Mjengwa na huruma ya mauji mbalali hivi ni kweli??

makongorosi

Member
Apr 24, 2009
49
3
Wanajamvi nimekutana, na habari iliyotolewa na ndugu Mjengwa ktk gazeti la rahia mwena yenye kichwa cha habari 'Mbalali wafe wangapi ndiyo serikali isikie kilio chao?.
Ndugu zangu mimi siamini kabisa kama kweli huyu ndugu mjengwa ana uchungu wa dhati kuulizia swala la mauji mbalali ili hali akijua kabisa wahusika ni kinani na yeye ndiye mmoja wapo aliyechangia waingie madarakani ili waendeleze uuaji wao.
Hakuna asiyejua kuwa kuna mauji mengi zaidi ya mbalali kila siku yanatokea lakini chanzo ni hii serikali liyopigiwa debe na bwana mjengwa. Mjengwa amesahau kuwa kuna watu wengi wanakufa kwa kukosa matibabu mahospitalini kwa sababu ya ufisadi wa watu wachache waliopo madarakani ambao walipigiwa debe na ndugu mjengwa.
Mjengwa amesahau kuwa kuna watu wanajinyonga kwaajili ya kukata tamaa jinsi maisha yalivyokuwa magumu kwani kuna watu hawana uhakika wa mlo hata mmoja.Mjengwa amesahau kuwa kuna baba aliyejinyonga baada ya kushindwa kumpeleka mtoto shule ili hali kuna viongozi wa ccm wanaosemesha watoto nje ya nchi kwa fedha za ufisadi ambazo kumsomesha mtoto mmoja wa kigogo nje ni sawa na kusomesha karibu watoto 200 tanzania.

Mjengwa amepungukiwa na kumbukumbu kwa wananchi wa vijijini wanaojifunglia njiani huku wengine wakipoteza maisha kutokana na kusafiri mbali kwenda kupata huduma ya uzazi ili hali pesa za kununu uongozi zikiwepo na we mjengwa ukipiga makofi na kuwapongeza.
Mjengwa umesahau Tabaka kubwa la wenye nacho na wasiokuwa nacho, kiasi kwamba wasio nacho wamekata tamaa na kuamua kutumia njia ya mkato kuuwa watu kwa kuwa sera mbovu za ccm zimeshindwa kuondoa umaskini. Hawa wote wanaokufa kwa kuvamiwa umefumba macho na kuona kama ni mauji??
Mjengwa umesahau jinsi matrafiki wanaowekwa na vigogo wanavyochukua rushwa na kushindwa kusimamia vyema sheria za barabarani hivyo kusababisha ajali zisizo za razima kwa watanzania wengi kila kukicha kupoteza maisha. Kutokana na ccm na serikali yake kushindwa kudhibiti rushwa imebidi trafiki kuruhusu vyombo vya usafiri visivyo na viwango hivyo kuongeza idadi ya watu wanaokufa kila siku barabarani.
Yapo mengi tu yanayonifanya niamini kuwa bwana mjengwa hana uchungu wa dhati kwa raia wa tanzania kumetokea mauji Arusha watu wamepoteza maisha na mjengwa kimya au kwakuwa walikuwa wanachadema hivyo hukuweza kuuona uchungu??
Ndugu mjengwa mauji yapo mengi sana Tanzania, ukichambua kwa undani chanzo chake ni ccm na serikali yake ambapo wewe mpiga debe wao.
 
Ndugu mjengwa mauji yapo mengi sana Tanzania said:
Ndg yangu ukiandika thread jitahidi kuipitia na kuhariri makosa ya kiuandishi kabla ha kutuma. Pamoja uzuri wake, thread yako ina makosa mengi sana ya spelling.

Kuhusu hoja unayoandika, hivi Mjengwa ni jiwe lisilobadilika? Inawezekana ni kweli kuwa wakati wa kampeni aliipigia debe ccm na huenda vilevile alipewa chochote na viongozi wa hicho chama, kama wengi wetu tulivyoamini, lakini si vibaya kuamini vilevile kwamba sasa huenda amebadilika. Na hata kama hajabadilika, je,akae kimya anapoona watanzania wenzie wanapigwa risasi na kuuawa kwa sababu zisizo za msingi!!??

Ushauri wangu kwako ni kwamba usimchukie mtu kwa kiwango kinachopitiliza ubinadamu na uwe tayari kuamini kuwa mwenzio amebadilika. Inawezekana Mjengwa aliamini kuwa ccm ni bora kuliko vyama vingine lakini sasa kwa kuangalia mwenendo wa nchi, kiuchumi, kisiasa na kijamii, imani yake hiyo imeanza kupungua.

Sisi tunaoamini katika NGUVU YA UMMA lazima tumkaribishe tena kwa shangwe na vifijo.
 
Nashukuru kwa ushauri wako ndugu Gosbertgoodluck wa kuhariri habari kabla ya kutuma , lakini kweli nimeamini msemo unaosema nyani haoni kundule ebu tazama hapo chini kweli umehariri habari yako?, badala ya kutumia neno ya umetumia neno ha. lakini kwa kwa mimi sijali ili mradi nimeelewa maudhui ya ujumbe wako.



Ndg yangu ukiandika thread jitahidi kuipitia na kuhariri makosa ya kiuandishi kabla ha kutuma. Pamoja uzuri wake, thread yako ina makosa mengi sana ya spelling.

Kuhusu hoja unayoandika, hivi Mjengwa ni jiwe lisilobadilika? Inawezekana ni kweli kuwa wakati wa kampeni aliipigia debe ccm na huenda vilevile alipewa chochote na viongozi wa hicho chama, kama wengi wetu tulivyoamini, lakini si vibaya kuamini vilevile kwamba sasa huenda amebadilika. Na hata kama hajabadilika, je,akae kimya anapoona watanzania wenzie wanapigwa risasi na kuuawa kwa sababu zisizo za msingi!!??

Ushauri wangu kwako ni kwamba usimchukie mtu kwa kiwango kinachopitiliza ubinadamu na uwe tayari kuamini kuwa mwenzio amebadilika. Inawezekana Mjengwa aliamini kuwa ccm ni bora kuliko vyama vingine lakini sasa kwa kuangalia mwenendo wa nchi, kiuchumi, kisiasa na kijamii, imani yake hiyo imeanza kupungua.

Sisi tunaoamini katika NGUVU YA UMMA lazima tumkaribishe tena kwa shangwe na vifijo.
 
Back
Top Bottom