Hizi habari za Mama Anna kumharibia Ben si za kweli hata kidogo.Kati ya watu wenye ma argument bongo, watu wenye ushawishi Ben Mkapa ni mmoja wapo.The man has been an Editor of the Daily News for aeons, hata kabla hajaenda foreign kina Kaduma walivyokuwa wanachemsha kwenye mazungumzo na ma Henry Kissinger huko Mkapa ndiye alikuwa anaenda ku save the day, this is way back in the late sixties and early seventies, baadaye Nyerere akamtupa balozini na halafu Foreign.
Mkapa kaenda kwenye mkutano wa Commonwealth wakati wazungu wamempigia kampeni ya kumsuta Mugabe, akawageuzia kibao wazungu na kuwasema kisawasawa, kwa usomi wa hali ya juu, akamtetea Mugabe, na si hivyo tu, baada ya hapo mpaka Tony Blair akamuomba aje kufanya kazi naye.Huyu si mtu wa kuendeshwa endeshwa na mke wake kirahisi.
Matatizo aliyojikuta nayo Mkapa yote aliyataka mwenyewe.Hizi habari za kumtupia Mama Anna lawama zinaturudisha kule kule kwenye mfumodume unaosema mwanamke ndiye chanzo cha matatizo, na Adam alifanya dhambi ya asili kwa sababu ya Eva.
Hogwash.Mkapa alijua kila kitu alichofanya na alitaka kufanya hivyo.Mama Anna, kwa watu wanaoijua familia ya Mkapa on a personal level kama mimi, wanajua kwamba hakuwa na uwezo wa kumu influence Ben Mkapa hivyo.