Mkapa above the law?: Allegations

To me Mkapa was just as good as a 'national traitor". Arogant and corrupt leader to remember. He was just imposed by Nyerere, i wish Nyerere could have seen how the thing ended the last term. We lost all our gold under Mkapa's leadership.
 
Haya ni maoni yangu ambayo ni vigumu kuthibitisha empirically. Hata hivyo, tafuta vigezo vyovyote vya kiongozi bora uwapime hawa ndugu zetu wawili. Tatizo la Mkapa alikuwa hapendi mtu mwingine am-outshine, na nafikiri ni sababu moja ya kutuachia JK maana alijua siku ya siku tutamkumbuka sana. In fact ni aibu kulinganisha hawa viongozi wawili-moja ni monitor wa darasa la I na mwingine ni kiranja mkuu, haiji. Kwa maneno ya Mzee Mwinyi ni makosa kulinganisha mlima na kichuguu!

Labda kukusaidieni wale ambao wanasema matatizo ya leo yaliachwa na Mkapa. Yes, ni kweli kabisa. Sasa cha kujiuliza ni kwa nini tuyaone au tuyabebee bango leo? Kwa nini walimu na kila mtu anagoma leo na sio jana? Moja ya maelezo hapa ni kwamba mosi, Mkapa alikuwa na uwezo wa kushawishi kuhusu mipango na sera zake. Kama ni madai ya walimu yalikuwepo na walimu walielezwa sababu za kuchelewa kulipwa na wakaelewa, wakasubiri na wakalipwa. Kama ni wazee wa EAC walielezwa kwa nini wanalipwa wanavyolipwa na kwa nini wale ambao hawakulipwa hawakulipwa, walielewa, japokuwa waliendelea kunung'unika lakini walikubaliana. Uwezo wa kushawishi ni sifa muhimu ya kiongozi wa kisiasa ambayo hawa ndugu zetu wa leo wanapwaya mno. Wao wanafikiri wanaweza kutawala kwa amri, hawataweza. Bahati mbaya hii tabia chafu ya kutawala kwa amri inaelekea imesambaa kwenye taasisi zote hadi chini, ni hatari na haitawasaidia!

Pili, wakati wa Mkapa kila idara ilikuwa inafanya kazi. Kila waziri aliwajibika ipasavyo. Wanafunzi wa vyuo vikuu walipogoma watu walimnyooshea kidole waziri husika, na wala sio rais. Katika awamu zote tatu zilizopita kulikuwa na mawaziri vinara: Akina Sokoine wakati wa Nyerere, akina Mrema wakati wa Mwinyi na akina Magufuli wakati wa Mkapa. Leo hii mawaziri wote wanaonekana kama vile hawapo, na kila kitu kinamtegemea rais-hiyo ndiyo failure ya uongozi. Kwa nini mawaziri kipindi hiki hawafanyi kazi na kwa nini hakuna mawaziri vinara? Hakuna hatari kwa kiongozi kama kukumbatia majukumu yote na kutokuwaamini wale uliowateua, na hasa pale ambapo uwezo wa kiongozi mwenyewe ni mdogo!

Endeleeni kumshambulia Mkapa, lakini ukweli ni kwamba yeye alishafanya sehemu yake, tunataka hawa waliopo nao wafanye. Sasa kama barabara ya KM 5 ya Sam Nujoma inachukua zaidi ya miaka mitatu kukamilika-bado unatafuta uthibitisho kwamba hawa wenzetu wamekwama na akina Magufuli walikuwa bora mara 600 zaidi ya hawa akina...(hivi by the way waziri wa ujenzi siku hizi ni nani vile? Tazama hata majina ya mawaziri hatuyajui halafu utasema hawa wanafanya kazi?).

Ugomvi hapa ni nini hasa?! Kwamba Mkapa alikuwa bora kuliko hawa jamaa zetu wa sasa hivi nalo ni jambo la kujadili? Of course, hata kwa Africa, kwa aina ya viongozi tulio nao, huwezi kumkwepa Mkapa katika list ya viongozi bora! Inaweza ikauma lakini ndio ukweli huo. Hii inakuonyesha jinsi tulivyo na uhaba wa viongozi bora katika bara letu.

Wanasiasa bana...Miye mshanichosha kabisaa!
Siamini kabisa macho yangu...Lakini kwasababu hivi sasa majukumu nayo ni mengi..Nakuachieni muendelee tu na sifa hizo...Inasikitisha sana kuona kwamba unatumia vigezo ambavyo kabla ya hapo ulisema huwezi kudhibitisha empiricaly na huku ukiwa umeshammwagia kiongozi huyo misifa ya kufa mtu.

Watendaji wake si ndio wametufikisha hapa? Wewe unazungumzia kusikika kwenye magazeti ama utendaji?
Magufuli si alisimamia zoezi zima ambalo lina mgogoro hadi sasa kuhusu uuzwaji wa nyumba na viwanja vya serikali kwa bei chee?

Unaposema Mkapa alikuwa hataki kuwa outshined...Then kwanini kuna baadhi yenu mnakataa hata kumtaja kwenye issue yoyote kwa kuogopa na huku mkijuwa kuwa utendaji wa serikali yake umechangia kutufikisha hapa? RICHMOMD,KAGODA,EPA,DEEP GREEN,KIWIRA NK NI NANI?

Yani uanataka kuniambia mikataba yote mibovu nani responsible?

Nchi yetu historia yake changa..Yeye alisimamia ubinafsishaji..Ndiyo hapa katufikisha...Na wewe unasema ni bora?

Nyie ndugu zangu wa chadema hata kama mnataka wanachama wapya na viongozi wajitowe ccm na kujiunga na nyie hiyo si style.
 
Kitila,
Mkuu usiseme nalaumu tuu bila kupima..
Mimi najua nini Uongozi bora kwa sababu nimeishi ncxhi zenye viongozi bora..na kipimo cha Uongozi bora hakiwezi kupimwa kama nafuu ya mgonjwa aliyekuwa kitandani kwa kutumia kipima joto wakati bado yupo ktk coma.
Kila siku nauliza swali moja tu Ni kipi Mkapa alikifanya ambacho wewe unaweza kusimama hapa na kuwambia kila Mtanzania akakubaliana na wewe.. Nini hiyo intro ya theory ya Macroeconomy! maanake sii kitu cha kwake ila ni policy ambayo ipo kaikuta na kaambiwa aitumie, hakuitumia vizuri...aliboronga!
Kitu alichofanya ni sawa na kutoa choo cha shimo ukaweka cha kuvuta lakini hakuna maji ndani ya nyumba.. Mnachoshangilia ni kuona choo cha kuvuta of which kulingana na mazingira yetu(hakuna maji) hakifai na ndicho chanzo cha maradhi yote..UFISADI..

Sasa hiyo hali nzuri mnayozungumzia nambie mkuu maanake kama unajua uchumi maanake ndiko naziona sifa nyingi za Mkapa sikuona miundombinu mipya wala miradi mipya ya uzalsiuhaji zaidi ya kuitumia ile ile ya mwalimu kuuza.. Kuhusu Kodi bila shaka Ukibinafsisha serikali itaanza kukusanya jambo ambalo Nyerere wala mwinyi wasingeweza kufanya kutokana na kwamba zile mali ni za serikali..Hata wewe ungekuwa rais chini ya mfumo huu wa kiuchumi ungeweza kukusanya kodi.. sasa tutazame muundo wa Ukusanyaji kodi..

Nchi nzima haina kipimo cha mapato ya mtu kuweka asilimia ya kodi zaidi ya kukisia.. Ukileta gari toka Japan atalipishwa fedha yoyote anayofikiria mpimaji akidanganya kutazama kitabu..Gari umenunua Usd. 500 unaambiwa kodi ni dollar 5000 at the same time jamaa yake anapitisha bure kwa kibali cha Ikulu..Wananchi wanalipishwa kodi kuliko viwanda vyote vya wageni ambao wanaingia 75% ya pato la taifa (GDP), no wonder we end up making less than 2% ya mauzo yote.
For real mkuu, nambie Mkapa kafanya kitu gani huo Uwanja wa Taifa, bridge to nowhere na barabara za mikopo au? mimi sioni zaidi ya kuona kilimo kilishuka, maji yakawa taabu (City water), Umeme wa mgao tukakaangwa na Richmond, Afya - Muhimbili imekufa wakati wake na Kibaya zaidi let the record show kuwa ktk historia ya Tanzania, kwa mara ya kwanza watu walikufa njaa wakati wa Mkapa.. Cholera, ndui na maradhi kibao yakarudi nchini baada ya kuendelea kutumia madawa mabaya..U name it yaani inachefua roho kumsikia Mkapa...ALL THESE ARE FACTS!
I mean guys what good mnaweza kunambia hata kama tukiacha Ufisadi nje!..
Na mkuu hakuna aliyesema Kikwete ni mbora, ana matatizo ya Uongozi bora kwa kuwa dhaifu ktk madaraka aliyokabidhiwa...Mkapa hakuwa dhaifu na ndio maana alituumiza bila kutupa uhuru wa kumnyooshea kidole. Vijiwe kama JF vilifungwa mara tatu wakati wa Mkapa, yes Kikwete kweli dhaifu angekuwa Mkapa JF ingekwisha fungwa siku nyingi..wenngine hapa hatupo duniani.
Mkuu mimi sioni kabisa Ubora wa Mkapa zaidi ya mgonjwa wetu Tanzania kuendelea kulala hospital akiwa ktk koma!.. hizo monitor haziwezi kunisaidia kitu ikiwa hakuna dalili za mgonjwa kurudi Uzima wake..
 
Kitila,
Mkuu usiseme nalaumu tuu bila kupima..
For real mkuu, nambie Mkapa kafanya kitu gani huo Uwanja wa Taifa, bridge to nowhere na barabara za mikopo au? mimi sioni zaidi ya kuona kilimo kilishuka, maji yakawa taabu (City water), Umeme wa mgao tukakaangwa na Richmond, Afya - Muhimbili imekufa wakati wake na Kibaya zaidi let the record show kuwa ktk historia ya Tanzania, kwa mara ya kwanza watu walikufa njaa wakati wa Mkapa.. Cholera, ndui na maradhi kibao yakarudi nchini baada ya kuendelea kutumia madawa mabaya..U name it yaani inachefua roho kumsikia Mkapa...ALL THESE ARE FACTS!
I mean guys what good mnaweza kunambia hata kama tukiacha Ufisadi nje!..

