Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,441
- 7,780
Mke wa bilionea, marehemu Reginald Mengi ameendelea kukumbana na vigingi vya sheria baada ya mahakama ya rufaa kuondoa maombi yake ya kupinga uamuzi uliobatilisha wosia wa mwisho wa marehemu Reginald Mengi.
Mahakama imekubali hoja za upande wa watoto wakubwa wa marehemu na kubaini viapo vilivyoletwa na Jacquline Mengi na wakili wake vina makosa.
May mwaka huu Jaji Yose Mlyambina wa mahakama kuu aliukataa wosia unaodaiwa kuandikwa na Reginald Mengi kwa madai haukufata misingi ya kisheria.
Watoto wakubwa wa Reginald Mengi walipinga wosia huo wakisema baba yao hakuwa kwenye nafasi ya kuandika wosia kwasababu alikuwa anakabiliwa na matatizo makubwa ya kiafya tangu 2016.
Familia ya Dkt. Mengi ipo kwenye mgogoro mkubwa wa kisheria juu ya mirathi ya marehemu ambao ulianza punde baada ya kifo chake huku ndugu zake wakitaka kuteuliwa wasimamizi wa mirathi.
Hukumu iliyopita, jisomee=> HAPA
Mahakama imekubali hoja za upande wa watoto wakubwa wa marehemu na kubaini viapo vilivyoletwa na Jacquline Mengi na wakili wake vina makosa.
May mwaka huu Jaji Yose Mlyambina wa mahakama kuu aliukataa wosia unaodaiwa kuandikwa na Reginald Mengi kwa madai haukufata misingi ya kisheria.
Watoto wakubwa wa Reginald Mengi walipinga wosia huo wakisema baba yao hakuwa kwenye nafasi ya kuandika wosia kwasababu alikuwa anakabiliwa na matatizo makubwa ya kiafya tangu 2016.
Familia ya Dkt. Mengi ipo kwenye mgogoro mkubwa wa kisheria juu ya mirathi ya marehemu ambao ulianza punde baada ya kifo chake huku ndugu zake wakitaka kuteuliwa wasimamizi wa mirathi.
Hukumu iliyopita, jisomee=> HAPA