MJADALA: Je, ni sahihi waimbaji wa nyimbo za dini kushiriki matamasha ya kidunia?

Huyo jamaa amejivika tu ngozi ya kondoo,kuna baadhi ya wasanii wakubwa wa bongo fleva anawaandikia nyimbo za mapenzi na bang za club,kwahiyo ni mtu alijificha tu hayupo real.
Dah, sikujua hili mkuu
 
Ni sahihi sana tu...hata yesu mwenyew alikaa na wenye dhambi....
Naogopa sana wadadamu tunapopata ujasiri wa kusema ile ni dhambi ila hii nifanyayo sio dhambi. Huwa nakumbuka sana wimbo wa wakatoliki usemao:
"Wenye afya hawamuhitaji daktari, wanaomhitaji ni walio wagonjwa….
Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi, ili wapate kutubu!"
 
Kumbuka alikuwa mfalme
Nikufundishe neno, mfalme ni Kristo tu. Daudi alicheza mpaka nguo ikadondoka, alikuwa anamchezea nani? FIESTA? Huyo mwwnamziki alikuwa anacheza maunonhayo anamkatia nani? Maana yangu ni je, tamasha lilihusu nini, na Daudi alicheza kwenye tamasha lipi? Sanduku la Agano vs tamasha la shetani
 
Nikufundishe neno, mfalme ni Kristo tu. Daudi alicheza mpaka nguo ikadondoka, alikuwa anamchezea nani? FIESTA? Huyo mwwnamziki alikuwa anacheza maunonhayo anamkatia nani? Maana yangu ni je, tamasha lilihusu nini, na Daudi alicheza kwenye tamasha lipi? Sanduku la Agano vs tamasha la shetani

Well said 👏👏👏
 
Huwezi kusema ameenda kuhubiri injili wakati amelipwa ili kwenda kuburudisha watu kwenye tamasha la kumsifu shetani...

Umejionesha hapa una uelewa mdogo sana (kama unao anyway hata huo mdogo), kwa hiyo duniani ni Injili na shetani tu.... kwa maana hakuna burudani kwa ajili ya binadamu tu bali lazima iwe ni aidha Mungu au shetani..!!
 
Ilikuwa kwenye tamasha la FIESTA? Think!!

Kwani kuitwa FIESTA ndio maana yake tamasha la shetani..?

Wakulima tumekuwa tukisherehekea mavuno kwa kuimba na kucheza ngoma za asili, na hata hivyo burudani zimekuwepo tangu na tangu na pia matamasha ya kitaifa.... kwahiyo kila lifanyikalo nje ya nyumba za ibada ni la shetani..!!
 
Daah haya mambo ya imani siku hizi hata sitakagi kuhukumu sana, maana tunaweza tukawa tunahukumu hapa kumbe hatujui labda mwenzetu alivyotoka pale alitambua kosa lake akaenda kumlilia Mungu wake amsamehe ila sisi tumekaa huku tunamjadili vibaya.

Tukumbuke kwamba kuwa mtumishi wa Mungu hakukufanyi uwe malaika kwamba hautatenda dhambi hilo hata Mungu analijua, hata kina Solomon na David na unabii wao walitenda dhambi (walizini waliua) lakini walikuwa na imani kali na mwisho wa siku walimlilia Mungu awasamehe na bila shaka aliwasamehe.

One thing I believe for sure hawa watumishi wa Mungu (wengi wao) wanajua sana kuishi na Mungu, tunaweza tukaona huku wanatenda dhambi tunasikia oohh sijui mchungaji amezini sijui padre ameua tunawahukumu na kuwatolea kashfa za kila aina kana kwamba sisi ni watakatifu sana.

Lakini hatujui wakiwa peke yao majumbani mwao wanaongea nini na Mungu hatujui wanamlilia Mungu kiasi gani awasamehe, na tukumbuke kuwa hakuna dhambi chini ya jua isiyosameheka isipokuwa dhambi moja tu ya kumkufuru Mungu basi and to God there is always a second chance for as long as we are still alive.
Atamlilia mara ngapi????? Maana anaendelea kufanya fiesta na kukata maunoo kila siku...Yule jamaa ni mpiga hela tuu...
 
Nikufundishe neno, mfalme ni Kristo tu. Daudi alicheza mpaka nguo ikadondoka, alikuwa anamchezea nani? FIESTA? Huyo mwwnamziki alikuwa anacheza maunonhayo anamkatia nani? Maana yangu ni je, tamasha lilihusu nini, na Daudi alicheza kwenye tamasha lipi? Sanduku la Agano vs tamasha la shetani
Hiyo Nongwa...Kwani kanisani wanaenda watakatifu watupu....Ushetani huko kanisani wanachangisha sadaka alafu wanaenda kufungua biashara binafsi
 
Kwa waandaaji walidhamiria kupeleka mziki wa injili kwa hao watu, na ilikuwa target nzuri sababu mnawakusanya pamoja afu mnawapiga nondo za Injili

Na pia walitaka kunufaika pia kwa kuleta ladha ya tofauti kwa mashabiki wao

Kwa Mwimbaji nae pia hilo ndo lengo, pamoja na kuhakikisha kuwa wimbo wake unawafikia walengwa wake, Wimbo wake huu mpya, umeimbwa kuwalenga wakristo walio kengeuka, ambao wakiwa kanisani wanasinzia, ila wanapenda kuparty na kwenda kunywa beer, Wimbo una lengo la kuwafanya wakumbuke wanachofanya kuwa si sawa afu watafakari mienendo yao na wamuombe Mungu awasaidie.Hawa sio wakristo ambao ungewapata kokote kule kwa wingi ,zaidi ya kwenye TigoFiesta. Na wamejaa mtaani.