Aliweza kuwaua watanzania kwa makumi huko Pemba na akafanikiwa kuwalazimisha wengine kwa mamia waikimbie nchi na kupiga kambi jirani kama wakimbizi. In a nutshell Mkapa remains the worst President Tanzania ever had - labda atapikuliwa na huyu wa sasa.
 
kpleo.jpg
 
Ndio. Rais Mstaafu ana kinga ya kutoshitakiwa kwa maaamuzii
yoyote aliyoyafanya akiwa madarakani, hata hivyo kinga hiyo haizuii rais kushtakiwa yeye binafsi katika kesi za madai. Kinga hiyo inaweza kuondolewa na iwapo mbunge yoyoote atatoa hoja ya rais kutumia madaraka yake vibaya kwa lengo la
kujinufaisha isivyo halali, bunge likaridhia hiyo hoja, likatoa Azimio la Bunge kumuomba rais aondoe kinga kwa rais mstaafu ili ashitakiwe.
Mwamuzi wa mwisho ni rais anaweza kulisaini hilo azimio ama kuliacha. Hata hivyo kama raisi hata lisaini, Bunge linaweza kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais. Ikipitishwa na robo 3 ya wabunge wa kuchaguliwa, raisi anafukuzwa kazi na serikali yake yote.(mafao wanapata) Bunge linavujwa. Nchi inakuwa chini ya Jaji Mkuu(wizara chini ya makatibu wakuu) atakayeiamuru tume ya uchaguzi kuitisha uchaguzi mkuu mpya na kuundwa serikali mpya itakayopitisha azimio la kuondoa kinga ya rais mstaafu kushitakiwa na hivi ndivyo itakavyokuwa 2010,

Mwamu kumshtaki y
 
Imetolewa mara ya mwisho: 27.11.2008 0008 EAT
• Jinamizi la Mramba, Yona lahamia kwa Mzee Mkapa, Mtoto wa miaka 11 naye atoa mpya,Auliza mafisadi Richmond wako wapi?

*Mtoto wa miaka 11 naye atoa mpya
*Auliza mafisadi Richmond wako wapi?

Na Mwandishi Wetu
Majira

KUKAMATWA kwa vigogo wawili katika Serikali ya Awamu ya Tatu, Bw. Basil Mramba (aliyekuwa Waziri wa Fedha) na Bw. Daniel Yona (aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini) kumeanza kuibua tafsiri mpya huku jinamizi la vigogo hao likionekana kuhamia kwa bosi wao wakati huo, Rais mstaafu, Mzee Benjmain Mkapa, Majira limebaini.

Vigogo hao walikamatwa na kufikishwa kortini juzi kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa makosa mbalimbali yanayohusu kuiingia Serikali hasara kutokana na uamuzi wao katika masuala mbalimbali walipokuwa mawaziri hususani mkataba kwa kampuni ya ukaguzi wa kampuni ya Alex Stewart.

Wakati wananchi wakifurahia kuanza kuonekana kwa makucha yaliyokuwa yamejificha ya Serikali ya Awamu ya Nne, wataalamu wa masuala ya siasa na utawala, wameanza kulitazama suala hilo kwa mtazamo mpana zaidi wakisema kashifa dhidi ya mawaziri Mramba na Yona ni wazi kuwa inakwenda mbali zaidi na kumgusa mkuu wao wa kazi.

Miongoni mwa watu wa kwanza kuvunja ukimya juu ya kufikishwa mahakamani vigogo hao na kusisitiza kuwa kunamgusa pia Mzee Mkapa ni Profesa Ibrahim Lipumba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) na mchumi anayeheshimika kwenye Benki ya Dunia.

Profesa Lipumba amezidi 'kumshikia bango' Mkurugenzi wa Mashitaka ya Umma (DPP), Bw. Eliezer Feleshi, atangaze haraka yamuzi wa kumfungulia mashitaka Rais Mkapa.

Akihutubia katika mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Msingi Ruanda Nzovwe mkoani Mbeya, alisema Rais Mkapa ndiye anayejua masuala yote kuhusu upotevu wa fedha nyingi za umma ikiwemo katika masuala ambayo Mramba na Yona wametuhumiwa.

''Mkapa naye awekwe ndani, alikuwepo wakati wa mchakato…yeye ndiye alikuwa Rais, bila kuwekwa ndani, hakutakuwa na haki iliyotendeka…wahusika wote pia wa EPA wawekwe ndani kuanzia mdogo hadi mkubwa,'' alisema Prof. Lipumba.

Hata hivyo kauli hiyo ya Profesa Lipumba ni sawa na mzigo mzito kwa DPP ambaye huenda akawa na wakati mgumu kuamua iwapo kuna hoja na haja ya kufikia kumshitaki Rais Mkapa hasa wakati huu ambapo Rais Jakaya Kikwete alikwishaweka bayana zaidi ya mara mbili kuwa hafikirii kuwashitaki Marais waliomtangulia.


Mara ya kwanza Rais Kikwete aliweka msimamo huo alipokuwa kwenye ziara yake ndefu ya nchi za Skandinavia na kusisitiza msimamo wake huo alipokuwa akijibu swali la Mhariri wa MwanaHALISI, Bw. Saed Kubenea wakati Rais alipohutubia taifa kupitia kwa wahariri wa vyomnbo vya habari.

Mtoto wa miaka 11

Katika mkutano huo kiliibuka kituko kufuatia mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwakibete aliyejitambulisha kwa jina la Rupia Chaula (11) kumuuliza swali Profesa Lipumba sababu za watuhumiwa wa Richmond kutofikishwa mahakamani wakati wale wa EPA wameshaanza kuchukuliwa hatua hizo.

"Kwa nini watuhumiwa wa EPA wamepelekwa mahakamani na wa Richmond hawajapelekwa mahakamani?" aliuliza mwanafunzi huyo huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria mkutano huo.

