Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,656
CHADEMA imefanya mambo mengine yapite aidha kimyakimya ama kukosa mijadala critical ya wananchi. Baadhi ya mambo hayo ni:
Kuvunjwa kwa mkataba wa Tsh trillion moja na ushee na kampuni moja nje ya nchi (kwa wasiojua trillion moja ina masifuri 12 yaani 1,000,000,000,000/=)
Msanii wa Bongo fleva kuzindua album yake hapo jana tarehe 14. Maandalizi na matangazo yalikuwa mengi. Sijui matokeo yamekuwaje.
Ugonjwa mbaya wa corona ni kama vile Watanzania wameupotezea lakini la hasha. CHADEMA imesababisha habari zote hizi kukosa mijadala mipana.
Nawaombeni sasa muda wenu tuweze kulijadili hili.
Mwanzoni mwa wiki hii Waziri wa Mambo ya Ndani Simbachawene alitoa taarifa rasmi kuwa ule mkataba tata wa vifaa vya Jeshi la Zimamoto wa takriban Tsh. Trillion moja umevunjwa kati yake na kampuni iliyokuwa imepewa/imeshinda Hiyo zabuni. Na akasisitiza kwamba hakuna hasara tuliyopata wala tutakayopata.
Mimi nina maoni tofauti kidogo na waziri.
Kwanza nikiri wazi mimi si mjuzi wa sheria za mikataba lakini hata kama wapo wajuzi hapa, hatutaweza kuujadili mkataba kwa maudhui yake kwakuwa hatujawahi kufahamu kilichokuwa ndani yake. Labda tufanye zile za kibush lawyer tu.
Yangu ni haya hapa
Ule mkataba tumeingia hasara kubwa mpaka sasa. Wote tunatambua mkachato wa kuandaa tenda mpaka kupata wazabuni na hatimaye kusaini mikataba ulivyo mrefu, na kila hatua ni pesa.
Tulishatumia muda nguvukazi, rasilimali na pesa nyingi tu kwenye hili jambo. Hivyo tumepata hasara ya kwanza.
Mpaka kufikia kuhitaji hivyo vifaa tafsiri yake ni kwamba tuna upungufu. Hivyo kama mchakato ungeenda vema, vifaa tajwa vingefika kwa wakati na hilo ombwe la ukosefu/upungufu lingezibika na kumaliza hilo jambo. Mchakato huu umefeli, sasa kuanza mwingine ni gharama nyingine tena hizo. Tumepata hasara ya pili.
Vifaa tajwa vingekuwa vya kisasa. Hivyo kama mchakato ungeenda vema, ingekuwa ni nafasi adhimu kwa vijana wetu kwenda kujifunza maarifa mapya kwa faida ya taifa huku tukizalisha ajira mpya. Hasara ya tatu hii.
Ni wazi kabisa vifaa hivi vingekuja na mitambo ambayo ingehitaji maeneo mapya ya kuifunga. Hili lingefanikiwa Watanzania wengi wangepata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja na wangechangia pato la taifa kwa kufanya biashara na kuleta nafuu kwenye kaya zao. Hasara ya nne hii.
Kama hili lingewezekana basi kungekuwa na michakato ya ujenzi. Hapa wakandarasi wa ndani, wataalam wa mazingira, wafanyabiashara na wahusika wengine wangepata sehemu ya kuingiza chochote kulingana na fani zao. Mkataba umesitishwa. Hasara ya tano hii.
Kwa kuvunjwa mkataba huu ukiwa hatua za mwisho umetia DOA kwenye biashara za kimataifa. Na tumeonesha umakini duni. Mahusiano ya kidiplomasia pia yanaweza kutetereka kidogo. Hasara ya sita hii.
Usiri na kutoshirikishwa bunge letu kupitia kamati husika. Kama haya mambo yangefanyika kwa uwazi na kwa taratibu tulizojiwekea. Yasingefika huku. Bunge lilifichwa hivyo wananchi walifichwa pia. Matokeo ndio haya. Hasara ya saba hii.
Ndugu waziri pengine hizi hasara hujazizingatia lakini huko mbeleni mambo yanaweza kuwa mabaya zaidi kama yule jamaa aliyepata hii tenda akiamua kwenda mahakama ya kimataifa kulalamika.
Sitaki kulisemea hili kwakuwa sifahamu maudhui ya mkataba kwenye zabuni kubwa kama hizi tena zinazohusika na jeshi ama kwa sehemu vifaa vya kijeshi kuna vitengo kama tisa ni lazima vijulishwe na vishiriki kutoa maamuzi:
Mamlaka ya Rais
Mkuu wa Majeshi
Mtunza Bohari Mkuu
Usalama wa Taifa
Mlipaji Mkuu wa Serikali (hazina)
Bunge
Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Benki Kuu
Mzabuni Mkuu Taifa
Je, kwa hatua zote za mchakato wa huu mkataba hawa wamehusishwa? Na hata sasa je wamehusishwa?
Mchakato wa kuvunja mkataba hupitia njia ileile uliyoanza nayo, huruki hatua. Je kwa uharaka huu wa kuvunja huu mkataba, hatua zote zimefuatwa?
