Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Nchi yetu bado ni changa na inahitaji sheria kali na maamuzi magumu.. mimi pia namuunga mkono mtoa mada
 
Umenena ndugu, yaani hatupumui kila siku ni kadi za harusi. Tumechoka jamani raisi tuondolee balaa hili umaskini unatunyemelea kwani tusipochangia tunatengwa na marafiki
 
Harusi huwa ni jumamosi unaamkia kazini na uchovu jumapili???

Cha muhimu hapo ni hiyo michango kwa watu masikini iangaliwe namna ya kupunguzwa kbs.
 
Nakubaliana na wewe.Hizi harusi ni shida kabisa saizi.Kila siku kadi kadi! Umaskini tunautengeneza wenyewe.
 
Mi nashauri sherehe ziwepo sana tu,sema serikali itoze kodi kubwa sana ili waoaji wajitathmini kama kufunga harusi kwa sherehe au kimyakimya.Maana sherehe ni mambo ya kitajiri.
 
Hakuna upumbavu uliotukuka kama sherehe ya harusi leo, halafu kesho huna kitu mfukoni, kisa....kuna kajamaa kameoana na muhuni mwenzako....nyoooo!

Kunichangisha mimi uje na dozer
 
Tukubali tusikubali michango ya harusi , send-off na kitchen parties ni kero na ni kujimaliza kiuchumi kwa baadhi ya watu.Kwanza asilimia kubwa ya michango hiyo haifiki kwa walengwa. Kuna haja gani ya kuchanga m.20 alafu maarusi wanapewa na kamati m.1 ati zawadi. Ni vyema michango ya pesa zote wapewe maarusi wakaanzie maisha na kusiwe na send-ff wala kitchen parties ila familia ya mioaji na anayeolewa waweke pamoja resources zao kufanikisha shghuli.Pia kusiwe na biashara ya mahari
 
Duh eti sherehe mwisho saa kumi na mbili jioni! Hivi kwani sherehe ya harusi imekuwa disco toto!? Wanaohudhuria sherehe za harusi ni watu wazima wanaojielewa mie sioni tatizo hapo!!

Kuhusu kuchangia kila mtu ana utashi wake hulazimishwi!
 
Tuko mstari mmoja mkuu, mi huwa nakereka sana, sherehe yako unishughulishe mie, mipango yako niigharamie mie, haiingii akilini. Ndiyo kama unavyosema tunachanga kuogopa kutengwa.
 
Jambo zuri hili naamini sio wote wanaotoa michango ya harusi wanaifurahia,
wengi wanaogopa kutengwa na jamii.
Hii michango ipigwe marufuku kwani ni matumizi mabaya ya fedha.
 
Utakuta kwa mwaka kadi zaidi ya 20 kila moja 70000 zidisha mwenyewe sh.ngapi kwa mwaka zinapotea.
 
Duh eti sherehe mwisho saa kumi na mbili jioni! Hivi kwani sherehe ya harusi imekuwa disco toto!? Wanaohudhuria sherehe za harusi ni watu wazima wanaojielewa mie sioni tatizo hapo!!

Kuhusu kuchangia kila mtu ana utashi wake hulazimishwi!

Tatizo usipochangia unatengwa.
 
Hivi hizo sherehe huwa mnalazimishwa kuchangia? Huhitaji usimamizi wa serikali kwa jambo la hiari
 
Back
Top Bottom