Akijibu swali hilo Prof. Lipumba alisema anakubaliana na hoja zilizotolewa na kijana huyo na kusema kuwa huo ndio ukweli wa kinachotendeka katika utawala uliogubikwa na tuhuma za ufisadi kwa kuwakumbatia vigogo bila kuwafikisha katika mikono ya sheria.

"Wezi wa fedha za EPA ni wezi kama walivyo watuhumiwa wa Richmond, wachukuliwe hatua za kisheria na kufikishwa mahakamani kama wengine …Wao ndio wanahusika na mikataba mibovu…mikataba ya kifisadi ivunjwe iingiwe mikataba mipya yenye maslahi kwa wananchi,'' alisema Prof. Lipumba.

Hata hivyo, kauli ya Profesa Lipumba ya kutaka Rais Mkapa ashitakiwe, huenda ikakumbana na utata wa kinga aliyonayo kiongozi huyo kikatiba, kinga amabayo hata hivyo rejea ya kisheria na kesi mbalimbali za mfano kutoka sehemu mbalimbali duniani, ina acha maswali mengi zaidi kuliko majibu.

Utafiti wa Majira umeonesha kuwa kwa mujibu wa ibara ya 46 ya Katiba ya Muungano Rais amepewa kinga dhidi ya kushitakiwa kwa makosa ya jinai au madai kwa kipindi akiwa madarakani na hata baada ya kuacha madaraka iwapo aliyoyatenda (akiwa madarakani) yamo katika mambo anayopaswa kuyafanya kwa mujibu wa kiapo chake.

Ibara hiyo imekuwa ikiibua utata wa tafsiri hapa nchini hasa juu ya ni wakati gani Rais aliyeko madrakani au mstaafu atachukuliwa kuwa ametenda jambo lililo nje ya kiapo chake au utekelezaji wake wa kawaida kisheria.

Katika ripoti za Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu hapa nchini bado hakujafikishwa shauri ambalo lingeweza kuifanya mahakama kutoa tafsiri kamili na ya moja kwa moja juu ya ukomo wa kinga ya Rais kwa mujibu wa ibara hiyo.

Shauri pekee ambalo walau lilijaribu kugusa nguvu za kiutendaji za Rais juu ya maamuzi yake lakini si moja kwa moja kinga ya kushitakiwa ni lile la Mwalimu Peter Mhozya V AG (Civil Case no 206, 1993) ambapo mlalamikaji alitaka Rais Alli Hassan Mwinyi aondolewe madarakani kwa kushindwa kulinda katiba ya nchi kwa 'kunyamazia' Zanzibar kujiunga na Umoja wa Nchi za Kiislamu (OIC).

Jaji Barnabas Samatta wakati huo, pamoja na kulitupa shauri hilo kwa kuwa kikatiba Mahakama haina nguvu za kumwondoa madarakani Rais, bali Bunge, hakujadili suala la kama Rais anaweza kushitakiwa au la kama ambavyo mwalimu huyo alivyokuwa amejaribu kufanya..

Hata hivyo maoni ya wanasheria jadidi waliobobea katika masuala ya katiba kama Profesa Issa Shivji, Profesa Jwan Mwaikusa na Dkt. Sengondo Mvungi katika maandiko yao na wanapopata nafasi ya kutoa maoni yao, yamekuwa yakionesha kuwa kinga ya kikatiba ya Rais ina ukomo.

Nchini Marekani, walau suala la kinga ya Rais limeshawekwa bayana kuwa lina ukomo awapo madarakani na hata anapokuwa ameshamaliza madaraka yake.

Awali katika shauri maarufu la Nixon v. Fitzgerald (1982), katika uamuzi wake wa majaji watano dhidi ya wanne, Mahakama ya Rufaa ya nchi hiyo iliamua kuwa katika shauri la Rais Richard Nixon kutakiwa kuunganishwa katika mashitaka kutokana na uamuzi wa kumfukuza kazi ofisa wa umma kuidhinishwa naye, ilihukumiwa kuwa Rais alikuwa na kinga ya kutoshtakiwa kwani hapo alikuwa ametekeleza nguvu zake za kisheria.

Lakini mtazamo huo ulibadilishwa katika shauri jingine mashuhuri la Jones V Clinton, Mahakama ya Rufani ya nchi hiyo ilipokubaliana na uamuzi wa Mahakama Kuu kuwa Rais Bill Clinton wakati huo akikabiliwa na kashfa ya ngono, hakuwa juu ya sheria kwa sababu alilolifanya ni suala binafsi lisilohusu miiko ya ofisi yake.

Katika shauri la kwanza Rais Nixon alikuwa ameshtakiwa kwa kuhusishwa na uamuzi alioufanya kama Rais na ni tofauti na shauri la Clinton ambapo kesi ilihusu masuala yake binafsi yasiyo sehemu ya kiapo chake cha Urais na aliyoyafanya kabla hajawa Rais.

Tofauti baina ya kesi hizi mbili zinaweza kuipa nguvu nadharia ya wasomi wa hapa nchini kuwa baadhi ya vitendo vya marais vina kinga iwapo tu vilifanywa kwa mujibu wa sheria na viapo vyao na si pale ambapo wamehusika kufanya 'madudu.'
 
Ndio. ........ .....hivi ndivyo itakavyokuwa 2010,

Acha ndoto Pasco
This is just a suppositioh incase opposition wins 2010. Please dont say its imposible!. The Bible says 'Nothing is impossible under the sun'.

Hata Obama alianza tuu kama ndoto. Kenya, Zambia, Malawi na sasa Zimbabwe kote ni ndoto tu.

