamke. Nilipotoka nje haraka haraka kwenda kutazama lakini moyo ulishtuka baada ya kukutana na sura ambayo miaka saba iloyopita tulikua tumelazwa wodi ya wazazi pamoja. Mlinzi akiwa anamzuia, yule mama alilalamika
"Nataka mtoto wangu, mlimuiba miaka mingi mkaniharibia maisha yangu, nipeni mtoto wangu" kweli aliyosema hayakuwa uwongo nguvu zilinishia lakini nilifanya kitendo cha haraka kuwaita polisi waje kumtoa kabla mume wangu hajarudi.
Alipotolewa nilimripoti kama chizi kisha niliwasiliana na lile kundi la kijambazi wamtafute na wamuue huku nikiwapa hela nono. lakini baada ya siku tatu kupita yule mwanamke alirudi kama awali kumbe wale majambazi hawakumuua na hela wametokomea nazo, nilipowaita polisi waje wamtoea waliniambia akirudi tena basi watachunguza kama yule mama ni chizi na pia watamsikiliza.

Naombeni ushauri ndugu zangu nifanyaje ili nisijulikane kwani mama halali wa Jackson anamtaka mtoto wake kila nikituma majambazi wamuue wanatokomea bila kumuua. Nifanyaje kwani napenda ndoa yangu sitaki kurudi maisha ya zamani?
Simulizi mzuri mnoo
Nasubiri muendelezo wake....
 
Huwezi kujiExpose kimaeleza kwa staili hiyo alaf et "naombeni msaada"..No! Hiyo bongo muvi lete part 2 yake..
 
Watu wanadhulumu pesa lakin ww mtoto wa mti?na unapanga kumuua mama yake mzazi?
~kwa nn unamoyo wa kikatili namna hiyo??
~DAMU ya mtu haidhuiliwi hata siku moja mama.na hiyo damu ina hiyo damu inalia mbele za MUNGU jumlisha machoz ya mama yake.hakika utakutana na mkono wa MUNGU.
Aiseee usamehewe bure
 
"MKASA"
NILIIBA MTOTO KWENYE WODI YA WAZAZI ILI NITUNZE NDOA YANGU


Nilikua nafanya biashara ya kuuza mwili wangu, kila aliyetaka kunitumia alipanda dau awezavyo! Kwa siku ilikua radhi nilale na wanaume zaidi ya watatu ilimradi nipate hela itakayonikimu, lakini sikuwahi ata siku moja kufikiria kwamba nitaolewa
Lakini siku moja alitokeza mwanaume mmoja na kuninunua nilipompa mapenzi ya maana mwishoni alitamka maneno ya kunioa. Haikuwa kawaida kwangu kwani tangu nianze biashara ya kujiuza sikuwahi kutamkiwa na mwanaume yeyote kutaka kunioa.
Sikutafuta ushauri wala sikutaka kusubiri, suala lile nililifikisha kwetu ambapo walikua wanajua nafanya kazi kiwanda kikubwa pale mbeya mjini.

Baada ya kuwaeleza kuhusu kuolewa kwangu hawakukataa na harusi yetu mimi pamoja na David ilifanikiwa bila kipingamzmizi nikawa mwanamke kweli niliwekwa ndani ya jumba ya kifahari nikasahau uchangudoa wa miaka ya nyuma.
Nikiwa katika ndoa na David tulianza jitihada za kutafuta mtoto lakini ziligonga mwamba kila alipojaribu sikubahatika kushik mimba. la hasha! nilijua tatizo langu kwani nilipokuwa najiuza kipindi cha nyuma niliwahi kutoa mimba zaidi ya tano huwenda ndio ikawa sababu ya Mimi kutoshika mimba.
Nilimrudia daktari aloyekua ananitoa mimba, nakumuuliza kuhusu swala la kushika mimba lakini majibu niliyopata sikuwa na uwezo wa kubeba mimba wala kuzaa taarifa iliyothibitishwa na vipimo. Kichwa kilipata moto ni mwaka mmoja tu tangu niolewe na kila nilipokumbuka maneno ya David kuhusu mtoto ndio nilichanganyikiwa "Nahitaji mtoto sijakuoa uje kunijazia choo, la sivyo utarudi nilipokuchukua" yalikua ni maneno kila kukicha ata ule upendo ukawa umepungua.
Nilianza kutafta ushauri kwa marafiki na mashoga zangu japo wengine walinicheka na kunikejeli ila siwezi msahau mmoja wa rafiki yangu alipo nishauri
"Shoga yangu acha kuigiza kama umekuja mjini leo, Huyo David amekukuta ushakuwa mjanja ndio maaana kakuoa, Yaaani hujapata utamu wa ndoa unataka kuachika kisa mtoto? " alinivuta sikio kisha akaninong'oneza
"We hujui kwa sasa kuna mimba bandia?" Nilishangaa kidogo kwan ujanja wangu wote sikuwahi sikia mimba bandia. Lakini yule rafiki yangu alinielezea mimba hiyo kwa kununua matumbo ya bandia kila baada ya kipind fulani cha mimba kisha nikikaribia kujifungua naingia leba kama mama mjamzito kisha niibe mtoto katika wodi ya wazazi.
Halikuwa wazo rahisi kuiba mtoto lakini shoga yangu aliniongezea kwa kusema anajua pa kupata hayo matumbo bandia na pia ana manurse katika hosptali kubwa hapa mjini mbeya ambao wanaweza kunisaidia kuiba mtoto

