Malunde-Malundi
JF-Expert Member
- Jan 10, 2008
- 1,288
- 130
mkenya aomba watz kuwe na tume ya taifa ya kubadilisha katiba kutenganisha mamlaka ya bunge/mahakama/mamlaka
Yahya M,
Tanesco wameshafanya vitu vyao. Hata hivyo mchango wangu ni huu:
Power separation haipo kwenye katiba ya sasa, natoa mifano miwili:
1. Kazi mojawapo ya Bunge ni kuisimamia serikali, mawaziri wote wanapokuwa wabunge, mathalani wakiwa bungeni wanakuwa ni sehemu ya bunge au serikali? Nani anamsimamia mwenzake??
2. Kazi mojawapo ya Bunge ni kutunga sheria, lakini sheria nyingi zinatungwa na serikali na kupelekwa bungeni kama muswada na bunge likipitisha bado muswada hauwi sheria mpaka rais ausaini. Hapa anayetunga sheria ni nani? Bunge si kama rubber stamp?? Na kama sheria hiyo ni ya uhalifu na mahakama ikamtia mtuhumiwa hatiani na anapaswa kunyongwa, hawezi kunyongwa mpaka rais asaini. Uhuru wa mahakama uko wapi??
QUOTE=DENYO;
Asante kwa kusoma maoni yangu kama nilivyoandika.
Lakini amechakachua hoja yako kwa kutosoma hoja ya Celina Kombani na Mkwere.
YAHYA M.
Asante kwa kusoma maoni yangu kama nilivyoandika ninaomba mchakato huu uendelee moja kwa moja i can now trust you guys -big up.
mkenya aomba watz kuwe na tume ya taifa ya kubadilisha katiba kutenganisha mamlaka ya bunge/mahakama/mamlaka
Ukisema elimu ya ulazima una maana gani.Labda ungefafanua.Hata hivyo mjadala wa muda mfupi kiasi hicho hauzi kusaidia kutoa elimu,kwanza wangapi wana TV?Elimu ya uraia kwa ujumla inahitajika.Swali ni kwamba nani atatoa elimu hiyo?Lakini jambo la msingi hapa ni kwamba swala la katiba kwa serikali makini sio la kusukumwa sukumwa,kupangiwa mijadala nk.Ni issue ya kutekelezwa kwa wakati.Huu sio wakati wake,swala hili limepitwa na wakati sana.Lilipashwa kutekelezwa siku nyingi sana.Serikali ya kikwete ikae na wadau wote ili tupate katiba mpya haraka.Mambo mengi yanakwenda hovyo kwa sababu ya katiba tuliyo nayo.It's so irrelevant to our situation.
Yahya,
Mara nyingi tunashuhudia viongozi wetu wakiiweka ajenda ya katiba kisiasa zaidi, na tena hujiri pale tu kuwapo na mpenyo fulani wa kuibukia kisiasa au kujilinda kisiasa kwa nafasi zao (nje ya chama tawala)hususan katika chaguzi ndogo, chaguzi kuu, mipasuko ya kisiasa itokeapo ama katika chaguzi za ndani ya vyama vya siasa ndipo mambo haya muhimu huwa na nafasi. Ni vema tukajijengea utamaduni mahsusi sasa wa kuyazungumzia masuala muhimu na nyeti ya kitaifa kwa kupata maoni ya wananchi na kuyaheshimu ikiwemo katiba ya nchi yetu.
Lakini je! Ni kweli watanzania tunasubiri mpaka kuwepo na jambo fulani ndipo tudai katiba yetu ibadilishwe? Ama je! Tunahitaji katiba ibadilishwe pale tu wanasisa tunaowahusudu wanaposhindwa katika jambo fulani ndipo dai la katiba mpya lichomoze?
Binafsi nadhani jibu ni HAPANA, tusigeuze suala la katiba liwe kama UA (flower) huchomoza na kusinyaa. Bali suala la katiba ya nchi yapaswa kuwa ni jambo kuu la kitaifa kwa mustakabali mzuri wa ustawi wetu na vizazi vyetu, iwapo hatutakuwa na njia bora za kusikiliza wananchi tunataka nini (kupitia maoni) basi yaweza kuwa ni hasara kubwa tena yenye matokeo yenye mlengo wa uvunjifu wa amani siku za usoni.
Tumeshuhudia tume HALALI zikiundwa na serikali katika kutoa maoni ya wananchi juu ya mambo muhimu ikiwamo katiba, mfano wa tume hizo ni ile ya hayati Nyalali na ile ya jaji Kissanga. Matokeo ya wananchi kupitia tume hizi mbili tena kwa nyakati tofauti ilikuwa ni dhihirisho tosha sana kutambua nini chapaswa kufanywa na watawala katika kuheshimu nguvu ya wananchi juu ya marekebisho ya katiba mpya. Siku ya uhuru mwaka huu mzee wetu balozi H.Mbitta akiwa katika mahojiano ya moja kwa moja na kituo fulani hapa nchini alitoa angalizo la mahitaji ya katiba mpya, akifafanua kwa kusema katiba iliyokuwepo haikidhi hali ya sasa ya wananchi na ujumla wake. Rais mstaafu nae amepata kutoa tamko lenye mlengo wa hitajio la katiba mpya, alitoa angalizo hilo hivi karibuni katika moja ya khotuba yake iliyosomwa na balozi Mulamula(kama sijakosea jina hili). Hizi zatosha kuwa ni ishara za viongozi wastaafu wa nchi hii wakihitaji mabadiliko ya katiba ambapo wanaona umuhimu huo baada ya kungatuka madarakani.
Hapa nchini hakuna jitihada za makusudi za kudai katiba mpya, imekuwa ikisomeka kwa wanasiasa mbalimbali wakitoa hoja za kudai katiba mpya kwa kila mmoja kivyake,,hakuna muunganiko wa nguvu ya pamoja na kutoa tamko hata ikibidi maandamano rasmi ya kudai katiba mpya,,na ikibidiiiii ..kuwepo na hamasa miongoni mwa viongozi kushinikiza nchi nzima kufanya maandamano ya amani katika kufikisha ujumbe murua kwa walengwa ili hatua mbadala kuchukuliwa na hatimae kuzaa tena matunda kwa njia ya MAONI YA WANANCHI kwa kudai katiba mpya
Tunahitaji katiba mpya kwa ustawi wa taifa letu na rasilimali zake kiujumla.
NAWAKILISHA !!!
Umeliona hilo mkuu, hii ni changamoto kubwa kwa serikali yetu kutambua kuwa THE WORLD IS WATCHING
Shukrani kwa Mchango wako
Yahya
and this time is not perfect at all washauri wenzako na management muanzishe tuongee mchana au hata jioni this time especiall sundays watu wamepumzika au wengine wako church, na baadhi wamelala because of previous day hangovers
Shukrani, muda umekaa vibaya kweli, wengine tutakuwa church!
Ahsante,
Nchi yetu inaingia nusu karne punde huku tukiwa na katiba iliyotengenezwa mahsusi kwa watu mili.9 tu, hivi sasa nchi yetu ina takriban watu mil.42.
Katika muundo wa katiba tuitumiayo...kiujumla haikidhi hali ya wananchi kwa sasa ktika nnyanja zote za kiutawala, kiulinzi, kiuchumi, kijamii na hata kisiasa bali katiba hii iliyopo ni mahsisi kwa ajili ya wachache tu na wananchi ni kama wanaburuzwa na watawala.
Nchi yetu ni kisiwa cha amani, amani hii ni asili ya wananchi wa Tanzania, Wananchi wanapodai katiba mpya si kwa tamaa ya mambo fulani wategemeayo kimaslahi...bali ni katika mustakabali wa jamii iliyopo na maendeleo yake kiustawi wa ujumla. Haitoingilika akilini katika jamii ya wastaarabu watanzania ifikie hatua ya kudai katiba mpya kwa vurugu na kuvunja amani iliyopo ilhali ni jambo muhimu kwa ustawi wa taifa letu na raia wake, tuepushe yanayojiri nchi za wenzetu bali tuwe na angalizo jema kwa nchi yetu
Wananchi tumelalamika juu ya katiba, viongozi wastaafu serikalini wamelalama juu ya katiba, wanasiasa wanalalama juu ya katiba...JE TUSUBIRI NA HAWA WALIOPO MADARAKANI WAKISHASTAAFU NAO WAANZE KUDAI KATIBA KWA WARITHI WAO? KWA NINI ISIWE SASA?
Itapendeza watawala ifike muda sasa walione kwa macho mawili suala zima la katiba, wananchi wanataka nini ili kuweka misingi imara na madhubuti kwa muendelezo mwema wa taifa letu,,MABADILIKO YA KATIBA KWA SASA HAYAKWEPEKI...ILA KWA WENYE UCHU FULANI HAWAONI MANTIKI YA MABADILIKO YA KATIBA YA TANZANIA KWA SASA.
Nichukue fursa hii kuwashukuruni sana wanaJF wote walioshiriki katika mada hii, Mawazo na michango ilikuwa mingi na muda wetu studio ni mfinyu ila tumejitahidi kwa uwezo wetu kuyatumia mawazo yote kama yalivyo. Wiki ijayo tunakusudia tena kuwa mjadala juu ya Katiba sehemu ya pili. Na safari hii kwa kwenda hatua nyingine ya kuwashirikisha Jaji Joseph Warioba na Profesa Shivji na waandishi wa Habari wakomavu Jijini Mwanza. Litakapopata baraka za kiofisi na taratibu kukamilika kwa mialiko hiyo na uthibitisho tutawajulisha wanaJF.
Nashukuru sana kwa sauti zenu kwa Umma
Pamoja tutaleta Chachu ya Mabadiliko katika Taifa letu kwa masilahi ya Umma.
Jumapili Njema
Yahya M
Kwani katiba ya sasa haitoshi?
Ingekuwa vizuri akaleta mjadala wa kuleta maendeleo Tanzania