But I have to admit I am a dreamer just like Martin Luther King Jnr 'I have A Dream...'.
 
Rais Mstaafu ana kinga ya kutoshitakiwa kwa maaamuzii yoyote aliyoyafanya akiwa madarakani,

Kinga ya Rais mstaafu, chini ya Ibara ya 46 (3), ni dhidi ya "jambo lolote alilofanya yeye kama Rais" na sio "kwa maaamuzii yoyote aliyoyafanya akiwa madarakani." Rais akifanya uamuzi wa, kwa mfano, kubaka mfanyakazi jikoni Ikulu, au kufungua kampuni Ikulu kinyume na maadili ya uongozi, au kushirikiana na Waziri wa Madini kununua mgodi kwa idhini ya Waziri wa Madini, hapo hatakuwa hana kinga akistaafu.

hata hivyo kinga hiyo haizuii rais kushtakiwa yeye binafsi katika kesi za madai.

Provision ya kinga dhidi ya madai, chini ya Ibara ya 46 (2), haihusiani na Rais Mstaafu bali wa madarakani.
Kinga hiyo inaweza kuondolewa

Haiwezi.

Kinga dhidi ya Rais mstaafu kwa mambo aliyoyafanya kama Rais ni absolute, categorical and unqualified. Haiwezi kuondolewa na chombo au kiumbe chochote kile.

na iwapo mbunge yoyoote atatoa hoja... ya rais kutumia madaraka yake vibaya kwa lengo la kujinufaisha isivyo halali, bunge likaridhia hiyo hoja, likatoa Azimio la Bunge kumuomba rais aondoe kinga kwa rais mstaafu ili ashitakiwe.

Rais wa Tanzania hana nguvu ya kutangua kinga ya Ibara ya 46 ( 3 ). Na Bunge haliwezi kupinda Katiba.

Mwamuzi wa mwisho ni rais anaweza kulisaini hilo azimio ama kuliacha.

Hicho kitu umetunga!

Hata hivyo kama raisi hata lisaini, Bunge linaweza kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais. Ikipitishwa na robo 3 ya wabunge wa kuchaguliwa, raisi anafukuzwa kazi na serikali yake yote

Rais afukuzwe kazi kwa kukataa kutia saini ? Sasa kama hana choice ya kutia ama kutotia kwa nini kuwe na hiyo step ya kupitia thru idhini ya Rais? Na mbona mwanzoni umesema "mwamuzi wa mwisho ni Rais"? Uko wima hapo ulipo wewe ? Hebu levuka, unajua jinsi ya ku speed up kulevuka ? Kanywe maji mengi, au shtua kakikombe ka kahawa, halafu pata nap fupi.

mafao wanapata) Bunge linavujwa.

Tundiko zima ni punch lines za kipindi cha Mahoka.
 
Kinga ya Rais mstaafu, chini ya Ibara ya 46 (3), ni dhidi ya "jambo lolote alilofanya yeye kama Rais" na sio "kwa maaamuzii yoyote aliyoyafanya akiwa madarakani." Rais akifanya uamuzi wa, kwa mfano, kubaka mfanyakazi jikoni Ikulu, au kufungua kampuni Ikulu kinyume na maadili ya uongozi, au kushirikiana na Waziri wa Madini kununua mgodi kwa idhini ya Waziri wa Madini, hapo hatakuwa hana kinga akistaafu.



Provision ya kinga dhidi ya madai, chini ya Ibara ya 46 (2), haihusiani na Rais Mstaafu bali wa madarakani.


Haiwezi.

Kinga dhidi ya Rais mstaafu kwa mambo aliyoyafanya kama Rais ni absolute, categorical and unqualified. Haiwezi kuondolewa na chombo au kiumbe chochote kile.



Rais wa Tanzania hana nguvu ya kutangua kinga ya Ibara ya 46 ( 3 ). Na Bunge haliwezi kupinda Katiba.



Hicho kitu umetunga!



Rais afukuzwe kazi kwa kukataa kutia saini ? Sasa kama hana choice ya kutia ama kutotia kwa nini kuwe na hiyo step ya kupitia thru idhini ya Rais? Na mbona mwanzoni umesema "mwamuzi wa mwisho ni Rais"? Uko wima hapo ulipo wewe ? Hebu levuka, unajua jinsi ya ku speed up kulevuka ? Kanywe maji mengi, au shtua kakikombe ka kahawa, halafu pata nap fupi.



Tundiko zima ni punch lines za kipindi cha mahoka.

Pamoja na maelezo yote hapo juu wote ni mahoka ibara 46 (3) ya mawe? au maji? au mbuzi? au mchicha? au riwaya ya shigongo?

Wewe kuhani umezidi kuichanganya hii mada kuliko mwanzo. Kama una maelezo sahihi weka hapa jamvini! Kukosoa kunahitaji umakini laa sivyo utaharibu kuliko mwanzo.
 
Tangu kesi za mafisadi zianze siku chache zilizopita, watanzania wengi walifurahi kuona kuwa sasa kweli serikali yao inafanya kazi kama walivyotegemea. Ni watanzania wachache tu ambao walikuwa wamefaidika na ufisadi ndio waliokarahika na kuanza kwa kesi hizo.

Nimekuwa najiuliza hii nguvu na kasi ya uendeshaji wa kesi hizi imetoka wapi. Mwanzoni nilidhani kuwa JK alitishiwa maslahi yake na hao mafisadi, baadaye nikadhani kuwa huenda ameamua kuonyesha rangi yake kweli kweli kuitumikia Tanzania kwa maslahi ya umma. Lakaini leo nilivyosoma gazeti la Nipashe, nimegundua kuwa kuwa kuendeshwa kwa kesi hizi kunatokana na shinikizo kutoka kwa wafadhili (soma hapa chini).