Nilikubali wazo lile na baada ya mwezi mmoja niliweka tumbo la mimba la bandia, Furaha ilirejea ndani ya nyumba kwa mume wangu sio kwake tu bali ata familia yake na yangu ilifurahia swala lile.
Tumbo la bandia likawa linabadilishwa kuendana na miezi huku nikiwa nazuia mume wangu David kushika tumbo kwa visingizio mbali mbali.
Miezi Tisa ilipofika nilienda katika hosptali kubwa hapa mbeya ambapo nilikua nishawalipa manurse watakohusika kuiba mtoto. Nililazwa wodi ya wazazi kama siku mbili na siku ya tatu wale manurse walikamilisha ule mpango wa kuniibia mtoto wa mama mmoja ambaye nilimjua mpaka sura kwani alikua analala kitanda cha pembeni yangh ndani ya wodi.
Kitendo cha kuiba mtoto niliruhusiwa siku hiyo hiyo kwenda nyumbani jambo lilowashangaza weng lakini tulizima midomo yao kwa ujanja ujanja.
Alikua ni mtoto wa kiume tukampa jina la Jackson huku Huduma za nyumbani kwa mama mzazi akinipa yule rafiki yangu ambaye alikua anajua siri hiyo.
Miaka ikasonga jackson akazidi kukua huku akipata matunzo zaidi kwani familia aliyoletwa ilikua ni ya kitajiri.
Lakini siri ni ya MTU mmoja wakizidi wawil basi sio siri tena. Yule rafiki yangu akanigeukia akanifanya Mimi ndio mtaji wake wakupata hela kila anapohitaji kwani alinambia nisipompa hela anaweza akavujisha siri ya kuwa Jackson sio mtoto wangu kwa David ama kwa mama mtoto aliyeibiwa kwan anamjua. Vitisho hivyo nilivichoka nikaona ipo siku nitakosa hela ataniharibia ndoa yangu hivyo nilichofanya nilituma majambazi wamuue na suala lile likafanikiwa sasa nikawa najua hakuna anayejua siri yangu zaidi ya wale manurse na pia hakuwa tena katika ile hosptali.
******
Sasa Jackson wangu yuko darasa la kwanza akiwa amepata malezi bora kutoka kwa baba na mama wa bandia.
Balaa limeanza wiki iliyopita siku moja nikiwa ndani ya nyumba, Mme wangu kazini na Jackson shuleni ndipo niliposikia zogo kwenye geti baina ya mlinzi na sauti ya mwanamke. Nilipotoka nje haraka haraka kwenda kutazama lakini moyo ulishtuka baada ya kukutana na sura ambayo miaka saba iloyopita tulikua tumelazwa wodi ya wazazi pamoja. Mlinzi akiwa anamzuia, yule mama alilalamika
"Nataka mtoto wangu, mlimuiba miaka mingi mkaniharibia maisha yangu, nipeni mtoto wangu" kweli aliyosema hayakuwa uwongo nguvu zilinishia lakini nilifanya kitendo cha haraka kuwaita polisi waje kumtoa kabla mume wangu hajarudi.
Alipotolewa nilimripoti kama chizi kisha niliwasiliana na lile kundi la kijambazi wamtafute na wamuue huku nikiwapa hela nono. lakini baada ya siku tatu kupita yule mwanamke alirudi kama awali kumbe wale majambazi hawakumuua na hela wametokomea nazo, nilipowaita polisi waje wamtoea waliniambia akirudi tena basi watachunguza kama yule mama ni chizi na pia watamsikiliza.

Naombeni ushauri ndugu zangu nifanyaje ili nisijulikane kwani mama halali wa Jackson anamtaka mtoto wake kila nikituma majambazi wamuue wanatokomea bila kumuua. Nifanyaje kwani napenda ndoa yangu sitaki kurudi maisha ya zamani?

duh!
 
Duh kwel jf imechoka yaan unatutungia erick shigongo halafu unataka ushauri pumbavu kweli wewe kachukue ushauri fb huku jf tunauza ushauri saizi.
 
Ni kweli au umeitunga ndugu kama ni kweli hapo pa kuiba mtoto si kuhukumu lakini kuua daaaah we mwanamke si mtu mzuri kabisa.
Cooked story..hivi ukae na mimba bandia miezi tisa...wanaishi nchi tofauti??chumba kimoja?dont play wt our mind
 
Kwa nini usingefata mtoto kwenye kituo cha watoto yatima wapo wengi wametekelezwa na wazaz wao huko... Usitende dhambi ya kuua tena utakua mgeni wa nani kesho mbinguni? Utajir,pesa'magari'majumba ni vtu vya kupita,acha kuwa mtumwa wa shetani'.kuna maisha baada ya maisha ya duniani... Mpe mwanamke mwenzako mtoto wake
 
hii chai japo ya leo ina sukari...
tusubiri part 2 ( je mama mtoto atapata mtoto wake)
 
Yani huu uongo!
kwa hiyo ulikaa na mume wako miezi tida hajagusa tumbo lako, unalala naye kitanda kimoja hajashtuka, yale mambo yetu mnafanya na tumbo lako la sponji hagundui....basi naye ni wa bandia kama ilivyokuwa mimba yako
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom