Mjadala huru! Ni sekta ipi inayoendeshwa na Serikali inafanya vizuri?

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,227
26,048
1. Mradi wa mwendokasi Dar. Huku mabasi hayafanyiwi maintainance, yanaharibika watu hawajali, kila siku watu zaidi ya laki 1 wanatumia mabasi haya na fedha zinakusanywa na mamlaka husika Ila kila siku mradi uko hovyo!

Vituo vyake vinazidi kuchakaa na mabasi yanazidi kuchakaa.

Haieleweki Kama waliopewa kazi ya kuendesha mradi hawawezi au la! Serikali ndo wanaendesha mradi

2. Bandari za Dar, Mtwara, Kigoma, Mwanza.

Huku nako hakueleweki, mapato yanakusanywa Ila inaelezwa ni kidogo kuliko ilivopaswa! Ucheleweshwaji wa mizigo kila siku imekuwa wimbo.

Serikali ndo wanaendesha mradi ingawa Kuna sehemu ndogo imewasha sekta binafsi ambayo inasemwa hii haina malalamiko sana!

3. Reli ya Kati. Hii imeanzia Dar , inaenda Mwanza, Kigoma na Katavi, huku nako hakufai. Treni zina hali mbaya , miundombinu nayo haifai.

Kila siku ni bora ya jana na wasafiri wanaotumia usafiri huu wanaelewa hali ikoje.

4. Reli ya TAZARA. Hii aieleweki kama iko hai ama imekufa. Kwa ufupi haieleweki

5. Viwanja vya mpira mikoa yote ukiwemo uwanja wa Taifa. Hii nayo haifai iko hovyo kwenye hali mbaya kupindukia.

Uwanja wa a Taifa ndo hadi watu wanakojoa kwenye masinki ya vyoo!

6. Vituo vya mabasi. Hivi viko hoehahe. Kila siku mapato makubwa yanakusanywa Ila haieleweki yanaenda wapi

Kwa mtazamo wangu naunga mkono Bandari ya Dar es Salaam kupatiwa mwekezaji binafsi kuiendesha.

Serikali isimamie kitengo cha ulinzi wa Usalama tu. Pia katika kuhakikisha tunafanya vizuri kwenye Bandari Bandari zote ziendeshwe kwa mfumo huo.

Kikubwa apatikane mwekezaji wa maana tu kama Mwekezaji aliyepewa NMB na wawekezaji wengine makini ambao tumeona walivyofanya kazi nzuri!
 
1. Mradi wa mwendokasi Dar. Huku mabasi hayafanyiwi maintainance, yanaharibika watu hawajali, kila siku watu zaidi ya laki 1 wanatumia mabasi haya na fedha zinakusanywa na mamlaka husika Ila kila siku mradi uko hovyo...
TRA mkuu
 
Atcl, tanesco nk yalishwahi kua na wabia wa kuyaendesha, hao ndio walioyaua.

Ukiangalia kwa mantiki inatakiwa ataftwe mbia wa kuiendesha ccm ambayo ndio inaongoza nchi kwa miaka zaidi ya 60 na haya Madudu na hovyo hovyo zinazoendelea nchini kwani wanaccm na viongozi wao wa sasa wameshindwa kwenye kila kitu.

Huyu mama yeye wanamuingiza chaka kila siku. Ngoja tutaona tu.
 
Atcl, tanesco nk yalishwahi kua na wabia wa kuyaendesha, hao ndio walioyaua.

Ukiangalia kwa mantiki inatakiwa ataftwe mbia wa kuiendesha ccm ambayo ndio inaongoza nchi kwa miaka zaidi ya 60 na haya Madudu na hovyo hovyo zinazoendelea nchini kwani wanaccm na viongozi wao wa sasa wameshindwa kwenye kila kitu.

Huyu mama yeye wanamuingiza chaka kila siku. Ngoja tutaona tu.
NMB Je?
 
Kwahio hao Wabia watakuja na watendaji wao kutoka Mwezini ?

Au tumesahau ubinafsishaji wa Viwanda vyetu vikiwemo vya nguo na mpaka baadhi ya mashamba watu walivyoyatumia kukopea mikopo na ku- dissapper kama walivyo-appear

Tatizo lipo wapi, kama hao wawekezaji wanaona kuna potential ya wateja si waje waingie kwenye game tufanye nao bega kwa bega ?,

Kama ni Meli walete zao, Kama ni Train walete zao, kama ni mabasi walete yao...., basi competition iendelee haya mambo ya watu kujitengenezea 10% katika kusign hii mikataba nadhani miaka kumi baadae tutakuwa tunaongelea kwamba fulani alituingiza kwenye mikataba mibovu (we never learn)
 
Jadili mada yote na icho kipengele
serikali inataka kuuza kila kitu,
kama wanashindwa kusimami hiyo bandari ni nini sasa wataweza,
wakishamaliza kuuza bandari, wataenda airport.. wakimaliza kila kitu,
wauze hadi ikulu.

serikali iliyopita ilituambia na kutuaminisha kuwa inaweza kufanya biashara na kujisimamia ndio maana ikanunua hadi ndege, ikafufua ttcl nk.

serikali hii inakiri haiwezi kusimamia inataka kubinafsha.

kweli tumepatikana.
 
Kwahio hao Wabia watakuja na watendaji wao kutoka Mwezini...
Ndugu yangu, tatizo la Tz ni siasa na ubinafsi zaingilia mambo mengi ya msingi....

serikali huwa inataka ifanye kila kitu, na kupenda ' Monopoly' karibu kwenye kila kitu ili kukwepa competition...na haitaki weka 'plain field' ya kuruhusu competion itakayoleta ufanisi wenye tija.....

waulize kampuni ya Fast jet na kilichotokea....Tz kaazi kwelikweli na safari bado ni ndefu.
 
Mimi siku nikiwa rais wa hii nchi.

ntabinafisha kila kitu na kuacha sekta muhimu km za maji, afya, usafiri na umeme...maana ishajihidhirisha serikali haiwezi kufanya biashara kutokana na incompetent culture ambayo imeshamiri miongoni mwa wafanyakazi wa serikali

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom