"Wapinzani ni wajinga na hawana Adabu". Hii ni kauli ya Mkapa. Mzee gani huyu? Nitaiga nini kutoka kwake? Mzee mzima ametoka Dar kwenda Arumeru kutoa matusi?
Je, na mimi nikipewa jukwaa pembeni nikaanza kutoa hotuba kuwa Mkapa ni Mjinga na hana adabu, maneno hayo hayo aliyotumia jukwani tutafika? Inaelekea ametoa matusi kibao ila TBC wameona hayo ndo yanafaa kutuletea kwenye Taarifa ya habari ya saa mbili usiku.
Kwa busara hii inayopaswa kutiliwa shaka na kila Mwenye akili, Mkapa ana sifa zote za kuwa "Mzee wa Dar es Salaam".
Je, na mimi nikipewa jukwaa pembeni nikaanza kutoa hotuba kuwa Mkapa ni Mjinga na hana adabu, maneno hayo hayo aliyotumia jukwani tutafika? Inaelekea ametoa matusi kibao ila TBC wameona hayo ndo yanafaa kutuletea kwenye Taarifa ya habari ya saa mbili usiku.
Kwa busara hii inayopaswa kutiliwa shaka na kila Mwenye akili, Mkapa ana sifa zote za kuwa "Mzee wa Dar es Salaam".
Katika namna iliyowashangaza wengi akizindua kampeni za CCM jana huko Arumeru Mashariki, Rais mstaafu Benjamin Mkapa alidai kuwa meneja wa kampeni za CHADEMA, Vincent Nyerere, sio mmoja wa wanafamilia wa Mwalimu Julius Nyerere akidai kipindi chote alichofanya kazi na mwasisi huyo wa Taifa hakuwahi kutambulishwa mtoto yeyote mwenye jina hilo katika familia hiyo.
Mkutano huo wa CCM umeshindwa kuvunja rekodi ya umati wa watu waliofurika juzi wakati CHADEMA ilipozindua kampeni zake, ambapo licha ya kuwa na vikundi vingi vya burudani, idadi ya watu haikulingana na ile ya wapinzani wao.
Source: Tanzania Daima.
Jana nimebahatika kusikiliza sehemu ya Hotuba ya Mheshimiwa Benjamin Mkapa Katika Uzinduzi wa Kampeni za CCM arumeru.
Moja ya mambo aliyofafanua ni habari za yeye kutoa masharti kabla ya kuzindua kampeni hizo na habari za yeye kuhusishwa na ufisadi wa Ardhi Arumeru.
Kwa mujibu wa bwana mkapa hizi habari ziliandikwa na wapinzani kwenye mitandao yao.
Wanajamvi mnaweza kunisaidia link ya huu mtandao wa wapinzani? Mimi ni mpinzani damu damu lakini nasikitika sijawahi kupata bahati ya ku access huo mtandao wa wapinzani.
Natanguliza shukrani.
Vivy.
Last edited by a moderator: