Wakuu,
Naomba mwenye data za mgombea mwenza azimwage.
Ningeomba pia nitoke nje ya mada kidogo ili kujenga ulinganifu wa muungano na mgombea mwenza. Mgombea mwenza ni mtu muhimu sana kwa sababu ni kiongozi wa pili kimadaraka. Sasa Zanzibar wana bendera yao, wimbo wao wa taifa, leo wamesema ni nchi iliyoungana na ''hakuna'' maana Tanganyika haipo. Mafuta ni yao ingawa ardhi ni ya muungano. Wanabunge lao,raisi wao,Katiba yao,mikoa yao, Ajira zao lakini pia ajira ni muungano. Sasa kwanini sisi Watanganyika tulipe gharama za muungano ambao practically haupo?.
Gharama mojawapo ni hii ya kutulazimisha kuwa na mgombea kutoka visiwani! why?
Naomba kuelimishwa tafadhali! :confused2:
Mi siwalaumu walioziunganisha Tanganyika na Zanzibar. Pengine kwa wakati ule wa vita baridi na matishio ya kuvamiwa, muungano ulikuwa sahihi. Lakini kwa sasa kama muungano wenyewe ndio huo, wa nchi moja kuwa na dola yake wakati nyingine haina, then huu muungano uangaliwe upya. Umekwisha wakati wa kufanywa watoto, na kuzuiwa kuhoji.Una pointi ila nadhani jibu lake halitapatikana mapema.
naona data za huyu jamaa mgombea mwenza! sina data zake jamani mwenye nazo azimwage hapa ili tuangalie record zake kiuongozi.
Amethibitishwa rasmi leo kuwa ndiye mgombea mwenza pamoja na Dr. Slaa katika kikao kilichofanyika leo
Una pointi ila nadhani jibu lake halitapatikana mapema.
THE CHADEMA Presidential candidate Dr Willibrod Slaa (left) and his running mate, Said Mzee Said display their forms received from the National Electoral Commission (NEC) Chairman, Judge Lewis Makame in Dar es Salaam on Monday
mbona kama amelazimishwa? anaonekana bado ni CUF huyu
anyway hivi ana CV gani huyu bwana maana tunamgoogle lakini hakuna kitu
Si bora awe amelazimishwa (kama alivyolazimishwa Dkt Slaa) kuutmikia umma kuliko fisadi Gharib Bilal (ex-Mlimani students tunakumbuka sana uhuni wake) aliyeteuliwa kishkaji kupoza mzuka wa washabiki wake Zenji?
Kikubwa hapa ni Slaa. Wagombea-wenza Tanzania hawajawahi kuwa muhimu. Si Shein wala aliyemtangulia wamefahamika. Hili tumaini lililoibuka Tanzania sasa linatokana na kukubali kwa Slaa kuwa Mgombea. Mengine yote hayana neno. Nobody will think about hawa wagombea wenza wakati wa kukipigia CHADEMA kura.