Alifahamika kwa jina la MBOKOO!
Alikuwa kibaka mwenye miraba minne, Ambaye alikuwa kero kubwa kwa wakazi wa Kigamboni!
Taarifa za uhalifu wake ziliwahi kuwa kero zilivyoripotiwa kila siku kwa matukio tofauti kiasi Cha kujaza REPORT BOOK (RB) ya polisi kila kuchwao akituhumiwa kuhusika na uharifu mbalimbali.
Updates June 2021
Kibaka mbokoo baada ya kumaliza kutumikia kifungo huko Zanzibar na kutoka jera mapema mwaka huu!
Alirudi uraiani kujiunga na jamii ingawa aliendelea na ukabaji!
Jitihada za kipolisi za kumuonya na kumsihi aachane na ukabaji zilifanyika lakini hakuwa msikivu!
Baada ya jitihada za kiungwana kugonga mwamba!
Kibaka mbooko aliuwawa katika majibizano mapema Mwezi uliopita kwa kupigwa na kitu kizito wakati akiwa katika majukumu yake ya ukabaji!
Alikuwa kibaka mwenye miraba minne, Ambaye alikuwa kero kubwa kwa wakazi wa Kigamboni!
Taarifa za uhalifu wake ziliwahi kuwa kero zilivyoripotiwa kila siku kwa matukio tofauti kiasi Cha kujaza REPORT BOOK (RB) ya polisi kila kuchwao akituhumiwa kuhusika na uharifu mbalimbali.
- Inaelezwa kwamba MBOKOO alikuwa na uwezo wa kukaba hata kikundi cha watu kwa mpigo akiwa peke yake.
- Kutokana umahiri wake wa ukabaji, inasadikika mwili wake ulikuwa hausikii maumivu anapopigwa ngumi, panga au risasi haikuwa rahisi kumuumiza
- Alisumbua sana makachero kumkamata kutokana na mbinu zake alizotumia kuwakwepa akisaidiwa na baba yake ambae alisadikika kuwa mshirikina.
- Kibaka MBOKOO aliwahi kuhisiwa kuhusika na tukio na uvamizi na uporaji wa hostel za wanafunzi waliokuwa wamepanga Midizini, Jambo ambalo lilizua taharuki kutokana na uporaji na ulawiti katika tukio hilo la kusikitisha!
- Kibaka MBOKOO Aliwahi kukamatwa na kufungwa Mara kadhaa lakini alipoachiwa hakuacha tabia yake ya ukabaji
- Aliripotiwa kukaba watu mbalimbali wakiwemo wanajeshi na kuwaumiza vibaya!
- Inasimuliwa Kuna wanajeshi wawili walivaa hijabu usiku wa manane ili wakutane na MBOKOO Wamkamate, lakini aliwazidi nguvu hawakufanikiwa!
- MBOKOO Alikuwa na mshipa wenye nguvu sana kiasi kwamba akikupiga ngumi utadondoka mbali mithili ya mdori uliopigwa ngumi!
- Uharifu wa MBOKOO Uliwahi kusumbua vichwa vya makachero kutafuta namna ya kumtia nguvuni.
- Doria ya kumsaka ilipamba Moto Sana enzi za kamishna Kova, kiasi kwamba siku moja KIBAKA. Huyo (MBOKOO) alionekana kwenye kivuko na wasamaria wema kureport haraka polisi ili akamatwe!
- Polisi waliwahi eneo la kivuko na kuamru kisiegeshwe ili wamtie nguvuni MBOKOO Haraka iwezekanavyo!
- Kwa jinsi alivyokuwa kero kibaka huyo, ilivutia hadi kamishna kutamani kumuona akitiwa nguvuni, lakini AMBUSHI Ile iligonga mwamba baada ya MBOKOO kujitosa baharini Kama sub Marine Ambapo alionekana kuibukia mbele na kuteka mtumbwi wa wavuvi kabla ya kutokomea Zanzibar!
- Lipongezwe Sana Jeshi la polisi kwa mtandao mpana Ambapo inasadikika walimkamatia huko Zanzibar kwa kusaidiana na wakojani!
- Zipo tetesi kwamba walimhasi na kumharibu kiasi Cha kupoteza nguvu zake za ukabaji .
- Tangu hapo Kigamboni ikawa shwari na salama; mwaka unaenda wa tano Kibaka MBOKOO hasumbui ni dhahiri alidhibitiwa, maana kwa Kariba yake hakustahili kufungwa maana angesumbua hadi wafungwa.
Updates June 2021
Kibaka mbokoo baada ya kumaliza kutumikia kifungo huko Zanzibar na kutoka jera mapema mwaka huu!
Alirudi uraiani kujiunga na jamii ingawa aliendelea na ukabaji!
Jitihada za kipolisi za kumuonya na kumsihi aachane na ukabaji zilifanyika lakini hakuwa msikivu!
Baada ya jitihada za kiungwana kugonga mwamba!
Kibaka mbooko aliuwawa katika majibizano mapema Mwezi uliopita kwa kupigwa na kitu kizito wakati akiwa katika majukumu yake ya ukabaji!