Mjadala: Upinzani utaanzaje kujipanga kwa uchaguzi wa serikali za mitaa wa 2024 na hatimae uchaguzi mkuu wa uraisi wa 2025 ndani ya mazingira magumu?

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,934
20,372
Lengo la mada hii ni kuona wale wapenda demokrasia na siasa za kweli wakijongea hapa na kushusha nondo na madini mbalimbali katika kufanya kitu chitwa "brain storming".

Katika muktadha huo basi, tutaweza kuangalia sera za chama cha CCM ambacho ndicho chaongoza serikali ya Tanzania kwa sasa na pia ilani ya chama hicho na utekelezaji wake na wapi wamefikia.

Pia mada hii itatoa fursa ya kuangalia hali ya uchumi wa Tanzania kati ya 2015 na 2021 na baada ya hapo ni wapi tumekwama, sababu za kukwama na nini kifanyike kwa maana ya kwamba je, serikali ina washauri wanofaa wa uchumi "Think Tanks", taasisi binafsi za kuchambua sera za kiuchumi na wadau mbalimbali na nini nafasi yao katika kuishauri serikali katika nyakati ngumu au nyakati tata.

Hali kadhalika mada itakaribisha maoni ya upinzani, hali yake kisiasa, uwezo wake wa kuendeleza harakati na nini kifanyike ili kuleta chagizo ambalo litaweza kutikisa hali ya kisiasa nchini hususan CCM.

Hakika uchaguzi wa Kenya umetoa funzo kubwa kwa wale wanofuatilia harakati za kisiasa na kutufumbua macho wengi wetu kuwa kweli Wakenya wana demokrasia ya kweli.

Lakini kuna mambo matatu makubwa ambayo ndiyo yaliyonichagiza kuamua kuanzisha mada hii.

Kwanza, ni Tume Huru ya Uchaguzi ya Kenya ambayo imeonyesha hali yake ya kuwa yajitegemea, ni huru na haina mashinikizo kutoka sehemu yoyote ile. Tume ikatangaza ushindi wa Rais Ruto licha ya kwamba Rais aliyepita Bwana Uhuru Kenyatta alikuwa waziwazi akimuunga mkono Bwana Raila Odinga. Hata humu JF yumo mwenzetu mmoja na wengine kadhaa ambao walionyesha kuumunga mkono Bwana Odinga.

Bwana Odinga alipinga matokeo hayo kwa kudai kulikuwa na mizengwe ya udanganyifu na mwishowe mahakama uamuzi wa kuthibitisha ushindi wa Bwana Ruto, uamuzi ambao wapiga kura wengi wa Kenya waliukubali kuwa ulikuwa wa haki na ukweli.

Lakini ushindi wa Rais Ruto ulionyesha kuwastua wana CCM na wafuasi wao kwani katika uchaguzi wa Kenya hakukuwepo na ahadi ya goli la mkono.

Hii dhana ya goli la mkono ni kuthibitisha kuwa CCM ni chama dola na kina uwezo wa kuamua kuwa madarakani kwa muda wowote ambao chama hicho kitapenda kukaa na chaguzi zote zitaamuliwa na wao kwa kutumia vyombo vya dola.

Pili, wenzetu Wakenya uchaguzi wao ulikuwa na maandalizi ya kutosha, kuanzia wapiga kura kujiandikisha hadi kila kituo cha kupigia kura kuwa tayari kimepokea fomu zote za kupigia kura.

Moja ya sababu kubwa ya hapa ni uwezo wa wagombea wa upinzani kuweza kuchukua fomu au kujiandikisha uzuri kituoni salama bila kubughudhiwa na kuthibitishwa na kisha kuketi mahala au kwenda nyumbani kusubiri matokeo salama.

Hali nyingine ni kwa vituo vya kupigia kira kuendelea kupokea wapiga kura na kufungwa mara tu na inapothibitika kwamba wapiga kura wote wa CCM na vyama vingine wametumia haki yao hiyo ya kikatiba kufanikisha zoezi hilo.

Tatu, mitandao ya "internet" ni muhimu sana katika nyakati za uchaguzi na husaidia taasisi kama tume ya uchaguzi kufanya kazi zake kwa ufanisi zaidi kwa kuweka fomu za kujiandikisha katika tovuti yake ambapo wapiga kura wataweza kunywila fomu hizo kwa haraka na kuzirudisha vituoni bila kuchelewa.

Pia hiyo itasaidia kuwawezesha wapiga kura kufuatilia matokeo ya uchaguzi mitandaoni bila kusubiri kwa muda mrefu. Pia mitandao itasaidia kurahisisha mawasiliano baina ya watanzania waliopo maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi bila kuzuiwa wala kukwamishwa.

