Mkanganyiko wa biashara ya kamari: Mitandao vs vyombo vya habari

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,791
Tuliandika, tunaandika na tutaandika tena na tena lakini ni kama mamlaka zimetiwa upofu machoni na kuweka nta masikioni.. Ni wazi kuna mfaidikaji/wafaidikaji bila kujali madhara makubwa ya baadae

Nilikaa kwenye hii biashara kwa mwaka mzima... Haya ndio niliyaona
Ni biashara ya faida kubwa
Ni biashara yenye mtandao mkubwa
Ni biashara yenye udanganyifu mkubwa
Ni biashara yenye utapeli mkubwa
Ni biashara yenye wizi mkubwa
Ni biashara yenye makengeza mengi sana

Sasa wafaidikaji ni akina nani?
1. Wamiliki
2. Watendaji wa mamlaka(Commissions na rushwa)
3. Serikali(mapato)
4. Washindi
5. Wachezeshaji
6. Vyombo vya habari(kuuza matangazo nk)

Wakosoaji ni akina nani?
1. Wananchi viona mbali kupitia mitandao ya kijamii
2. Waliofilisika kupitia kamari
3.Waliozimishwa ndoto zao kupitia kamari
4. Wanafunzi na wanachuo waliofeli na kuharibu masomo yao kwasababu ya kamari
5. Wanandoa na wote waliovuruga familia zao kwasababu ya kamari
6. Na wengine wote ambao kupitia kamari makutana na mengi magumu kama kesi, ajali, madawa nknk

Makundi hasa ya vijana yaliathirika na kamari ndio mashuhuda wazuri kwenye hii kampeni ya kupinga na kutoa maonyo mengi kuhusiana na huu mchezo mbaya kabisa

Wenzetu waliokwisha onja shubiri na machungu ya shubiri sasa wameweka sheria kali na ngumu kwenye hii biashara, sisi tunawaona maboya.. Tutakuja kulia kilio kikubwa sana

Serikali iko kimya kwakuwa inapokea mapato ambayo hata hivyo ni kiduchu ... Vyombo vya habari vinaisherehesha hii biashara kwa kuitangaza, kuchezesha na kutangaza washindi kila siku.. Nao wa watangazaji wao wamepata vyanzo vyepesi vya mapato.. Huwaambii kitu

Pengine kwasasa ni tv na radio za kidini tu ndio hawafanyi hii biashara..wengine woote wametekwa huko... Umasikini mbaya sana, hasa umaskini wa fikra uduni wa elimu, na ufinyu wa maono.. Wanachojali ni commision kwenye bukubuku za masikini walalahoi

Kamari kutokana na nature yake sio biashara ya kuhusishwa na mamlaka za nchi imejaa uhuni na udanganyifu mkubwa.. Kwahiyo inahujumu uchumi pakubwa sana, maana hizo bukubuku zinazokusanywa kila siku zinaishia mifukoni mwa wajanja wachache na kuondoshwa nchini kwa njia za kimafia

Kamari inalifilisi taifa
Kamari inawatia ufukara wananchi
Kamari inaangamiza vipaji na vipawa vingi
Kamari ni janga la taifa.. Lakini kuipiga vita kwakuwa washika dau ndio wafaidikaji wakubwa na badala ya kula siha wanaambulia makombo...

Thread 'Udanganyifu unaofanywa kwenye michezo ya kubahatisha na kamari' Udanganyifu unaofanywa kwenye michezo ya kubahatisha na kamari

Thread 'Kamari: Janga lingine lililofumbiwa macho' Kamari: Janga lingine lililofumbiwa macho

Alamsiki Tanganyika!
 
Umeandika kitu kikubwa sana kwa wenye akili na kuyatazama mambo kiundani zaidi....

