Mjinga mmoja wa IT ameniulia gari langu

Exactly..... Exaaaaactly!

Mchakato wa bima na ajali ni mrefu, costly, corrupt, exploitative and stressfull!

Mshana Jr. anachukulia mambo kirahisi rahisi anatuambia hatujui mambo ya BIMA eti jamaa a-relax kwa sababu kagongwa yeye, atalipwa na bima ya yule mwingine, vipi kama yule mwingine hana bima ?

Eti beak down tow truck ni bure siku ya ajali kwa vile ajali ni dharura hakuna aliyepanga. Basi wagonjwa wangetibiwa bure na maiti zisingeshikiliwa maana hakuna aliyepanga kuumwa wala kufa.
Mimi nimezungumzia mchakato ulivyo ..wewe unazungumzia madhaifu ya watendaji...hapo ndio ambapo hukuelewa
 
Hii ni Total Loss


Kama una bima kubwa chukua mpunga wote kanunue gari mpya , usichukue Salvage.
Sio wewe unaeamua "kuchukua mpunga wote."

Bima ndio inaamua kivyao, unilaterally.

Na hata wakikupa "mpunga wote," bado haitoshi kununua "gari mpya" kwa gharama ile uliyoagizia kutoka Japan.

Never ever!

Business machinations za makampuni ya bima sio rahisi kama Mshana Jr. anavyotaka kutuaminisha. Tunayo first hand experience.
 
Haijalishi.

Doesnt matter what kinda car it is. Mlolongo wa kupata fidia ya BIMA ya gari ni mrefu na wa kinyonyaji.
Mkuu,mwaka jana July nilipata ajalia maeneo ya kimara temboni,kuna boda alijichanganya nikamlamba,akavunjika mguu.Gari yangu ilipasuka taa,kioo na bampa la mbele,uzuri gari yangu nikitaka comprehensive.
Nikaanza kufuatilia documentations polisi pale Kiluvya,
asikwambie mtu ule mchakato ni mrefu,mgumu,unachosha sana,kila askari unayemfuata anakuomba rushwa,kwa kweli nilitoa rushwa tu ili nimalize ile mambo.
Sasa kama mtu unataka kufanya mchakato Kiparoko,paroko,nakuambia utachoma mafuta na muda hadi utashangaa.
Mambo polisi sio marahisi bila kutoa rushwa,huo ndio ukweli.
 
Sio wewe unaeamua "kuchukua mpunga wote."

Bima ndio inaamua kivyao, unilaterally.

Na hata wakikupa "mpunga wote," bado haitoshi kununua "gari mpya" kwa gharama ile uliyoagizia kutoka Japan.

Never ever!

Business machinations za makampuni ya bima sio rahisi kama Mshana Jr. anavyotaka kutuaminisha. Tunayo first hand experience.
Kuna mahesabu yao ikiwemo depreciation charges huwa wanapiga,utashangaa hapo jamaa bima wanamlipa 5M tu kama gari ni white off..
bima hawalipi tu hovyo hovyo...
 
Sema gari inapona hiyo vitu vyote vipo ilala hapo watafute wataalamu wa kunyosha body Ila nunua hivyo vitu sijui fender zote bonnet,taa,shocks,radiator inarudi road yupo jamaangu aligonga ng'ombe na Benz yake ilikua chakavu mbele lakini ilivyorudi utadhani haikupata ajali ila kanunua vitu vyote maana ina bonnet ya aluminium haikubali kunyooshwa ni ya 2018 ila hela imetoka aisee...
Aligonga ng,ombe maneno ya tanga kuja Dar au kwenda Arusha Moshi January nilionaga ngo,mbe kagongwa road ndo yy nn

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mahakamani kesi inakaa muda gani, na kipindi hicho unatumia usafiri gani na wakili wako analipwa na nani? Na nani anai tow gari kutoka njia panda Dodoma kuipeleka garage karibu na unakoishi ili uweze kuifuatilia kama BIMA wataamua kui fix?

Ajali sio suala rahisi kama unavyomwambia eti arilaksi!

Police report yenyewe unaweza kuifuatulia mwezi mzima wanajidai polisi mhusika yuko msibani, wanataka rushwa.

Na gereji za Wachina nazo (supposed to be the best of all) usidhani wako profesheno kiviiiile, wanahitaji kuwafuatilia kama garage zetu za Kiswahili.
Nakuelewa Sana Mwanangu Nilishawahi Kugonga Bodaboda Na Abiria Wake kule Unga Limited Kipindi, Niko Arusha, Hakuna Rangi Niliacha ona, Watu Wanadhani Ni Rahisi Hivyo, Mtu Mzima Nilimwaga Hadi Chozi kwa Mkuu Wa Traffic ndio Kupewa Gari Yangu
 
Nakuelewa Sana Mwanangu Nilishawahi Kugonga Bodaboda Na Abiria Wake kule Unga Limited Kipindi, Niko Arusha, Hakuna Rangi Niliacha ona, Watu Wanadhani Ni Rahisi Hivyo, Mtu Mzima Nilimwaga Hadi Chozi kwa Mkuu Wa Traffic ndio Kupewa Gari Yangu
Ndio hapo sasa, namshangaa huyu Mshana Jr, ....kwenye mambo ya kufuatilia bima za ajali kuna ku relax ???

Mimi kesi yangu polisi anaeandika maripoti aliniomba nichangie ujenzi wa kanisa lao
 
Ndio hapo sasa, namshangaa huyu Mshana Jr, ....kwenye mambo ya kufuatilia bima za ajali kuna ku relax ???

Mimi kesi yangu polisi anaeandika maripoti aliniomba nichangie ujenzi wa kanisa lao
Hahaa ujenzi wa kanisa tena.
Ila mkuu mchakato wa bima hadi ulipwe tena hyo third party asee kuna mlolongo sana.
Ni mpaka upate hiyo court judgement halafu kwenye kufatilia hyo lazima ofisa mpelelezi ale hela ndio uipate tena kwa kusubiri mwezi au miezi 2 bado hapo hujaenda bima kwenyewe.
 
Nakuelewa Sana Mwanangu Nilishawahi Kugonga Bodaboda Na Abiria Wake kule Unga Limited Kipindi, Niko Arusha, Hakuna Rangi Niliacha ona, Watu Wanadhani Ni Rahisi Hivyo, Mtu Mzima Nilimwaga Hadi Chozi kwa Mkuu Wa Traffic ndio Kupewa Gari Yangu
Ndio hapo sasa, namshangaa huyu Mshana Jr. huyu...

Kwenye ajali na kufuatilia bima kina ku relax ???

Mimi kesi yangu polisi aliyekuwa anashughulikia paperwork za ajali linambia nimchagine ujenzi wa kanisa lao
 
Pole sana mkuu,ndio maana wazee wenye hekima zao wanashauri kama una hela ya mawazo usinunue gari,kwani unaweza ukafa kwa presha bure...
Kuna brother angu kanunua roli halijamaliza hata wiki limepiga chini,juzi naongea nae sauti kama mgonjwa vile,
 
Back
Top Bottom