Hayo mambo matatu ndiyo yamechangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha uchaguzi wa hawa majirani zetu jambo ambalo ni la kujivunia kwao na kulitamani hapa kwetu Tanzania.

Sasa basi, Tanzania yaelekea kufanya Uchaguzi wake Mkuu wa Urais mwaka 2025 na kabla ya hapo utakuwepo uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024. Jambo la msingi ambalo CCM na serikali yake yapaswa kufanya ni kutorudia hali ya mwaka 2019 ambapo vyama vya siasa baada ya kukaa pembeni kwa miaka mitatu hadi minne ndiyo vikaja kushiriki uchaguzi.

Jambo jingine ni CCM na serikali yake kuhakikisha wapinzani hawapati bughudha kutoka kwa vyombo vya dola hasa Polisi na Usalama wa Taifa.

Wakati sasa umefika wa wapinzani kuamua kuwa imetosha na kazi ianze. Lakini wanaanza vipi kampeni ilihali mikutano imepigwa marufuku?

Hapa ndipo penye kiini cha mada na wapinzani wapaswa kuja na mikakati na mipango sahihi na thabiti.

Kuna kitu chaitwa "Tools for Activists" au kwa kiswahili ni nyenzo kwa wanaharakati ambazo hutumika kuandaa shughuli za chama mbadala. Napenda kutoa picha ya chama mbadala yaani "alternative party" kwa CCM.

Chama mbadala kitatoa mawazo mbadala kuhusu nini kifanyike katika maeneo ya siasa, uchumi na kijamii.

Moja ya sababu kubwa ya vyama vya upinzani kama CHADEMA kushindwa katika kukabiliana na chama chenye nguvu kama CCM ni kushindwa kuunda nyenzo sahihi za wanaharakati wake na kuzitumia kufasaha. Nyenzo hizi husaidia shughuli za chama, wanachama na wafuasi kuwa pamoja na kueneza ujumbe.

Kwa kuwa CHADEMA ndiyo chama pekee na kikubwa cha upinzani kwa sasa, itabidi chama hicho kipigwe msasa na nakshi ili kiweze kuwa na taswira ya chama tishio na kilicho tayari hasa kuchukua madaraka ya kuongoza Tanzania.

Hivyo basi, tuangalie safu yake ya uongozi, makada wake na wanachama wake ambao wataamua kusimama katika chaguzi zijazo. Sasa hilo ni suala ambalo CHADEMA wenyewe wapaswa kuamua haraka maana katika saa ya kisiasa muda huu ndiyo chama kipo katikakati.

Baada ya kuangalia huko juu kwenye uongozi tushuke chini kidogo kuangalia idara ya uenezi na propaganda. Hivyo ni lazima kwanza CHADEMA wakiri kwamba hakuna watu wenye uwezo au waliopo ni wachache . Hivyo kuwepo na timu maalum ambayo itashughulika na masuala ya teknolojia na mitandao yote IG, Twitter na kwingine na hilo ni jambo la dharura.

Hizi nyenzo au "tools for activists" zipo za aina mbili zipo za kawaida kabisa yaani kwenye uwanja wa kisiasa na zipo zile ambazo hutumika mitandaoni.

Sasa baada ya kuongea hayo na kutambulisha mada hii ambayo kama nilivyoomba hapo mwanzoni kwamba iwe endelevu hadi ifikapo wakati wa chaguzi zote (2024 na 2025) ningependa kuungwa mkono na wadau wote ambao wanataka kuona Tanzania yarudisha uchumi wa kati na uchumi huo hautetereki.

Kisha nitaendelea kutoa kidogokidogo zile nyenzo ambazo wanaharakati na wanasiasa wa upinzani wazihitaji ili kuiga mazuri ya uchaguzi wa Kenya na busara za mzee Raila Odinga kukubali kushindwa uchaguzi bila kinyongo.

Karibuni sana ndugu zanguni na naomba tuache utani na maneno yasiyofaa.
 
Mimi kwa maono na maoni na mtazamo wangu

1. Tunapozungumzia upinzani Tanzania tunazungumzia CHADEMA.. Hapa ndio penye upinzani wa kweli na think tank ya nchi

2. Pili kwasasa ni kama vile inaonekana CHADEMA imelala na kupoteza mwelekeo lakini hizi ni propaganda za maadui wa CHADEMA.! Hiki chama sio volcano mfu bali ni volcano iliyolala inayosubiri kulipuka muda ukifika

3. Watawala wana hofu kubwa na CHADEMA na hapa ndipo kwenye tatizo la msingi. Maana hawalali wako macho wakikesha kutafuta mbinu zozote mpya na za zamani halali na haramu zitakazowavusha tena 2025... Kwenye hili kuna udhibiti mkubwa wa wapinzani unaoweza kutokea utakaovunja haki za binadamu kwa mapana mno

4. Kuweka haki na mazingira sawa kuanzia kampeni mpaka uchaguzi mkuu 2025 ni bomu la nyuklia linaloogopwa mno na walioko madarakani sasa! Maana wanajua fika kwamba kama wakidondoka ndio itakuwa milele hiyo lakini hapa hoja si kudondoka tu bali yatakayotokana na hilo anguko maana wengi kati yao watakuwa wapangaji wapya kwenye yale majengo ya serikali yanayohifadhi watu waliotenda jinai na kukengeuka sheria mbali mbali za nchi yetu kipindi wakiwa madarakani
 
Mimi kwa maono na maoni na mtazamo wangu
1. Tunapozungumzia upinzani Tanzania tunazungumzia CHADEMA.. Hapa ndio penye upinzani wa kweli na think tank ya nchi

2. Pili kwasasa ni kama vile inaonekana CHADEMA imelala na kupoteza mwelekeo lakini hizi ni propaganda za maadui wa CHADEMA.! Hiki chama sio volcano mfu bali ni volcano iliyolala inayosubiri kulipuka muda ukifika

3. Watawala wana hofu kubwa na CHADEMA na hapa ndipo kwenye tatizo la msingi. Maana hawalali wako macho wakikesha kutafuta mbinu zozote mpya na za zamani halali na haramu zitakazowavusha tena 2025... Kwenye hili kuna udhibiti mkubwa wa wapinzani unaoweza kutokea utakaovunja haki za binadamu kwa mapana mno

4. Kuweka haki na mazingira sawa kuanzia kampeni mpaka uchaguzi mkuu 2025 ni bomu la nyuklia linaloogopwa mno na walioko madarakani sasa! Maana wanajua fika kwamba kama wakidondoka ndio itakuwa milele hiyo lakini hapa hoja si kudondoka tu bali yatakayotokana na hilo anguko maana wengi kati yao watakuwa wapangaji wapya kwenye yale majengo ya serikali yanayohifadhi watu waliotenda jinai na kukengeuka sheria mbali mbali za nchi yetu kipindi wakiwa madarakani
Well said, ahsante sana mkuu kwa kukaribia hapa?

1. Uko sawa kabisa Chadema ndie baba la upinzani, ila think tank pia ni lazima wawepo wa nje ya Chadema kwa kukosoa kwenye lengo la kurekebisha hapa na pale.

2. Chadema kulala ni ni dhahiri ila chinichini yapaswa kutumia zile zile nyenzo au "tools" ambazo kadri tunavyokwenda na mjadala ntaziongelea hapa.

3. Ni kweli CCM wana hofu na hii yaweza kuthibitishwa na ziara za hivi jaribuni huko magharibi mwa Tanzania kwa mheshimiwa Kinana baada ya kuombwa msaada. Na hii pia ni kutokana na kwamba kumuondoa mzee Mangula ambako ni stratejia ya CCM kwamba raisi wa sasa apite NEC bila kupingwa ni tatizo kubwa ambalo limezidi kuiweka pabaya.

Hapohapo huu ndo wakati vyombo vya habari vya nje vikaanza kupewa mwongozo wa namna ya kuripoti habari za kampeni na pia wawakilishi wa mataifa ya nje kuishawishi serikali kuachana na shughuli za kuwadhibiti wapinzani kwa kutumia nguvu nyingi na badala yake kukaribisha mijadala chanya.

4. Upo sawa kabisa ni wajibu wa serikali kuruhusu shughuli za kisiasa ziendelee kwani ni wao wenyewe wameweka mazingira yaliyopo sasa hivyo moto wa Chadema ni budi kukolezwa kuanzia sasa. Lakini kama hiyo ni ngumu ndipo twarudi kwenye zine nyenzo au tools ambazo zitasaidia kuweka hamasa mbali na viwanja vya mikutano.
 
Well said, ahsante sana mkuu kwa kukaribia hapa?

1. Uko sawa kabisa Chadema ndie baba la upinzani, ila think tank pia ni lazima wawepo wa nje ya Chadema kwa kukosoa kwenye lengo la kurekebisha hapa na pale.

