Mashaxizo
JF-Expert Member
- Jun 13, 2013
- 6,707
- 3,327
Kama wajumbe wameenda kwenye bunge la Katiba kusimamia maslahi ya wananchi waliowatuma, kitu gani kinawafanya watake kujificha kwenye maamuzi ya mwanvuli wa kura ya siri katika kupitisha, kukataa au kubadilisha vipengele vya Rasimu ya Katiba?.
Wananchi wanataka kufahamu kile wajumbe wao wamekikubali na kukikataa bungeni ili iwe ni historia iliyoandikwa kwa kila mjumbe na siyo kwa mwanvuli wa wajumbe wote wa bunge la Katiba.
Kujificha kwenye kura za siri katika maamuzi haya muhimu ya kitaifa ni kujenga taifa la waoga na wanafiki kitu ambacho ni hatari sana katika mstakabali wa Taifa endelevu.
Wananchi wanataka kuweka historia wazi kwa kila mjumbe kwa kizazi hiki na cha baadaye.
Kama kuna watu wameingia kwenye Bunge la Katiba bila kuelewa umuhimu wao katika mstakabali wa taifa na mpaka sasa bado wameendelea kuwepo, basi hawataweza kusamehewa kwa makosa makubwa kama haya kwa taifa.
Kila mjumbe lazima aubebe msalaba wake wa kuingia kwenye bunge la Katiba na siyo kujificha kwenye mwanvuli wa corrective responsibility.
Moja ya nguzo kuu ya CCM iliyochangia kwa chama kudumu mpaka sasa katika ahadi zake ni pamoja na kusema kweli daima na fitina ni mwiko.
Huyu Shekhe ni kibaraka wa Maccm! Na hapo ndio naamini ccm wamejazana mle!
Kikwete mbona unajisuta? Si wewe ukietaka katiba mpya!
Sasa mbona umejaza wapuuzi mle?