Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mambo Jambo

JF-Expert Member
Jul 11, 2008
1,100
81
Hii Kitu nilitaka kuipost hapa miezi kadhaa iliyopita sema nikasahau, leo kuna jamaa kanipigia anataka nimtumie dolali za mchango wa harusi ya binamu yake ambaye hata simjui wala sijawahi msikia.

Tuendelee:-

Wakuu hii kitu bado bongo ipo tena siku hizi ni project kubwa na za garama ya juu.

Watu wanakutana kila wiki mara moja kwenye baadhi ya bar, wanakunywa na kusaza katika hivyo vikao vya maandalizi, vikao hivyo huchukua miezi miwili hadi mitatu. Na katika vikao hivyo watu hutoa ahadi ya kiasi cha fedha watakachotoa kwa ajili ya harasi, wanaume hutoa michango ya bachela parti na harusi kuu, na kina dada hutoa michango ya sendi off, bridoshawa, kichenipati, na harusi kuu.

Kwa kifupi zoezi hili linakula hela nyingi sana, nimeambiwa sometimes you can be asked to contribute to more than 10 wedding a year, na ukitoa chini ya laki moja unaonekana mtu wa hovyo hovyo.

Jamani ndugu zangu naombeni mwongozo mimi naona kama hii ni too much.

Badala ya michango ya vikao vya harusi basi tuihamishie kwenye Elimu na Matibabu.

MJ

====================
View attachment 235905

Kwa kweli michango ya harusi, sijui kitchen Party, Bag party, Send off party na kadhalika imekuwa too much. Unakuta mtu unakuwa na kadi za kudai michango hadi zaidi ya kumi kwa wakati moja. Tabu ya nyongeza ni kwamba viwango vinavyotegemewa ni vya juu. Tutafika?

Je, haijafika mahali wanajamii ya Tanzania tukapunguza madoido na gharama za shughuli hizi?

==============

Katika kumbukumbu zangu mimi, Harusi mtu ulikuwa unafanya kwa uwezo wako, unaita marafiki zako na ndugu mnasherekea hicho kilichopo.

Sasa mtu anakuletea Kadi tena ina kiwango na Watu hawakuchangii sababu wanakupenda ni kama wanakukopesha kwamba na wao siku yao ikifika na wewe utachanga.

Michango Inafika mpaka mamilioni ya pesa watu wanakuja wanakunywa na kula wewe na mwenza wako mnaenda kuanza maisha (wengine hata nyumba hamna) na deni la watu kama mia moja waliokuchangia ambao na wewe inabidi uwachangie.

Jamani hivi kuchangia harusi sasa imekuwa lazima?

Nahisi sasa harusi zinatuletea umasikini, yani mtanzania wa kawaida nina kadi tisa mpaka sasa.

Bado natafutwa na jamaa yangu mwingine, yani simu imejaa meseji za watu wanakumbushia michango.

Jamani hatuwezi kuwa na utaratibu mbadala kwenye hili swala? Tupungiziane stress.

Halafu na hii tabia ya mtu anakutumia tu ujumbe uje siku fulani mahala fulani kuna kikao cha harusi, kumbe kesha kuweka kwenye kamati ya harusi we bila kujua afu ukifika wanaweka kiwango cha kila mwanakamati kutoa.

Nadhani tuhitaji mbadala wa hili.

Napata kadi za kuchangia harusi karibu kila mwezi naletewa karibu kadi 3, @50,000 approximately =150 , 000 .

Haya majanga sana ,mshahara wangu 550,000 , which means 30% michango harusi ,Ninaacha haya mambo ,mimi mwenyewe sitafanya hiyo mambo, yaani kila weekend tupo busy kuchangisha harusi.

Kama tunataka kutokomeza umasikini na wakati tunatiana umasikini ,siwezi tena.

Jamani kama huna uwezo usisumbue watu bwana ,funga ndoa ya kawaida tuache mambo ya kuiga.
Ni kawaida kwa jamii yoyote duniani kuoa ama kuolewa na hasa kwa binadamu aliyekamilika. Kimsingi kuoa ni jambo la heri kwa mtu kupata mwenzi. Na ndugu jamaa na marafiki kuchangia kwa mawazo mali na misaada mingine ya kijamii ili kufanikisha shughuli hiyo kukamilika.