2. Chadema kulala ni ni dhahiri ila chinichini yapaswa kutumia zile zile nyenzo au "tools" ambazo kadri tunavyokwenda na mjadala ntaziongelea hapa.

3. Ni kweli CCM wana hofu na hii yaweza kuthibitishwa na ziara za hivi jaribuni huko magharibi mwa Tanzania kwa mheshimiwa Kinana baada ya kuombwa msaada. Na hii pia ni kutokana na kwamba kumuondoa mzee Mangula ambako ni stratejia ya CCM kwamba raisi wa sasa apite NEC bila kupingwa ni tatizo kubwa ambalo limezidi kuiweka pabaya.

Hapohapo huu ndo wakati vyombo vya habari vya nje vikaanza kupewa mwongozo wa namna ya kuripoti habari za kampeni na pia wawakilishi wa mataifa ya nje kuishawishi serikali kuachana na shughuli za kuwadhibiti wapinzani kwa kutumia nguvu nyingi na badala yake kukaribisha mijadala chanya.

4. Upo sawa kabisa ni wajibu wa serikali kuruhusu shughuli za kisiasa ziendelee kwani ni wao wenyewe wameweka mazingira yaliyopo sasa hivyo moto wa Chadema ni budi kukolezwa kuanzia sasa. Lakini kama hiyo ni ngumu ndipo twarudi kwenye zine nyenzo au tools ambazo zitasaidia kuweka hamasa mbali na viwanja vya mikutano.
CHADEMA kina mbinu nyingi sana zinazobadilika kila wakati kuendana na wakati, mazingira na mahitaji ya nyakati.. CHADEMA digital ni mojawapo ya mbinu iliyowachapa vilivyo wapinzani wao in this case CCM
Pia nipende tu kukuhakikishia kwamba kuna think tank nyingine nje ya CHADEMA na ndani ya mamlaka inatoa support kubwa sana kwakuwa nayo imechoshwa mno na hiki kikongwe CCM

Hizi think tanks zote ni tool mojawapo yenye nguvu sana kuelekea kuikomboa nchi ndio maana nimeziweka zote kwenye kundi moja ndani ya CDM japo kiutendaji kila moja ina jukumu lake
 
Mimi kwa maono na maoni na mtazamo wangu
1. Tunapozungumzia upinzani Tanzania tunazungumzia CHADEMA.. Hapa ndio penye upinzani wa kweli na think tank ya nchi

2. Pili kwasasa ni kama vile inaonekana CHADEMA imelala na kupoteza mwelekeo lakini hizi ni propaganda za maadui wa CHADEMA.! Hiki chama sio volcano mfu bali ni volcano iliyolala inayosubiri kulipuka muda ukifika

3. Watawala wana hofu kubwa na CHADEMA na hapa ndipo kwenye tatizo la msingi. Maana hawalali wako macho wakikesha kutafuta mbinu zozote mpya na za zamani halali na haramu zitakazowavusha tena 2025... Kwenye hili kuna udhibiti mkubwa wa wapinzani unaoweza kutokea utakaovunja haki za binadamu kwa mapana mno

4. Kuweka haki na mazingira sawa kuanzia kampeni mpaka uchaguzi mkuu 2025 ni bomu la nyuklia linaloogopwa mno na walioko madarakani sasa! Maana wanajua fika kwamba kama wakidondoka ndio itakuwa milele hiyo lakini hapa hoja si kudondoka tu bali yatakayotokana na hilo anguko maana wengi kati yao watakuwa wapangaji wapya kwenye yale majengo ya serikali yanayohifadhi watu waliotenda jinai na kukengeuka sheria mbali mbali za nchi yetu kipindi wakiwa madarakani
Mwanaccm mm nakuunga mkono kabisa.

Na yule Lisu akitua tu ndo machungu yatakapo anzia tukumbuke kila kitu kimepanda bei na kila uchao makampuni yanapunguza wafanyakazi na hili linatokea baada ya uchumi wa nchi kuyumba.

Ila nakiasa chama changu tuu kiingilie mfumuko wa bei kwani kinaweza kuondolewa na mandamano pale bei za vyakula hali inaweza kuwabadilisha wananchi.
 
Kwanza unapozungumzia upinzani "kujipanga ndani ya mazingira magumu" hapa nakuona hujawatendea haki wapinzani, kwanini uwatake wajipange kwenye mazingira magumu, badala ya kuhakikisha panakuwepo na uwanja sawa wa kufanya shughuli za kisiasa? hapa umeonesha kuipendelea CCM.