Na piaaa, kuhoji hili suala unakuwa hauna tofauti Na Mafarisayo walio hoji kama ni halali kwa Yesu kwenda Kula nyumban kwa Zakayo Mla Rushwa na mtoza Ushuru na kuhoji kama ni halali kwa kupakwa mafuta yule mama kahaba.

Jibu la Yesu lilikuwa simple kuwa wenye njaa ndo wanaohitaj chakula, wagonjwa ndo wanaohitaji kumuona Daktari.

Huyo mwanamziki ndo mwanamziki pekee ambae nimeona had sasa aliefanikiwa kuifikisha injili kwa walengwa.

Wengine wanapeleka injili kwa wachungaji, Injili peleka kwa walevi huko
 
Yupo sahihi sana, zaidi ya sana

Na ukiona wewe ni mkristo, unaejali kuhusu injili kupenya halafu unajiuliza hili suala, basi jua uinjilishaji wako una walakini

Hakuna watu wanaopaswa kusikiliza wimbo wa Goodluck, zaid ya wakristo walio kengeuka, ambao ndo wamejaa siku hizi. Na hakuna sehemu kwa kuwapata zaidi ya huko Fiesta

Goodluck Gozbert amekuwa kama agent wa siri wa Injili, anae nena kama wao, na kufikisha ujumbe kwa lugha na namna inayo waingia vizuri

Ila recently nimegundua wimbi kubwa la "wakristo "wanafiki ambao wakiwa sirini wanafanya yaliyo imbwa (wanasinzia ibadani, ila wakiwa kwenye story na cmu na aina yoyote ya ulevi, sio lazima pombe, hawazinzii)

Hawa wakiusikia huu wimbo unawachoma, na wanaishia kuuchukia

Neno langu ni kuwa, watu watafakari njia zao,na waamue kama wanataka kuendelea kuishi maisha ya unafiki au real
 
Aliomba mwenyewe nafasi ya fiesta hakuitwa
Kwa waandaaji walidhamiria kupeleka mziki wa injili kwa hao watu, na ilikuwa target nzuri sababu mnawakusanya pamoja afu mnawapiga nondo za Injili

Na pia walitaka kunufaika pia kwa kuleta ladha ya tofauti kwa mashabiki wao

Kwa Mwimbaji nae pia hilo ndo lengo, pamoja na kuhakikisha kuwa wimbo wake unawafikia walengwa wake, Wimbo wake huu mpya, umeimbwa kuwalenga wakristo walio kengeuka, ambao wakiwa kanisani wanasinzia, ila wanapenda kuparty na kwenda kunywa beer, Wimbo una lengo la kuwafanya wakumbuke wanachofanya kuwa si sawa afu watafakari mienendo yao na wamuombe Mungu awasaidie.Hawa sio wakristo ambao ungewapata kokote kule kwa wingi ,zaidi ya kwenye TigoFiesta. Na wamejaa mtaani.

Na piaaa, kuhoji hili suala unakuwa hauna tofauti Na Mafarisayo walio hoji kama ni halali kwa Yesu kwenda Kula nyumban kwa Zakayo Mla Rushwa na mtoza Ushuru na kuhoji kama ni halali kwa kupakwa mafuta yule mama kahaba.

Jibu la Yesu lilikuwa simple kuwa wenye njaa ndo wanaohitaj chakula, wagonjwa ndo wanaohitaji kumuona Daktari.

Huyo mwanamziki ndo mwanamziki pekee ambae nimeona had sasa aliefanikiwa kuifikisha injili kwa walengwa.

Wengine wanapeleka injili kwa wachungaji, Injili peleka kwa walevi huko
 
Huyo dogo simkubali ila nimekumbuka kuwa Yesu alisema nilikuja kwa ajili ya wenye dhambi

Alisema hivyo baada ya kusakamwa kuwa anakaa na wenye dhambi, watoza ushuru, makahaba na masikini
 
Albamu hamnunui. Mtu akijitahidi aone anatengeneza pesa mnadai anafanya ushetani.

Mwanadamu hawezi kuishi kwa neno tu. Let him be!
 
Yaani watu wanabarikiwa sababu ya huyo
goodluck?? Hivi unajua pia huyu jamaa ni
choko?
Una uhakika au unajiongelesha tu inaonekana wewe ndio michezo yako matako wewe jiheshimu mtu mzima kumuongelea mwenzio hivyo??! Umeboa kinoma
 
Amani iwe nanyi nyote.

Nimeona clip ikimuonyesha muimbaji wa nyimbo za injili mchini, Goodluck Gozbert akitumbuiza kwenye tamasha la Tigo Fiesta huko Mwanza. Nimeshangaa na kujiuliza maswali;

i/Mtumbuizaji anaelewa maudhui ya tamasha lile?
ii/Waandaaji walifikiria nini kumleta muimbaji wa nyimbo za injili kwenye tamasha linalokutanisha watu wa imani tofauti tofauti?
iii/Je, kilichofanyika ni halali kidini na kijamii pia?

Karibuni tujadili na kueleweshana pale pasipoeleweka.

Nawasilisha.


Kwani hizo nyimbo za Injili huwa wanawaimbia malaika mbinguni?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom