Mkuu kama una data, hebu tuambie aliyewapa wahindi Shirika la reli.
Pili aliyebinafsisha ATC na TTCL.
Leo hii tukisema mashirika yarudishwe serikalini tunaweza kuyaendesha!
Ubinafsishaji wa ubia ndiyo solution nzuri, yaani tuwe 51% and above.
Mashirika yaliyoanzishwa au angalau kupewa kauhai baada ya Mkapa mfano ni Kiwira, mgodi ambao unaonyesha utakuja kutusaidia mbele.
Kuimarishwa kwa TPDC hasa kwenye sekta ya mafuta na gesi.
Chuo kikuu kinachomilikiwa na serikali UDOM.
Shirika la nyumba (NHC) ingawa bado halijawanufaisha walalahoi, angalau halijauzwa na linaonyesha kuimarika kimtaji.
Chuo Kikuu cha Dodoma ni Mkapa's brainchild, Kikwete amekuja kuhimiza tu mifuko ya pensheni itumbukize fedha zake pale na kujenga chuo ambacho majengo yake ingawa ni ya gharama kubwa lakini ni ya kiwango cha chini na sidhani yatadumu hata muongo mmoja na nusu!! Tunazalisha wahitimu kila mwaka lakini hakuna ajira wala mitaji ya kuwawezesha kujiajili they end up joining the army of the unemployed!