Nionavyo kwa vyovyote vile, chaguzi za Serikali za Mitaa 2024, na ule Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa kiasi kikubwa zitaathiriwa na upatikanaji wa Katiba Mpya, au kutopatikana kwake [ Chadema walishasema hawatashiriki uchaguzi].

Kama Katiba Mpya itapatikana, mfano ile Rasimu ya Warioba, na ikaweka haki sawa kwa vyama vyote, hasa kwenye mazingira ya kufanya shughuli za kisiasa, na mchakato mzima wa uchaguzi [kampeni, kupiga kura, kuzihesabu, mpaka kutangaza washindi], naamini kabisa, upinzani hasa Chadema, watapata ushindi mkubwa kwenye chaguzi zote mbili.

Naandika hivi kwasababu imeshathibitika mara zote, kushindwa kwa Chadema kwenye chaguzi, huwa hakutokani na kutopigiwa kura na wafuasi wake, bali ni mbinu chafu zinazofanywa na watawala wa CCM na washirika wao [ polisi, na tume ya uchaguzi] kuwapora Chadema ushindi.

Lakini ikiwa Katiba Mpya haitapatikana, au ikapatikana isiyokidhi viwango kwa kuendekeza baadhi ya mambo yasiyo ya haki kwa vyama vya upinzani, Chadema walishasema hawatashiriki uchaguzi.

Lakini kama wakishiriki, basi naamini chaguzi zote mbili, [S/M na Mkuu 2025] hazitakuwa na lolote la maana kwa upinzani, zaidi wataendelea kuishi kwa kutegemea fadhila toka kwa CCM, wapewe baadhi ya mitaa na majimbo maisha yaendelee.
 
Mwanaccm mm nakuunga mkono kabisa.
Na yule Lisu akitua tu ndo machungu yatakapo anzia tukumbuke kila kitu kimepanda bei na kila uchao makampuni yanapunguza wafanyakazi na hili linatokea baada ya uchumi wa nchi kuyumba.
Ila nakiasa chama changu tuu kiingilie mfumuko wa bei kwani kinaweza kuondolewa na mandamano pale bei za vyakula hali inaweza kuwabadilisha wananchi
 
Kwanza, napenda kuomba uongozi wa JF kuiachia hii mada iwe endelevu hadi ifikapo wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024 na hatimae uchaguzi mkuu wa uraisi wa mwaka 2025.

Lengo la mada hii ni kuona wale wapenda demokrasia na siasa za kweli wakijongea hapa na kushusha nondo na madini mbalimbali katika kufanya kitu chitwa "brain storming".

Katika muktadha huo basi, tutaweza kuangalia sera za chama cha CCM ambacho ndicho chaongoza serikali ya Tanzania kwa sasa na pia ilani ya chama hicho na utekelezaji wake na wapi wamefikia.

Pia mada hii itatoa fursa ya kuangalia hali ya uchumi wa Tanzania kati ya 2015 na 2021 na baada ya hapo ni wapi tumekwama, sababu za kukwama na nini kifanyike kwa maana ya kwamba je, serikali ina washauri wanofaa wa uchumi "Think Tanks", taasisi binafsi za kuchambua sera za kiuchumi na wadau mbalimbali na nini nafasi yao katika kuishauri serikali katika nyakati ngumu au nyakati tata.

Hali kadhalika mada itakaribisha maoni ya upinzani, hali yake kisiasa, uwezo wake wa kuendeleza harakati na nini kifanyike ili kuleta chagizo ambalo litaweza kutikisa hali ya kisiasa nchini hususan CCM.

Hakika uchaguzi wa Kenya umetoa funzo kubwa kwa wale wanofuatilia harakati za kisiasa na kutufumbua macho wengi wetu kuwa kweli wakenya wana demokrasia ya kweli.

Lakini kuna mambo matatu makubwa ambayo ndiyo yalonichagiza kuamua kuanzisha mada hii.

Kwanza, ni tume huru ya uchaguzi ya Kenya ambayo imeonyesha hali yake ya kuwa yajitegemea, ni huru na haina mashinikizo kutoka sehemu yoyote ile. Tume ikatangaza ushindi wa raisi Ruto licha ya kwamba raisi aliepita bwana Uhuru Kenyatta alikuwa waziwazi akimuunga mkono bwana Raila Odinga. Hata humu JF yumo mwenzetu mmoja na wengine kadhaa ambao walionyesha kuumunga mkono bwana Odinga.

Bwana Odinga alipinga matokeo hayo kwa kudai kulikuwa na mizengwe ya udanganyifu na mwishowe mahakama uamuzi wa kuthibitisha ushindi wa bwana Ruto, uzmuzi ambao wapiga kura wengi wa Kenya waliukubali kuwa ulikuwa wa haki na ukweli.

Lakini ushindi wa Raisi Ruto ulionyesha kuwastua wana CCM na wafuasi wao kwani kwani katika uchagzu wa Kenya hakukuwepo na ahadi ya goli la mkono. Hii dhana ya goli la mkono ni kuthibitisha kuwa CCM ni chama dola na kina uwezo wa kuamua kuwa madarakani kwa muda wowote ambao chama hichgo kitapenda kukaa na chaguzi zote zitaamuliwa na wao kwa kutumia vyombo vya dola.

Pili, wenzetu wa Kenya uchaguzi wao ulikuwa na maandalizi ya kutosha kuanzia wapiga kura kujiandikisha hadi kila kituo cha kupigia kura kuwa tayari kimepokea fomu zote za kupigia kura . Moja ya sababu kubwa yamhapa ni uwezo wa wagombea wa upinzani kuweza kuchukua fomu au kujiandikisha uzuri kituoni salama bila kubughudhiwa na kuthibitishwa na kisha kuketi mahala au kwenda nyumbai kusubiri matokeo salama.

Hali ingine ni kwa vituo cha kupigia kira kuendelea kupokea wapiga kura na kufungwa mara tu na inapothibitika kwamba wapiga kura wote wa CCM na vyama vingine wametumia haki yao hiyo ya kikatiba kufanikisha zoezi hilo.

Tatu, mitandao ya "internet" ni muhimu sana katika nyakati za uchaguzi na husaidia taasisi kama tume ya uchaguzi kufanya kazi zake kwa ufanisi zaidi kwa kuweka fomu za kujiandikisha katika tovuti yake ambapo wapiga kura wataweza kunywila fomu hizo kwa haraka na kuzirudisha vituoni bila kuchelewa. Pia hiyo itasaidia kuwawezesha wapiga kura kufuatilia matokeo ya uchaguzi mitandaoni bila kusubiri kwa muda mrefu. Pia mitandao itasaidia kurahisisha mawasiliano baina ya watanzania waliopo maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi bila kuzuiwa wala kukwamishwa.

Hayo mambo matatu ndiyo yamechangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha uchaguzi wa hawa majirani zetu jambo ambalo ni la kujivunia kwao na kulitamani hapa kwetu Tanzania.

Sasa basi, Tanzania yaelekea kufanya uchaguzi wake mkuu wa uraisi mwaka 2025 na kabla ya hapo utakuwepo uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024. Jambo la msingi ambalo CCM na serikali yake yapaswa kufanya ni kutorudia hali ya mwaka 2019 ambapo vyama vya siasa baada ya kukaa pembeni kwa miaka mitatu hadi minne ndo vikaja kushiriki uchaguzi.

Jambo jingine ni CCM na serikali yake kuhakikisha wapinzani hawapati bughudha kutoka kwa vyombo vya dola khasa polisi na usalama wa taifa.

Wakati sasa umefika wa wapinzani kuamua kuwa IMETOSHA na kazi ianze. Lakini wanaanza vipi kampeni ilhali mikutano imepigwa marufuku?

Hapa ndipo penye kiini cha mada na wapinzani wapaswa kuja na mikakati na mipango sahihi na thabiti.

Kuna kitu chaitwa "Tools for Activists" au kwa kiswahili ni nyenzo kwa wanaharakati ambazo hutumika kuandaa shughuli za chama mbadala. Napenda kutoa picha ya chama mbadala yaani "alternative party" kwa CCM.

Chama mbadala kitatoa mawazo mbadala kuhusu nini kifanyike katika maeneo ya siasa, uchumi na kijamii.

Moja ya sababu kubwa ya vyama vya upinzani kama Chadema kushindwa katika kukabiliana na chama chenye nguvu kama CCM ni kushindwa kuunda nyenzo sahihi za wanaharakati wake na kuzitumia kufasaha. Nyenzo hizi husaidia shughuli za chama, wanachama na wafuasi kuwa pamoja na kueneza ujumbe.

Kwa kuwa Chadema ndiyo chama pekee na kikubwa cha upinzani kwa sasa, itabidi chama hicho kipigwe msasa na nakshi ili kiweze kuwa na taswira ya chama tishio na kilicho tayari khasa kuchukua madaraka ya kuongoza Tanzania. Hivyo basi, tuangalie safu yake ya uongozi, makada wake na wanachama wake ambao wataamua kusimama katika chaguzi zijazo. Sasa hilo ni suala ambalo Chadema wenyewe wapaswa kuamua haraka maana katika saa ya kisiasa muda huu ndo chama kipo katikakati.

