Sn2139
JF-Expert Member
- Apr 9, 2010
- 834
- 250
...Mkapa ana mapungufu yake, kama walivyo Watanzania wengine wote na Marais wote waliowahi kuitawala nji hii..
...lakini kama tukiwa-rank hawa wanne kwa waliyoyafanya katika nchi hii, hasa kwenye uchumi, Mkapa amewaacha akina Nyerere, Mwinyi na Jakaya kwa mbali mnoo..
...Hivyo mpaka pale atakapopatikana mzuri zaidi ya Mkapa na asiye na madhaifu ya Mkapa, bado ana haki yakutembea kifua mbele...
Una haki ya kumsifia, huenda ni kutimiza ule usemi wetu wa kisuahili ...asifuye mvua....
Mafanikio ya uchumi kwa kuuza bank, madini, mashirika ya umma, nyumba za serikali mbona ni rahisi kama kuteremka mlima? Hata mtoto wa darasa la nne ukimpa nafasi ya raisi wakati huo kisha ukamruhusu kuuza mashirika yaliyoanzishwa na Nyerere ataweza kukusanya pesa ya kutosha na kuonesha mafanikio ya muda. Subiri matokeo ya sera hiyo miaka michache ijayo ndiyo utajuuta kumfaham Mkapa mwenye kipara