Mkapa Adai heshima kwa Viongozi wastaafu.

Mie nadhani kasema jambo la maana....hebu tumpe heshima mzee wetu......pamoja na mapungufu bado kaijengea misingi nchi hii.......tumuheshimu kwa mazuri aliyotuachia....

Tatizo ni kwamba kuna maovu ukitenda, basi mema yako yanakuwa na maana ndogo sana kama si kupotea kabisa. Ndio maana inakuwa taabu sana kukumbuka mema ya Idd Amin, Hitler, Mobutu, n.k. Maskandali makubwa ya ufisadi, mauaji ya kisiasa, kuzalisha wakimbizi wa kwanza wa Kitanzania, kauli za jeuri na kibri kwa wananchi ndiyo kumbukumbu nzito alizowaachia Watanzania. Labda aanze kwa kuomba radhi, kuacha kauli mbovu na kutojihusisha na siasa za vyama ndipo chati ipande. Hakuna sababu ya kumfanya kuonekana chini ya mzee rukhsa kihadhi zaidi ya kwamba haonyeshi kuheshimu wananchi; bado anafikiri jeuri itamrejeshea heshima aliyokuwa akiipata akiwa magogoni.
 
nilivyomuelewa alimlenga JK laivu

Amavubi: Kwa nini asimweleze JK mwenyewe? kuna msemo unasema " Heshima kitu cha bure kila mtu anakitaka" kwa maana hiyo heshima huja yenyewe hailazimishwi!! Mbona Baba wa Taifa aliheshimika bila kulazimisha au kudai? Kama Mkapa anaona haheshimiki ajiulize aliwaudhi nini watanzania? Kwanza kama nakumbuka vizuri aliwahi kusema eti watanzania ni wavivu wa kufikiri !!! watu wavivu wa kufikiri wanaweza wakawa na uwezo wa kuheshimu???
 
Sio kosa lako,kipindi Mkapa anatawala nchi bado ulikuwa mikononi mwa wazazi wako walisimamia show na ugumu wa maisha umekuja baada ya kuanza kuyajua maisha ya kujitegemea(2006 above) lazima umtukane JK.

Join Date : 6th September 2012
Posts : 60
Rep Power : 314
Likes Received 13
Likes Given 5
KARIBU JF
 
Back
Top Bottom