Kigamboni hapafai au sehemu ya barabara ndo haifai?Kama unasikia maajabu ndiyo haya!
Daraja la kigamboni lililojengwa Kwa mabilioni ya Pesa! Daraja lililojengwa Kwa Nondo za kuagiza toka nje, daraja ambalo huvuki mpaka ulipie!
Maungo ya barabara yake baada ya daraja ni mabovu haijawahi tokea! Barabara ina mashimo na madimbwi kiasi kwamba hata kutembea Kwa miguu haifai!
Nimetoka kigamboni sahivi na kikirikuu changu shock-up zote hazifai;
Ni mambo ya ajabu sana sehemu ambapo ni uso Wa nchi kama daraja ni panakuwa pabovu namna hiyo kama vile nchi haina viongozi!
Inamaana wameshindwa hata kutia mafta greda likasawazisha watu wapite? Kutwa kukusanya road license za magari lakini barabara ni mbovu! Mbovu, mbovu kila mahali!
Sijui nini cha kujivunia Tanzania, kila mahali kero tupuuu!
(HATA UWANJA WA TAIFA MVUA IKINYESHA MTU ALIYEKAA V.I.P ANANYESHEWA NA MVUA)
Njia zoote kuanzia mitaa hadi njia kuu kuna mashimo tupu ! Sijui serikali iko wapi!
" haya ndiyo matokeo ya kuongozwa na watu wanaojuwa kusoma na kuandika"
Mmenitia hasara ya kununua tena shock-up ovyo kabisa nyie watu!