Hata hivyo uchangiaji huu umekuwa wa kiholela mno, kwani waoaji na wanaoolewa ni vyema wakawa na utaratibu mzuri wa kugawa kadi hizo. Nasema hivi kwa sababu kuwa mgawa kadi anapaswa kufanya mawasiliano na mtu anayetaka ampe kadi kwa ajili ya kumchangia mchango huo. badala ya kuzigawa kadi hizo pasipo hiari ya mchangiaji, maana mgaw kadi unashangaa anakuletea kadi, ama anaibwaga mezani kwako kama ni ofisin au anawaachia watoto kama ni nyumbani.

Ombi langu kwa waoaji wote fanyeni mawasiliano kabla ya kugawa kadi maana sasa zimekuwa kero kiasi kwamba ndani ya mwezi mmoja unaweza kugawiwa kadi zisizopungua kumi na wote wantaka mchango usiopungua elfu hamsini. kwa namna hii hatuwezi kwenda kabisa.

Hata hivyo niwaombe watanzaia wenzangu tunahitaji kubadilika ili mitizamo yetu isilenge zaidi katika uchangiaji wa harusi, tunahitaji kuchangia zaidi katika elimu kwani kuna vijana wetu hawana hata dwati la kukalia, yatima, wajane na wenine wengi wenye mahitaji badala ya kuchangia harusi.

Kufanya harusi kubwa katika kumbi kubwa zenye kugharimu mamilion ya shilingi za kazi gani, kwani hazina tija kwa maendeleo ya taifa hili ambalo wananchi wake wako katiak wimbi la umaskini mkubwa.


Sitoi tena Michango ya Harusi

BAADA ya matukio ya harusi ya Jumamosi iliyopita natoa onyo ole wake atakayeniomba mchango wa harusi, sitaki utani. Labda kwanza nikueleze jinsi tulivyopata misukosuko sana kwenye uchangiaji wa ile harusi, maana siku hizi hakuna pa kukimbilia, kila asubuhi unaamshwa saa kumi na mbili na meseji kwenye simu;

"Ndugu, rafiki na jamaa wa familia ya Pingapinga inakukumbusha kuwa harusi ya mtoto wao imekaribia hivyo mchango wako unahitajika", baada ya wiki meseji huwa kali zaidi;"Siku zinaisha kwa nini hautoi mchango, unajua familia ya Pingapinga ina shughuli ya harusi ya mtoto wao, toa upesi au la usitulaumu."

Basi hizi meseji zilikuwa nyingi kuliko zile za kampuni yangu ya simu inayobuni namna ya kunitoa mkwanja kila wiki. Hatimaye nikatoa faini, maana nisiite mchango, maana mchango haulazimishwi.

Sasa Jumamosi ndiyo ikawa siku ya harusi, kadi nililetewa mapema , nikahakikisha koti langu la kuendea harusini nalicheki vizuri, maana haya makoti yanayokaa kabatini miezi ni muhimu kucheki vizuri maana unaweza kukuta panya kazalia kwenye mfuko halafu wakatimka kutoka kwenye makazi yao wakati uko katikati ya kucheza mduara wa harusi.


Kweli tukaingia ukumbini viti vilikuweko swafi, meza zimepambwa kwa maua na MC alitukaribisha kwa maneno mengi yaliyojaa vichekesho visivyochekesha, au vichekesho vingine vimesharudiwa na kila MC hapa mjini halafu akawa analazimisha watu wapige vigelegele!

Yote bure watu walikuwa wamenuna maana hakukuwepo na dalili ya hata chupa moja ya kinywaji, ila ahadi kibao zikawa zinatolewa na MC, mara ‘Roli la bia linakuja toka breweries, mara shampeni leo inatoka Ufaransa kwa helikopta."

Ghafla wahudumu waliovalia vikofia kichwani wakapitisha sambusa mojamoja na kinywaji round moja kwa kila mtu, wakisindikizwa na MC akituhamasisha tule tufurahi na bwana harusi. Kwa kweli hela yangu ikaanza kuniuma, kwanza nililazimishwa kulipa, halafu sioni chochote hawa jamaa vipi?

Wakati ukumbi mzima ukiwa umeendelea kununa utadhani kikao cha msiba, MC akatuambia eti bwana harusi ana machache kabla ya kutuaga kwenda kupumzika na mkewe. Pamoja na kisirani tulikuwa na hamu kumsikia mshenzi huyu anataka kusema nini.

