Mjadala - Kitabu cha unyama wa Paul Kagame: Behind the Presidential Curtain: Inside Out of real Paul Kagame

Be specific mkuu.Hao "rafiki" zake walikuwa wa kiume au wa kike?Nataka njue.Unaweza kukuta ni gay!Who knows!
Alikuwa anamtmbea luten mmoja akiwa Marekani hadi mkewe Jannet akastukia. Unajua mkuu hiki kitabu kinavutia sana ukizigatia aliyekiandika ni Mlinzi (mtu wa karibu sana na raisi).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wabhejha nkoi!Huyu Kagame ni hopeless fulani
Nimefuatilia kumbe hata mwezi wa tatu Police huko UK wamemtahadhalisha Marara kuwa Kagame anamfuatilia kwa kukodi wauaji wamuue huko huko aliko.
392ac37a-2702-11e8-bb7d-85110f4c5caa.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dhamira zinawasuta.The guilty are afraid. Maovu yao kuanikwa.Wanaona aibu rafiki wa mjomba wao kuanikwa uhuni wake.
Sema huyu mtu atakuja kufa kifo kibaya sana, ikiwa haya yaliozungumzwa humu ameyatenda kiukweli! Ni mtu katili mno na mara nyingi makatili hufa vifo vya fedhea sana. you live by the Gun, you die by the Gun!
 
Jana kwangu ilikuwa siku nyingine ya kufurahia kuwa sehemu ya member wa jamii forum. Hii ilitokana mwanajamii mmoja nzagambadume kupost link ya kitabu kilichoandikwa na mlinzi wa raisi Kagame aliyekimbilia UK kuepuka kifo kilichokuwa tayari mlangoni mwake.

KWA NINI NAMTAJA KIKWETE NA MEMBE

Kwanza ijulikane wazi kuwa Watanzania wengi tulifahamu kuwa Kikwete alikuwa raisi mpole na kufikia hatua ya tukamuita raisi dhaifu aliyezungukwa na marafiki wabaya (walio na hulka ya kujinufaisha wao na familia zao). Nakumbuka nikiwa navuka Mtukula kwenda Kampala siku hiyo sitausahau hasa baada ya kukuta kundi la raia wa Rwanda wakiwa na mizigo yao wakifurushwa kurudishwa Rwanda bila kujali walikuwa na mifugo au makazi,wameoa Watanzania au Watanzania wamewaoa walilazimishwa kurudi makwao kwa amri ya raisi Jakaya Kikwete!!.

Pale mpakani alikuwepo mama mmoja na mwanae wamelala kandoni kidogo mwa barabara huku mtoto akiwa na hali mbaya bila nguo ndipo utu wa Kitanzania niliuona pale kwani yule mama kama alitoka hapo basi hatasahau maisha yake yote kwani alichangiwa na abiria wa Kitanzania kwa kupewa vyakula, nguo na pesa na katika basi gumzo ilikuwa Kikwete ana bifu na Kagame lao binafsi lkn limesababisha hadi wasiohusika wanataabika ukweli hata mimi nilikuwa mmoja wa waliokuwa wanamshutumu raisi. Tulienda mbali kwa kusema huu ukatili si angeuelekeza kwa wezi walioko serikalini mwake lkn msimamo wa Kikwete ulikuwa palepale na hadi anatoka madarakani sikumbuki kama Kikwete alishawahi kwenda ziara Rwanda.

MEMBE ambaye alikuwa mtu wa karibu wa raisi Kikwete wengi tulijua ni usalama wa Taifa (TISS) hivyo tulifahamu kuwa linalotokea baina ya Tanzania na Rwanda basi kwa namna moja Membe alikuwa anafahamu tukizingatia kuwa alishakuwa waziri wa mambo ya nje kwa miaka kadhaa.

KITABU CHA NOBLE MARARA
Kitabu hiki ukianza tu kukisoma sio tu utastaajabu usiyoyafahamu kuhusu Kagame ila utashangaa kwa nini tuna urafiki na mtu dizaini hii (Kagame na Rwanda). Kitabu kimemweka wazi Kagame maisha yake,tabia yake,ukatili wake,namna anavyosuka mipango ya mauaji na namna anavyoplan kujisafisha namna alivyokuwa anazini na wake za watu wake wa karibu akiwa analindwa na ma body guards wake!!