Zamani pindi twakuwa tulikuwa twaambiwa kamari mbaya wala msiicheze, hakika ya kamari ni uhuni na njia mbaya wakisema wakubwa

Ila unfortunately Leo betting haitwi kamari Bali mchezo wa kubahatisha daah
 
Ukweli mchungu tunaobet hii ni ngumi ndoige KWA BAHATI MBAYA SANAAA SASA MKUU Mshana Jr Wamiliki wengi wa kampuni ni vigogo serikalini ukiachana na Abas Tarimba kuna kigogo wa Trab na trat ambae anamiliki M-Bet aliipigia promo zamani maiato yalikua 20% akaenda bungeni akaipigia promo kwamba "Wakamaria wanakatwa parefu ivyo wapunguziwe makato ili wacheze kwa amani" Bahati mbaya zaidi bunge likapitisha hoja..kabla hatujakaa sawa juzi tena kaomba mswada wa kupunguza makato iwe 10% tu....Sasa inahitaji kiongozi mwenye ROHO YA CHUMA kupambana na ili janga kwasababu naiona ni kama sekta nyeti kwa kiongozi wa kawaida kupambana nayo

Kazi ipo
 
Ukweli mchungu tunaobet hii ni ngumi ndoige KWA BAHATI MBAYA SANAAA SASA MKUU Mshana Jr Wamiliki wengi wa kampuni ni vigogo serikalini ukiachana na Abas Tarimba kuna kigogo wa Trab na trat ambae anamiliki M-Bet aliipigia promo zamani maiato yalikua 20% akaenda bungeni akaipigia promo kwamba "Wakamaria wanakatwa parefu ivyo wapunguziwe makato ili wacheze kwa amani" Bahati mbaya zaidi bunge likapitisha hoja..kabla hatujakaa sawa juzi tena kaomba mswada wa kupunguza makato iwe 10% tu....Sasa inahitaji kiongozi mwenye ROHO YA CHUMA kupambana na ili janga kwasababu naiona ni kama sekta nyeti kwa kiongozi wa kawaida kupambana nayo

Kazi ipo
....Sasa inahitaji kiongozi mwenye ROHO YA CHUMA kupambana na ili janga kwasababu naiona ni kama sekta nyeti kwa kiongozi wa kawaida kupambana nayo
 
Umeandika kitu kikubwa sana kwa wenye akili na kuyatazama mambo kiundani zaidi....

Zamani pindi twakuwa tulikuwa twaambiwa kamari mbaya wala msiicheze, hakika ya kamari ni uhuni na njia mbaya wakisema wakubwa.........

Ila unfortunately Leo betting haitwi kamari Bali mchezo wa kubahatisha daah
Kamari ni haramu China na wametenga mji mmoja kwa wapenda kamari waende huko...
 
Inaonesha media zetu hazina watu kama Ruge kwa ufikiriaji wao umeishia hapo

R.I.P RUGEMALILA
 
Kamari inalifilisi taifa
Kamari inawatia ufukara wananchi
Kamari inaangamiza vipaji na vipawa vingi
Kamari ni janga la taifa.. Lakini kuipiga vita kwakuwa washika dau ndio wafaidikaji wakubwa na badala ya kula siha wanaambulia makombo...
 
Habari kila mmoja,

Ndugu wapendwa kiuhalisia kama jamii tunaelekea kwenye eneo ambalo sio sahihi hasa jinsi palivyoshamiri michezo hii ya betting au kubahatisha.

Ukiangalia nchi kama china miaka 40 au 30 nyuma haikua na kiwango hiki kikubwa cha uchumi ila serikali na watu wake waliamua kuwekeza kweny uzalishaji na teknolojia kiujumla ili kuweza kwenda mbele,ukija huku kwetu ni tofauti kabisa,sasa hv mpka tv na redio ya serikali inachezesha betting(ajabu kabisa).

Kuna mengi ya kujiuliza hv kweli huku ndo tumeona kama njia sahihi ya kutufikisha kwenye maendeleo ya kweli, jibu ni hapana bali ni kuendelea kuukuza umaskini na kuwanenepesha mabepari!

Jambo hili linasikitisha sana kiuhalisia.
 
Back
Top Bottom