Bwana harusi akasimama hata suti aliyovaa ilikuwa haijamkaa sawasawa, akakohoa kidogo akaanza, "Asante MC, kwanza naomba nimshukuru Mungu kwa kumuumba mke wangu, kwa hilo Mungu uko juu, kiukweli hapa nimepata mke mtulivu, mpole asiye na makeke, yaani najisikia nina bahati sana.

"Naomba niwashukuru wakwe zangu kwa kukubali kupokea robo tu ya mahari na kuruhusu ndoa hii ifanyike. Pia nishukuru kwa zawadi zao za kitanda, godoro, kabati na makochi asante sana.

"Naomba nitoe shukrani kwa bosi wangu kwa kunipa likizo fupi ili nikamilishe shughuli hii, pia wafanyakazi wenzangu kwa zawadi yenu ya jiko la gesi. Namshukuru mke wa kaka yangu kwa kutuazima gauni la harusi, na kaka yangu kwa suti hii niliyovaa. Natoa shukrani kwa mtengeneza keki, nitairudisha keki kwako kesho kama tulivyokubaliana.

"Nawashukuru wazazi wangu kwa kuja na kikundi cha ngoma toka kijijini, kweli kimeziba pengo la burudani katika harusi hii. Naishukuru kamati ya wazee wa kanisa kwa kufanikisha kumshawishi mke wangu aolewe na mimi, niwape aksante kwa akina mama waliopika sambusa hizi tulizokula kwa kweli zilikuwa tamu sana, kwa kweli leo ni furaha tupu. "MC wewe ni rafiki yangu nashukuru kwa kukubali kuwa mc wa shughuli hiikwakweli upo vizuri, aksante sanaaaaa!

Yaani inamaanisha ela zetu za mchango sijui zilinunua nini maana kila kitu almost kilikuwa bure.. mnaoowa karibuni poleni msinihesabu.

Ni kipindi kingine cha mwaka ambapo kila mwisho wa mwaka kadi za michango ya harusi inakuwa mingi, inakuaje mtu anataka kufanya sherehe kubwa na hana uwezo?

Kwanini usifanye hiyo harusi kutokana na uwezo wako ulionao, ni mpaka usumbue watu wakuchangie?

Tena kinachoudhi ni mtu ameshakaa na mke/mme na wana watoto anataka kupasha kiporo chake nae anataka afanye sherehe kubwa na anachangisha!!

Na kero nyingine mtu anakupa kadi ya mchango wa ndugu yake ambaye humjui.

Sijawahi kupewa au kuona mtu akichangisha kwa ajili ya maendeleo kama vile ada ya shule etc kama majirani zetu na harambee zao zenye maendeleo, sijui wenzangu mnafikiria vipi.

Moja ya kero kubwa na ambayo kwa mtizamo wangu inaweza kuwa kikwazo kwa wananchi wa kawaida kuendana na kaulimbiu ya hapa kazi tu, ni namna tunavyoendesha sherehe mbalimbali za kijamii, kama vile harusi, send-off party, kitchern party na sasa imeongezeka sherehe zingine kama ubatizo, kipaimara, graduation na engagement party.

Raia maskini hulazimika kuchanga pesa nyingi na wengi hulazimika kuingia kwenye mikopo ambayo huwatesa mno, mtu hulazimika kuchangia hata kama hana pesa kwa kuogopa kutengwa na jamii.

Tatizo la pili ni muda ambao sherehe hufanyika. Nyingi huisha usiku sana, "sherehe inaisha saa saba usiku au saa nane, unafika nyumbani saa tisa usiku, kupata usingizi saa kumi alfajiri, asubuhi unatakiwa uwepo kazini saa moja asubuhi. Hivi hapo ufanisi utakuwepo kweli?"

Tatizo la tatu ni siku za sherehe, ukiondoa harusi, sehemu kubwa ya sherehe zilizobakia hufanyika katikati ya wiki, jambo ambalo hupunguza kwa kiasi kikubwa utendaji kazini na wakati fulani huathiri mahudhurio ya wafanyakazi.