Hapo ndipo nilipochoka kabisa,

Yaani kweli Tanzania tuna haja ya kuwa na serikali kubwa kama hii ya JK iawapo maamuzi makubwa ya nachi yanaendelea kutolewa na wafadhili?


BTY: Kwa Vile DPP ametumia madaraka yake vibaya kuzuia kuendeshwa kwa kesi dhidi ya Karamagi ambayo ina ushahidi wa kutosha kutoka TAKUKURU, kwa nini naye asiwajibishwe?


DPP adaiwa kumkingia kifua Nazir Karamagi
2008-11-27 12:07:13
Na Abdallah Bawazir


Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP), amezuia kupelekwa mahakamani aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi.

Karamagi anatuhumiwa kutumia madaraka vibaya katika kusaini mkataba wa mgodi wa madini wa Buzwagi.
Imedaiwa kuwa, DPP alichukua hatua ya kuzuia kufikishwa mahakamani kwa Karamagi kutokana na ushahidi dhidi ya tuhuma zinazomkabili kutojitosheleza.

Kesi dhidi ya Karamagi, ilikuwa iwasilishwe katika Mahakama ya Kisutu, jijini Dar es Salaam baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kukamilisha kazi yake.

Habari kutoka ndani ya kikao watendaji wa serikali na wafadhili wanaochangia bajeti ya serikali kilichofanyika Dar es Salaam jana, zilisema kuwa Takukuru walikwisha baini matumizi mabaya ya madaraka katika sakata zima la Buzwagi, lakini DPP akakataa kesi dhidi ya Karamagi isifunguliwe.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mabalozi wote ambao nchi zao zinachangia bajeti kuu ya serikali na Makatibu Wakuu wa wizara mbalimbali.

Chanzo chetu cha habari kutoka ndani ya kikao hicho, kilieleza kuwa, wafadhili walielezwa kuwa, Takukuru ilipeleka majalada ya kesi mbili kwa DPP, ikiwemo inayowahusu mawaziri wawili wa zamani, Basil Mramba na Daniel Yona ambayo ilitajwa juzi katika Mahakama ya Kisutu pamoja na la Buzwagi.


Ilielezwa kuwa, liliporudi jalada la mawaziri hao wawili wa zamani, lilipitishwa kwa ajili ya kupelekwa mahakamani, lakini la Buzwagi DPP alisema hakuna ushahidi wa kutosha kuifikisha kesi hiyo mahakamani, hivyo kulifunga.

Inadaiwa kuwa, uamuzi huo wa DPP, umeikasirisha Takukuru, ambayo ndiyo iliyokuwa ikikusanya ushahidi ili kesi hiyo iweze kufikishwa mahakamani kwa kuanza kusikilizwa.

Chanzo hicho cha habari cha kuaminika, wafadhili walielezwa kwamba, majalada ya kesi nyingine nne kubwa, zikiwemo zinazoihusu kampuni ya uchimbaji madini ya Meremeta na Deep Green, bado yapo kwa DPP yakisubiri uamuzi wake.

Pia Mabalozi hao waliwaomba kushawishi nchi za Ufaransa, Uswisi, Afrika Kusini, Mauritius, Hong Kong kutoa ushirikiano ili kesi hizo tatu ziweze kukamilika.

Ilidaiwa kuwa, nchi hizo zimekuwa hazionyeshi ushirikiano mara maaofisa wa Takukuru wakihitaji taarifa.

Jitihada za Nipashe za kumpata DPP, Elieza Feleshi jana ziligonga mwamba, kwani baada ya kuwasiliana naye alieleza kuwa, yupo kwenye kikao na kutaka apigiwe baada ya nusu saa.

Lakini baada ya muda huo kupita na kupigiwa, alipokea msaidizi wake ambaye alieleza kuwa, bado yupo kwenye kikao na hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, kikao hicho kilikuwa bado kikiendelea.

Nipashe ilipowasiliana na msemaji wa Wizara ya Katiba na Sheria, Omega Ngolle kuhusiana na suala hilo, alisema angeeleza kwa undani suala la jalada la Buzwagi, lakini hakufanya hivyo alipopigiwa simu baadaye.

Sakata la mkataba wa Buzwagi kusainiwa nje ya nchi kwa mara ya kwanza liliibuliwa Bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, wakati akichangia bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.

Zitto alidai kuwa, waziri huyo wa zamani alikwenda kusaini mkataba huo, London nchini Uingereza, kwa kutumia mfumo wa mikataba wa zamani wakati serikali ikiwa inajadiliana na wawekezaji kurekebisha mikataba ya madini nchini.

Suala hilo alilieleza katika mkutano wa nane wa Bunge mjini Dodoma, ambapo alihoji hatua ya Nazir Karamagi kusaini mkataba huo nje ya nchi.

Baadaye, Zitto aliwasilisha hoja binafsi bungeni, akiomba kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge, kuchunguza hali hiyo.

Zitto alieleza kushangazwa na uamuzi wa Karamagi kusaini mkataba wa madini kati ya serikali na kampuni maarufu ya madini hapa nchini ya Barrick Gold Mine kwa ajili ya mgodi ya Buzwagi nchini Uingereza badala ya Dar es Salaam.

