Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,802
- 11,961
Hali ya usafi wa mazingira ilivyo Mkoani Morogoro katika Kata ya Mbuyuni, Mtaa wa Msikiti wa Masai karibu na Muslim University of Morogoro.
Mkandarasi wa usafi anaitwa Kajenjere lakini inadaiwa zaidi ya mwezi hajafika eneo husika kukusanya taka, hivyo kusababisha hali kuwa mbaya hadi taka zimeanza kutengeneza funza.
Serikali ya mtaa wanalijua na kila siku linajadiliwa kwenye vikao lakini halijafanyiwa kazi.
UPDATES...
Akizungumzia hali hiyo, Mwenyekiti wa Mbuyuni, Jerald Mawanja amesema "Mkandarasi aliyepewa hii tenda anaitwa Kajenjere, kazi imemshinda na hakuna chochote anachokifanya au hatua zinazochukuliwa dhidi yake.
"Alianza vizuri akawa anapita kila wiki kukusanya taka, akawa anapita baad aya wiki mbili ikaja tatu na sasa ni zaidi ya mwezi. Kwa mazingira ya mitaa yetu kutozoa taka zaidi ya mwezi unataegemea nini kitokee.
"Kunapokuwa na changamoto kama hivi huwa tunaenda kuripoti kwa Afisa Afya ambaye ndiye anatakiwa kulifanyia kazi jambo hilo, lakini hakuna taarifa yoyote, hali ni mbaya na kuna uwezekano wa kutokea kwa milipuko ya magonjwa.
"Hali hii si mtaani kwetu tu bali Kata nzima kuna changamoto hii ya takataka kutozolewa."
Mkandarasi wa usafi anaitwa Kajenjere lakini inadaiwa zaidi ya mwezi hajafika eneo husika kukusanya taka, hivyo kusababisha hali kuwa mbaya hadi taka zimeanza kutengeneza funza.
Serikali ya mtaa wanalijua na kila siku linajadiliwa kwenye vikao lakini halijafanyiwa kazi.
UPDATES...
Akizungumzia hali hiyo, Mwenyekiti wa Mbuyuni, Jerald Mawanja amesema "Mkandarasi aliyepewa hii tenda anaitwa Kajenjere, kazi imemshinda na hakuna chochote anachokifanya au hatua zinazochukuliwa dhidi yake.
"Alianza vizuri akawa anapita kila wiki kukusanya taka, akawa anapita baad aya wiki mbili ikaja tatu na sasa ni zaidi ya mwezi. Kwa mazingira ya mitaa yetu kutozoa taka zaidi ya mwezi unataegemea nini kitokee.
"Kunapokuwa na changamoto kama hivi huwa tunaenda kuripoti kwa Afisa Afya ambaye ndiye anatakiwa kulifanyia kazi jambo hilo, lakini hakuna taarifa yoyote, hali ni mbaya na kuna uwezekano wa kutokea kwa milipuko ya magonjwa.
"Hali hii si mtaani kwetu tu bali Kata nzima kuna changamoto hii ya takataka kutozolewa."