Ili kuendana na kauli mbiu ya hapa kazi tu, napendekeza wizara inayohusika na ustawi wa jamii ifanye yafuatayo;

  • Ipige marufuku michango yote ya sherehe, na atakayechangisha aadhibiwe vikali
  • Sherehe zote zifanyike weekend au siku za mapumziko
  • Mwisho wa sherehe zote uwe saa kumi na mbili jioni, adhabu kali itolewe kwa atakayezidisha muda

Familia ziendeshe sherehe kwa gharama zao wenyewe, wasiruhusiwe kuchangisha kwa mtu asiye mwana familia, nchi nyingine kama Zambia wameweza, kwanini sisi tushindwe. Kama nawe unakerwa na jambo hili, toa pendekezo, huenda wahusika nao wakapitia uzi huu.

Alamski!

 
Hapa nilipo nna kadi sita ambazo harusi zote zinafanyika mwezi huu mwishoni na Disemba kila moja si chini ya alfu hamsini.
 
Mimi kinachonishangaza ni huu utaratibu unaosema eti ukichangia elfu hamsini unakwenda na mpenzi wako,,,,lakini ukichangia elfu 25 unenda peke yako na kadi imeandikwa kabisa ni single.....

Utasema concert....
Wabongo bana.....

Yaani huwezi kupata date ukaamua kwenda nae kwenye harusi
kwa kuwa ulitoa mchango wa single.....aghhhh...

Na bila mchango hualikwi....
 
Kinachokera zaidi mtu akiwa anakaribia kuoa/kulewa atakuwa karibu na wewe sana , akishapata mchango kwako ni kwaheri, i think kama tuchangie elimu na misiba tuu, anaehamua kuoa lywake.
 
Michango ni hiari ndugu zanguni hakuna anayekulazimisha kuchanga, na kama inakukela sana weka kabisa tangazo kama professor mmoja wa UDSM alikuwa ameandika kwenye mlango wa ofisi yake "MICHANGO YA HARUSI IMESITISHWA". Sidhani kama kuna mtu anakulazimisha kuchanga.

Usipende kufanya kitu kinachokuumiza na kukukosesha amani kwa sababu ya kuogopa.

Kama hutaki kuchangia sema no kama unachanga changa bila kinyongo ndo faida ya kuwa mwanajamii na kusaidiana!
 
Mie nawashauri hii michango wanayokusanya badala ya kutumia hela zote kufanya harusi kubwa bora watumie hizi hela kuanzia maisha yao ya ndoa.ndoa nyingi nimeona harusi kubwa baada mwezi au miezi wana ndoa wanalalamika maisha magumu.Kwanini hii michango isitumiwe kwa manufaa zaidi baada ya ndoa kuliko siku ya ndoa?
 
Wajameni, hakuna kitu kero kama michango ya harusi kwa sasa... imepoteza maana!! Unakuta mtu anakupangia kabisa - wewe nimekupangia laki tatu tu!!! mtu income ya kawaida halafu anataka harusi ya mil 25 na ukiuliza kachanga ngapi anakwambi milioni moja!!! Very sick tradition... na mara nyingi unakuta mtu anaoa mkewe [meaning they are already living together or have already done everything wanandoa do!!

Sasa subiri sijui chicken party, send-off, bachelors, inner party etc. etc.

It is not a culture to embrace especially now that we need to put all our efforts in development
 
Budget ya Harusi siku hizi si chini ya mil.10,15, 20 ...wtf mimi naona tumezidi kuwa wapofu kula all that amount for one day tunachezea resorces...ukiangalia majirani zetu wanahitaji mtaji wa 50,000, 100,000, 200,000/- kuondokana na umaskini kwa biashara ya vitumbua, mandazi nk...
tuna culture ya kutumia sana kwa ufahari..lol
 
Budget ya Harusi siku hizi si chini ya mil.10,15, 20 ...wtf mimi naona tumezidi kuwa wapofu kula all that amount for one day tunachezea resorces...ukiangalia majirani zetu wanahitaji mtaji wa 50,000, 100,000, 200,000/- kuondokana na umaskini kwa biashara ya vitumbua, mandazi nk...
tuna culture ya kutumia sana kwa ufahari..lol

Huu ndio ukoma wa jamii yetu ya sasa... tunaweka vipaumbele sehemu zisizostahili!!!

Kuna jamaa mmoja wa nje ya afrika kuna siku alisema maneno makali kidogo lakini he was right; alisema
You africans are so amazing, you spend fortune on funerals but nothing on birth and that is where god bless you with a life; mothers and children deaths can be prevented.

