MJADALA: Uliza chochote kuhusu mchakato wa uagizaji magari

KIMOMWEMOTORS

JF-Expert Member
May 17, 2018
358
670
Mara kadhaa tumekuwa tukianzisha mada mbalimbali zenye lengo la kutoa elimu, dhumuni likiwa ni kupeana uelewa zaidi na kukumbushana mambo mbalimbali kuhusu uagizaji wa magari.

Leo tungependa kusikia masuala tofauti tofauti kutoka kwenu wadau ili tuzidi kupeana uzoefu na elimu zaidi.

Shukrani na karibuni sana.
 
Hivi Mercedes-Benz E220 Cabriolet W124 ina mchakato gani na gharama kiasi gani hadi ifike Bongo?
 
Hivi Mercedes-Benz E220 Cabriolet W124 ina mchakato gani na gharama kiasi gani hadi ifike Bongo?
Shukrani wka swali zuri boss. Hizi gari zipo za miaka kuanzia 1990s mpaka miaka ya 2000. Igekua vizuri ungeniambia ni ya mwaka gani unayohitaji. Ila halijaharibika kitu, nimekupigia hesabu hii ya mwaka 2001 ambayo ni kama mfano utakaosaidia kukupatia picha ya makadirio ya gharama kwa wastani. Hii link niliyoweka hapa chini ni gari ambayo nimeitolea mfano inayotaikana kutoka SBT. Gari hiyo manunuzi na usafiri ni dola 3950 sawa na Tsh 9,144,000, Ushuru wake ni Tsh 5,092,000 na gharama za bandari kama Wharfage, Port charges, Shipping Line na Agent Fee ni Tsh 1,000,000. Jumla kuu kwa gari hii niTsh 15,236,000

 
Back
Top Bottom