Baada ya kuangalia huko juu kwenye uongozi tushuke chini kidogo kuangalia idara ya uenezi na propaganda. Hivyo ni lazima kwanza chadema wakiri kwamba hakuna watu wenye uwezo au waliopo ni wachache . Hivyo kuwepo na timu maalum ambayo itashughulika na masuala ya teknolojia na mitandao yote IG, Twitter na kwingine na hilo ni jambo la dharura.

Hizi nyenzo au "tools for activists" zipo za aina mbili zipo za kawaida kabisa yaani kwenye uwanja wa kisiasa na zipo zile ambao hutumika mitandaoni.

Sasa baada ya kuongea hayo na kutambulisha mada hii ambayo kama nilivyoomba hapo mwanzoni kwamba iwe endelevu hadi ifikapo wakati wa chaguzi zote (2024 na 2025) ningependa kuungwa mkono na wadau wote ambao wanataka kuona Tanzania yarudisha uchumi wa kati na uchumi huo hautetereki.

Kisha nitaendelea kutoa kidogokidogo zile nyenzo ambazo wanaharakati na wanasiasa wa upinzani wazihitaji ili kuiga mazuri ya uchaguzi wa Kenya na busara za mzee Raila Odinga kukubali kushindwa uchaguzi bila kinyongo.

Karibuni sana ndugu zanguni na naomba tuache utani na maneno yasofaa.
Maridhiano maridhiano maridhiano
 
Hebu wakati mwingine tuache ushabiki na tuongeage ukweli...pamoja na matatizo ya chama tawala yaliyopo(mimi sina chama)....je pale Chadema kama wakipewa nchi , kuna team yakutosha kabisa inayoweza kuongoza nchi?Yaani kuanzia Rais,Waziri Mkuu, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Kiongozi nk nk....mbona sioni mtu wa level hizo pale??? au ndiyo akina Lema,Mbowe?
 
Hebu wakati mwingine tuache ushabiki na tuongeage ukweli...pamoja na matatizo ya chama tawala yaliyopo(mimi sina chama)....je pale Chadema kama wakipewa nchi , kuna team yakutosha kabisa inayoweza kuongoza nchi?Yaani kuanzia Rais,Waziri Mkuu, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Kiongozi nk nk....mbona sioni mtu wa level hizo pale??? au ndiyo akina Lema,Mbowe?
Sasa kama wakina mwigulu nape January wameweza huo uwaziri wewe ni nani hata ushindwe?
 
Time is money.

Bila timeframe ya Maridhiano hiyo ni POLITICAL miscalculation

Maridhiano yanatakiwa yakamilike au yavunjike b4 December 2022.

CDM iamue kujenga chama Kwa kufanya mikutano ya hadhara Nchi nzima, mikutano hiyo ilenge kuelimisha umma juu ya umuhimu wa KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA.

CDM waamue kukubali liwalo na liwe kuhakikisha mikutano ya hadhara inafanyika, wananchi wako nyuma Yao.

Walio nje ya nchi LISSU na wenzie warudi haraka waache blaa blaa Eti hawana nauli.

Wakiendelea na mwendo huu wa kutochukua hatua mapema, Nchi itaingia Kwa machafuko.

Ameeeeen.
 
Hebu wakati mwingine tuache ushabiki na tuongeage ukweli...pamoja na matatizo ya chama tawala yaliyopo(mimi sina chama)....je pale Chadema kama wakipewa nchi , kuna team yakutosha kabisa inayoweza kuongoza nchi?Yaani kuanzia Rais,Waziri Mkuu, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu Kiongozi nk nk....mbona sioni mtu wa level hizo pale??? au ndiyo akina Lema,Mbowe?

Kwa taarifa yako hakuna chama chochote kitashindwa kuongoza nchi hii, kama CCM wameweza hakuna chama chochote kitashindwa. Wakati wa wakoloni walikuwa wanasema hatutaweza kuongoza hii nchi, lakini hadi leo hii nchi ipo. Kenya hapo enzi za KANU walikuwa wanasema hakuna chama kitaweza kuongoza zaidi yake. Lakini hadi leo kila uchaguzi kuna chama tofauti na Kenya inatuzidi kila kitu kuanzia uchumi, biashara, demokrasia nk. Kitu pekee tunawazidi Wakenya ni eneo la kijiografia.
 
Time is money.

Bila timeframe ya Maridhiano hiyo ni POLITICAL miscalculation

Maridhiano yanatakiwa yakamilike au yavunjike b4 December.