You also spend alot on celebrating weddings but you spend less on teaching about faithful marriage

Ilikuwa kauli nzito lakini ina ukweli!!
 
kinachokera zaidi mtu akiwa anakaribia kuoa/kulewa atakuwa karibu na wewe sana , akishapata mchango kwako ni kwaheri, i think kama tuchangie elimu na misiba tuu, anaehamua kuoa lywake

Mkuu umenena... ila hapo kwenye misiba mie ningependa tu-replace na kuchangia wagonjwa ili wapate huduma!!!
 
Kuna vitu siyo sahihi kwenye harusi zetu naamini tunaweza kufurahi bila kutumia hela nyingi sana mimi katika harusi item zifuatazo zinanikera..

1. MC yaani mchekeshaji wa masaa tu 200,000 etc sioni mantiki kabisaaa kwanini asiye rafiki tu anaongoza kwa raha halafu bure kama vikao vyetu infomal sehemu zingine za starehe lol

2. Mapambo ebwana wanakamua sijapata kuona bila sababu ya msingi

3. Ukumbi weka kwenye uwanja wa wazi au nyumbani kwa mzee wako finito lol
 
Mimi nadhani michango ya harusi tungebadilisha matumizi yake, badala ya kunywa na kula hizo mil 10, 15 au 20 kwa usiku mmoja, ni bora hiyo hela wakakabidhiwa bwana na bibi harusi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya makazi au iwe kama mtaji wa biashara, utakuta mtu anafanya harusi ya mil 15 au 20, lakini hana kiwanja wala nyumba.. unakuta amepanga Sinza, Kijitonyama au mbezi beach, hehe hehe.....
We need to change our attitudes and mindset!
 
Hivi huu utaratibu wa sherehe za arusi na patashika zake ni utamaduni wa kabila gani Tanzania? Au ni utamaduni wetu kama watanzania? Au ni utaratibu tuliouiga kutoka utamaduni wa watu gani?

Nchi zilizo endelea kama hapa Marekani hachangishwi mtu, sherehe zinategemea uwezo.

Kwa sababu ni hurka yetu kukopi kila kitu kutoka dunia ya kwanza hata kama ni ugonjwa au udhaifu, nauliza tena ni utamaduni wa nchi gani unafanana na utamaduni huu wa Tanzania wa kuchangishana fedha kwa hila za kishetani?

Labda nyie mlioa miaka ya 196.. mtuambie. baba, mama, shangazi na wajomba zenu waliwachangisha akina nani ili nyie muozwe??

Ili ndoa iitike ni lazima sherehe zake ziwe za kukata kwa Nyengo?

Masikini ni yule atumiaye kipato asichokuwa nacho.

Pendekezo langu kwenu nyie ambao hamjaoa ni hili.

Achaneni na ununda huu wa kudhani sherehe kubwa ndo fahari ya ndoa.
Acheni kuchangia harusi za watu wengine kwa mtindo huu usiojulikana asili yake.

Jiandaeni kufunga harusi Private ambazo zitahusisha ndugu wa karibu tu na bajeti ndogo kabisa ya uwezo wa mfuko wako.

Kuna harusi hapa Marekani jumla ya watu wote katika harusi ni 40 tu. ukitoa wanandoa. Pamoja na ukweli kwamba wana ndugu jamaa na marafiki debe zima.

Kupanga ni kuchagua, hakuna mwenyenia ya wazi ya kuchagua kitu kibaya lakini tuliowengi sikuzote hushindwa kupanga, na hivyo kushindwa kuchagua.

Sasa hawa wenye mifedha ya nguvu wanaandaa sherehe ndogo, sisi tuytemeao makalio nusu wazi tunaandaa sherehe kama wana wa Wafalme.

Kama kuna nchi moja ilojaaa majuha waotao mchana si nyingine ni nchi yetu tukufu Tanzania.

Nahisi Utamaduni wetu wa kuandaa sherehe zilizo zidi uwezo wetu na hamu yetu unatokana na ukweli kwamba, vipato vingi Tanzania si halali.

Kwani viapatao vingi kwa namna moja au nyingine vina uhusiano na wizi udanganyifu na uuaji.

