Hmaster
JF-Expert Member
- Dec 27, 2010
- 346
- 86
Tangu kuanza kwa hili la madai ya katiba mpya ambayo ndiyo itakuwa dira yetu watz wote, naona kemekuwa na upinzani mkubwa mno kutoka kwa watawala. Ukifuatilia utagundua ya kwamba jamii nzima inakubali kwamba katiba ya sasa imepitwa na wakati na kwamba kinachotakiwa ni kuandikwa kwa katiba mpya. Sasa hawa jamaa wenye dola wana maslahi gani na katiba ya sasa hadi waing'ang'anie tu hiyohiyo? Naomba tulijadili hili kwa pamoja wana JF!