Kwako Simbachawene,
Waziri wa Mambo ya Ndani.
Jr
Kuvunjwa kwa mkataba wa Tsh trillion moja na ushee na kampuni moja nje ya nchi (kwa wasiojua trillion moja ina masifuri 12 yaani 1,000,000,000,000/=)
Msanii wa Bongo fleva kuzindua album yake hapo jana tarehe 14. Maandalizi na matangazo yalikuwa mengi. Sijui matokeo yamekuwaje.
Ugonjwa mbaya wa corona ni kama vile Watanzania wameupotezea lakini la hasha. CHADEMA imesababisha habari zote hizi kukosa mijadala mipana.
Nawaombeni sasa muda wenu tuweze kulijadili hili.
Mwanzoni mwa wiki hii Waziri wa Mambo ya Ndani Simbachawene alitoa taarifa rasmi kuwa ule mkataba tata wa vifaa vya Jeshi la Zimamoto wa takriban Tsh. Trillion moja umevunjwa kati yake na kampuni iliyokuwa imepewa/imeshinda Hiyo zabuni. Na akasisitiza kwamba hakuna hasara tuliyopata wala tutakayopata.
Mimi nina maoni tofauti kidogo na waziri.
Kwanza nikiri wazi mimi si mjuzi wa sheria za mikataba lakini hata kama wapo wajuzi hapa, hatutaweza kuujadili mkataba kwa maudhui yake kwakuwa hatujawahi kufahamu kilichokuwa ndani yake. Labda tufanye zile za kibush lawyer tu.
Yangu ni haya hapa
Ule mkataba tumeingia hasara kubwa mpaka sasa. Wote tunatambua mkachato wa kuandaa tenda mpaka kupata wazabuni na hatimaye kusaini mikataba ulivyo mrefu, na kila hatua ni pesa.
Tulishatumia muda nguvukazi, rasilimali na pesa nyingi tu kwenye hili jambo. Hivyo tumepata hasara ya kwanza.
Mpaka kufikia kuhitaji hivyo vifaa tafsiri yake ni kwamba tuna upungufu. Hivyo kama mchakato ungeenda vema, vifaa tajwa vingefika kwa wakati na hilo ombwe la ukosefu/upungufu lingezibika na kumaliza hilo jambo. Mchakato huu umefeli, sasa kuanza mwingine ni gharama nyingine tena hizo. Tumepata hasara ya pili.
Vifaa tajwa vingekuwa vya kisasa. Hivyo kama mchakato ungeenda vema, ingekuwa ni nafasi adhimu kwa vijana wetu kwenda kujifunza maarifa mapya kwa faida ya taifa huku tukizalisha ajira mpya. Hasara ya tatu hii.
Ni wazi kabisa vifaa hivi vingekuja na mitambo ambayo ingehitaji maeneo mapya ya kuifunga. Hili lingefanikiwa Watanzania wengi wangepata ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja na wangechangia pato la taifa kwa kufanya biashara na kuleta nafuu kwenye kaya zao. Hasara ya nne hii.
Kama hili lingewezekana basi kungekuwa na michakato ya ujenzi. Hapa wakandarasi wa ndani, wataalam wa mazingira, wafanyabiashara na wahusika wengine wangepata sehemu ya kuingiza chochote kulingana na fani zao. Mkataba umesitishwa. Hasara ya tano hii.
Kwa kuvunjwa mkataba huu ukiwa hatua za mwisho umetia DOA kwenye biashara za kimataifa. Na tumeonesha umakini duni. Mahusiano ya kidiplomasia pia yanaweza kutetereka kidogo. Hasara ya sita hii.
Usiri na kutoshirikishwa bunge letu kupitia kamati husika. Kama haya mambo yangefanyika kwa uwazi na kwa taratibu tulizojiwekea. Yasingefika huku. Bunge lilifichwa hivyo wananchi walifichwa pia. Matokeo ndio haya. Hasara ya saba hii.
Ndugu waziri pengine hizi hasara hujazizingatia lakini huko mbeleni mambo yanaweza kuwa mabaya zaidi kama yule jamaa aliyepata hii tenda akiamua kwenda mahakama ya kimataifa kulalamika.
Sitaki kulisemea hili kwakuwa sifahamu maudhui ya mkataba kwenye zabuni kubwa kama hizi tena zinazohusika na jeshi ama kwa sehemu vifaa vya kijeshi kuna vitengo kama tisa ni lazima vijulishwe na vishiriki kutoa maamuzi:
Mamlaka ya Rais
Mkuu wa Majeshi
Mtunza Bohari Mkuu
Usalama wa Taifa
Mlipaji Mkuu wa Serikali (hazina)
Bunge
Mwanasheria Mkuu wa Serikali
Benki Kuu
Mzabuni Mkuu Taifa
Je, kwa hatua zote za mchakato wa huu mkataba hawa wamehusishwa? Na hata sasa je wamehusishwa?
Mchakato wa kuvunja mkataba hupitia njia ileile uliyoanza nayo, huruki hatua. Je kwa uharaka huu wa kuvunja huu mkataba, hatua zote zimefuatwa?
Kwako Simbachawene,
Waziri wa Mambo ya Ndani.
Jr