Mbali ya kuhoji uhalali wa Karamagi kusaini mkataba huo, kinyume cha maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete ambaye aliagiza kupitiwa upya kwa mikataba yote mipya ya madini, Zitto alikielezea kitendo hicho kuwa kinaongeza wasiwasi wa kuwepo kwa ushawishi wa rushwa.

Hata hivyo, hoja hiyo ilitupiliwa mbali na Bunge na hatimaye Zitto aliishia kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa kile kilichoelezwa amelidanganya Bunge kuhusiana na madai yake hayo.

Alipewa adhabu hiyo kwa madai ya kutoa kauli ya uongo Bungeni dhidi ya Karamagi, inayohusu kusaini mkataba na kampuni ya Barrick, juu ya mradi wa Buzwagi, jijini London nchini Uingereza.

SOURCE: Nipashe
 
kwa maoni yangu sidhani kama JK anaweza kumuonolea Ben Kinga coz anaogopa naye yasije kumkuta. Sheria ya kinga iko wazi ila nani amfunge paka kengere
 
Pamoja na maelezo yote hapo juu wote ni mahoka ibara 46 (3) ya mawe? au maji? au mbuzi? au mchicha? au riwaya ya shigongo?

Kwa sababu ziko sehemu moja tu katika ulimwengu wa Sheria na Katiba Tanzania, mara nyingi ukisema "kinga za Ibara ya 46" unaeleweka unazungumzia nini. Ikisemwa "kinga za Ibara ya 46" tunamaanisha ibara za Katiba. Isitoshe kulikuwa na clue ya wazi kabisa, niliposema hapo juu kwamba Bunge haliwezi kupingana na Katiba.

Sasa maana ushajua tunaongelea Katiba, rudi basi ka point out "umahoka" wa chochote nilichokisema.
 
‘Tunamtaka Mkapa'

• CUF yamtaka Rais Kikwete aharakishe kumshitaki

na Christopher Nyenyembe, Mbeya
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

SIKU mbili baada ya mawaziri wawili wa Serikali ya Awamu ya Tatu kufikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia madaraka yao vibaya wakiwa watumishi wa serikali katika ngazi za uwaziri, rais mstaafu Benjamin Mkapa, naye ameanza kuandamwa kuwa anapaswa kufikishwa mahakamani kwa tuhuma kama hizo zinazowakabili waliokuwa wasaidizi wake.

Chama cha Wananchi (CUF) ambacho mara kadhaa kimekuwa kikimshutumu Mkapa kukiuka miiko ya uongozi wakati akiwa madarakani, juzi jioni kilifufua tena madai yake hayo huku kikimtaka Rais Jakaya Kikwete kumfikisha mahakamani haraka ili aunganishwe katika kesi zinazowakabili waliokuwa wasaidizi wake katika uendeshaji wa serikali.
Kauli hiyo ya CUF ambayo imekuwa ikitolewa na wanaharakati wengine kadhaa kwa muda mrefu sasa, ilitolewa na Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho cha upinzani, Profesa Ibrahim Lipumba, wakati akihutubia wananchi wa Jiji la Mbeya katika viwanja vya Ruanda - Nzovwe juzi jioni.

Prof. Lipumba, aliuambia umati wa wananchi wa Mbeya kuwa Mkapa anapaswa kufikishwa mahakamani na kuunganishwa katika kesi zinazowakabili aliyekuwa Waziri wake wa Fedha, Basil Mramba na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona, kwa makosa yote 13 wanayotuhumiwa kuyafanya chini ya utawala wake.

“Ni lazima rais mstaafu, Benjamin Mkapa, afikishwe mahakamni kujibu tuhuma za ufisadi ambazo kwa kiasi kikubwa zilifanyika kipindi cha utawala wake. Anapaswa kufikishwa mahakamani kwa sababu katiba ya nchi haielezi kuwa rais atalindwa hata kama amehusika katika masula ya rushwa na ufisadi,” alisema Prof. Lipumba.

Prof. Lipumba alisema Mkapa ana kila sababu ya kuwaomba radhi Watanzania na kutoa maelezo jinsi utawala wake ulivyogubikwa na matukio ya rushwa kubwa zilizowahusisha viongozi wa ngazi za juu serikalini na yeye kushindwa kuzuia matukio hayo yasitokee.

“Mkapa anapaswa aende akatubu kwanza kanisani kisha arudi kwa wananchi aeleze kuwa amekwenda kutubu kwa kuachia mali za nchi kutumika vibaya, yakiwemo madini ambayo Watanzania, licha ya kuwa mali yao, hawanufainiki nayo na badala yake wanawanufaisha wageni,” alisema Prof. Lipumba.


Aliishutumu Serikali ya Awamu ya Tatu kwa kushindwa kutumia vema rasilimali za nchi kuinua uchumi wa Watanzania na kuwaachia wawekezaji wa kutoka nje kuvuna rasilimali hizo jinsi watakavyo. Aliongeza kuwa hata matabaka yaliyopo baina ya maskini na matajiri katika jamii ya Tanzania yalistawi zaidi katika awamu hiyo ya uongozi wa Mkapa.

Kauli hiyo ya Prof. Lipumba ilionekana kuwagusa wananchi wengi waliohudhuria mkutano huo, kutokana na kile kilichoelezwa na baadhi yao kuwa, imetolewa wakati muafaka, ambapo Mramba na Yona wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kutumia vibaya madaraka yao, na fikra hizo bado zikiwa akilini mwa wengi.