CDM iamue kujenga chama Kwa kufanya mikutano ya hadhara Nchi nzima, mikutano hiyo ilenge kuelimisha umma juu ya umuhimu wa KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA.

CDM waamue kukubali liwalo na liwe kuhakikisha mikutano ya hadhara inafanyika, wananchi wako nyuma Yao.

Walio nje ya nchi LISSU na wenzie warudi haraka waache blaa blaa Eti hawana nauli.

Wakiendelea na mwendo huu wa kutochukua hatua mapema, Nchi itaingia Kwa machafuko.

Ameeeeen.

Kwa taarifa yako CDM wakithubutu kufanya mikutano kukiwa na Katazo, wengi wataishia jela tumeona hayo kwa Mbowe, na wengine watapata vilema vya maisha, na hata vifo kutokana na vipigo vya vyombo vya dola, na hakutakuwa na uwajibishwaji wa hayo. Ww unaongea kinadharia huku ukifumbia macho ukweli.
 
Upinzani wa hapa nchini hawana mpango wowote mpaka sasa wa kushinda chaguzi za 2024 na 2025.
Nimewasikia viongozi wa CDM, Mnyika na Mbowe wakisisitiza kutoshiriki uchaguzi wa 2024 na 2025 bila kwanza kupatikana KATIBA mpya na Tume huru ya Uchaguzi.

Tafsiri ya HOJA zao ni:

1. KUSUSIA uchaguzi.

2. Kushinikiza madai Yao yapatikane kabla ya Uchaguzi, yaani kugomesha wananchi Ili uchaguzi usifanyike Hadi madai muhimu kufanyiwa KAZI.

Hoja NO 2. yaweza onekana NYEPESI Kwa watawala wakaipuuza bt Hali ya kiuchumi inaweza sababisha uungwaji mkono mkubwa sana ndani ya JAMII mbali na wananchi Walio Wanachama wa Vyama kinzani.

Chama Tawala wakisaidiwa na deep state mara zote kimekuwa na THINK tanks wawezao kuona MBALI na kurekebisha mapema.

Tuliona mfano wa kupatikana Jina la Magufuli asiyetegemewa Ili kuinusuru chama kuanguka.

Natabiri mifumo isiyoonekana kuwa nyuma ya hoja ya KATIBA mpya na TUME huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote kama njia pekee ya kuinusuru Nchi na machafuko ya chaguzi kandamizi.

Ameeeen.
 
Tusizunguke sana sijui kuna mbinu yoyote ya kuleta katiba ama sijui CDM wajipange. Bila nchi kupinduliwa, ama wafuasi wa CDM/wananchi kuleta machafuko, tusitegemee mabadiliko yoyote ya maana, sana sana watu wengi hawatajitokeza kupiga kura.

Hiyo Kenya tunayoona wanaheshimiana ni kwakuwa kulitokea machafuko baada ya uchaguzi wa 2007. Ifahamike wakati wa Moi wakenya walikuwa waoga kuliko sisi. Ongeeni maelezo yoyote na mbinu zozote mzitakazo lakini itakuwa kufurasha genge tu, machafuko ndio yataifanya demokrasia ya nchi hii iwe bora.
 
Nimewasikia viongozi wa CDM, Mnyika na Mbowe wakisisitiza kutoshiriki uchaguzi wa 2024 na 2025 bila kwanza kupatikana KATIBA mpya na Tume huru ya Uchaguzi.

Tafsiri ya HOJA zao ni:

1. KUSUSIA uchaguzi.

2. Kushinikiza madai Yao yapatikane kabla ya Uchaguzi, yaani kugomesha wananchi Ili uchaguzi usifanyike Hadi madai muhimu kufanyiwa KAZI.

Hoja NO 2. yaweza onekana NYEPESI Kwa watawala wakaipuuza bt Hali ya kiuchumi inaweza sababisha uungwaji mkono mkubwa sana ndani ya JAMII mbali na wananchi Walio Wanachama wa Vyama kinzani.

Chama Tawala wakisaidiwa na deep state mara zote kimekuwa na THINK tanks wawezao kuona MBALI na kurekebisha mapema.

Tuliona mfano wa kupatikana Jina la Magufuli asiyetegemewa Ili kuinusuru chama kuanguka.

Natabiri mifumo isiyoonekana kuwa nyuma ya hoja ya KATIBA mpya na TUME huru ya Uchaguzi kabla ya Uchaguzi wowote kama njia pekee ya kuinusuru Nchi na machafuko ya chaguzi kandamizi.

Ameeeen.
Sawa wacha tusubiri tuone.
 
Back
Top Bottom