Fedha haramu siku zote hutumika katika namna iliyo haramu. Kibaya zaidi fedha haramu hujenga utamaduni haramu katika jamii bila kujali mipaka.

Watu wenye vipato halali nchini Tanzania ghafla wameshitukia wakijitumbukiza katika utamaduni haramu ambao asili yake ni ibilisi kwa kudhani kwamba wana enzi asili yao.

Kila mtu angependa kunya mavi mengi na makubwa kwa mpigo vile afanyavyo Tembo.

Je Kuna mwenye makalio makubwa ya kuwa na ngebe ya kumwiga Tembo huko msalani?

Huu utaratibu wa kuazima makalio ya wengine yakusaidie huko msalani ni utamaduni gani??
 
Itisha michango kuwa umepata nafasi ya masomo nje ya nchi unaomba uchangiwe ili upate nauli ....wachache sana watakuchangia....
 
Mimi nimeishafanya uamuzi wa kutochangia harusi hovyo. Ni watu wachache tu walio karibu sana na mimi ndio ninaowachangia. Hata hivyo viwango vya kuchangia wanvyoviweka havinipi shida kwa sababu harusi za watu nisiowajua siendi hata nikipewa kadi. Kwa hiyo mimi najiamulia ni nani nimchangie na kiasi gani. Lakini uamuzi huo umenifanya nichukiwe na watu. Mimi sijali. Niko tayari kuchangia mtoto wa jirani aliyekosa au kupungukiwa karo, au mgonjwa aliye hospitalini, au mtu aliyefiwa. The paradox is mgonjwa anakaa hospitali miezi watu hawaendi kumjulia hali au wanaokwenda hawaendi na msaada wowote. Lakini akifariki hao hao wanalala kwenye msiba siku tatu au hata nne na michango wanatoa kwa mbwembwe kwa kuwa watu wanakuwa wanashuhudia. Lengo hapa ni kujitangaza na sikusaidia. It is completely irational.
 
Huwa nasema siku zote bora hata harusi za waislam ambazo hazina complication nyingi, watu wakipiga mpunga na ndizi kazi kwisha. Utakuta mtu anabudget ya harusi ya milioni 20, halafu yeye ana milioni 1, sasa huu umekua mradi au? sasa hiyo pesa akipata yote anapeleka kwenye harusi then ikiisha wanarudi kuwa maskini. Watu kama wanaomba michango basi iwe kwa ajili ya maisha na sio kwa ajili ya kula siku moja then kwisha. Mimi Mungu akisaidia nikawa na mipango ya harusi sitawachangisha watu, na kila aliyekaribu nami nitamwalika. Hapo hapo mtu akiambiwa achangie yatima au wagonjwa wnakua wagumu sana kufanya hivyo
 
Mkuu umenena... ila hapo kwenye misiba mie ningependa tu-replace na kuchangia wagonjwa ili wapate huduma!!!
Tatizo ni kwamba mtu akiwa anaumwa huwa haitangazwi sana, lakini akiaga dunia ndo habari inasambazwa kwa kasi. Unaweza ukawa na moyo wa kusaidia mgonjwa lakini usipate taarifa na ghafla tu unakuja kujulishwa habari ya msiba.
 
Kuna kitu kwenye kikao za harusi zinaitwa "UCHAKAVU" ina maanisha michango ya kula na kunywa pale kwenye kiao cha harusi, watu wanapiga beer na nyama choma kwenda mbele....usishangae ukatoa uchakavu 50,000 wakati umekunya beer mbili na kipande cha kuku..........hizi tuache jamani
 
Kuna kitu kwenye kikao za harusi zinaitwa "UCHAKAVU" ina maanisha michango ya kula na kunywa pale kwenye kiao cha harusi, watu wanapiga beer na nyama choma kwenda mbele....usishangae ukatoa uchakavu 50,000 wakati umekunya beer mbili na kipande cha kuku..........hizi tuache jamani

heeeeeeeee, yani hapo mkuu umelenga!.
ebwana kuna kikao kimoja nilihudhuria, mshkaji alikunywa bia 4, kumbe watu wanamuangalia tu spidi yake, kufika kwenye uchakavu si akatoa 1000/=, acha akunjwe shati alipie,. hakuna usawa mie ninywe maji ya 300 mwingine anywe bia 5 halafu tutoe sawa uchakavu, Lol.
 
Back
Top Bottom