Mtu anayeandika kitabu hiki kumbuka ni mtu aliyekuwa anamlinda Kagame kuanzia asubuhi gadi asubuhi nyingine, yeye mwenyewe kashiriki mauaji akifikiria anailinda Rwanda na Kagame kumbe ni chuki na kujiimarisha tu kwa Kagame rafiki wa karibu wa Tanzania kwa sasa!! Hadi anatoroka alikuwa tayari yuko kwenye target za Kagame

Katika haya maelezo mafupi sana nimeelewa sasa kuwa Mh. raisi Mstaafu Kikwete alibaini na kujilidhisha pasipo shaka kuwa urafiki na huyu mtu sio kabisa hasa baada ya majeshi ya Tanzania kuwapa kichapo M23 jeshi katili la Kagame kipindi hicho huko DRC

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila huenda maana hata aliyetuumba nae huenda ikawa propaganda maana hatumuoni, au baba yako nae ni propaganda maana unauhakika gani kama ni baba yako? Au hata mwanao pia huenda akawa propaganda, wakati mwingine tuwe tunawaza vizuri
Inaweza kuwa propaganda tu,hakuna uthibitisho hapa kama Kagame kufanya hayo yote

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitabu kinasisimua nimesoma UK wa 119 kumbe mke wa kagame nae Ni katili
Kuna mwanamama anaitwa Mrs inyumba aliuawa kwa order yake
Kwa mujibu wa mwandishi,Mrs inyumba alikuwa mmoja wa watu waliopigania chama chá rpf kabla hata ya kuongoza serikali,Mrs inyumba alijitoa kwa Hali na Mali na alikuwa na heshima kubwa ktk chama chá rpf,mrs kagame akaona wivu akamtumia agent wake wa nauaji aitwae jack ku m poison ,baada ya kuugua akapelekwa Holland kwa matibabu ,lkn akawa Hana fedha akaomba msaada kwa chama chake chá rpf lkn mrs kagame aliikataa maana walijua atakufa tu kwakuwa mishe ya sumu waliipanga, kanali karengenya akatoa hela zake mfukoni kumsaidia Mrs inyumba matibabu ndipo karengenya akawekwa ktk target ya mauaji
Kwa mujibu wa mwandishi,Mrs kagame alikuwa na wivu kwakuwa Mrs inyumba alikuwa mwanamke maarufu Sana kiasi kwamba angeweza hata kugombea na akashinda hayimaye Mrs inyumba akafariki na siku ya funeral kagame akamwagia sifa kedekede (kinafiki)
Mkasa huu upo page 119
Kitabu Ni kizuri mno najisomea taratibu
Sky Eclat
britanicca
instanbul
Upepo wa Pesa
The Great Haya
sikongefdc
fazili
AbaMukulu
Frank Wanjiru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Matola umezaliwa mwaka gani kama bifu la Kikwete na Kagame hulifahamu? Kwa mara ya kwanza raia wa Rwanda walifukuzwa nchini magari ya uhamiaji yalikuwa yametanda nchi nzima kuwasaka raia wa Rwanda. Kitabu hiki kinaeleza uharisia wa Kagame hata kama leo hii ndiye rafiki mkuu wa Magu
Bora usingeandika hii thread, hakuna tulichoambulia zaidi ya porojo zako tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilisoma kwenye gazette moja la Ulaya, Janet Kagame ndiye muendeshaji wa miradi ya familia. Huwa anasafiri sana kwenda Marekani kwa shughuli za biashara na kusimamia matibabu ya mume wake.

Tofauti na wake wa madiktekata wengine kama Grace Mugabe,Janet Kagame ana play a low profile. Hata shopping anafanya ya kawaida tu si kufuru.
 
Nilitamani kuona umeandika kwa undani kidogo kuhusu uhasama wa Kikwete na Kagame

Sent using Jamii Forums mobile app
Uhasama wa Kikwete na Kagame ulianza pale Kikwete alipoingilia kati uvamizi wa majeshi ya M23 huko DRC mkuu. Kagame hakupenda kwa kuwa M23 walikuwa kule wakiiba madini ya Congo ndipo Kagame akamkejeli Kikwete kuwa atamtandika. Raisi Kikwete kipindi hicho akaona hii ni dharau iliyovuka mipaka kwanza M23 ilipigwa vibaya pia akaamuru Wanyarwanda wote walioko nchi kama wahamiaji haramu waondoke nchini. Kama umeshawahi kufika mkoa wa Kagera karibia asilimia 90 ya wafugaji wakubwa ni Wanyarwanda sasa ilikuwa ng'ombe wanauzwa hadi 20,000/= ili mradi ufike Rwanda. Wengi wa hawa watu walikuwa washaondoka Rwanda miaka mingi hata mimi na wewe hatujazaliwa lkn Kikwete hakuangalia hili. Fuatilia historia au uliza anayekuzidi umri atakuambia kuhusu hili kwani isingekuwa busara majeshi yetu yangevamia Rwanda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom