Mjasiliamali hakai mbali na fulsa katika mipango ya maisha yake.

mrpeople

Senior Member
Aug 3, 2019
132
113
Amani ya Bwana Mungu iwe nanyi wapendwa.
Katika maisha kujitambua na kufikiria kuwa unahitaji kuwa nani huwa inasaidia sana na haswa ukiwaza uzao wako unataka uwaje kimaisha.

Niwaombe radhi ambao kwa namna moja au nyingine huwa hawapendi sana kujadili taswira za maisha yao baadae au baada ya uzee.
Wapendwa huu ni msimu wa mvua karibia mikoa yote Tanzania na kila mkoa kuna kila aina ya fulsa ambazo nyingi bado hatujaziona na kama tumeziona basi hatujaamua kuzikimbilia huenda kwa kuzitambua au kutozitambua. Mfano, vijana wenzangu tunaotokea mikoa ya Iringa, Njombe, Tanga, Arusha, Mbeya nk. Mikoa tajwa inafulsa za kilimo cha miti, ndizi, mahindi nk na ardhi iwe ya urithi au ya kununua inapatikana.

Ombi langu vijana kama unafanya kazi omba ruhusa au chukua likizo msimu huu nenda kalime, kapande miti, kapande migomba ya kutosha au zao linalopatikana kwenye eneo ambalo upo familia nalo, panda mazao ya mda mfupi na pia panda mazao ya mda mrefu na hakikisha unayatunza na kuyalinda kwa gharama yoyote ile.

Vijana huu ndo mda wa kuuandaa uzee wako huko mbeleni uweje. Tuache tabia za kuangalia mali za wazazi bali tutafute mali zetu kwa bidii na Mungu atabariki mazao ya mashamba yetu, tuache kuchukua likizo au ruhusa za misimu ambayo haina uzalishaji na kuishia kuuza sura tu kula kulala.

Mwisho ombeni sana kuwa na afya na tujitunze ila tusisahau kuwa wewe ni baba wewe ni mama je unatamani uje uishi maisha gani na familia yako au uzeeni mwako.

Mda ndo huu jiulize unataka uje uishi maisha gani huko mbeleni??? Tumia afya yako sasa kutafuta neema ya uzeeni.

Mungu awabariki sana kwa kila wazo jema ambalo unahitaji kulifanya mkono wa Bwana usikupungukie.
 
Mkuu, naona umeandika tu kana kwamba hayo mashamba kila mmoja anayo na yapo tu.....
Yaani umeandika kana kwamba kila unae msahauri hapa, likizo yake ni msimu huu wa mvua ama anajichukulia tu likizo atakavyo....
Naona umeandika tu kana kwamba unao washauri wanazo fedha tu mfukoni, kiasi cha kutekenya tu kisha waende likizo, shambani na waandae maisha yao ya uzeeni.....

Yes, nina tambua kwamba afya ni kitu cha kutunza zaidi hasa kwenye kipindi cha ujana. Vipi wale ambao maradhi na ulemavu umewajeruhi ikingali wakiwa vijana...!!??
 
Mkuu, naona umeandika tu kana kwamba hayo mashamba kila mmoja anayo na yapo tu.....
Yaani umeandika kana kwamba kila unae msahauri hapa, likizo yake ni msimu huu wa mvua ama anajichukulia tu likizo atakavyo....
Naona umeandika tu kana kwamba unao washauri wanazo fedha tu mfukoni, kiasi cha kutekenya tu kisha waende likizo, shambani na waandae maisha yao ya uzeeni.....

Yes, nina tambua kwamba afya ni kitu cha kutunza zaidi hasa kwenye kipindi cha ujana. Vipi wale ambao maradhi na ulemavu umewajeruhi ikingali wakiwa vijana...!!??
duuh
 
Amani ya Bwana Mungu iwe nanyi wapendwa.
Katika maisha kujitambua na kufikiria kuwa unahitaji kuwa nani huwa inasaidia sana na haswa ukiwaza uzao wako unataka uwaje kimaisha.

Niwaombe radhi ambao kwa namna moja au nyingine huwa hawapendi sana kujadili taswira za maisha yao baadae au baada ya uzee.
Wapendwa huu ni msimu wa mvua karibia mikoa yote Tanzania na kila mkoa kuna kila aina ya fulsa ambazo nyingi bado hatujaziona na kama tumeziona basi hatujaamua kuzikimbilia huenda kwa kuzitambua au kutozitambua. Mfano, vijana wenzangu tunaotokea mikoa ya Iringa, Njombe, Tanga, Arusha, Mbeya nk. Mikoa tajwa inafulsa za kilimo cha miti, ndizi, mahindi nk na ardhi iwe ya urithi au ya kununua inapatikana.

Ombi langu vijana kama unafanya kazi omba ruhusa au chukua likizo msimu huu nenda kalime, kapande miti, kapande migomba ya kutosha au zao linalopatikana kwenye eneo ambalo upo familia nalo, panda mazao ya mda mfupi na pia panda mazao ya mda mrefu na hakikisha unayatunza na kuyalinda kwa gharama yoyote ile.

Vijana huu ndo mda wa kuuandaa uzee wako huko mbeleni uweje. Tuache tabia za kuangalia mali za wazazi bali tutafute mali zetu kwa bidii na Mungu atabariki mazao ya mashamba yetu, tuache kuchukua likizo au ruhusa za misimu ambayo haina uzalishaji na kuishia kuuza sura tu kula kulala.

Mwisho ombeni sana kuwa na afya na tujitunze ila tusisahau kuwa wewe ni baba wewe ni mama je unatamani uje uishi maisha gani na familia yako au uzeeni mwako.

Mda ndo huu jiulize unataka uje uishi maisha gani huko mbeleni??? Tumia afya yako sasa kutafuta neema ya uzeeni.

Mungu awabariki sana kwa kila wazo jema ambalo unahitaji kulifanya mkono wa Bwana usikupungukie.
Umeongea sahihi kabisa, vijana tunatakiwa tuwekeze sana katika ardhi.
Kuna watu wameshaanza kupinga kwa kutoa post uchwara, ila me binafsi naona uko sahihi sababu kuna mikoa hapa Tanzania unapata shamba zuri la kilimo ekari kwa laki moja tu
 
Sijalazimisha bali ushauri kwa mwenye chanzo au fulsa hiyo, huenda hujanielewa ukajiangalia wewe na ukawasemea wengine.

Kuna watu wanayo mashamba hawana hela ila afya ipo vizuri basi watumie afya zao kama fulsa sio lazima uwe na vibarua maana tunasema kuwa na afya njema ni fulsa kubwa sana.

Likizo, mara nyingi ukitoa walimu ambao likizo zao zipo fixed kada nyingine hasa za serikali na baadhi ya private likizo unaamua mda wa kuomba.

Mwisho katika maisha usipende sana kuwakatisha tamaa wenzako bali watie moyo katika kudhubutu.

Amini usiamini kitendo cha kuwakatisha tamaa wenzako kwa namna yoyote katika kutimiza jambo jema Mungu atakupiga mda na wakati wowote
Mkuu, naona umeandika tu kana kwamba hayo mashamba kila mmoja anayo na yapo tu.....
Yaani umeandika kana kwamba kila unae msahauri hapa, likizo yake ni msimu huu wa mvua ama anajichukulia tu likizo atakavyo....
Naona umeandika tu kana kwamba unao washauri wanazo fedha tu mfukoni, kiasi cha kutekenya tu kisha waende likizo, shambani na waandae maisha yao ya uzeeni.....

Yes, nina tambua kwamba afya ni kitu cha kutunza zaidi hasa kwenye kipindi cha ujana. Vipi wale ambao maradhi na ulemavu umewajeruhi ikingali wakiwa vijana...!!??
 
Mkuu mi nawaza kuwekeza japo sina mtaji ila mtaji wa afya niliyonayo naamini ntafika ninapotaka kufika eeeh mwenyezi Mungu bariki mawazo, malengo na vitendo vyangu katika kuwekeza
At least hujaandika kuhusu mapenzi...
 
Back
Top Bottom