Mzee Benjamin Mkapa (Mungu amrehemu) kwenye kitabu chake katika sura za mwisho alitafakari kidogo juu ya mambo kiongozi wa umma anayozushiwa pamoja na utendaji wake mzuri.
Mzee Mkapa alisimulia namna Costa Rica Mahalu Balozi mwema alivyozushiwa zigo la rushwa tena kwa kusingiziwa na likamtesa kisawasawa hadi ikabidi Ben mwenyewe asimame kortini kama shahidi wa utetezi.
Ben alikumbuka pia kwa machungu na hasira tuhuma alizopewa na zikamchafua sana licha ya kwamba sio za kweli na nzito mno. Maswala kama ya kuwa alitumia jina la ikulu kujipatia mkopo binafsi wa Bilioni 1 wakati si kweli na kwamba migodi ya makaa ya mawe aliwapa wakwe zake na sivyo ilivyokuwa yalikuwa tuhuma zilizomsikitisha sana.
Mambo ya namna hiyo yalimfanya akatamka kwamba 'The public service is so thankless' yaani utumishi wa umma humalizika kwa teke la punda, hauna wema.
Binafsi nikitafakari hatima za viongozi waliowahudumia vyema wananchi nyakati fulani namna wanavyoondolewa madarakani kwa fedheha bila kukumbuka chembe ya fadhila zao na utumishi wao mwema nabaini kwamba BEN alikuwa sahihi.
Nawasihi viongozi wa umma wajiandae kisaikolojia kwa habari hii ya teke la punda ili wasipate maumivu makubwa pale wanaporudishiwa mabaya kwa mema.
Mzee Mkapa alisimulia namna Costa Rica Mahalu Balozi mwema alivyozushiwa zigo la rushwa tena kwa kusingiziwa na likamtesa kisawasawa hadi ikabidi Ben mwenyewe asimame kortini kama shahidi wa utetezi.
Ben alikumbuka pia kwa machungu na hasira tuhuma alizopewa na zikamchafua sana licha ya kwamba sio za kweli na nzito mno. Maswala kama ya kuwa alitumia jina la ikulu kujipatia mkopo binafsi wa Bilioni 1 wakati si kweli na kwamba migodi ya makaa ya mawe aliwapa wakwe zake na sivyo ilivyokuwa yalikuwa tuhuma zilizomsikitisha sana.
Mambo ya namna hiyo yalimfanya akatamka kwamba 'The public service is so thankless' yaani utumishi wa umma humalizika kwa teke la punda, hauna wema.
Binafsi nikitafakari hatima za viongozi waliowahudumia vyema wananchi nyakati fulani namna wanavyoondolewa madarakani kwa fedheha bila kukumbuka chembe ya fadhila zao na utumishi wao mwema nabaini kwamba BEN alikuwa sahihi.
Nawasihi viongozi wa umma wajiandae kisaikolojia kwa habari hii ya teke la punda ili wasipate maumivu makubwa pale wanaporudishiwa mabaya kwa mema.