Wengi wa wahudhuriaji wa mkutano huo walionekana kuwa wasikivu zaidi na hakukuwa na tukio lolote la fujo wala kusukumana, jambo lililotafsiriwa kuwa ni kuguswa kwa wananchi na hatua hiyo ya serikali ya kuwafikisha vigogo hao mahakamani.

Suala la watu kutaka Mkapa afikishwe mahakamani limekuwa likijadiliwa mara kwa mara na wakati fulani mwaka jana, Rais Kikwete alipata kuwataka Watanzania wanaomsakama kiongozi huyo mstaafu kumwacha apumzike.

Wengi wa watu wanaotaka Mkapa achukuliwe hatua za kisheria pamoja na kutambua kuwa ana kinga juu ya maamuzi yoyote aliyoyafanya wakati akiwa madarakani, wanamhusisha na baadhi ya miradi kama ule wa ubinafsishaji wenye utata wa mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira.

Hata hivyo wakati shinikizo la Mkapa likipoa na kuibuka mara kwa mara, mapema mwaka huu, yeye mwenyewe alipata kukaririwa akisema kwamba, tuhuma zote za matumizi mabaya ya madaraka na nyingine zinazoelekezwa kwake ni za uongo na kuzushiwa, ingawa hakuwa tayari kutoa ufafanuzi.

Wakati huo huo, Mwandishi Wetu Happinnes Katabazi anaripoti kuwa, wanasiasa wawili, Mramba na Yona, waliofikishwa kortini juzi wakituhumiwa kutumia madaraka yao vibaya, wanaendelea kusota mahabusu, baada ya jana kushindwa kupata dhamana.

Mramba na Yona, hawakutokea kabisa mahakamani jana, tofauti na ilivyokuwa ikitarajiwa na wengi kuwa baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana juzi, ambapo ndugu na jamaa zao walikuwa wakihaha bila mafanikio kuwawekea dhamana, wangefanikisha dhamana zao jana.
 
Tangu kesi za mafisadi zianze siku chache zilizopita, watanzania wengi walifurahi kuona kuwa sasa kweli serikali yao inafanya kazi kama walivyotegemea. Ni watanzania wachache tu ambao walikuwa wamefaidika na ufisadi ndio waliokarahika na kuanza kwa kesi hizo.

Nimekuwa najiuliza hii nguvu na kasi ya uendeshaji wa kesi hizi imetoka wapi. Mwanzoni nilidhani kuwa JK alitishiwa maslahi yake na hao mafisadi, baadaye nikadhani kuwa huenda ameamua kuonyesha rangi yake kweli kweli kuitumikia Tanzania kwa maslahi ya umma. Lakaini leo nilivyosoma gazeti la Nipashe, nimegundua kuwa kuwa kuendeshwa kwa kesi hizi kunatokana na shinikizo kutoka kwa wafadhili (soma hapa chini).


Hapo ndipo nilipochoka kabisa,

Yaani kweli Tanzania tuna haja ya kuwa na serikali kubwa kama hii ya JK iawapo maamuzi makubwa ya nachi yanaendelea kutolewa na wafadhili?


BTY: Kwa Vile DPP ametumia madaraka yake vibaya kuzuia kuendeshwa kwa kesi dhidi ya Karamagi ambayo ina ushahidi wa kutosha kutoka TAKUKURU, kwa nini naye asiwajibishwe?

Kichuguu....

Inawezekana ikawa vyote.... nguvu ya wafadhili ambao ndio walishinikiza hata uchunguzi wa kwanza ufanyike baada ya serikali kusema kuwa madai ya Dr Slaa ni uzushi na uongo.

Kikwete na serikali pia, mimi (binafsi) nawapatia credit kwa kuamua kulichukua hili swala kwa uzito unaostahili. Ingawa sina hakika kama hizi case zitafika kokote kule, kwa sasa naona ni mwanzo mzuri kuwafikisha mafisadi ndani ya jela ili na wao waonje joto la huko.
 
Kichuguu,

..hata mimi nilikuwa najiuliza maswali kama yako.

..mwanzoni nilitaka kumpa pongezi JK, lakini kuna teuzi mbalimbali alizozifanya JK zilizonilazimisha kuamini kwamba hakuwa na nia ya kupambana na rushwa hata kidogo.

..Raisi ambaye anateua watu kama Dr.Rashidi wa tanesco[DG Tanesco], Andrew Chenge, Basil Mramba, na Mustafa Mkulo, kwa kweli sidhani kama yuko serious na masuala ya kupiga vita rushwa.

..halafu sijui kama una taarifa kwamba, Balozi.Fulgence Kazaura, ambaye alinukuliwa na Kamati ya Mwakyembe akisema "Richmond ni biashara ya 'bwana mkubwa'," ameondolewa kama Mwenyekiti wa Tanesco. unaweza ukatoa kisingizio kwamba muda wake ulikwisha.

..hizi taarifa za Wafadhili kushinikiza watuhumiwa wa rushwa wapelekwe mahakamani nadhani ni za kuaminika. it happened before wakati wa utawala wa Raisi Mwinyi. wafadhili ndiyo walimshinikiza Raisi Mwinyi amuondoe Prof.Malima toka Hazina.
 
Mkuu Kichuguu,

Heshima mbele sana, leo baada ya kuongea sana na wanaohusika na abdo ninaendelea kuongea nao, ni very clear kwa 100% kwamba ni nguvu ya sauti kali kutoka ndani ya CCM ndizo zimemfanya muungwana kuchaia mlango, lakini kuna mengi yanayoendelea behind the scene, nitarudi baadaye kule kwenye thread ya kushikwa kwao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom