nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
TUESDAY, DECEMBER 4, 2012
Bw. Samson Chacha Boroyi
KADA wa CHADEMA Bw. Samson Chacha Boroyi ambaye ni Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA) Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza, amejiengua katika chama hicho huku akikiponda chama hicho kuwa kinaongoza nchini kwa kuwafanya watu Chambo na kuongozwa kwa maslahi ya Ukanda .
Akizungumza na vyombo vya habari Jijini Mwanza amewataja waziwazi baadhi ya viongozi wa CHADEMA wakiwemo wale wa Kitaifa kuwa hawataki kutii Sheria, Kanuni na Taratibu za nchi hivyo siku wakipatiwa Dola, hali itakuwa mbaya kuliko ya Misri na Libya.
Mwalimu Samson Boroyi ameyasema hayo huku akikiita Chama hicho kuwa ni Kampuni ya kundi dogo la vigogo wa Kanda ya Kaskazini japokuwa wamekuwa wakijinadi kuwa ni Taasisi ya Kisiasa, alidai kwamba viongozi wa Chama hicho wakiwemo Katibu Mkuu Dkt Willbroard Slaa wamekuwa wakiitumia CHADEMA vibaya kwa kushindwa kufuata Katiba yake na hata kuwa watu wasiotii sheria za Nchi na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Bw.Boroyi ambaye pia alikuwa Katibu Mwenezi wa Chadema Kata ya Nyamanoro wilayani Ilemela, alieleza kwamba pamoja na chama hicho kuendeshwa kama kampuni ya mtu binafsi, kundi hilo dogo ndilo linalotoa maamzi bila kuzingatia Katiba yake na maslahi ya wengi.
Ameongeza kuwa hata Bw Wenje alitoa ahadi ambayo ameshindwa kuitekeleza tangu aitangaze kwenye mikutano yake ya hadhara na kujigamba kusomesha watoto 1,960 katika Sekondari za Kata na kuzipatia madawati, kuboresha huduma ya Hospitali ya wilaya ya Nyamagana ya Butimba wakati hali ni kinyume na mbwembwe hizo.
Hata hivyo Bw.Boroyi hakuwa tayari kutaja chama atakachojiunga nacho hadi hapo baada ya wiki mbili,atakapokuwa ametafakari kwa kina ni Chama kipi bora atakachojiunga nacho ili asikosee tena kama alivyopotea muda wake kujiunga na Chadema toka mwaka 2007akiwa mwanachama hai kwa Kadi namba 0359614 na kuahidi kuirejesha Kadi hiyo kwa Katibu wa Wilaya ya Ilemela Jumatatu ijayo ili kuthibitisha kukiacha kabisa chama hicho.
Posted by Albert G.Sengo
Bw. Samson Chacha Boroyi
KADA wa CHADEMA Bw. Samson Chacha Boroyi ambaye ni Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA) Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza, amejiengua katika chama hicho huku akikiponda chama hicho kuwa kinaongoza nchini kwa kuwafanya watu Chambo na kuongozwa kwa maslahi ya Ukanda .
Akizungumza na vyombo vya habari Jijini Mwanza amewataja waziwazi baadhi ya viongozi wa CHADEMA wakiwemo wale wa Kitaifa kuwa hawataki kutii Sheria, Kanuni na Taratibu za nchi hivyo siku wakipatiwa Dola, hali itakuwa mbaya kuliko ya Misri na Libya.
Mwalimu Samson Boroyi ameyasema hayo huku akikiita Chama hicho kuwa ni Kampuni ya kundi dogo la vigogo wa Kanda ya Kaskazini japokuwa wamekuwa wakijinadi kuwa ni Taasisi ya Kisiasa, alidai kwamba viongozi wa Chama hicho wakiwemo Katibu Mkuu Dkt Willbroard Slaa wamekuwa wakiitumia CHADEMA vibaya kwa kushindwa kufuata Katiba yake na hata kuwa watu wasiotii sheria za Nchi na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Bw.Boroyi ambaye pia alikuwa Katibu Mwenezi wa Chadema Kata ya Nyamanoro wilayani Ilemela, alieleza kwamba pamoja na chama hicho kuendeshwa kama kampuni ya mtu binafsi, kundi hilo dogo ndilo linalotoa maamzi bila kuzingatia Katiba yake na maslahi ya wengi.
Ameongeza kuwa hata Bw Wenje alitoa ahadi ambayo ameshindwa kuitekeleza tangu aitangaze kwenye mikutano yake ya hadhara na kujigamba kusomesha watoto 1,960 katika Sekondari za Kata na kuzipatia madawati, kuboresha huduma ya Hospitali ya wilaya ya Nyamagana ya Butimba wakati hali ni kinyume na mbwembwe hizo.
Hata hivyo Bw.Boroyi hakuwa tayari kutaja chama atakachojiunga nacho hadi hapo baada ya wiki mbili,atakapokuwa ametafakari kwa kina ni Chama kipi bora atakachojiunga nacho ili asikosee tena kama alivyopotea muda wake kujiunga na Chadema toka mwaka 2007akiwa mwanachama hai kwa Kadi namba 0359614 na kuahidi kuirejesha Kadi hiyo kwa Katibu wa Wilaya ya Ilemela Jumatatu ijayo ili kuthibitisha kukiacha kabisa chama hicho.
SIKILIZA AKIONGEA na WAANDISHI
[JFMP3]http://ak-media.soundcloud.com/5rGvAbGlSOv3.128.mp3[/JFMP3]
[JFMP3]http://ak-media.soundcloud.com/5rGvAbGlSOv3.128.mp3[/JFMP3]
Posted by Albert G.Sengo
Tumtakie kila la heri kwenye safari yake ya kuelekea upotevuni. Better few but better. Jeshi lenye wapiganaji wenye ari, nia na dhamira, wanaojua wanachokifanya ndilo hatimaye hushinda, not just a collection of individuals.
Katika safari hii, wapo watakaokata tamaa, wapo watakaosonga mbele, wapo watakaosaliti, wapo watakaokuwa watiifu, wapo watakaogeuka nyuma, wapo watakaosema mbele kwa mbele, nyuma mwiko, wapo watakaotaka njia za mkato, wapo watakaojua safari hii yahitaji uvumilivu na kujitoa, wapo watakaoanguka, wapo watakaobeba silaha zao na kusonga mbele, wapo watakaofika mpaka mwisho wapo watakaoishia njiani hata kama walitamani kuona mwisho mwema wa kile ambacho kila Mtanzania mpenda nchi yake anatamani kukiona miaka michache ijayo.
Kama tayari ameimba kibwagizo cha Nape cha elements za ubaguzi, ishara ya mtu asiyeweza kujenga hoja dhidi ya CHADEMA, hana haja ya kuwadanganya watu anafikiria. Kama hana uwezo wa kufikiria beyond his tribe and religion, he deserves what he has done.
Watu wa Kanda ya Ziwa hatundanganyiki tena. Mnakotaka kulalia, ndiko tulikoamukia. Watu wa Mkoa wa Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla, kama mababu zetu walivyoshikamana na Watanzania wote wakati kupambana dhidi ya mkoloni, kizazi cha sasa hatutakubali kudanganywa kwa nyimbo hizi za kuchelewesha ukombozi wa pili wa Tanzania.