Mjumbe Maalum wa Marekani Nchini Afghanistan atangaza kujiuzulu

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,492
9,263
Mjumbe maalumu wa Marekani kwa Afghanistan, Zalmay Khalilzad ametangaza kujiondoa katika wadhfa wake kufuatia kile kinachoelezwa namna mbaya ya Marekani katika kujiondoa kwake nchini Afghanistan.

Anakosolewa kwa kutofanikisha shinikizo la kutosha la mazungumzo ya amani kwa kundi la Taliban pale yalipoanza wakati utawala wa Rais Donald Trump, lakini Waziri wa Mambo ya Nje Anthony Blinken amemshukuru kwa kazi yake. Katika pongezi zake hizo kwa balozi huyo wa zamani wa Marekani kwa Umoja wa Mataifa na Afghanistan alisema anatanguliza shukrani zake kwa miongo kadhaa ya kuwahudumia Wamarekani.

Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Zalmay Khalilzad atakuwa kando ya kiti chake juma hili, baada ya kuhudumu nafasi hiyo kwa zaidi ya miaka mitatu katika tawala zote za Trump na Biden. Na tayari kiti chake atakikalia, Thomas West.
 
Back
Top Bottom