Ni gari nzuri kwa bajeti yako tafuta NT-30 ya 2004 unaweza pata nzuri kabisa kwa $3,000Wadau nimejichanga toka 2014 mpaka leo nimetimiza lengo la kama 8000 USD nataka kuagiza Nisaan X-trail toka japan. Mwenye ujuzi wa hiz gari msaada tafadhali. Vipi ulaji wa mafuta, spea, ugumu kwa barabara za bonyokwa hukoooo...
-4,000CIF.
Ina uvungu mkubwa sana hivyo hainasi kwnye magema ya barabara za bonyokwa, pia ina mfumo mzuri sana wa 4WD unapita mahali pengi patakapokushangaza hata wewe mwenyewe.
Kwa safari ndefu kale kadude ni roketi...prado nyingi na magari makubwa makubwa yatakuwa yanasoma namba na balansi yake ni nzuri.
Na nafasi ya abiria (haswa seat ya nyuma) na mizigo ni ya kutosha kqbisa.
Ila zingatia service, usivushe service ya oil...hakikish coolant ipo ya kutosha...hiyo gari injini yake ni QR 20, ikichemsha hasara yake ni kubwa..
Na epuka spear za kanjanja basi maisha yako na xtrail utaipenda sana.